Hoja za kuikataa katiba pendekezwa hazina mashiko kabisa

Hoja za kuikataa katiba pendekezwa hazina mashiko kabisa

Joined
Mar 7, 2015
Posts
21
Reaction score
1
HOJA ZA KUIKATAA KATIBA PENDEKEZWA HAZINA MASHIKO, MASLAHI YA WANANCHI YAMEZINGATIWA KWA KINA, SI KWELI KWAMBA INAWALINDA VIONGOZI PAMOJA NA CCM


MAKALA NO. 3

Kwa muda mrefu kumekuwepo hoja nyingi hasa kutoka vyama vya siasa, wanaharakati, wanasiasa, wanasheria pamoja na wachambuzi wa masuala ya kisiasa juu ya uhalali na ubora wa rasimu ya katiba inayopendekezwa na bunge maalum la katiba. Kwa ujumla wake hoja nyingi zinagawanyika katika makundi yafuatayo:-


Kwamba, bunge maalum lilikiuka mamlaka yake kisheria na kufanya kinyume cha matakwa ya sheria ya mabadiliko ya katiba (sura ya 83 toleo la mwaka 2014).


Kwamba, maoni ya wananchi katika rasimu ya pili ya katiba yaliachwa na hayakuzingatiwa( hapa hoja nyingi zinajikita katika suala la muundo wa muungano kutokana na takwimu za tume kuhusu maoni ya watu binafsi, vyama vya siasa, taasisi binafsi na za serikali kuhusu muundo wa muungano.


Kwamba, mchakato mzima wa kupatikana katiba pendekezwa ulikuwa na mapungufu mengi Kwamba, katiba inayopendekezwa imejali maslahi ya CCM pamoja na viongozi na siyo maslahi ya wananchi kama rasimu ya pili ilivyokwa imesheheni.


Maoni ya namna hii yamekuwa yakitolewa na watu wengi akiwemo aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya katiba Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba pamoja na baadhi ya waliokuwa wajumbe wa Tume hiyo na hivyo kuwashawishi watu wasiikubali rasimu ya katiba inayopendekezwa.


Hoja ya kwanza inakosa mashiko kabisa kisheria na kiuhalisia. Hoja hizi hazikuzingatia historia pamoja na dhana halisi ya kisheria kuhusu bunge maalum la katiba ( Consituent Assembly) ambayo ni kwamba bunge maalum ni mwakilishi wa mamlaka ( sovereignty) ya watu. Kujitungia katiba yao nikwa nikwa mujibu wa mamlaka ( sovereignty) ya watu. Ifahamike kwamba rasimu yenyewe ya katiba inaweza kuandikwa na kamati iliyoteuliwa na bunge lenyewe ( rejea mchakato wa kuandika katiba ya India ya 1950) au rasimu inaweza kuandaliwa na kuandikwa na Tume ( rejea mchakato wa kuandika katiba ya Uganda 1995). Mifumo yote hii haibadili wala kuondoa dhana au mamlaka ya bunge maalum kama chombo cha wananchi kama ilivo katika vifungu vya 25 (1) na 28(1) vya sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya 83 toleo la mwaka 2014 ingawa kisiasa bunge maaalum lililochaguliwa na wananchi moja kwa moja linakuwa na nguvu zaidi kutokana na uwiano wa matabaka na makundi katika jamii.


Kisheria dhana ya bunge maalum haiathiriwi wala kubadilika kwa kuangalia nani niwajumbe wa bunge maalum ilimradi wawe wamepatikana kwa njia halali iliyoainishwa na sheria husika kama ilivyo kwetu hapa Tanzania ni sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya 83 toleo la mwaka 2014 katika kifungu cha 22(1) (a)-(c) na (i)-(x). pia angalia David Mukholi (1995) Uganda’s Fourth Constitution: History, Politics and Law, kampala: Fountaion Publishers, uk.49), Mahendra p. Singh, V.N. Shukla’s Constitution of India 9[SUP]th[/SUP] Edn. Lucknow: Easten Book, uk.A-24-A-25.


Kwabahati mbaya sana pia wapo wanasheria wenye mlengo kama huu yakwamba bunge maalum halikuwa na mamlaka ya kurekebisha rasimu yapili ya katiba, bila yashaka nikwa sababu ya mapenzi ya vyama vyao pamoja na ushabiki wa kisiasa pasipokujali misingi ya taaluma yao ikiwemo kuwa waadilifu na kusema ukweli. Wamekuwa wakitoa tafsiri potofu juu ya mamlaka ya bunge maalum la katiba kwamba halikuwa na mamlaka yakile bunge maalum lilichofanya kurekebisha na kuboresha misingi ya rasimu ya pili iliyopendekezwa. Natumia furusa hii kuwaelimisha kwamba kifungu cha 25(1) kinasomwa pamoja na kifungu cha 28(1) ndipo mantiki sahihi ya mamlaka ya bunge maalum la katiba yanapatikana.

Kwa kwamujibu wa kifungu cha 28(1) bunge maalum lilikuwa na kazi ya kutunga katiba inayopendekezwa wala siyo kupitisha rasimu ya Tume kama inavyoelezwa na baadhi ya watu. Bila shaka bunge maalum lilikuwa namamlaka ya kutunga rasimu ya katiba inayopendekezwa bila kufungwa na rasimu yapili ya Tume.


Baadhi ya tafsiri potofu zinazotolewa zinaonesha kama vile Tume ndiyo ilikuwa na mamlaka ya kutunga katiba inayopendekezwa ambapo siyo kweli. Tume haikuwa na wawakilishi wa wananchi, ilikuwa na watu wenye weledi wa kukusanya maslahi tofauti ya wananchi ili yawasilishwe kwenye bunge maalum. Bunge maalum ndicho chombo kilichokuwa kimesheheni wawakilishi wa wananchi na ndiyo maana bunge maalum likapewa mamlaka ya kutunga katiba inayowafaa wananchi nasiyo kubariki yaliyoletwa na Tume.


Kuhusu hoja yakwamba maoni ya wananchi yameachwa siyo ya kweli kabisa ni uzushi tu wakisiasa kwa kuzingatia maelezo pamoja na tafsiri niliyotoa hapo juu kuhusu mamlaka pamoja na ukomo wa mamlaka ya bunge maalum la katiba. Hoja yakwamba wananchi waliowengi walipendekeza muundo wa serikali tatu siyo sahihi na haithibitiki kwa mujibu wa takwimu zilizowasilishwa na Tume yenyewe kwa ushahidi ufuatao: ukiangalia kwa makini takwimu zilizotolewa na Tume yenyewe ( angalia jedwali 3,uk.9) kwamba, waliotoa maoni mbele ya tume ni watu 351,664 kati ya hao, 47,820 tu (asilimia 14) ndio waligusia muundo wa muungano. Asilimia 86 hawakuzungumzia muundo wa muungano kwa maana yoyote iwe ya serikali moja, mbili, tatu au muungano wa mkataba. Wao walikuwa na mambo tofauti kabisa kuhusu maisha yao. Isitoshe, kati ya waiogusia muundo wa muungano, asilimia 30 walitaka serikali mbili, asilimia 37 walipendekeza serikali tatu, na asilimia 25 walitaka muungano wa mkataba, asilimia nane walitaka serikali moja.


