#COVID19 Hoja ya Polepole na hoja ya Gwajima juu ya chanjo ya Covid-19

#COVID19 Hoja ya Polepole na hoja ya Gwajima juu ya chanjo ya Covid-19

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Polepole: Moja, Polepole yeye anasema kuwa corona ni ugonjwa uliotengenezwa na big pharma ili yapige pesa. Kuwa mabeberu wanaachana na kuvamia nchi kuiba mafuta na sasa wanatengeneza magonjwa ili kupiga pesa.

Pili, Anasema kuwa kasi ya kirusi kubadilika(ku-mutate) inatia shaka, si ya kawaida.

Tatu, anauliza chanjo hiyo itamkinga kwa muda gani? Akatolea mfano kuwa chanjo zingine hudumu maisha yote ya mtu, je hii inadumu muda gani? Hapo anamaanisha kuwa atahitajika kuinunua mara ngapi?

Gwajima yeye anasema kuwa chanjo zile zina serial number, kuwa ukichanja zinakusajili. Kwamba ipo kama barcode, itafika wakikuwekea detector itasoma iwapo umechanja au haujachanja. Kuna mahali amewahi husisha chanjo hii na habari za 666 na ujio wa mfumo mpya, ndiyo maana anasema kuwa watu waananunua dhahabu kwa wingi ili kujiandaa na mfumo mpya, mfumo ambao pengine pesa za makaratasi zisiwe na thamani.

Pia anahoji kuwa kama ukichanja bado utatakiwa kuvaa barako, kutumia sanitizer, utaugua na utaambukiza wengine, ya nini kuchanja?

Amewahi kusema kuwa chanjo ya mRNA inabadilisha watu na kuwafanya mazombie, hivyo akashauri kuwa wanajeshi wasichanjwe.

Kifupi hizi ndizo hoja za hawa wabunge wawili walio mbele kupinga uchanjaji.

Mi kwa maoni yangu ni kuwa hawa jamaa hawana hoja za msingi bali ni Conspiracy theorist tu.
 
Hoja ya Polepole kuwa virusi vinaweza kuwa vimetengenezwa ina mashiko, virusi vinaweza kutengenezwa na kutumika kama bio-weapons, virusi hivi vinaua kama vile vya asili tu. Lakini kusema unapinga chanjo kwasababu kirusi ni cha kutengenezwa na siyo cha asili ni hoja dhaifu. Kirusi cha kutengeneza na kile cha asili vyote njia ya kupambana navyo ni chanjo. Kukataa chanjo kwa sababu hiyo ni kama kusema, "kama mmeamua kuniua niueni." Kuwa kirusi cha kutengeneza siyo sababu ya kukataa chanjo. Tumuulize, ni kweli kirusi ni cha kutengeneza, na kinaua, tupambane nacho vipi?

Kusema vinabadilika badilika kila mara, hilo linatokea kama kirusi kina hosts wengi sana. Hapa kama kirusi kimeambukiza watu wengi sana lazima kina kuwa na nafasi ya kubadilikabadilika kubwa. Ukipunguza idadi ya watu wanaoambukizwa hata kasi ya kirusi kumutate itapungua. Kama Africa ambayo haichukui tahadhari ya kutosha, itakuwa uwanja wa kirusi kumutate. Hata virusi vya mafua ya kawaida hubadilika badilika na WHO ipo macho sikuzote kufuatilia mutation yake.

Tukizungumzia mafua ya kawaida, mafua ni ugonjwa wa ndege, sasa kirusi kile kikibadilika kinaweza kuambukiza nguruwe na kuleta mafua ya nguruwe, au kikabadilika na kuleta mafua kwa binadamu, na kile kilicholeta mafua ya nguruwe kinaweza ruka tena na kuleta mafua kwa binadamu. Watu wa Afya wako chonjo kwenye machinjio za ndege juu ya kuzuka virusi hivyo. Na vinaibuka mara kwa mara. So jambo la kirusi kubadilika mara kwa mara lipo kwa virusi vingi, vikipata mazingira mazuri vinafanya hivyo kwa kasi kubwa.

Kuhusu chanjo inakulinda kwa muda gani hilo linategemea mambo mengi. Chanjo Inatarget aina ya kirusi kilichopo. Kama kirusi kikibadilika kabisa kiasi cha kufanya kinga iliyozalishwa na chanjo isiweze kukitambua, itakuwa haina kazi tena. Muda wa chanjo kufanya kazi unategemea sana mutation rate ya kirusi. Kama kipo stable, chanjo inaweza kukitokomeza kabisa, kama polio.

