Hongera CP Hamduni Salum kwa kumpigia simu Elioth Lyimo na kuagiza maafisa wa TAKUKURU mkoani Kilimanjaro wafungue jalada la uchunguzi


Kwamba:

"Hata hivyo mzee Lyimo hakuridhika na akaamua kutafuta haki yake kimyakimya. Akaenda kuripoti TAKUKURU lakini hawakumsaidia, akaripoti polisi hawakumsaidia. Baadae akamwambia Godbless E.J. Lema ambaye alilifikisha kwa Waziri mkuu lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa."

Pamoja na kuwa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa, waziri mkuu naye akaendelea na mapambio ya sifa kwa malaika wa Mungu.

Hii nchi imechezewa sana!
 
JUMA RAIB (Mayor wa Moshi) alikuwa mwizi wa magari, na alikuwa na kesi hakimu mkazi Moshi 2012, amekuwa na matukio mengi sana;

Mtu ambaye alimvamia Antony Benedict Lyimo aliyekuwa diwani wa Nganga Mfumuni, kwenye kampeni pale Pasua alivamia na kumpasua kichwani ,kesi ilikwenda polisi lakini kazimwa;
Raib no jambazi na amepwa umeya na mwendazake, hii si sawa kabisa;
 
Mzee Lymo aliibiwa pesa, then akakaa kimya?

Duh?

Nyinyi watu si wa kuwaamini haraka haraka, vyombo vyetu vya usalama vikikuta Sabaya ana hatia nitaamini.
Wewe soma habari vizuri,unaambiwa alifika hadi kwa Waziri Mkuu.
 
Kwa kifupi utawala wa awamu ya tano ulikuwa wa kinyang'anyi kuanzia wanasiasa, mahakama hadi vyombo vya dola!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…