Kwahiyo waliopendekeza serikali tatu ni theluthi moja tu ya waliogusia muundo wa muungano na ni asilimia 5 tu walitoa maoni, waliotaka serikali mbili na muungano wa mkataba ni asilimia 55, yaani zaidi ya nusu ya waliotoa maoni juu ya muundo wa muungano. Hata ukichanganya waliotaka serikali moja na serikali mbili ni asilimia 38, inazidi kidogo wale waliotaka serikali tatu. Kwa takwimu hizi za Tume usahihi wa kwamba wananchi waliowengi walitaka muundo wa serikali tatu uko wapi? Hoja hii haina mashiko wala ushahidi wa maana, na kuendelea kwa waliokuwa watumishi wa Tume kwamba serikali tatu ndizo zilitakiwa na wananchi wengi itakuwa nikutwambia kwamba wao wenyewe ndiyo wanataka muundo wa serikali tatu ila wasitumie mgongo wa Tume maana kwenye takwimu za Tume mahitaji ya serikali tatu kwa wananchi waliowengi hayathibitiki kabisa.

Pia nivema ifahamike kwamba haikuwa makusudio ya sheria ya mabadiliko ya katiba wala siyo dhana ya bunge maalum la katiba kwamba kila hoja iliyowasilishwa na Tume ilikuwa lazima kupitishwa na bunge maalum na kama bunge lingefanya hivyo lingekuwa limepoteza maudhui yake na ikumbukwe kwamba Tume iliyasahau mengi muhimu ya wananchi na ndiyo umaalum wa bunge la katiba unapatikana kwa kurekebisha, kuboresha, kupitisha na kutunga katiba inayowafaa wananchi kulingana na mahitaji pamoja na mazingira ya nchi.


Nafasi ya bunge maalum niyakipekee kabisa katika mchakato wa kutunga katiba mpya. Nafasi yake ni nzito kuliko ile ya Tume na muhimu kuliko kura ya maoni nikwa sababu bunge maalum ndiyo chombo cha kufanya maamuzi mazito, siyo Tume.Ningelishangaa sana kama bunge maalum lingebariki baadhi ya misingi iliyokuwa imewekwa na Tume kwenye rasimu ambayo ingepitishwa na bunge maalum na kisha kupitishwa na wananchi ingeleta balaa na maangamizi kwa Watanzania hasa ule muundo wa serikali tatu. Bunge lilikuwa na kazi ya kuhakikisha kwamba inapitisha mambo ambayo hayawezi kuzaa vurugu, kuvunja utulivu, amani pamoja na mshikamano na umoja wananchi,( National and territorial integrity).


Kuhusu hoja ya kwamba mchakato wa kupatikana katiba pendekezwa hauna uhalali na kwamba katiba pendekezwa siyo halai, naomba kuwauliza wanaotoa kauli hii kwamba nikipi si halali kati ya haya yaliyopelekea kupatikana kwa katiba pendekezwa, Ni sheria ya mabadiliko ya katiba? Ni wajumbe wa Tume ya mabadiliko ya Katiba? Ni Tume yenyewe? Ni rasimu ya Tume? Ni bunge maalum? Ni kanuni za bunge maalum? Au ni rasimu ya katiba pendekezwa. Iwapo maswali haya yatajibiwa kwa kuzingatia hoja na uchambuzi niliofanya pamoja na uhalisia wa matakwa ya kisheria na siyo ya maslahi ya vyama vya siasa au kundi Fulani la watu itakuwa wazi kwamba rasimu ya katiba inayopendekezwa unao uhalali wote wa kupigiwa kura na wananchi kwa kadri watakavoona wao.


Hoja nyingine inayotolewa sana ambayo kwa upande wangu ninasema nidhaifu na haina mashiko ni ile yakwamba katiba pendekezwa imejali zaidi maslahi ya CCM pamoja na viongozi na siyo maslahi ya wananchi. Wanaosema hivi hawajaisoma na kuilewa katiba inayopendekezwa na badala yake wanaongozwa ima na hisia tu au ni wale ving’ang’anizi wa rasimu ya pili au niwale wenye tamaa ya kuiona Tanzania inavurugika ili watimize ndoto zao za kuwa viongozi wakati watanzania wakipata shida. Katika sura ya pili sehemu kwanza ya katiba inayopendekezwa Ibara ya 11(1) inabainisha wazi kwamba lengo la katiba hii ni kulinda, kuimarisha na kudumisha, haki, usawa, udugu, amani, umoja na utangamano wa wananchi wa jamhuri ya muungano kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga Taifa huru lenye democrasia, utawala bora, maendeleo endelevu na kujitegemea na ibara ndogo ya 3 imetaja malengo makuu ya katiba hii kitaifa ambayo yamezingatia mahitaji muhimu ya watanzania wote. Imetajwa kwamba lengo kuu la katiba hii kitaifa ni kuboresha maisha ya watanzania katika Nyanja zote za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kimazingira. Seheme ya pili, Ibara ya 12(1) imetaja wazi kwamba katiba hii inalengo la kisiasa na nilengo la kitaifa na kwamba serikali itahakikisha inadumisha democrasia, na kuondoa ubaguzi wa aina zote pia katika ibara ndogo ya 2(a), (b) na (c) katiba pendekezwa imeweka wazi kwamba litakuwa nijukumu la serikali kuchukua hatua ambazo zimeainishwa ndani ya ibara hii kuhakikisha lengo la katiba hii kisiasa linafanikiwa kwa watanzania pia bunge limetakiwa kutunga sheria zitakazowezesha lengo hili muhimu linafikiwa.


Katika sehemu ya tatu ya katiba pendekezwa inataja malengo ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kuwa malengo ya kitaifa ambapo katika ibara ya 13(1) lengo la Taifa kiuchumi imetajwa kuwa serikali itahakikisha Taifa linajenga uchumi wa kisasa utakaowawezesha wananchi na Taifa kujitegemea kwa kuzingatia matumizi ya elimu ya sayansi na technolojia katika Nyanja zote za uzalishaji mali kwa kuhimiza mapinduzi ya kilimo, ufugaji na uvuvi, mapinduzi ya viwanda na kujenga sekta muhimu ya nishati na mwasiliano na miundo mbinu ambapo katika ibara ndogo ya 2(a)-(g) katiba inatoa jukumu kwa serikali kuhakikisha inachukua hatua stahiki ambazo pia pia zimetajwa kuhakikisha lengo la Taifa kiuchumi linakamilika pia bunge limetakiwa kutunga sheria zitakazowezesha lengo hili muhimu linafikiwa.


Ibara ya 14(1) imeweka lengo la Taifa kijamii kwamba serikali itahakikisha inajenga jamii yenye ustawi na uwezo wa kushiriki katika shughuli za kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ambapo ibara ndogo ya 2(a)-(f) Serikali ina jukumu la kuchukua hatua stahiki ili kufikia lengo hili na pia bunge litatunga sheria kuhakikisha lengo hili muhimu linafikiwa.


Ibara ya 15(1) imetaja lengo la Taifa kiutamaduni kwamba nikukuza, kudumisha, na kuhifadhi utamaduni wa Taifa pia wa wananchi ambapo katika ibara ndogo ya 2(a)-(e) serikali imetakiwa kuchukua hatua stahiki ili kuhakikisha lengo hili muhimu la kitaifa linafikiwa.


