Hoja za kibunge hujibiwa kibunge, tumwachie Spika Ndugai amalizane na Bunge la EU na sisi wengine tuchape kazi

Yule Balozi aliyewajibu EU jana naye ni mwanachama wa CHADEMA?
 
Kiherehere cha watu wengine kinatia kinyaa!
Maoni ya wabunge saba tu kati ya wabunge 71 wanaounda moja ya kamati za bunge la EU wanayashupalia kana kwamba ndio msimamo wa Kamati nzima, ama wa Bunge zima la EU!!!

Tukumbuke kuwa bunge la Umoja wa Nchi za Ulaya lina jumla ya wabunge 705, na hakuna maazimio yaliyotolewa na kamati ndogo, ama ya bunge dhidi ya Tanzania!

Kinachoendelea ni mihemuko ya watu wasioitakia mema Tanzania, wakisahau kuwa, inapotokea Jumuiya ya Kimataifa kuiwekea vikwazo vya aina yoyote, waathirika wakubwa ni pamoja na wao, baba zao, na mama zao, huku wanawapigania wakiendelea kula kuku kwa mrija huko ughaibuni. Ndio uzuzu huo!
 
Hapa UMEKURUPUKA hoja hizo ni kwa serikali ya Tanzania hazilihusu bunge la Tanzania.
 
Na huyo balozi wenu alikuwa anabwabwaja nini
 
Wewe hiyo kazi unaifanya saa ngapi kila siku umbeya tu humu. Kila mtu anajua anavyofanya kazi sio jukumu lako kuwaambia kwani hakuna anayekula kwako.
 
This is thinly veiled censorship.

Katika nchi ya kidemokrasia, wananchi wana haki za kikatiba kujadili mambo ya nchi yao.

In fact, wabunge wamewekwa kuwakilisha maoni ya wananchi.

Kwa hiyo wananchi wanajadili mambo, wanafikisha maoni yao kwa wabunge, wabunge wanayajadili na kuyatungia sheria pamoja na kuyatolea misimamo.

Sasa, hapo ukiwaambia wananchi wamuachie Spika hoja nzito kuhusu muelekeo wa taifa, umewanyima haki yao ya kikataba.

Umewanyanyapaa.

Umewaziba mdomo.

That is censorship.
 

Yaani bunge letu ndiyo uchaguzi wenyewe halafu unataka eti ndiyo wajibu. 😂
 
Wewe hiyo kazi unaifanya saa ngapi kila siku umbeya tu humu. Kila mtu anajua anavyofanya kazi sio jukumu lako kuwaambia kwani hakuna anayekula kwako.
Wewe huwa unanionaje bwashee kama nawe kila siku hauko Jf?

Chapa kazi bwashee vita vya uchumi havina macho!
 
Tumeshapata maelezo ya kutosha kutoka Kwa ubalozi wetu uliopo Belgium hivyo zile famba za Vijana wa Mbowe tunazitupilia huko!!!
 
Serikali ya Tanzania inasimamiwa na chombo gani?
Haijalishi nani anasimamia serikali ya Tanzania, tuhuma ni kwa serikali ya Tanzania na si bunge, hivyo kama kuna wa kujibu ni serikali ya Tanzania na si vingenevyo.
 
CCM yetu, Mwenyekiti Wetu bila kusahau na Serikali yetu ya CCM katika hili la Pesa za EU hakika tuna Kazi Pevu ya Kuwaelewesha Waliotusaidia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…