Hongera Diamond Platnumz hakika wewe ni mfano wa kuigwa

Hongera Diamond Platnumz hakika wewe ni mfano wa kuigwa

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2014
Posts
6,170
Reaction score
7,665
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Imekuwa ni nadra sana kumuona msanii wa Kitanzania akijitokeza katika jamii na kuchangia mambo mbali mbali kwa kigezo kuwa kazi zao hazina masilahi! Hii imekuwa tofauti kwa kijana wetu mpendwa Diamond Platnumz! Amekuwa akijitokeza sana katika mambo ya kijamii na kusaidia kadri awezavyo na kadri alivyo barikiwa!!!

Kujituma katika kazi zake ni kigezo kinacho nifanya nimpende Diamond, lakini Hata moyo wake wa kujitolea na kujituma kunanifanya nizidi kumpenda Diamond! Ikumbukwe juzi juzi tuu alichangia madawati 600, alimchangia kipepeo alie kuwa anatangazwa Clouds million 5, Diamond amewasaidia vijana wengi na anazidi kuwasaidia hakika huu ni moyo wa kipekee!!!

Leo amechangia millioni 20 (20,000,000) kwa GSM foundation kwa ajili ya matibabu ya watoto wenye vinchwa vikubwa wanao fanyiwa upasuaji!! Huu ni moyo wa kipekee na si kawaida kwa Wasanii wa Kibongo kufanya hivi kwa madai kuwa kazi zao hazilipi!!! Lakini kupitia Diamond tunajifunza mengi sanaaaa na Hapa ndio Tofauti ya Diamond na wasanii wengine huonekana!

Mungu amjalie huyu kijana aongezewe pale alipo toa! Ni wakati wa wasanii wengine kuiga mfano huu

Hakika Diamond ni mfano wa kuigwa na kila msanii!
 
Baba mzazi yu hali gani, kuna wakati alikuwa analia kwenye media Diamond kamtupa, sijui wanakomoana. Hata sielewi
 
Kazi ya Zari hiyo.
Ndio faida ya kuishi na mwanamke mtu mzima hahaha
 
Baba mzazi yu hali gani, kuna wakati alikuwa analia kwenye media Diamond kamtupa, sijui wanakomoana. Hata sielewi
Zile Media tuuu unaweza chomwa kisu wewe halafu zikaonesha wewe ndo umemchoma kisu
 
Ni kwa kutoa ndio tunapokea (lakini ni mpaka tuwe na hivyo cha kutoa) danya mimi na wewe tutatoa bei gani? Na wanajf wengine je?
Kwa uchache wa wingi wetu kwa kidogo tutakachojaliwa nasi tunapaswa kutoa chochote as JF members, na kama wazazi ndugu jamaa na marafiki
 
Diamond anafanya mambo ya kueleweka kwasababu ana mwanamke ambaye anajitambua. Na kumshauri vizuri....
Ila angekua na yule muuza uchi na yeye angeishia kujichekesha choice fm na kugharamia mawigi ya milioni 2.
Well done chibu.
 
Diamond licha ya mapungufu yake kama binadamu lakini jambo la maana sana alilolifanya ni kuwa karibu na watu wenye mtazamo chanya wa kimaisha..

Wanasema 'show me your friends and I will tell your future'!!
Bravo chibu! Na wengine waige mfano.. Kurudisha unachopata kwa jamii iliyokusapoti ni jambo la msingi sana kuliko kulingishiana marange rover instagram
 
Atazidishiwa zaidi ya hapo hakuna baraka na utajir kama ku invest kwa wenye shida Mungu amjaalie maisha marefu na hazina yake izidi kujaaa.
 
Back
Top Bottom