kipara kipya
JF-Expert Member
- May 2, 2016
- 18,833
- 23,276
Heshima kitu cha bure!Kama huyu ngalu mtoa post hajiheshimu wew ni nani hadi umuheshimu? Ngalu embu heshima nayo iheshimike sio kutoa heshima tu pasipo stahili heshima! Kumuheshimu mtoa post ya namna hii ni matumizi mabaya ya heshima
Je hawa ''stalwart ' wachache ni Vitimbakwiri?Wanabodi
Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.
Usisahau maneno hayoKabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar.
Sheria gani na ya mwaka gani iliyofuta majina hayo. Jina la Tanganyika lilifutwa na sheria ganiBaada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.
OKUadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,
1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania.
Tanzania Bara ni nchi gani? Rejea maneno yako hapo juu '' nchi zilizoungana ni Tanganyika na Zanzibar''Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.
Sawa2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani.
Pascal unahitaji Elimu ya Uraia ni si kutoa Elimu ya Uraia.Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.
ni muhimu zaidi kuwatoa ujinga vitimbakwiri hawa. Kuacha kufanya hivyo ni kuwatelekeza, jambo ambalo si zuri, watazaliana na ujinga wa kibaguzi kudai kitu kisichokuepo utaongezeka zaidi 🐒Wanabodi
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na kwa Maslahi ya Taifa, kila Jumatano kwenye gazeti la Mwananchi na Jumapili kwenye gazeti la Nipashe na kwenye kipindi cha KMT on Channel Ten TV, kila siku za Jumapili saa 3:00 usiku na marudio Jumatano saa 9:30 alasiri.
Hoja ya leo ni hoja za Utanganyika na Uzanzibari ambazo ni hoja muflis zinazosababishwa watu wanaitwa vitimbakwiri kujivunia uraia ambao haupo kutokana na ujinga tuu wa ukosefu wa elimu ya uraia kuhusu uraia wa Tanzania. Kwenye uraia, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari, tuna uraia mmoja tuu, Mtanzania. Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.
Hili ni Nipashe la Leo.
View attachment 2994081
Ukosefu wa Elimu ya Uraia Kuhusu Katiba, Sheria, Haki na Wajibu, ndio umesababisha, huu ubaguzi wa Utanganyika, na Uzanzibari, watu wakielimishwa kuhusu uraia, hawa vitimbakwiri muflis wanaoleta ujinga wa ubaguzi wa kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, ujinga huu utawatoka, wataerevuka na tutakuwa na Utanzania pekee!.
Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.
NB. Aliyesema wanasiasa wanaojinasibisha na Utanganyika na Uzanzibari, dini zao, kanda zao, au kabila zao, ni watu muflis, waliofilisika kisiasa, sio mimi ni Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na akaiandikia kitabu kinaitwa “Nyufa”. Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.
Uraia ni hoja ya kikatiba na kisheria. Kabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar. Baada ya muungano, tukaungana kuwa nchi moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwa na uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania.
Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.
Uadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,
1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.
2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.
Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.
Uadhimu wa Muungano.
Muungano wetu licha ya kuwa ni muungano adimu, pia ni muungano adhimu, wenye dhima ya kuungana milele!. Miungano yote duniani unaundwa kwa mikataba ya kisheria ya muungano. Mikataba hiyo inakuwa na kipengele cha jinsi ya kuivunja miungano hiyo. Kwenye zile Articles of Union za Muungano wetu, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja, muungano, hivyo zile Hati za Muungano sio mkataba wa muungano, ni makubaliano ya muungano, (not a contract, but an agreement) yenye dhima ya muungano wa milele, na ndio maana tunasema “muungano tutaulinda kwa gharama yoyote”.
Tangu tumeungana, na mimi tangu nimezaliwa na kupata akili, sikumbuki hata mara moja, kusikia vipindi vya elimu ya uraia kuhuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, hali inayopelekea Baadhi ya Watanzania kuanza kujinasibisha na Utanganyika wao, na Uzanzibari wao.
Kwa vile Tanganyika ilifutwa na jina la Tanganyika kufutwa, utanganyika nao ukafutika, Watanganyika tunajisabisha kwa Utanzania wetu, lakini kwa vile kwa vile jina la Zanzibar, halikufutwa, na kuna Uzanzibari ukaazi, hivyo baadhi ya Wanzanzibari, wanajinasibisha kwa Uzanzibari wao kama uraia wa Zanzibar, badala ya kujinasibisha na Utanzania wao, kungekuwa na vipindi vya elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu, kusingekuwepo, vitimbakwiri wowote, wanaojinasibisha kwa Utanganyika wao, au Uzanzibari wao kwasababu, uraia wa JMT ni uraia mmoja tuu, hakuna uraia wa Tanganyika, wala hakuna urais wa Zanzibar, kuna uraia mmoja tuu, uraia wa JMT.