Hivi kweli malengo makuu na muhimu ya katiba hii kitaifa yaliyotajwa katika ibara za 11,12,13,14 na 15 nikwa ajili ya CCM na viongozi? Au jamii inamahitaji mengine nje ya haya yaliyotajwa katika katiba hii pendekezwa? Kuna kosa gani iwapo hawa wanaosema katiba hii pendekezwa ni mbaya, haikujali maslahi ya wananchi na inalinda CCM na viongozi wa nchi nikiwaita wazushi? Katiba pendekezwa ni nzuri sana. MWANASHERIA.
MWESIGWA ZAIDI SIRAJI.
0784 646220
 
Balaza la wakristo hawataki katiba iliyoandikwa na wezi wa Escrow CCM na kuacha mawazo ya Watanzania walio wengi.jiulize ccm imeandika katiba kutetea wezi chenge ni mmoja wapo na hadi sasa ccm inawalinda waizi walioandika katiba kuwalinda.


swissme
 
Katiba pendekezwa kama katiba zingine za nchi zingine, haiwezi kuridhisha kila mtu, ila kama kulikuwapo na mbadala mzuri zaidi ya katiba pendekezwa, kwa nini tusichukue huo mbadala?? Naongelea rasimu ya Warioba, ilikuwa nzuri zaidi ya hii katiba pendekezwa na inakubalika kwa wananchi wengi zaidi ya hii pendekezwa.
Ijumaa niliangalia kipindi fulani tbc kuhusu katiba pendekezwa na wanawake. Waliletwa "wasomi" wanawake ktk jopo la watu wanaojadili kuhusu katiba pendekezwa itakavyosaidia wanawake, nilistaajabika kuona hao "wasomi" wakiorodhesha tu mambo ya katiba pendekezwa bila hata kuelezea itamsaidia vipi mwanamke na itatekelezwa kivipi.
Inasikitisha, ila ni wasomi wanawake ambao wamelishwa maneno na walikuja tetea maslahi yao.
Point yangu hapa ni kwamba, katiba pendekezwa haijauzwa na kama anatokea mtu anayejaribu kuiuza, haina mashiko kabisa!
Ukiilingakisha katiba pendekezwa na rasimu ya Warioba, hapo ndio utakapotambua kuwa katiba pendekezwa haina mashiko.
Binafsi sijaipata bado katiba pendekezwa, ila nimeona baadhi ya vipendere vyake vichache na kuvilinganisha na vipengere shindani vyake katika rasimu ya Warioba, katiba pendekezwa inabaki haina mashiko!
 
Unasemaje kuhusu "usafi" wa katiba pendekezwa iliyoandikwa na baadhi ya watu ambao sisiemu wenyewe wamekubali kuwa maadili yao ktk chama ni utata?? Je tuipitishe tu, sio ishu kubwa hii??
Tafadhari, ebu toa maoni yako hapa!
Pia nafikiri kama mdau mmoja alivyosema hapo juu, ishu kubwa ya katiba pendekezwa sio kilichomo bali kilichotolewa ukilinganisha na rasimu ya Warioba ambayo ndo ilitokana na mapendekezo ya wananchi.
 
Nikweli wapo ambao hawana maadili ambalo ni jambo binafsi siyo la Chama. katiba haikuandikwa na chama, iliandikwa na kamati ya bunge maalum la katiba. Hata kilichotolewa pia kuna kilichoingizwa ambacho Tume haikuwa imekiweka. pia siyo lazima kila kilichomo kwenye rasimu ilikuwa lazima bunge maalum kukikubali. Tume ilileta mapendekezo na siyo katiba.
 
Wewe mleta mada mimi nakwita wewe ni mzushi na muongo na pia unaidhalilisha fani yako.

Vipi utaitetea rasimu ambayo imepitishwa kinguvu nguvu bila ya kupata ridhaa ya Wazanzibari kwa kukosa theluthi tatu za Zanzibar, na nina hakika 100% ya kuwa hilo unalijua

Wakili mzima badala ya kutetea ukweli wewe unatetea unafiki wa Sitta kwa hiyo na wewe unakuwa mnafiki na mzushi kuliko huyo Sitta.
 
Mimi leo jumapili naogopa kumtukana huyu mbwa aliyeleta hii mada kwa maana hajitambui kbsa
 
Nikweli wapo ambao hawana maadili ambalo ni jambo binafsi siyo la Chama. katiba haikuandikwa na chama, iliandikwa na kamati ya bunge maalum la katiba. Hata kilichotolewa pia kuna kilichoingizwa ambacho Tume haikuwa imekiweka. pia siyo lazima kila kilichomo kwenye rasimu ilikuwa lazima bunge maalum kukikubali. Tume ilileta mapendekezo na siyo katiba.
Mwesigwa acha uwongo kwa kusema kuwa suala la maadili siyo la chama. Mbona CCM ilikataa maadili yaliyowekwa na Tume kwenye rasimu badala yake wakaandika vitu vya ajabu ajabu, yaaaniii ukiipa kura ya ndiyo hiyo katiba pendekezwa utakuwa among the stupid people ever lived in Tanzania. Mimi siwezi kuipa kura ya ndiyo katiba inayoruhusu uchumi wa nchi kuhamishwa.

hata huyo jamaa aliyeposti hii mada anadhalilisha fani yake. kwa kuunga mkono katiba ya hovyo hovyo
 
Wewe huna malezi kabisa. possibly umezaliwa na kukulia mtaani. Lete hoja na siyo matusi.
 
Huo ndio ukweli, Tatizo watu hamsomi mnasikia tu kinachosemwa. ukweli upo kwenye maandishi. Fuatilia utajua
 
HOJA ZA KUIKATAA KATIBA PENDEKEZWA HAZINA MASHIKO, MASLAHI YA WANANCHI YAMEZINGATIWA KWA KINA, SI KWELI KWAMBA INAWALINDA VIONGOZI PAMOJA NA CCM


MAKALA NO. 3

Kwa muda mrefu kumekuwepo hoja nyingi hasa kutoka vyama vya siasa, wanaharakati, wanasiasa, wanasheria pamoja na wachambuzi wa masuala ya kisiasa juu ya uhalali na ubora wa rasimu ya katiba inayopendekezwa na bunge maalum la katiba. Kwa ujumla wake hoja nyingi zinagawanyika katika makundi yafuatayo:-


Kwamba, bunge maalum lilikiuka mamlaka yake kisheria na kufanya kinyume cha matakwa ya sheria ya mabadiliko ya katiba (sura ya 83 toleo la mwaka 2014).


Kwamba, maoni ya wananchi katika rasimu ya pili ya katiba yaliachwa na hayakuzingatiwa( hapa hoja nyingi zinajikita katika suala la muundo wa muungano kutokana na takwimu za tume kuhusu maoni ya watu binafsi, vyama vya siasa, taasisi binafsi na za serikali kuhusu muundo wa muungano.


Kwamba, mchakato mzima wa kupatikana katiba pendekezwa ulikuwa na mapungufu mengi Kwamba, katiba inayopendekezwa imejali maslahi ya CCM pamoja na viongozi na siyo maslahi ya wananchi kama rasimu ya pili ilivyokwa imesheheni.


Maoni ya namna hii yamekuwa yakitolewa na watu wengi akiwemo aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya katiba Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba pamoja na baadhi ya waliokuwa wajumbe wa Tume hiyo na hivyo kuwashawishi watu wasiikubali rasimu ya katiba inayopendekezwa.