Polepole ni muumini wa mwisho wa dunia, 666, new world order na conspiracy kama hizo, hivyo anajaribu kutafsiri jambo hili kwa mtazamo huo. Si sawa.
 
Mbona kuna mtu alikuwa kachomwa chanjo tena alichomwa mapema kabisa baada ya rais kutangaza chanjo,

Ana umri wa 58, wiki iliyopita alijisikia homa akawa anapumua kwa shida, akalazwa akawekewa oksjen, baadae akafariki!
Na alikuwa kachomwa chanjo!

Hii imetokea kwa mmoja ninayemjua kabisa alichomwa, je wangapi huko wanakufa na corona wakati chanjo walichoma
 
Gwajima haeleweki kabisa. Hoja ya kusema kuwa kirusi kina serial number na ni kama bar code haina ushahidi wowote. Ni amezusha tu madai kuwa chanjo ya korona inatusajili. Ni madai yasiyo na ushahidi, na umeyatoa akiyahusianisha na habari alizosoma juu ya 666, new world order na conspiracy za namna hiyo.

Na kusema kwa sababu chanjo ni ya mRna basi itatufanya mazombie au kutubadilisha si sahihi. Kawaida virusi vikiingia kwenye seli huingiza Rna zao, hizo hufanya seli kutengeneza protini za kuzalisha virusi vingine. So kirusi kimoja kikiingia kinaitumia seli ya binadamu kuzalisha protini za kuzalisha virusi vingi hadi vinaua hiyo seli. Na kirusi cha UKIMWI kinafanya hivyo, hatujawahi badilika wala kuwa mazombie. Hata hiyo chanjo ya mRNA inafanya kwa kiasi kama hivyo. Inenda kusababisha protini fulani ya kirusi(siyo kirusi chote) izalishwe. Protini hiyo ikigunduliwa na kinga ya mwili inafanya mwili utengeneze kinga dhidi yake. Siku nyingine kirusi chenye protini ya aina ile kikiingia, mwili unakuwa na kinga tayari. Ni process ambayo virusi wamekuwa wanatufanyia miaka na miaka, ila sasa inatumika tu kupambana nao.

Na suala la Gwajima kusema kuwa mbona ukichanjwa utahitaji kuvaa barakoa, kupiga sanitizer, utaambukizwa na kuambukiza wengine lipo hivi. Chanjo moja inaweza isiweze kudeal na strains zote za virusi. Mara nyingi inakuwa inadeal na strain iliyopo wakati huo au iliyopo kwa wingi, hivyo basi tahadhari ni muhimu dhidi ya strains zingine. Na kingine ni kuwa chanjo hizi huwa siyo 100% hivyo lazima kujikinga na ule uwezekano mdogo. Hata UKIMWI kuna HIV-1 na HIV-2. Kama ikipatikana Chanjo ya HIV-1 inaweza isizuie HIV-2. Hivyo hata ukichanja utashauriwa kuvaa kondomu, utaweza kuambukizwa na utaweza kuambukiza wengine.

Ni vyema tukachanja, kadri tunavyochelewa tunazidi kujiweka pabaya.
 
Mbona kuna mtu alikuwa kachomwa chanjo tena alichomwa mapema kabisa baada ya rais kutangaza chanjo,

Ana umri wa 58, wiki iliyopita alijisikia homa akawa anapumua kwa shida, akalazwa akawekewa oksjen, baadae akafariki!
Na alikuwa kachomwa chanjo!

Hii imetokea kwa mmoja ninayemjua kabisa alichomwa, je wangapi huko wanakufa na corona wakati chanjo walichoma
Inaweza kuwa ni sababu ya kirusi kubadilika. Unaweza kuta virusi wanaoweza kudhibitiwa na chanjo kwenye mzunguko wapo 80% lakini 20% ni strain mpya. Na kadri watu wengi wasivyochanjwa ndiyo kasi ya kirusi kumutate inavyokuwa kubwa. Hata magonjwa ambayo tunachanjwa utotoni ingetokea kuna watu wamegoma kuchanja, zingeibuka strains ambazo zingeweza kuambukiza na kuua hata wale waliochanjwa.
 