Wiki ijayo, nitaendelea na kuwaletea hizi chokochoko za kuuchokoa muungano na kuanza kunyoosheasha vidole vya ubaguzi wa “Utanganyika na Uzanzibari” zilianzia wapi, dawa yake ni nini na tiba ya kudumu ya kuitibu sumu hii na kuiangamiza kabisa.
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=fPhb1_0doZmgD7T4Wakati huo huo, naendelea na darasa langu la elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria na haki on Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku.
Karibuni.
Paskali
Umunyoroshe nani wewe chawa?Kiukweli vitimbakwiri, wanaojiasibisha na Utanganyika na Uzanzibari ni wengi ila tunawamudu na tutawanyorosha!.
P
kuzira, kususa, kugoma tena kwa mihemko na ghadhabu kwa hoja na majadiliano ya kawaida na ya kiungwana namna hii si ndio utimbakwiri wenyewe huu. Sasa unapanic nini na wakati naona una mawazo na hoja nzuri tu?Mkuu P, with all due respect hii 'fallacious article' inakufanya uonekana ' a mendacious person'
Lakini pia ni 'intellectual abuse' kubwa sana kwa jamii ya Watanzania.
Je hawa ''stalwart ' wachache ni Vitimbakwiri?
CJ Nyalali na jopo
Dr Salim Ahmed Salim
PM and VP Warioba
Mr J.Butiku
Judge Kisanga
Hivi unataka ulimwengu uamini kwamba Mwanasheria Mkuu wa Serikali mstaafu (AG) , Waziri wa Katiba na Sheria , Waziri Mkuu mstaafu(PM) na Rais wa Bahari za dunia , Mh J.S. Warioba naye anahitaji elimu yako ya Uraia kupitia vipindi vyako ! real?
Usisahau maneno hayo
Sheria gani na ya mwaka gani iliyofuta majina hayo. Jina la Tanganyika lilifutwa na sheria gani
OK
Tanzania Bara ni nchi gani? Rejea maneno yako hapo juu '' nchi zilizoungana ni Tanganyika na Zanzibar''
Hii Tanzania bara umeipata wapi?
Sawa
Pascal unahitaji Elimu ya Uraia ni si kutoa Elimu ya Uraia.
Umesema '' Federation yenye nchi mbili , Tanzania na Zanzibar''
Ukasema zilizoungana ni Tanganyika na Zanzibar. Halafu ukasema nchi hizo zimeunda Tanzania.
Hapa chini unasema zilizoungana ni Tanzania na Zanzibar.
Tanzania is an 'entity' ! ni zao la Tanganyika na Zanzibar na kamwe haiwezi kuungana na mshirika wa nchi hizo mbili wala haiwezi kuwa na ushirika na nchi hizo mbili kwasababu Tanganyika na Zanzibar ni subset za Tanzania. period! haihitaji elimu yoyote ile
Acha upotoshaji na uongo ! please you're better than this ! Unaweza kutafuta vipindi si kwa njia hii.
Nimesoma article na sitairudia na wala sitasikiliza vipindi vyako tena si kwa maana mbaya, ni katika kulinda 'intellectual capacity yangu' . Yaani umefika mahali unatukana weledi na akili za watu bila aibu
Kila la heri na vipindi unavyotafuta 'in a deceitful behavior'' .
Ume ni disappoint sana na sijui editor aliwezaje kuruhusu hiyo article bila ku cheki consistency na facts
Naomba kuheshimu mawazo yako na maoni yako.Mkuu P, with all due respect hii 'fallacious article' inakufanya uonekana ' a mendacious person'
Lakini pia ni 'intellectual abuse' kubwa sana kwa jamii ya Watanzania.
Acha upotoshaji na uongo ! Unaweza kutafuta vipindi si kwa njia hii.
Nimesoma article na sitairudia na wala sitasikiliza vipindi vyako tena katika kulinda 'intellectual capacity yangu' . Yaani umefika mahali unatukana weledi na akili za watu bila aibu
Kila la heri na vipindi unavyotafuta 'in a deceitful behavior'' .
Ume ni disappoint sana
Vitimbakwiri vikibananishwa, vinakuwa vikali kweli kweli!.kuzira, kususa, kugoma tena kwa mihemko na ghadhabu kwa hoja na majadiliano ya kawaida na ya kiungwana namna hii si ndio utimbakwiri wenyewe huu. Sasa unapanic nini na wakati naona una mawazo na hoja nzuri tu?