Hoja ya kwanza inakosa mashiko kabisa kisheria na kiuhalisia. Hoja hizi hazikuzingatia historia pamoja na dhana halisi ya kisheria kuhusu bunge maalum la katiba ( Consituent Assembly) ambayo ni kwamba bunge maalum ni mwakilishi wa mamlaka ( sovereignty) ya watu. Kujitungia katiba yao nikwa nikwa mujibu wa mamlaka ( sovereignty) ya watu. Ifahamike kwamba rasimu yenyewe ya katiba inaweza kuandikwa na kamati iliyoteuliwa na bunge lenyewe ( rejea mchakato wa kuandika katiba ya India ya 1950) au rasimu inaweza kuandaliwa na kuandikwa na Tume ( rejea mchakato wa kuandika katiba ya Uganda 1995). Mifumo yote hii haibadili wala kuondoa dhana au mamlaka ya bunge maalum kama chombo cha wananchi kama ilivo katika vifungu vya 25 (1) na 28(1) vya sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya 83 toleo la mwaka 2014 ingawa kisiasa bunge maaalum lililochaguliwa na wananchi moja kwa moja linakuwa na nguvu zaidi kutokana na uwiano wa matabaka na makundi katika jamii.


Kisheria dhana ya bunge maalum haiathiriwi wala kubadilika kwa kuangalia nani niwajumbe wa bunge maalum ilimradi wawe wamepatikana kwa njia halali iliyoainishwa na sheria husika kama ilivyo kwetu hapa Tanzania ni sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya 83 toleo la mwaka 2014 katika kifungu cha 22(1) (a)-(c) na (i)-(x). pia angalia David Mukholi (1995) Uganda's Fourth Constitution: History, Politics and Law, kampala: Fountaion Publishers, uk.49), Mahendra p. Singh, V.N. Shukla's Constitution of India 9[SUP]th[/SUP] Edn. Lucknow: Easten Book, uk.A-24-A-25.


Kwabahati mbaya sana pia wapo wanasheria wenye mlengo kama huu yakwamba bunge maalum halikuwa na mamlaka ya kurekebisha rasimu yapili ya katiba, bila yashaka nikwa sababu ya mapenzi ya vyama vyao pamoja na ushabiki wa kisiasa pasipokujali misingi ya taaluma yao ikiwemo kuwa waadilifu na kusema ukweli. Wamekuwa wakitoa tafsiri potofu juu ya mamlaka ya bunge maalum la katiba kwamba halikuwa na mamlaka yakile bunge maalum lilichofanya kurekebisha na kuboresha misingi ya rasimu ya pili iliyopendekezwa. Natumia furusa hii kuwaelimisha kwamba kifungu cha 25(1) kinasomwa pamoja na kifungu cha 28(1) ndipo mantiki sahihi ya mamlaka ya bunge maalum la katiba yanapatikana.

Kwa kwamujibu wa kifungu cha 28(1) bunge maalum lilikuwa na kazi ya kutunga katiba inayopendekezwa wala siyo kupitisha rasimu ya Tume kama inavyoelezwa na baadhi ya watu. Bila shaka bunge maalum lilikuwa namamlaka ya kutunga rasimu ya katiba inayopendekezwa bila kufungwa na rasimu yapili ya Tume.


Baadhi ya tafsiri potofu zinazotolewa zinaonesha kama vile Tume ndiyo ilikuwa na mamlaka ya kutunga katiba inayopendekezwa ambapo siyo kweli. Tume haikuwa na wawakilishi wa wananchi, ilikuwa na watu wenye weledi wa kukusanya maslahi tofauti ya wananchi ili yawasilishwe kwenye bunge maalum. Bunge maalum ndicho chombo kilichokuwa kimesheheni wawakilishi wa wananchi na ndiyo maana bunge maalum likapewa mamlaka ya kutunga katiba inayowafaa wananchi nasiyo kubariki yaliyoletwa na Tume.


Kuhusu hoja yakwamba maoni ya wananchi yameachwa siyo ya kweli kabisa ni uzushi tu wakisiasa kwa kuzingatia maelezo pamoja na tafsiri niliyotoa hapo juu kuhusu mamlaka pamoja na ukomo wa mamlaka ya bunge maalum la katiba. Hoja yakwamba wananchi waliowengi walipendekeza muundo wa serikali tatu siyo sahihi na haithibitiki kwa mujibu wa takwimu zilizowasilishwa na Tume yenyewe kwa ushahidi ufuatao: ukiangalia kwa makini takwimu zilizotolewa na Tume yenyewe ( angalia jedwali 3,uk.9) kwamba, waliotoa maoni mbele ya tume ni watu 351,664 kati ya hao, 47,820 tu (asilimia 14) ndio waligusia muundo wa muungano. Asilimia 86 hawakuzungumzia muundo wa muungano kwa maana yoyote iwe ya serikali moja, mbili, tatu au muungano wa mkataba. Wao walikuwa na mambo tofauti kabisa kuhusu maisha yao. Isitoshe, kati ya waiogusia muundo wa muungano, asilimia 30 walitaka serikali mbili, asilimia 37 walipendekeza serikali tatu, na asilimia 25 walitaka muungano wa mkataba, asilimia nane walitaka serikali moja.


Kwahiyo waliopendekeza serikali tatu ni theluthi moja tu ya waliogusia muundo wa muungano na ni asilimia 5 tu walitoa maoni, waliotaka serikali mbili na muungano wa mkataba ni asilimia 55, yaani zaidi ya nusu ya waliotoa maoni juu ya muundo wa muungano. Hata ukichanganya waliotaka serikali moja na serikali mbili ni asilimia 38, inazidi kidogo wale waliotaka serikali tatu. Kwa takwimu hizi za Tume usahihi wa kwamba wananchi waliowengi walitaka muundo wa serikali tatu uko wapi? Hoja hii haina mashiko wala ushahidi wa maana, na kuendelea kwa waliokuwa watumishi wa Tume kwamba serikali tatu ndizo zilitakiwa na wananchi wengi itakuwa nikutwambia kwamba wao wenyewe ndiyo wanataka muundo wa serikali tatu ila wasitumie mgongo wa Tume maana kwenye takwimu za Tume mahitaji ya serikali tatu kwa wananchi waliowengi hayathibitiki kabisa.

Pia nivema ifahamike kwamba haikuwa makusudio ya sheria ya mabadiliko ya katiba wala siyo dhana ya bunge maalum la katiba kwamba kila hoja iliyowasilishwa na Tume ilikuwa lazima kupitishwa na bunge maalum na kama bunge lingefanya hivyo lingekuwa limepoteza maudhui yake na ikumbukwe kwamba Tume iliyasahau mengi muhimu ya wananchi na ndiyo umaalum wa bunge la katiba unapatikana kwa kurekebisha, kuboresha, kupitisha na kutunga katiba inayowafaa wananchi kulingana na mahitaji pamoja na mazingira ya nchi.


Nafasi ya bunge maalum niyakipekee kabisa katika mchakato wa kutunga katiba mpya. Nafasi yake ni nzito kuliko ile ya Tume na muhimu kuliko kura ya maoni nikwa sababu bunge maalum ndiyo chombo cha kufanya maamuzi mazito, siyo Tume.Ningelishangaa sana kama bunge maalum lingebariki baadhi ya misingi iliyokuwa imewekwa na Tume kwenye rasimu ambayo ingepitishwa na bunge maalum na kisha kupitishwa na wananchi ingeleta balaa na maangamizi kwa Watanzania hasa ule muundo wa serikali tatu. Bunge lilikuwa na kazi ya kuhakikisha kwamba inapitisha mambo ambayo hayawezi kuzaa vurugu, kuvunja utulivu, amani pamoja na mshikamano na umoja wananchi,( National and territorial integrity).


