Hoja ya "No reform, no election" mimi nakwenda na Lissu

Hoja ya "No reform, no election" mimi nakwenda na Lissu

MwajabuOmary

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2013
Posts
384
Reaction score
418
Suala hili limekua likikejeliwa na ccm bila kuja na hoja zenye mashiko.
Hoja zangu ni hizi:-

1. Kwa upande wangu mimi, nikiangalia kwa upande wa vyama vya upinzani nabaini kwamba ni kichaa peke yake ndio anaweza kushiriki uchaguzi wa October, 2025 akiwa anajua kwamba asilimia 85 ya wagombea wake wataenguliwa hata kabla ya kampeni kuanza.

2. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea wake ambao wanaweza kuuliwa na watu waliojificha katika mwavuli wa watu wasiojulikana.

3. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea ambao wakati wa kurudisha fomu Mkurugenzi anayo mamlaka ya kupokea au kutopokea fomu tena kwa utashi wake na bila kuchukuliwa hatua zozote na badala yake wanapandishwa vyeo.

4. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea ambao anajua kabisa wakati wa kurudisha fomu, wagombea hao wanaweza kutekwa na kupotezwa misituni

5. Ni kichaa peke yake anaweza kuingia katika uchaguzi wa October 2025 akiamini kuwa mawakala wake hawatapewa barua za uwakala kwa wakati.

6. Ni kichaa peke yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo akiamini kwamba kura zitaanza kupigwa asubuhi na mapema kabla ya wakala wake kufika.
Ni mjinga peke yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua dola ipo upande wa pili kusaidia.

7. Ni mwendawazimu pekee yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua kutangazwa mshindi haijalishi umepata kura kiasi gani bali kutangazwa mshindi kunategemea unatoka chama gani

8. Ni mjinga pekee ndio anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua kwamba TUME haina tawimu sahihi za wapiga kura.

9. Unakwendaje kwenye uchaguzi ambapo tayali vyama vingine vimekwishaanza kampeni za wazi wazi mwaka mmoja kabla ya kipindi cha kampeni kuanza na hakuna wa kukemea.

10. Ni mjinga peke yake anaeweza kusimamisha wagombea ambao wakati wa kurudisha fomu watakuta ofisi ya Mkurugenzi/msimamizi wa uchaguzi itakutwa imefungwa na ni nyakati za saa za kazi.

Kwa hayo machache tu japo na mengine mengi tu yapo unaingia kwenye uchaguzi ILI IWEJE.
VYAMA VYA UPINZANI MJITAFAKARI.

KWA UPANDE WANGU " NO REFORM NO KWENDA KUPIGA KURA"

NAWASILISHA
 
Okay, sawa.

Lakini unapaswa utambue kwamba, hakuna uwezekano wa kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu Mwaka huu wa 2025.

Aidha, ni kweli kabisa kwamba Hoja za Watu wa CHADEMA ni za kweli, pia ni za msingi. Hoja zao zina mashiko kuhusiana na Kukosekana kwa Mamlaka zinazoaminika kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi ulio huru, wa HAKI na ulio wa Wazi.

Jambo la muhimu zaidi la kuzingatiwa ni kwamba: KAMWE CCM HAITAWEZA KUKUBALI KWA HIYARI KUBADILISHA MIFUMO YA UCHAGUZI. NA KAMWE CCM HAITAWEZA KUKUBALI KWA HIYARI KUBADILISHA KATIBA YA NCHI.

KAMWE HAUPO KABISA UWEZEKANO WA KUBADILISHA KATIBA YA NCHI KWA NJIA ZA KIDEMOKRASIA. HAUPO UWEZEKANO!

Kwa bahati mbaya sana, huu ndio Ukweli mchungu Sana kupita kiasi!
 
Suala hili limekua likikejeliwa na ccm bila kuja na hoja zenye mashiko.
Hoja zangu ni hizi:-
1. Kwa upande wangu mimi, nikiangalia kwa upande wa vyama vya upinzani nabaini kwamba ni kichaa peke yake ndio anaweza kushiriki uchaguzi wa October, 2025 akiwa anajua kwamba asilimia 85 ya wagombea wake wataenguliwa hata kabla ya kampeni kuanza.
2. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea wake ambao wanaweza kuuliwa na watu waliojificha katika mwavuli wa watu wasiojulikana.
3. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea ambao wakati wa kurudisha fomu Mkurugenzi anayo mamlaka ya kupokea au kutopokea fomu tena kwa utashi wake na bila kuchukuliwa hatua zozote na badala yake wanapandishwa vyeo.
4. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea ambao anajua kabisa wakati wa kurudisha fomu, wagombea hao wanaweza kutekwa na kupotezwa misituni
5. Ni kichaa peke yake anaweza kuingia katika uchaguzi wa October 2025 akiamini kuwa mawakala wake hawatapewa barua za uwakala kwa wakati.
6. Ni kichaa peke yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo akiamini kwamba kura zitaanza kupigwa asubuhi na mapema kabla ya wakala wake kufika.
Ni mjinga peke yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua dola ipo upande wa pili kusaidia.
7. Ni mwendawazimu pekee yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua kutangazwa mshindi haijalishi umepata kura kiasi gani bali kutangazwa mshindi kunategemea unatoka chama gani
8. Ni mjinga pekee ndio anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua kwamba TUME haina tawimu sahihi za wapiga kura.
9. Unakwendaje kwenye uchaguzi ambapo tayali vyama vingine vimekwishaanza kampeni za wazi wazi mwaka mmoja kabla ya kipindi cha kampeni kuanza na hakuna wa kukemea.
10. Ni mjinga peke yake anaeweza kusimamisha wagombea ambao wakati wa kurudisha fomu watakuta ofisi ya Mkurugenzi/msimamizi wa uchaguzi itakutwa imefungwa na ni nyakati za saa za kazi.

