Hongera Azam FC, lakini...

Hongera Azam FC, lakini...

Yap, hamna tofauti yeyote. Hapo Prisons na JKT sawa ila Yanga imemzidi Simba.
Ni kweli kabisa mkuu me mwenyewe naona caf kama tff ya karia tu haiwezekani Simba waiweke nafasi ya 12 Africa na Yanga iwe nafasi ya 75 wakati Yanga ni Bora kuliko Simba sijui ata wanatumia vigezo gani
 
Kwa miaka kadhaa sasa watu wengi tumekuwa hatuielewi club ya Azam FC. Na hii ni kutokana na nguvu kubwa wanayotumia kuitangaza na kuboresha miundombinu vs kikosi na matokeo uwanjani.

Hakika timu imekuwa haieleweki na huwezi kuitofautisha na kina Mbeya City, Kagera Sugar, etc.

Mwaka huu tunaona kama wanataka kuwa serious maana tayari kuna sajili nzuri zimefanyika na naamini wataendelea kufanya hivyo maana bado kuna maeneo machache yanapaswa kuongezwa nguvu.

Kwanza upande wa Golikipa. Huyu mganda kama ndiyo mnatarajia kumtumia kama No. 1 msimu ujao basi hapo kuna kasoro. Huyu si mzuri sana hata yule Mghana Abdulrazack Barola anamzidi sana tu. Lazima atafutwe Golikipa wa ukweli wa kuhimili michuano mikubwa ijayo.

Pili bado nina wasiwasi na nafasi ya kiungo mkabaji. Lazima atafutwe mtu mwenye nguvu na kasi.

Kadhalika ongezeka straika mpambanaji ili kutoa ushindani kwa Dube ambaye naona ana kismati cha majeraha.

Mwisho kama Ntibanzonkiza yupo free mchukueni ni mpambanaji mzuri tu na anaweza kusainia kuwa na kikosi kipana na anaweza kutumika kwenye baadhi ya mechi na ASFC.

Kwa miaka hii zaidi ya kumi ambayo mpo ligi kuu mlitakiwa kuwa tayari mmejenga fan base nzuri ila inashindikana sababu mnakuwa kama vile hampo serious. Watoto wanaokuwa wangekuta kuna timu inazinyanyasa Simba na Yanga wale wasingejiunga huko. Na nafasi hiyo mnayo

Kila la kheri.
Hivi unafikiri kujenga fanbase ni rahisi tu kama kupika ugali wa dona ?
 
Ni kweli kabisa mkuu me mwenyewe naona caf kama tff ya karia tu haiwezekani Simba waiweke nafasi ya 12 Africa na Yanga iwe nafasi ya 75 wakati Yanga ni Bora kuliko Simba sijui ata wanatumia vigezo gani
Kuwa serious mkuu. CAF hawa wenye champions lg ama wepi?

Kama hujashiriki wala huna leseni yao watakutambuaje.
 
Utaishia kulalama na yule Babu yenu. Simba ni kunyanyua vikombe, nyie kunyanyua watu kwenye viti kama fashisti dada kule ug miaka hiyo. Simba oyeee....
 
Kwa miaka ya hivi karibuni ni mwaka huu ndio Azam wameonyesha kweli wako "serious" kutokana na usajili wa nguvu waliofanya mpaka sasa toka walipoachana na wakina Kipre Tcheche. Ifike mahali tuache pembeni ushabiki wa Simba na Yanga na tuwapongeze Azam kwa hatua waliyochukua mpaka sasa hivi kwenye usajili wao. Watu wengi hapa wanawachukulia poa sana Azam lakini kwangu mimi kitendo cha kuwasajili Kola na Idris Mbombo kwenye eneo la ushambuliaji wakati tayari wana Dube imeonyesha jinsi gani wana nia na kiu ya kubeba mataji mwaka huu.

Nilichogundua hapa wapenda mpira wengi wa watanzania huwa hawatazami ligi za majirani zetu ndio maana mpaka sasa wanauchukulia poa sana usajili wa Azam. Lakini kwa mtu anayemfahamu Mbombo toka akiwa Zambia akaenda Sudan akarudi tena Zambia kabla ya kwenda Misri atajua jamaa ni mnyama kiasi gani mbele ya goli japo Misri hakufanya vizuri kabisa.

Wito wangu kwa Simba na Yanga wafanye usajili wa nguvu kwani ligi kuu itakuwa ngumu sana kutokana na usajili alioufanya Azam mpaka sasa hivi. Na pia wakumbuke kuwa timu ndogo nazo zimepata mpunga wa kutosha kutoka kwa mdhamini Azam Media kwa hiyo zitakakaza sana.
 
Ni mpumbavu na Mbwa peke yake anayeweza kutumia nafasi za CAF zinaozbadilika msimu baada ya msimu kudai ubora wa timu. kwa sababu mla tambuu wenu kawalisha maembe ng'ong'o basi na nyie mnafuata mkumbo.
Luc Eymael. Yanga ni Mbwa na Nyani. Wanapiga tu makelele hawajui mpira. Ubora wa team unapimwa kwa kuchukua Ubingwa na kufika hatua za mbali kimataifa.

Luc Eymael hakukosea.
2864830_IMG_3816.jpg
2864830_IMG_3816.jpg
 
Back
Top Bottom