Naunga mkono hoja, kazi ya kuwatoa ujinga vitimbakwiri hawa inaendelea kwa kipindi cha TV kila Jumatano na Jumapili na makala za magazeti ya Mwananchi Jumatano na Nipashe Jumapili.ni muhimu zaidi kuwatoa ujinga vitimbakwiri hawa. Kuacha kufanya hivyo ni kuwatelekeza, jambo ambalo si zuri, watazaliana na ujinga wa kibaguzi kudai kitu kisichokuepo utaongezeka zaidi 🐒
Alijisemeaga Magufuli...Mayalla maana yake ni njaa. Mzee sasa ameamua ku kiss a** ili alambe asali kidogo. Kuna baadhi ya wasomi wa Tanzania wanatuangusha sana.Mkuu P, with all due respect hii 'fallacious article' inakufanya uonekana ' a mendacious person'
Lakini pia ni 'intellectual abuse' kubwa sana kwa jamii ya Watanzania.
Je hawa ''stalwart ' wachache ni Vitimbakwiri?
CJ Nyalali na jopo
Dr Salim Ahmed Salim
PM and VP Warioba
Mr J.Butiku
Judge Kisanga
Hivi unataka ulimwengu uamini kwamba Mwanasheria Mkuu wa Serikali mstaafu (AG) , Waziri wa Katiba na Sheria , Waziri Mkuu mstaafu(PM) na Rais wa Bahari za dunia , Mh J.S. Warioba naye anahitaji elimu yako ya Uraia kupitia vipindi vyako ! real?
Usisahau maneno hayo
Sheria gani na ya mwaka gani iliyofuta majina hayo. Jina la Tanganyika lilifutwa na sheria gani
OK
Tanzania Bara ni nchi gani? Rejea maneno yako hapo juu '' nchi zilizoungana ni Tanganyika na Zanzibar''
Hii Tanzania bara umeipata wapi?
Sawa
Pascal unahitaji Elimu ya Uraia ni si kutoa Elimu ya Uraia.
Umesema '' Federation yenye nchi mbili , Tanzania na Zanzibar''
Ukasema zilizoungana ni Tanganyika na Zanzibar. Halafu ukasema nchi hizo zimeunda Tanzania.
Hapa chini unasema zilizoungana ni Tanzania na Zanzibar.
Tanzania is an 'entity' ! ni zao la Tanganyika na Zanzibar na kamwe haiwezi kuungana na mshirika wa nchi hizo mbili wala haiwezi kuwa na ushirika na nchi hizo mbili kwasababu Tanganyika na Zanzibar ni subset za Tanzania. period! haihitaji elimu yoyote ile
Acha upotoshaji na uongo ! please you're better than this ! Unaweza kutafuta vipindi si kwa njia hii.
Nimesoma article na sitairudia na wala sitasikiliza vipindi vyako tena si kwa maana mbaya, ni katika kulinda 'intellectual capacity yangu' . Yaani umefika mahali unatukana weledi na akili za watu bila aibu
Kila la heri na vipindi unavyotafuta 'in a deceitful behavior'' .
Ume ni disappoint sana na sijui editor aliwezaje kuruhusu hiyo article bila ku cheki consistency na facts
Cha kushangaa ni Paskali kudai anatoa elimu ya Uraia lakini hataki kujibu maswali. Pascal Mayalla njoo wajibu watu humu. La sivyo badilisha title. Badala ya kusema unatoa elimu ya Uraia Sema tunatoa mawazo yako kuhusu Muungano.Kama 2 ni muungano wa federation na kilanchi inaendelea kua na utawala wa ndani sasa je raisi wa tanganyaka yuko wapi?.
Hata mimi nakubaliana kabisa ni majadiliano ya kiungwana. Nisichokubaliana nacho ni ' exploitation ya sehemu ya jamii yetu' ili kutengeneza mazingira fulani. Ukisoma hiyo article kama si msomaji utakubaliana nayo 100%.kuzira, kususa, kugoma tena kwa mihemko na ghadhabu kwa hoja na majadiliano ya kawaida na ya kiungwana namna hii si ndio utimbakwiri wenyewe huu. Sasa unapanic nini na wakati naona una mawazo na hoja nzuri tu?