Mbona kuna mtu alikuwa kachomwa chanjo tena alichomwa mapema kabisa baada ya rais kutangaza chanjo,

Ana umri wa 58, wiki iliyopita alijisikia homa akawa anapumua kwa shida, akalazwa akawekewa oksjen, baadae akafariki!
Na alikuwa kachomwa chanjo!

Hii imetokea kwa mmoja ninayemjua kabisa alichomwa, je wangapi huko wanakufa na corona wakati chanjo walichoma
Umeona eenhh???!!!.Mimi sichanji km ni kufa nitakufa kifo kilichoamriwa na Mwenyezi MUNGU.
 
Gwajima haeleweki kabisa. Hoja ya kusema kuwa kirusi kina serial number na ni kama bar code haina ushahidi wowote. Ni amezusha tu madai kuwa chanjo ya korona inatusajili. Ni madai yasiyo na ushahidi, na umeyatoa aliyahusianisha na habari alizosoma juu ya 666, new world order conspiracy za namna hiyo.

Na kusema kwa sababu chanjo ni ya mRna basi itatufanya mazombie au kutubadilisha si sahihi. Kawaida virusi vikiingia kwenye seli huingiza Rna zao, hizo hufanya seli kutengeneza protini za kuzalisha virusi vingine. So kirusi kimoja kikiingia kinaitumia seli ya binadamu kuzalisha protin za kuzalisha virusi vingi hadi vinaua hiyo seli. Na kirusi cha UKIMWI kinafanya hivyo, hatujawahi badilika wala kuwa mazombie. Hata hiyo chanjo ya mRNA imfanya kwa kiasi kaam hivyo. Inenda kusababisha protin fulani ya kirusi(siyo kirusi chote) izalishwe. Protini hiyo ikigunduliwa na kinga ya mwili inafanya mwili utengeneze kinga dhidi yake. Siku nyingine kirusi chenye protini ya aina ile kikiingia mwili unakuwa na kinga tayari. Ni process ambayo virusi wamekuwa wanatufanyia miaka na miaka, ila sasa inatumika tu kupambana nao.

Na suala la Gwajima kusema kuwa mbona ukichanjwa utahitaji kuvaa barakoa, kupiga sanitizer, utaambukizwa na kuambukiza wengine lipo hivi. Chanjo moja inaweza isiweze kudeal na strains zote za virusi. Mara nyingi inakuwa inadeal na strain iliyopo wakati huo au iliyopo kwa wingi, hivyo basi tahadhari ni muhimu dhidi ya strains zingine. Na kingine ni kuwa chanjo hizi huwa siyo 100% hivyo lazima kujikinga na ule uwezekano mdogo. Hata UKIMWI kuna HIV-1 na HIV-2. Kama ikipatikana, Chanjo ya HIV-1 inaweza isizuie HIV-2. Hivyo hata ukichanja utashauriwa kuvaa kondomu, utaweza kuambukizwa na utaweza kuambukiza wengine.

Ni vyema tukachanja, kadri tunavyochelewa tunazidi kujiweka pabaya.
Elimu Yako tafadhari.
 
Mbona kuna mtu alikuwa kachomwa chanjo tena alichomwa mapema kabisa baada ya rais kutangaza chanjo,

Ana umri wa 58, wiki iliyopita alijisikia homa akawa anapumua kwa shida, akalazwa akawekewa oksjen, baadae akafariki!
Na alikuwa kachomwa chanjo!

Hii imetokea kwa mmoja ninayemjua kabisa alichomwa, je wangapi huko wanakufa na corona wakati chanjo walichoma
Na ao hawatangazwi ujue
 
Gwajima haeleweki kabisa. Hoja ya kusema kuwa kirusi kina serial number na ni kama bar code haina ushahidi wowote. Ni amezusha tu madai kuwa chanjo ya korona inatusajili. Ni madai yasiyo na ushahidi, na umeyatoa aliyahusianisha na habari alizosoma juu ya 666, new world order conspiracy za namna hiyo.