Kuhusu hoja ya kwamba mchakato wa kupatikana katiba pendekezwa hauna uhalali na kwamba katiba pendekezwa siyo halai, naomba kuwauliza wanaotoa kauli hii kwamba nikipi si halali kati ya haya yaliyopelekea kupatikana kwa katiba pendekezwa, Ni sheria ya mabadiliko ya katiba? Ni wajumbe wa Tume ya mabadiliko ya Katiba? Ni Tume yenyewe? Ni rasimu ya Tume? Ni bunge maalum? Ni kanuni za bunge maalum? Au ni rasimu ya katiba pendekezwa. Iwapo maswali haya yatajibiwa kwa kuzingatia hoja na uchambuzi niliofanya pamoja na uhalisia wa matakwa ya kisheria na siyo ya maslahi ya vyama vya siasa au kundi Fulani la watu itakuwa wazi kwamba rasimu ya katiba inayopendekezwa unao uhalali wote wa kupigiwa kura na wananchi kwa kadri watakavoona wao.


Hoja nyingine inayotolewa sana ambayo kwa upande wangu ninasema nidhaifu na haina mashiko ni ile yakwamba katiba pendekezwa imejali zaidi maslahi ya CCM pamoja na viongozi na siyo maslahi ya wananchi. Wanaosema hivi hawajaisoma na kuilewa katiba inayopendekezwa na badala yake wanaongozwa ima na hisia tu au ni wale ving'ang'anizi wa rasimu ya pili au niwale wenye tamaa ya kuiona Tanzania inavurugika ili watimize ndoto zao za kuwa viongozi wakati watanzania wakipata shida. Katika sura ya pili sehemu kwanza ya katiba inayopendekezwa Ibara ya 11(1) inabainisha wazi kwamba lengo la katiba hii ni kulinda, kuimarisha na kudumisha, haki, usawa, udugu, amani, umoja na utangamano wa wananchi wa jamhuri ya muungano kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga Taifa huru lenye democrasia, utawala bora, maendeleo endelevu na kujitegemea na ibara ndogo ya 3 imetaja malengo makuu ya katiba hii kitaifa ambayo yamezingatia mahitaji muhimu ya watanzania wote. Imetajwa kwamba lengo kuu la katiba hii kitaifa ni kuboresha maisha ya watanzania katika Nyanja zote za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kimazingira. Seheme ya pili, Ibara ya 12(1) imetaja wazi kwamba katiba hii inalengo la kisiasa na nilengo la kitaifa na kwamba serikali itahakikisha inadumisha democrasia, na kuondoa ubaguzi wa aina zote pia katika ibara ndogo ya 2(a), (b) na (c) katiba pendekezwa imeweka wazi kwamba litakuwa nijukumu la serikali kuchukua hatua ambazo zimeainishwa ndani ya ibara hii kuhakikisha lengo la katiba hii kisiasa linafanikiwa kwa watanzania pia bunge limetakiwa kutunga sheria zitakazowezesha lengo hili muhimu linafikiwa.


Katika sehemu ya tatu ya katiba pendekezwa inataja malengo ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kuwa malengo ya kitaifa ambapo katika ibara ya 13(1) lengo la Taifa kiuchumi imetajwa kuwa serikali itahakikisha Taifa linajenga uchumi wa kisasa utakaowawezesha wananchi na Taifa kujitegemea kwa kuzingatia matumizi ya elimu ya sayansi na technolojia katika Nyanja zote za uzalishaji mali kwa kuhimiza mapinduzi ya kilimo, ufugaji na uvuvi, mapinduzi ya viwanda na kujenga sekta muhimu ya nishati na mwasiliano na miundo mbinu ambapo katika ibara ndogo ya 2(a)-(g) katiba inatoa jukumu kwa serikali kuhakikisha inachukua hatua stahiki ambazo pia pia zimetajwa kuhakikisha lengo la Taifa kiuchumi linakamilika pia bunge limetakiwa kutunga sheria zitakazowezesha lengo hili muhimu linafikiwa.


Ibara ya 14(1) imeweka lengo la Taifa kijamii kwamba serikali itahakikisha inajenga jamii yenye ustawi na uwezo wa kushiriki katika shughuli za kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ambapo ibara ndogo ya 2(a)-(f) Serikali ina jukumu la kuchukua hatua stahiki ili kufikia lengo hili na pia bunge litatunga sheria kuhakikisha lengo hili muhimu linafikiwa.


Ibara ya 15(1) imetaja lengo la Taifa kiutamaduni kwamba nikukuza, kudumisha, na kuhifadhi utamaduni wa Taifa pia wa wananchi ambapo katika ibara ndogo ya 2(a)-(e) serikali imetakiwa kuchukua hatua stahiki ili kuhakikisha lengo hili muhimu la kitaifa linafikiwa.


Hivi kweli malengo makuu na muhimu ya katiba hii kitaifa yaliyotajwa katika ibara za 11,12,13,14 na 15 nikwa ajili ya CCM na viongozi? Au jamii inamahitaji mengine nje ya haya yaliyotajwa katika katiba hii pendekezwa? Kuna kosa gani iwapo hawa wanaosema katiba hii pendekezwa ni mbaya, haikujali maslahi ya wananchi na inalinda CCM na viongozi wa nchi nikiwaita wazushi? Katiba pendekezwa ni nzuri sana. MWANASHERIA.
MWESIGWA ZAIDI SIRAJI.
0784 646220

Mwesigwa, angalia analysis yako isisje ika-jeopodise kazi yako. One might question your analysis capacity to handle complicated cases brought before you! Bagambila balinsi bali Igulu kuhulila.
 
BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA
BARUA YA KICHUNGAJI
“Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi
zenu” (Lk. 21: 19)
Sisi Maaskofu wenu tulikutana kusali na
kutafakari pamoja huko Arusha tarehe 16 – 17
Februari 2015. Moja ya mambo tuliyoyazingatia
ni suala lililo mbele yetu, la kupigia Kura ya
Maoni Katiba Inayopendekezwa.
Tunazidi kuendelea kukumbusha kwamba
Katiba ni chombo kitakatifu, kinacholenga
kufikia maridhiano kama taifa juu ya namna
tunavyotaka kuishi pamoja kwa amani na
utulivu.
Tunapotafakari kipindi chote cha mchakato wa
kuunda Katiba, tunaona mazuri mengi
yamefanyika. Lakini yapo mambo mengine
ambayo yamefanyika na yametugusa na
kutufanya tuhofie namna mambo yanavyoweza
kujengeka na kuleta madhara katika nchi yetu.
Hali hiyo inatulazimu kujiuliza kwa tafakari: Je,
tutaweza kuendelea kudumisha amani na
utulivu?
1. Mashaka yetu
Hadi sasa Katiba Inayopendekezwa haijawafikia
watu wengi.
Hatua muhimu mno ambayo ni kuelimisha watu
juu ya Katiba Inayopendekezwa haijafanyika,
kwahiyo wananchi wengi hawana ufahamu wa
kutosha juu ya maudhui na misingi yake.
Zoezi la uandikishaji wa wapiga kura katika
daftari la kudumu la wapigakura halijafikia
hatua yenye mwelekeo wa kulikamilisha. Hii
inatupa mashakama kubwa sana na hatuwezi
kuamini kuwa zoezi hilo litakamilika kabla ya
tarehe ya kupiga kura ya maoni.
Katika hali hii tunabaki na mahangaiko na
mashaka makubwa ya kutakiwa kupigia Kura
Katiba Inayopendekezwa ambayo hawaielewi
kikamilifu wala kujua matokeo yake kwa
mustakabali wa Taifa letu. Tunajiuliza, katika
mazingira kama haya amani haitatetereka?
Bahati mbaya sana wanasiasa viongozi wa nchi
wanaendelea kutoa maelezo ya kisiasa
yanayotoa majibu mepesi kwa maswali
magumu, kwa lengo la kufanikisha malengo yao
binafsi ya kisiasa. Huu siyo muda wa kufanya
hivyo!
Pamoja na mahangaiko na mashaka juu ya
suala la Katiba, bado yapo mambo mengi
mazito yanayoleta fadhaa kwa jamii yetu:
-Mfululizo wa matukio ya mauaji na/au
kunyofolewa viungo ndugu zetu wenye ulemavu
wa ngozi (Maalbino).
-Kuibuka kwa makundi ya wezi na vibaka
wakijigamba na kujipachika majina kama panya
road, mbwamwitu.
-Uvamizi wa vituo vya polisi ambapo watu
hujeruhiwa wakiwemo askari, na hata kuuawa
na silaha kuporwa.
-Matumizi ya nguvu kupita kiasi yafanywayo na
vyombo vya sheria na vyombo vya ulinzi dhidi
ya mikusanyiko ya watu.
-Hali ya wasiwasi na hofu inayoendelea
kujengeka miongoni mwa waumini wa dini
mbalimbali, ambayo inaonekana matokeo yake
ni kuligawaTaifa.
-Mifumo ya kutoa haki inakwama mno kutokana
na mienendo ya kifisadi inayozidi kuota mizizi.
-Taasisi za Serikali zinashindwa kuwapatia
wananchi wengi haki zao za msingi.
2. Msimamo wetu juu ya Mpango wa Kura ya
Maoni.
Tuangaliapo hali ya nchi yetu leo, tunapata hofu
kwamba uharakishwaji wa zoezi hili unaongeza
fadhaa na mpasuko ambao tayari upo katika
jamii yetu. Watu watawaka hasira kwasababu
wanaelewa maoni yao waliyotoa na kuzingatiwa
na Rasimu II (ya Tume ya Mabadiliko ya
Katiba) hayakuheshimiwa. Badala yake
matakwa ya kisiasa ya watu wachache ndio
yamepewa uzito mkubwa katika
KatibaInayopendekezwa. Katika muktadha huu
msimamo na Ushauri Wetu ni:
Zoezi la kupitisha KatibaInayopendekezwa
lipewe muda zaidi/liahirishwe, na kufanyika
baada ya Uchaguzi Mkuu, Oktoba 2015.
Tuonavyo sisi, sio jambo la busara kuendelea
kuwataka watu kupigia kura kitu wasichokijua.
Ikiwa watawala wataendelea kulazimisha, basi
wananchi wajitokeze na kupiga kura ya
kuikataa Katiba Inayopendekezwa.
Bado tunakumbuka vizuri, jinsi mchakato wa
kupata Katiba mpya ulivyoendeshwa kupitia
Bunge Maalum la Katiba. Kwa ufupi, uadilifu
ulikosekana, dhamiri za wajumbe wa Bunge
Maalum la Katiba ziliingiliwa na wengi wao
kulazimishwak utenda kwa hofu na unafiki,
uwazi ulikosekana, sheria haikuzingatiwa na
roho ya sheria yenyewe haikupewa tafakari
stahiki. Tunabaki kujiuliza motisha wa viongozi
wa kisiasa na serikali kulazimisha maoni yao
ulitokana na nini? Je, walisukumwa na moyo wa
uzalendo ama matakwa ya kibinafsi? Bado
tunaamini kuwa walisahau kwa makusudi
kwamba suala hilin linadai uwajibikaji mkubwa
kwa ajili yaTaifa letu.
Hitimisho
Tunawasihi waumini wetu kuendelea kuombea
amani taifa letu na kufanya kila linalowezeka ili
kuimarisha na kudumisha amani.
Tunaiomba Serikali kutumia mamlaka yake na
vyombo vyake vya sheria na vya ulinzi na
usalama kujenga amani na kuhimiza ushiriki wa
watu wote katika masuala yanayolihusu Taifa
letu.
Tunawasihi viongozi wa dini zote na kuwatia
moyo watambue kwamba wao ni wadau wa
kwanza katika kujenga umoja na moyo wa
kupokeana kwa stahamala bila kujali tofauti
zetu za kidini.
Tunaendelea kukazia UTAKATIFU wa mchakato
wa kuunda Katiba ambayo lazima iwe chombo
cha kulinda tunu na matakwa/matamanio ya
watu wote, na sio ya wachache tu.
Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, name
nitawasikiliza. Nanyi mtanitafuta, nakuniona,
mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote (Yer 29:
12 – 13).
Imetolewa na Maaskofu wa Baraza la Maaskofu
Katoliki – Tanzania
+Tarcisius NGALALEKUMTWA
RAIS WA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI
TANZANIA
 
HOJA ZA KUIKATAA KATIBA PENDEKEZWA HAZINA MASHIKO, MASLAHI YA WANANCHI YAMEZINGATIWA KWA KINA, SI KWELI KWAMBA INAWALINDA VIONGOZI PAMOJA NA CCM


MAKALA NO. 3

Kwa muda mrefu kumekuwepo hoja nyingi hasa kutoka vyama vya siasa, wanaharakati, wanasiasa, wanasheria pamoja na wachambuzi wa masuala ya kisiasa juu ya uhalali na ubora wa rasimu ya katiba inayopendekezwa na bunge maalum la katiba. Kwa ujumla wake hoja nyingi zinagawanyika katika makundi yafuatayo:-


Kwamba, bunge maalum lilikiuka mamlaka yake kisheria na kufanya kinyume cha matakwa ya sheria ya mabadiliko ya katiba (sura ya 83 toleo la mwaka 2014).


Kwamba, maoni ya wananchi katika rasimu ya pili ya katiba yaliachwa na hayakuzingatiwa( hapa hoja nyingi zinajikita katika suala la muundo wa muungano kutokana na takwimu za tume kuhusu maoni ya watu binafsi, vyama vya siasa, taasisi binafsi na za serikali kuhusu muundo wa muungano.


Kwamba, mchakato mzima wa kupatikana katiba pendekezwa ulikuwa na mapungufu mengi Kwamba, katiba inayopendekezwa imejali maslahi ya CCM pamoja na viongozi na siyo maslahi ya wananchi kama rasimu ya pili ilivyokwa imesheheni.


Maoni ya namna hii yamekuwa yakitolewa na watu wengi akiwemo aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya katiba Mh. Jaji Joseph Sinde Warioba pamoja na baadhi ya waliokuwa wajumbe wa Tume hiyo na hivyo kuwashawishi watu wasiikubali rasimu ya katiba inayopendekezwa.