Ninafuatilia lakini pia siwezi kuendelea kuinajisi akili yangu kwa kuamini kuna 'Federation ya nchi mbili, Tanzania na Zanzibar''. Hapana aisee! Huu upotoshaji wa Tanzania ni nchi tofauti kabisa na Zanzibar ni wa ki-CCM.si utulie upate elimu ya uraia, fatilia vipindi na makala mbalimbali ili kuongeza uelewa na ufahamu zaidi juu ya masuala haya ya Muungano. kughafilika au kupotoka ni mambo ya kawaida tu 🐒
Well kama ni utimbakwiri let it be, ninachosema hapa ni kwamba sikubaliani na upotoshaji.kuzira, kususa, kugoma tena kwa mihemko na ghadhabu kwa hoja na majadiliano ya kawaida na ya kiungwana namna hii si ndio utimbakwiri wenyewe huu. Sasa unapanic nini na wakati naona una mawazo na hoja nzuri tu?
Huu muungano unaosema kwamba ni 'adhimu na adimu' bila kujua maana yake unachanganya.si utulie upate elimu ya uraia, fatilia vipindi na makala mbalimbali ili kuongeza uelewa na ufahamu zaidi juu ya masuala haya ya Muungano. kughafilika au kupotoka ni mambo ya kawaida tu 🐒
Well narratedWanabodi
Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na kwa Maslahi ya Taifa, kila Jumatano kwenye gazeti la Mwananchi na Jumapili kwenye gazeti la Nipashe na kwenye kipindi cha KMT on Channel Ten TV, kila siku za Jumapili saa 3:00 usiku na marudio Jumatano saa 9:30 alasiri.
Hoja ya leo ni hoja za Utanganyika na Uzanzibari ambazo ni hoja muflis zinazosababishwa watu wanaitwa vitimbakwiri kujivunia uraia ambao haupo kutokana na ujinga tuu wa ukosefu wa elimu ya uraia kuhusu uraia wa Tanzania. Kwenye uraia, hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari, tuna uraia mmoja tuu, Mtanzania. Swali ni jee tuwatoe ujinga hawa vitimbakwiri muflis wanaotaka kutubagua kwa Utanganyika na Uzanzibari kwa kuwaelimisha elimu ya uraia, au tuwaache tuu na ujinga wao kujisikia sifa kujinasibisha na kujivunia Utanganyika na Uzanzibari?.
Hili ni Nipashe la Leo.
View attachment 2994081
Ukosefu wa Elimu ya Uraia Kuhusu Katiba, Sheria, Haki na Wajibu, ndio umesababisha, huu ubaguzi wa Utanganyika, na Uzanzibari, watu wakielimishwa kuhusu uraia, hawa vitimbakwiri muflis wanaoleta ujinga wa ubaguzi wa kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, ujinga huu utawatoka, wataerevuka na tutakuwa na Utanzania pekee!.
Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.
NB. Aliyesema wanasiasa wanaojinasibisha na Utanganyika na Uzanzibari, dini zao, kanda zao, au kabila zao, ni watu muflis, waliofilisika kisiasa, sio mimi ni Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na akaiandikia kitabu kinaitwa “Nyufa”. Mwalimu alisema dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, ni kama kula nyama ya mtu, ukiishakula huwezi kuacha!.
Uraia ni hoja ya kikatiba na kisheria. Kabla ya Muungano, tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar, hivyo tulikuwa na uraia wa Tanganyika, na uraia wa Zanzibar. Baada ya muungano, tukaungana kuwa nchi moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwa na uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania.
Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.
Uadimu wa Muungano
Miungano ya nchi zote duniani ni miungano ya aina mbili kuu,
1. Muungano wa Union, ambapo nchi mbili zinaungana na kuunda nchi moja. Zile nchi zote mbili zilizoungana , zote zinakufa na kuunda nchi moja mpya. Hivyo ndivyo ulivyo muungano wetu kimataifa, ni muungano wa Unioni, ile nchi ya Tanganyika imekufa, ile nchi ya Zanzibar imekufa, imezaliwa nchi moja mpya ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye urais mmoja tuu, uraia wa Tanzania. Hakuna tena uraia wa Tanganyika, wala uraia wa Zanzibar, kuna uraia mmoja wa Tanzania. Tanganyika haipo nafasi yake imechukuliwa na Tanzania Bara, na Zanzibar japo ipo, ila sio nchi ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yenye utawala wake wa ndani, lakini hakuna uraia wa Zanzibar, uraia ni mmoja tuu wa Tanzania.
