Hoja ya umri inaweza kuwa kikwazo kwa kampeni ya Joe Biden?

Hoja ya umri inaweza kuwa kikwazo kwa kampeni ya Joe Biden?

jastertz

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2020
Posts
407
Reaction score
768
Msemo unasema, muda haumngoji mtu, na kwa Joe Biden mwenye umri wa miaka 80, hilo linaweza kuwa tatizo. Je, rais wa Marekani anaweza kuwashawishi wapiga kura kwamba umri wake si hoja?

Bw Biden alitangaza Jumanne kwamba anataka kuhudumu kwa miaka mingine minne katika Ikulu ya White House. Wamarekani, kulingana na kura ya maoni ya hivi majuzi ya NBC News, hawana uhakika sana.

Utafiti unaonesha kuwa 70% ya Wamarekani - na 51% ya Wanademocrat wanafikiri kwamba hapaswi kugombea tena. Na inabainisha jambo moja kuu kwa takribani nusu ya wale wanaomtaka asimame kando mwaka wa 2024: ni umri wake.

Bwana Biden tayari ndiye rais mzee zaidi katika historia ya Marekani. Iwapo atashinda uchaguzi tena, ataapishwa akiwa na umri wa miaka 82 na kumaliza muhula wake wa pili wa miaka minne akiwa na miaka 86.

Kulingana na jedwali la takwimu za serikali ya Marekani, wastani wa kuishi kwa mzee wa miaka 82 ni miaka 6.77, na uwezekano wa 8% wa kifo ndani ya miezi 12 ijayo.

Je, hili inaweza kuwa kikwazo asichaguliwe muhula ujao?
 
Ana sera za kijinga sana, sidhani umri ni issue, hii miaka aliyoongoza imemuongezea Trump wafuasi.
 
Umri ni Namba tu

Ujana mwisho miaka 85 kama ilivyonenwa enzi za Mussa na Joshua!
 
Unaanza kuzeeka ukiwa na umri gani? Na katiba ya Marekani imeweka ukomo gani wa umri wa mtu kugombea? Ukijibu hayo maswali utakuwa umepunguza ujinga.
angalia statement yangu ya mwisho nimeandika pale kwa upande wa USA
 
angalia statement yangu ya mwisho nimeandika pale kwa upande wa USA

Akili huna, kwa USA :

1. Unaanza kuzeeka na umri gani.
2. Ni kipi kikomo cha kugombea?

Ukijibu hayo maswali, basi tena utakuwa umenielewa.
 
Umri hauwezi kuwa kikwazo kwao Wanarekani.Wampe tu.
 
Paul Biya wa Cameroon ana miaka 90 na hata hiajulikani anastafu lini Urais, Biden hadi akipata kipindi cha pila atamaliza na miaka 86. Akiweza kumaliza kampeni bila kutetereka kiafya urais anashinda.
 
Wamarekani wao Ni watu wa kundika historia kila siku, Safari hii wanataka rais mzee kupita wote waliopita kushika ofisi ya wh.
 
Back
Top Bottom