Hoja ya kwanza inakosa mashiko kabisa kisheria na kiuhalisia. Hoja hizi hazikuzingatia historia pamoja na dhana halisi ya kisheria kuhusu bunge maalum la katiba ( Consituent Assembly) ambayo ni kwamba bunge maalum ni mwakilishi wa mamlaka ( sovereignty) ya watu. Kujitungia katiba yao nikwa nikwa mujibu wa mamlaka ( sovereignty) ya watu. Ifahamike kwamba rasimu yenyewe ya katiba inaweza kuandikwa na kamati iliyoteuliwa na bunge lenyewe ( rejea mchakato wa kuandika katiba ya India ya 1950) au rasimu inaweza kuandaliwa na kuandikwa na Tume ( rejea mchakato wa kuandika katiba ya Uganda 1995). Mifumo yote hii haibadili wala kuondoa dhana au mamlaka ya bunge maalum kama chombo cha wananchi kama ilivo katika vifungu vya 25 (1) na 28(1) vya sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya 83 toleo la mwaka 2014 ingawa kisiasa bunge maaalum lililochaguliwa na wananchi moja kwa moja linakuwa na nguvu zaidi kutokana na uwiano wa matabaka na makundi katika jamii.


Kisheria dhana ya bunge maalum haiathiriwi wala kubadilika kwa kuangalia nani niwajumbe wa bunge maalum ilimradi wawe wamepatikana kwa njia halali iliyoainishwa na sheria husika kama ilivyo kwetu hapa Tanzania ni sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya 83 toleo la mwaka 2014 katika kifungu cha 22(1) (a)-(c) na (i)-(x). pia angalia David Mukholi (1995) Uganda’s Fourth Constitution: History, Politics and Law, kampala: Fountaion Publishers, uk.49), Mahendra p. Singh, V.N. Shukla’s Constitution of India 9[SUP]th[/SUP] Edn. Lucknow: Easten Book, uk.A-24-A-25.


Kwabahati mbaya sana pia wapo wanasheria wenye mlengo kama huu yakwamba bunge maalum halikuwa na mamlaka ya kurekebisha rasimu yapili ya katiba, bila yashaka nikwa sababu ya mapenzi ya vyama vyao pamoja na ushabiki wa kisiasa pasipokujali misingi ya taaluma yao ikiwemo kuwa waadilifu na kusema ukweli. Wamekuwa wakitoa tafsiri potofu juu ya mamlaka ya bunge maalum la katiba kwamba halikuwa na mamlaka yakile bunge maalum lilichofanya kurekebisha na kuboresha misingi ya rasimu ya pili iliyopendekezwa. Natumia furusa hii kuwaelimisha kwamba kifungu cha 25(1) kinasomwa pamoja na kifungu cha 28(1) ndipo mantiki sahihi ya mamlaka ya bunge maalum la katiba yanapatikana.

Kwa kwamujibu wa kifungu cha 28(1) bunge maalum lilikuwa na kazi ya kutunga katiba inayopendekezwa wala siyo kupitisha rasimu ya Tume kama inavyoelezwa na baadhi ya watu. Bila shaka bunge maalum lilikuwa namamlaka ya kutunga rasimu ya katiba inayopendekezwa bila kufungwa na rasimu yapili ya Tume.

Baadhi ya tafsiri potofu zinazotolewa zinaonesha kama vile Tume ndiyo ilikuwa na mamlaka ya kutunga katiba inayopendekezwa ambapo siyo kweli. Tume haikuwa na wawakilishi wa wananchi, ilikuwa na watu wenye weledi wa kukusanya maslahi tofauti ya wananchi ili yawasilishwe kwenye bunge maalum. Bunge maalum ndicho chombo kilichokuwa kimesheheni wawakilishi wa wananchi na ndiyo maana bunge maalum likapewa mamlaka ya kutunga katiba inayowafaa wananchi nasiyo kubariki yaliyoletwa na Tume.


Kuhusu hoja yakwamba maoni ya wananchi yameachwa siyo ya kweli kabisa ni uzushi tu wakisiasa kwa kuzingatia maelezo pamoja na tafsiri niliyotoa hapo juu kuhusu mamlaka pamoja na ukomo wa mamlaka ya bunge maalum la katiba. Hoja yakwamba wananchi waliowengi walipendekeza muundo wa serikali tatu siyo sahihi na haithibitiki kwa mujibu wa takwimu zilizowasilishwa na Tume yenyewe kwa ushahidi ufuatao: ukiangalia kwa makini takwimu zilizotolewa na Tume yenyewe ( angalia jedwali 3,uk.9) kwamba, waliotoa maoni mbele ya tume ni watu 351,664 kati ya hao, 47,820 tu (asilimia 14) ndio waligusia muundo wa muungano. Asilimia 86 hawakuzungumzia muundo wa muungano kwa maana yoyote iwe ya serikali moja, mbili, tatu au muungano wa mkataba. Wao walikuwa na mambo tofauti kabisa kuhusu maisha yao. Isitoshe, kati ya waiogusia muundo wa muungano, asilimia 30 walitaka serikali mbili, asilimia 37 walipendekeza serikali tatu, na asilimia 25 walitaka muungano wa mkataba, asilimia nane walitaka serikali moja.


Kwahiyo waliopendekeza serikali tatu ni theluthi moja tu ya waliogusia muundo wa muungano na ni asilimia 5 tu walitoa maoni, waliotaka serikali mbili na muungano wa mkataba ni asilimia 55, yaani zaidi ya nusu ya waliotoa maoni juu ya muundo wa muungano. Hata ukichanganya waliotaka serikali moja na serikali mbili ni asilimia 38, inazidi kidogo wale waliotaka serikali tatu. Kwa takwimu hizi za Tume usahihi wa kwamba wananchi waliowengi walitaka muundo wa serikali tatu uko wapi? Hoja hii haina mashiko wala ushahidi wa maana, na kuendelea kwa waliokuwa watumishi wa Tume kwamba serikali tatu ndizo zilitakiwa na wananchi wengi itakuwa nikutwambia kwamba wao wenyewe ndiyo wanataka muundo wa serikali tatu ila wasitumie mgongo wa Tume maana kwenye takwimu za Tume mahitaji ya serikali tatu kwa wananchi waliowengi hayathibitiki kabisa.

Pia nivema ifahamike kwamba haikuwa makusudio ya sheria ya mabadiliko ya katiba wala siyo dhana ya bunge maalum la katiba kwamba kila hoja iliyowasilishwa na Tume ilikuwa lazima kupitishwa na bunge maalum na kama bunge lingefanya hivyo lingekuwa limepoteza maudhui yake na ikumbukwe kwamba Tume iliyasahau mengi muhimu ya wananchi na ndiyo umaalum wa bunge la katiba unapatikana kwa kurekebisha, kuboresha, kupitisha na kutunga katiba inayowafaa wananchi kulingana na mahitaji pamoja na mazingira ya nchi.


Nafasi ya bunge maalum niyakipekee kabisa katika mchakato wa kutunga katiba mpya. Nafasi yake ni nzito kuliko ile ya Tume na muhimu kuliko kura ya maoni nikwa sababu bunge maalum ndiyo chombo cha kufanya maamuzi mazito, siyo Tume.Ningelishangaa sana kama bunge maalum lingebariki baadhi ya misingi iliyokuwa imewekwa na Tume kwenye rasimu ambayo ingepitishwa na bunge maalum na kisha kupitishwa na wananchi ingeleta balaa na maangamizi kwa Watanzania hasa ule muundo wa serikali tatu. Bunge lilikuwa na kazi ya kuhakikisha kwamba inapitisha mambo ambayo hayawezi kuzaa vurugu, kuvunja utulivu, amani pamoja na mshikamano na umoja wananchi,( National and territorial integrity).