2. Muungano wa Federation, ni nchi mbili au zaidi, zinaungano kuwa nchi moja, lakini zile nchi zote mbili zinaendelea kuwa utawala wake wa ndani, na serikali zao, chini ya utawala mkuu wan chi ya federal state, kama Marekani. Vivyo hivyo muungano wetu kwa ndani ya muungano ni muungano wa federation yenye nchi mbili, Tanzania na Zanzibar, yenye marais wawili, Rais wa JMT “mwenye R kubwa, na rais wa Zanzibar mwenye r ndogo, zenye serikali mbili, serikali ya JMT na serikali ya SMZ, mabunge mawili, Bunge la JMT na BLW, na zenye mahakama mbili, Mahakama ya JMT na Mahakama ya Zanzibar, ila kwenye uraia, bado ni uraia mmoja tuu wa JMT, ila kwa Zanziar, wana ukaazi, ule ukaazi sio uraia ni utambulisho tuu wa wakaazi wa Zanzibar lakini wote ni Watanzania.
Hivyo muungano wa Tanzania ni muungano adimu pekee duniani ambao kwa upande mmoja ni muungano wa union na upande wa pili ni muungano wa federation, hakuna muungano wa aina hii popote duniani.
Uadhimu wa Muungano.
Muungano wetu licha ya kuwa ni muungano adimu, pia ni muungano adhimu, wenye dhima ya kuungana milele!. Miungano yote duniani unaundwa kwa mikataba ya kisheria ya muungano. Mikataba hiyo inakuwa na kipengele cha jinsi ya kuivunja miungano hiyo. Kwenye zile Articles of Union za Muungano wetu, hakuna kipengele cha jinsi ya kuuvunja, muungano, hivyo zile Hati za Muungano sio mkataba wa muungano, ni makubaliano ya muungano, (not a contract, but an agreement) yenye dhima ya muungano wa milele, na ndio maana tunasema “muungano tutaulinda kwa gharama yoyote”.
Tangu tumeungana, na mimi tangu nimezaliwa na kupata akili, sikumbuki hata mara moja, kusikia vipindi vya elimu ya uraia kuhuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, hali inayopelekea Baadhi ya Watanzania kuanza kujinasibisha na Utanganyika wao, na Uzanzibari wao.
Kwa vile Tanganyika ilifutwa na jina la Tanganyika kufutwa, utanganyika nao ukafutika, Watanganyika tunajisabisha kwa Utanzania wetu, lakini kwa vile kwa vile jina la Zanzibar, halikufutwa, na kuna Uzanzibari ukaazi, hivyo baadhi ya Wanzanzibari, wanajinasibisha kwa Uzanzibari wao kama uraia wa Zanzibar, badala ya kujinasibisha na Utanzania wao, kungekuwa na vipindi vya elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria, haki na wajibu, kusingekuwepo, vitimbakwiri wowote, wanaojinasibisha kwa Utanganyika wao, au Uzanzibari wao kwasababu, uraia wa JMT ni uraia mmoja tuu, hakuna uraia wa Tanganyika, wala hakuna urais wa Zanzibar, kuna uraia mmoja tuu, uraia wa JMT.
Wiki ijayo, nitaendelea na kuwaletea hizi chokochoko za kuuchokoa muungano na kuanza kunyoosheasha vidole vya ubaguzi wa “Utanganyika na Uzanzibari” zilianzia wapi, dawa yake ni nini na tiba ya kudumu ya kuitibu sumu hii na kuiangamiza kabisa.
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=fPhb1_0doZmgD7T4Wakati huo huo, naendelea na darasa langu la elimu ya uraia kuhusu katiba, sheria na haki on Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku.
Karibuni.
Paskali
Yaani ' Federation ya nchi mbili , Tanzania na Zanzibar'' halafu tukae kimya kwasababu tunapewa elimu! NopeHuu ni mzaha
Si kweli, hoja za kibaguzi zimekuwepo muda mrefu , zilinyamaziwa kwasababu wanaosema ni Wazanzibar.Hivi karibuni, kumeibuka hoja za kibaguzi za baadhi ya wanasiasa, kutoa kauli za kibaguzi za kuwanyooshea watu vidole na kuwaita “Wao Wazanzibari”, “Sisi Watanganyika”. Miongozi mwa watu wanaotoa kauli hizo ni baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani, waliofilisika kisiasa, na baadhi ya wanaolaani kauli hizo, ni baadhi ya viongozi wa chama tawala, ambapo nimemsikia mmoja wa viongozi hao, akilaani vikali kauli hizo bungeni kwa maneno makali kabisa!, huko pia ni kufilisika kisiasa.
Tanzama hapa watoa elimu ya uraia wanavyojjichanganya.Baada ya Muungano, majina ya nchi hizi zote mbili, nchi ya Tanganyika, na nchi ya Zanzibar, yalibadilika na kuwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani, hivyo jina la Tanganyika likafutwa, ila jina la Zanzibar, liliendelea kuwepo, kutokana na uadimu na uadhimu wa huu muungano wetu.