Kwa hayo machache tu japo na mengine mengi tu yapo unaingia kwenye uchaguzi ILI IWEJE.
VYAMA VYA UPINZANI MJITAFAKARI.

KWA UPANDE WANGU " NO REFORM NO KWENDA KUPIGA KURA"

NAWASILISHA
Kwahiyo reform inatakiwa ifanyike wapi na wapi ili haya yote yaweze kuondoka? Na unadhani inaweza kuchukua muda gani? Na je, ni kweli reform ikifanyika haya maeneo yote uliyoyaorodhesha yatakuwa stable?
 
Kwahiyo reform inatakiwa ifanyike wapi na wapi ili haya yote yaweze kuondoka? Na unadhani inaweza kuchukua muda gani? Na je, ni kweli reform ikifanyika haya maeneo yote uliyoyaorodhesha yatakuwa stable?
Machafuko ama mapinduzi ya kijeshi pekee ndio yanaweza kuleta mabadiliko ya kweli.
 
Suala hili limekua likikejeliwa na ccm bila kuja na hoja zenye mashiko.
Hoja zangu ni hizi:-
1. Kwa upande wangu mimi, nikiangalia kwa upande wa vyama vya upinzani nabaini kwamba ni kichaa peke yake ndio anaweza kushiriki uchaguzi wa October, 2025 akiwa anajua kwamba asilimia 85 ya wagombea wake wataenguliwa hata kabla ya kampeni kuanza.
2. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea wake ambao wanaweza kuuliwa na watu waliojificha katika mwavuli wa watu wasiojulikana.
3. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea ambao wakati wa kurudisha fomu Mkurugenzi anayo mamlaka ya kupokea au kutopokea fomu tena kwa utashi wake na bila kuchukuliwa hatua zozote na badala yake wanapandishwa vyeo.
4. Ni kichaa peke yake anaeweza kuweka wagombea ambao anajua kabisa wakati wa kurudisha fomu, wagombea hao wanaweza kutekwa na kupotezwa misituni
5. Ni kichaa peke yake anaweza kuingia katika uchaguzi wa October 2025 akiamini kuwa mawakala wake hawatapewa barua za uwakala kwa wakati.
6. Ni kichaa peke yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo akiamini kwamba kura zitaanza kupigwa asubuhi na mapema kabla ya wakala wake kufika.
Ni mjinga peke yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua dola ipo upande wa pili kusaidia.
7. Ni mwendawazimu pekee yake anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua kutangazwa mshindi haijalishi umepata kura kiasi gani bali kutangazwa mshindi kunategemea unatoka chama gani
8. Ni mjinga pekee ndio anaeweza kushiriki uchaguzi huo huku akijua kwamba TUME haina tawimu sahihi za wapiga kura.
9. Unakwendaje kwenye uchaguzi ambapo tayali vyama vingine vimekwishaanza kampeni za wazi wazi mwaka mmoja kabla ya kipindi cha kampeni kuanza na hakuna wa kukemea.
10. Ni mjinga peke yake anaeweza kusimamisha wagombea ambao wakati wa kurudisha fomu watakuta ofisi ya Mkurugenzi/msimamizi wa uchaguzi itakutwa imefungwa na ni nyakati za saa za kazi.

Kwa hayo machache tu japo na mengine mengi tu yapo unaingia kwenye uchaguzi ILI IWEJE.
VYAMA VYA UPINZANI MJITAFAKARI.

KWA UPANDE WANGU " NO REFORM NO KWENDA KUPIGA KURA"

NAWASILISHA
Hongera sana
 
Machafuko ama mapinduzi ya kijeshi pekee ndio yanaweza kuleta mabadiliko ya kweli.
Sisemi kwamba nakuunga mkono ila tofauti na hapo njia zingine almost zote zitaangukia kwenye upande wa watawala.

Mabadiliko yanayozingatia kufuata utaratibu huwa hayaji tu kwa usiku mmoja, ni process na katika process ya namna hiyo lazima watu wakubali kuvuja jasho ila pia wasiogope kuvuja damu pale itakapo waladhimu.
 
Machafuko ama mapinduzi ya kijeshi pekee ndio yanaweza kuleta mabadiliko ya kweli.
CCM wasitufikishe huku..
Mh Rais ita wapinzani kaa nao mezani kuweka mazingira huru ya Uchaguzi 2025. Mh Kilwete, Late Kibaki , Karume, Komandoo Salmin na hata Kenyata na sasa Ruto, wote waliwaita wapinzani wao..wakateta na nchi zikasonga mbele

Usiwasikilize sana baadhi ya hao Wapambe wanakudanganya kama walivyofanya kwa Late Nyerere na Mkapa

Mama Tanzania ni mkubwa na muhimu kuliko CCM, CDM na ACT
 
Back
Top Bottom