Kuhusu hoja ya kwamba mchakato wa kupatikana katiba pendekezwa hauna uhalali na kwamba katiba pendekezwa siyo halai, naomba kuwauliza wanaotoa kauli hii kwamba nikipi si halali kati ya haya yaliyopelekea kupatikana kwa katiba pendekezwa, Ni sheria ya mabadiliko ya katiba? Ni wajumbe wa Tume ya mabadiliko ya Katiba? Ni Tume yenyewe? Ni rasimu ya Tume? Ni bunge maalum? Ni kanuni za bunge maalum? Au ni rasimu ya katiba pendekezwa. Iwapo maswali haya yatajibiwa kwa kuzingatia hoja na uchambuzi niliofanya pamoja na uhalisia wa matakwa ya kisheria na siyo ya maslahi ya vyama vya siasa au kundi Fulani la watu itakuwa wazi kwamba rasimu ya katiba inayopendekezwa unao uhalali wote wa kupigiwa kura na wananchi kwa kadri watakavoona wao.


Hoja nyingine inayotolewa sana ambayo kwa upande wangu ninasema nidhaifu na haina mashiko ni ile yakwamba katiba pendekezwa imejali zaidi maslahi ya CCM pamoja na viongozi na siyo maslahi ya wananchi. Wanaosema hivi hawajaisoma na kuilewa katiba inayopendekezwa na badala yake wanaongozwa ima na hisia tu au ni wale ving’ang’anizi wa rasimu ya pili au niwale wenye tamaa ya kuiona Tanzania inavurugika ili watimize ndoto zao za kuwa viongozi wakati watanzania wakipata shida. Katika sura ya pili sehemu kwanza ya katiba inayopendekezwa Ibara ya 11(1) inabainisha wazi kwamba lengo la katiba hii ni kulinda, kuimarisha na kudumisha, haki, usawa, udugu, amani, umoja na utangamano wa wananchi wa jamhuri ya muungano kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga Taifa huru lenye democrasia, utawala bora, maendeleo endelevu na kujitegemea na ibara ndogo ya 3 imetaja malengo makuu ya katiba hii kitaifa ambayo yamezingatia mahitaji muhimu ya watanzania wote. Imetajwa kwamba lengo kuu la katiba hii kitaifa ni kuboresha maisha ya watanzania katika Nyanja zote za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kimazingira. Seheme ya pili, Ibara ya 12(1) imetaja wazi kwamba katiba hii inalengo la kisiasa na nilengo la kitaifa na kwamba serikali itahakikisha inadumisha democrasia, na kuondoa ubaguzi wa aina zote pia katika ibara ndogo ya 2(a), (b) na (c) katiba pendekezwa imeweka wazi kwamba litakuwa nijukumu la serikali kuchukua hatua ambazo zimeainishwa ndani ya ibara hii kuhakikisha lengo la katiba hii kisiasa linafanikiwa kwa watanzania pia bunge limetakiwa kutunga sheria zitakazowezesha lengo hili muhimu linafikiwa.


Katika sehemu ya tatu ya katiba pendekezwa inataja malengo ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kuwa malengo ya kitaifa ambapo katika ibara ya 13(1) lengo la Taifa kiuchumi imetajwa kuwa serikali itahakikisha Taifa linajenga uchumi wa kisasa utakaowawezesha wananchi na Taifa kujitegemea kwa kuzingatia matumizi ya elimu ya sayansi na technolojia katika Nyanja zote za uzalishaji mali kwa kuhimiza mapinduzi ya kilimo, ufugaji na uvuvi, mapinduzi ya viwanda na kujenga sekta muhimu ya nishati na mwasiliano na miundo mbinu ambapo katika ibara ndogo ya 2(a)-(g) katiba inatoa jukumu kwa serikali kuhakikisha inachukua hatua stahiki ambazo pia pia zimetajwa kuhakikisha lengo la Taifa kiuchumi linakamilika pia bunge limetakiwa kutunga sheria zitakazowezesha lengo hili muhimu linafikiwa.


Ibara ya 14(1) imeweka lengo la Taifa kijamii kwamba serikali itahakikisha inajenga jamii yenye ustawi na uwezo wa kushiriki katika shughuli za kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ambapo ibara ndogo ya 2(a)-(f) Serikali ina jukumu la kuchukua hatua stahiki ili kufikia lengo hili na pia bunge litatunga sheria kuhakikisha lengo hili muhimu linafikiwa.


Ibara ya 15(1) imetaja lengo la Taifa kiutamaduni kwamba nikukuza, kudumisha, na kuhifadhi utamaduni wa Taifa pia wa wananchi ambapo katika ibara ndogo ya 2(a)-(e) serikali imetakiwa kuchukua hatua stahiki ili kuhakikisha lengo hili muhimu la kitaifa linafikiwa.


Hivi kweli malengo makuu na muhimu ya katiba hii kitaifa yaliyotajwa katika ibara za 11,12,13,14 na 15 nikwa ajili ya CCM na viongozi? Au jamii inamahitaji mengine nje ya haya yaliyotajwa katika katiba hii pendekezwa? Kuna kosa gani iwapo hawa wanaosema katiba hii pendekezwa ni mbaya, haikujali maslahi ya wananchi na inalinda CCM na viongozi wa nchi nikiwaita wazushi? Katiba pendekezwa ni nzuri sana. MWANASHERIA.
MWESIGWA ZAIDI SIRAJI.
0784 646220
Kazi kweli kweli. CCM wamekuhonga kiasi gani ili uandike huu utumbo? Iwapo wewe ndiye mfano wa wasomi tulionao Tanzania, basi bado tuna safari ndefu.
 
Wewe huna malezi kabisa. possibly umezaliwa na kukulia mtaani. Lete hoja na siyo matusi.

Najua Mkuu umetembelewa na zile zilizotengwa na ikulu ili kuipigia promo waraka wa ccm.. Ninaamini kuna wakati roho yako inakusuta lkn ndo tamaa imekuzonga..

Ila mie nafsi yangu hainitumi hata kidogo kuipigia kura katiba ambayo mwenyekiti wa rasimu yake alikuwa fisadi Chenge a.k.a mzee wa vijisenti a.k.a joka makengeza na ikapitishwa na ukoo wa panya..
 
Nikweli wapo ambao hawana maadili ambalo ni jambo binafsi siyo la Chama. katiba haikuandikwa na chama, iliandikwa na kamati ya bunge maalum la katiba. Hata kilichotolewa pia kuna kilichoingizwa ambacho Tume haikuwa imekiweka. pia siyo lazima kila kilichomo kwenye rasimu ilikuwa lazima bunge maalum kukikubali. Tume ilileta mapendekezo na siyo katiba.

Kwanini waliyaondoa yale yaliyopendekezwa na wananchi kama kweli katiba ni ya wananchi?
 
Najua Mkuu umetembelewa na zile zilizotengwa na ikulu ili kuipigia promo waraka wa ccm.. Ninaamini kuna wakati roho yako inakusuta lkn ndo tamaa imekuzonga..

Ila mie nafsi yangu hainitumi hata kidogo kuipigia kura katiba ambayo mwenyekiti wa rasimu yake alikuwa fisadi Chenge a.k.a mzee wa vijisenti a.k.a joka makengeza na ikapitishwa na ukoo wa panya..

Hahahaha...duh!
 
Nyie jidanganyeni tu na katiba yenu ya Chenge. Mngejua msingejitabisha hata kuzi-print na kuzisambaza. Ni utumiaji mbaya wa pesa za umma.
Hiyo katiba, tutachukua, hatuisomi, na kura tutapigia "HAPANA" kwa kila kilichomo!
 
Back
Top Bottom