Chaliifrancisco
JF-Expert Member
- Jan 17, 2015
- 26,021
- 79,710
Baada ya FIFA kuifungia nchi ya Sierra Leone kutokushiriki mashindano yoyote yanayosimamiwa na bodi hiyo ya soka duniania, shirikisho la mpira wa miguu Afrika, CAF limeipiga chini Siera Leone katika mechi za hatua ya makundi za kufuzu kwenda AFCON kutokana na serikali kuingilia masuala ya soka jambo ambalo ni kinyume na sheria na taratibu za FIFA.
Kenya inayoongoza Kundi F imejikusanyia point 7 huku ikifuatiwa kwa karibu na Ghana yenye point 6 na Ethiopia yenye point 1. Kufuatia kuenguliwa kwa Siera Leone kumeipa Kenya tiketi ya moja kwa moja na wataungana na wenzetu kutoka ukanda wa Afrika Mashariki, Uganda ambao tayari wameshafuzu.
Lengo la uzi huu ni kuikumbusha 'sirikali' kuwa mambo ya siasa hayana nafasi kwenye soka la sivyo rungu la FIFA litatushukia na kutupasua vipande vipande.
Baada ya Taifa Stars kufungwa na Lesotho kuna kauli za viongozi wa 'sirikali' zilizokuwa na utata kuhusiana na kufuzu kwa timu yetu ya taifa kwenda AFCON.
Nashauri sirikali isifanye jambo lolote litakalokuwa nje ya sheria za FIFA kwakuwa tutaharibu zaidi. Tucheze na Uganda na kama tukishinda tushinde kispoti au kufungwa kispoti. Nje ya hapo itakuwa ni majanga kwetu.
Nashauri mapema kwakuwa viongozi wa hii awamu wana maamuzi ya kustaajabisha sio ajabu ukashangaa matamko yasiyoeleweka na kutendeka mambo ambayo yatachafua ramani ya soka hapa nchini.
Nawasilisha.
Kenya inayoongoza Kundi F imejikusanyia point 7 huku ikifuatiwa kwa karibu na Ghana yenye point 6 na Ethiopia yenye point 1. Kufuatia kuenguliwa kwa Siera Leone kumeipa Kenya tiketi ya moja kwa moja na wataungana na wenzetu kutoka ukanda wa Afrika Mashariki, Uganda ambao tayari wameshafuzu.
Lengo la uzi huu ni kuikumbusha 'sirikali' kuwa mambo ya siasa hayana nafasi kwenye soka la sivyo rungu la FIFA litatushukia na kutupasua vipande vipande.
Baada ya Taifa Stars kufungwa na Lesotho kuna kauli za viongozi wa 'sirikali' zilizokuwa na utata kuhusiana na kufuzu kwa timu yetu ya taifa kwenda AFCON.
Nashauri sirikali isifanye jambo lolote litakalokuwa nje ya sheria za FIFA kwakuwa tutaharibu zaidi. Tucheze na Uganda na kama tukishinda tushinde kispoti au kufungwa kispoti. Nje ya hapo itakuwa ni majanga kwetu.
Nashauri mapema kwakuwa viongozi wa hii awamu wana maamuzi ya kustaajabisha sio ajabu ukashangaa matamko yasiyoeleweka na kutendeka mambo ambayo yatachafua ramani ya soka hapa nchini.
Nawasilisha.