Hongera mbunge Msigwa kwa kuirejesha Lipuli Fc ligi kuu (vpl)

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Kamwene wadimi na wanyalu wote wa hapo mshindo na viunga vyote vya mkoa wa Iringa.Niwapongeze kwa kuweza kuirejesha timu ya lipuli kwenye ligi kuu ya vodacom.

Nampongeza mwanamichezo DC Kasesela halikadhalika mdau wa michezo wa siku nyingi mbunge Peter Msigwa. Naelewa miaka ile ya 1984 kulikuwa na ushindani mkubwa wa African wonderers na lipuli na kwakuwa mbunge ulikuwa na meza ya mitumba palei miyomboni sina shaka ulikuwa shabiki wa A/wonderes.

Lakini leo ukiwa mbunge umeweza kusimama imara kuhakikisha timu pinzani imepanda daraja.Kumbe upinzani siyo uadui basi nikuombe upeleke falsafa hiyo huko SIASANI kwa ajili ya mustakabali mwema wa maendeleo ya mkoa wa Iringa na taifa kwa ujumla.

Hongereni sana wanyalu, tuwohungise!
 
Hongera Msingwa kwa uongozi bora Lipuli imerudi ligi kuu nilijua mchungaji ulikuwa unafunga na kuomba ili ije siku moja Iringa ipate timu hata kuona timu kubwa kama Mnyama Simba.Huku kwetu balaa Mh Mabula na dada yake timu zote mbili Mbao na Toto wala hawahangaiki nazo,tunazidi kumkumbuka WENJE wetu alikuwa anatupa hata pesa lakini haya majamaa MALUGUMYA kufa.Hata Alliance ilikuwa na mwelekeo mzuri yamemwachia Bwire pekee.Hongera Mtumishi Msingwa WATASHINDANA HAWATASHINDA.
 
Wanaaojua nani amefanya nini kufanikisha kwa hatua ya Lipuli ni wana Iringa wenyewe na Sika ikifika watasema nanyi. Dhania za kwenye Key-board/pad kwa ajili ya kutafutia ugali mtu hazisaidii.

Hongera TFF Iringa kwa mikakati mizuri kufanikisha tuwe na timu VPL mwakani.
 
Toeni siasa kwenye mpira. Msigwa ni nani? Wakati akina Sanga ndo wanapambana?
Mpira ni siasa ndugu yangu jiongeze na kama ulikuwa hujui Msigwa na Kasesela ni wanamichezo hasa.Unaijua historia ya Dar Young African (Yanga) wewe?
 
Msigwa amecheza namba ngapi?Bavicha tafuteni mtu wa kumuingiza kwenye football sio msigwa!Lini msigwa alionekana kwenye kiwanja japo cha draft achilia mbali football?.Ungesema mbowe ningewaelewa,Msigwa na football wapi na wapi.
Ile timu imepanda kwa nguvu za akina Mwakalebela na DC wa Iringa mjini
 
Maajabu haya, johnthebaptist ni Bavicha toka lini?
 
msigwa hana ubavu huo walioipandisha lipuli ni mzee Mvela, Mpangala, kasesera, na watu wote wa iringa
 
Vipi aliwaletaea kocha na kuwasajili wachezaji? Sijaelewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…