jastertz
JF-Expert Member
- Jul 4, 2020
- 407
- 768
Msemo unasema, muda haumngoji mtu, na kwa Joe Biden mwenye umri wa miaka 80, hilo linaweza kuwa tatizo. Je, rais wa Marekani anaweza kuwashawishi wapiga kura kwamba umri wake si hoja?
Bw Biden alitangaza Jumanne kwamba anataka kuhudumu kwa miaka mingine minne katika Ikulu ya White House. Wamarekani, kulingana na kura ya maoni ya hivi majuzi ya NBC News, hawana uhakika sana.
Utafiti unaonesha kuwa 70% ya Wamarekani - na 51% ya Wanademocrat wanafikiri kwamba hapaswi kugombea tena. Na inabainisha jambo moja kuu kwa takribani nusu ya wale wanaomtaka asimame kando mwaka wa 2024: ni umri wake.
Bwana Biden tayari ndiye rais mzee zaidi katika historia ya Marekani. Iwapo atashinda uchaguzi tena, ataapishwa akiwa na umri wa miaka 82 na kumaliza muhula wake wa pili wa miaka minne akiwa na miaka 86.
Kulingana na jedwali la takwimu za serikali ya Marekani, wastani wa kuishi kwa mzee wa miaka 82 ni miaka 6.77, na uwezekano wa 8% wa kifo ndani ya miezi 12 ijayo.
Je, hili inaweza kuwa kikwazo asichaguliwe muhula ujao?
Bw Biden alitangaza Jumanne kwamba anataka kuhudumu kwa miaka mingine minne katika Ikulu ya White House. Wamarekani, kulingana na kura ya maoni ya hivi majuzi ya NBC News, hawana uhakika sana.
Utafiti unaonesha kuwa 70% ya Wamarekani - na 51% ya Wanademocrat wanafikiri kwamba hapaswi kugombea tena. Na inabainisha jambo moja kuu kwa takribani nusu ya wale wanaomtaka asimame kando mwaka wa 2024: ni umri wake.
Bwana Biden tayari ndiye rais mzee zaidi katika historia ya Marekani. Iwapo atashinda uchaguzi tena, ataapishwa akiwa na umri wa miaka 82 na kumaliza muhula wake wa pili wa miaka minne akiwa na miaka 86.
Kulingana na jedwali la takwimu za serikali ya Marekani, wastani wa kuishi kwa mzee wa miaka 82 ni miaka 6.77, na uwezekano wa 8% wa kifo ndani ya miezi 12 ijayo.
Je, hili inaweza kuwa kikwazo asichaguliwe muhula ujao?