Na kusema kwa sababu chanjo ni ya mRna basi itatufanya mazombie au kutubadilisha si sahihi. Kawaida virusi vikiingia kwenye seli huingiza Rna zao, hizo hufanya seli kutengeneza protini za kuzalisha virusi vingine. So kirusi kimoja kikiingia kinaitumia seli ya binadamu kuzalisha protin za kuzalisha virusi vingi hadi vinaua hiyo seli. Na kirusi cha UKIMWI kinafanya hivyo, hatujawahi badilika wala kuwa mazombie. Hata hiyo chanjo ya mRNA imfanya kwa kiasi kaam hivyo. Inenda kusababisha protin fulani ya kirusi(siyo kirusi chote) izalishwe. Protini hiyo ikigunduliwa na kinga ya mwili inafanya mwili utengeneze kinga dhidi yake. Siku nyingine kirusi chenye protini ya aina ile kikiingia mwili unakuwa na kinga tayari. Ni process ambayo virusi wamekuwa wanatufanyia miaka na miaka, ila sasa inatumika tu kupambana nao.

Na suala la Gwajima kusema kuwa mbona ukichanjwa utahitaji kuvaa barakoa, kupiga sanitizer, utaambukizwa na kuambukiza wengine lipo hivi. Chanjo moja inaweza isiweze kudeal na strains zote za virusi. Mara nyingi inakuwa inadeal na strain iliyopo wakati huo au iliyopo kwa wingi, hivyo basi tahadhari ni muhimu dhidi ya strains zingine. Na kingine ni kuwa chanjo hizi huwa siyo 100% hivyo lazima kujikinga na ule uwezekano mdogo. Hata UKIMWI kuna HIV-1 na HIV-2. Kama ikipatikana, Chanjo ya HIV-1 inaweza isizuie HIV-2. Hivyo hata ukichanja utashauriwa kuvaa kondomu, utaweza kuambukizwa na utaweza kuambukiza wengine.

Ni vyema tukachanja, kadri tunavyochelewa tunazidi kujiweka pabaya.
UTAJISKIAJE HYO YA GWAJIMA NA POLE POLE YAKIWA NI YA UKWELI? KWA HIZI HOJA ZKO ZA KU COPY & PAST? nimeuliza tuu..😉
 
Inaweza kuwa ni sababu ya kirusi kubadilika. Unaweza kuta virusi wanaoweza kudhibitiwa na chanjo kwenye mzunguko wapo 80% lakini 20% ni strain mpya. Na kadri watu wengi wasivyochanjwa ndiyo kasi ya kirusi kumutate inavyokuwa kubwa. Hata magonjwa ambayo tunachanjwa utotoni ingetokea kuna watu wamegoma kuchanja, zingeibuka strains ambazo zingeweza kuambukiza na kuua hata wale waliochanjwa.
Yani unaposema virusi kubadilika unazungumzia kitu kama Delta?
 
Mbona kuna mtu alikuwa kachomwa chanjo tena alichomwa mapema kabisa baada ya rais kutangaza chanjo,

Ana umri wa 58, wiki iliyopita alijisikia homa akawa anapumua kwa shida, akalazwa akawekewa oksjen, baadae akafariki!
Na alikuwa kachomwa chanjo!

Hii imetokea kwa mmoja ninayemjua kabisa alichomwa, je wangapi huko wanakufa na corona wakati chanjo walichoma
Hivi mkuu ule uzi wako uliyozungumzia hilo suala bado upo au waliufuta?
 
UTAJISKIAJE HYO YA GWAJIMA NA POLE POLE YAKIWA NI YA UKWELI? KWA HIZI HOJA ZKO ZA KU COPY & PAST? nimeuliza tuu..😉
Inatakiwa kujenga hoja kwa kuchambua taarifa na maarifa yaliyopo. Si kwa kukisia-kisia.

Na hata hivyo nimesema kuwa hata kama kirusi ni cha kutengeneza, njia ya kukidhibiti ni chanjo na kujilinda. Huwezi pinga chanjo kwasababu kirusi ni cha kutengeneza. Ni sawa mtu aweke virusi kwenye kompyuta yako halafu useme, "hizi ni njama, sitengenezi."
 
Inatakiwa kujenga hoja kwa kuchambua taarifa na maarifa yaliyopo. Si kwa kukisia-kisia.

Na hata hivyo nimesema kuwa hata kama kirusi ni cha kutengeneza, njia ya kukidhibiti ni chanjo na kujilinda. Huwezi pinga chanjo kwasababu kirusi ni cha kutengeneza. Ni sawa mtu aweke virusi kwenye kompyuta yako halafu useme, "hizi ni njama, sitengenezi."
ww una hoja gani ya uhakika? sema tu ukweli..🙂
 
Back
Top Bottom