Nje ya Mada:
Wazazi ninawaasa jamani wazazi mnaotumia pombe kali keivant minyagi na mipombe mingine mibia mingano jamani wazazi chonde chonde wazazi pombe mnazokunywa msiwape watoto, kuna wazazi ni vichwa maji anataka familia yake yote wawe walevi wanywa pombe kwa hio anaanza kuwabugiza watoto pombe wakiwa watoto yaan mzazi unawanywesha watoto konyagi kweli?
Kweli mzazi watoto miaka 3-8 unapigisha nyagi kisa unataka nao waje kua wanywa pombe? Hii hapana kabisa, ipo hivi kuna mtoto hapa jirani anapitia changamoto ya kuugua kifua kisichoisha na usiku anapata tabu sana anapolala kifua kinambana vibaya mno pia ana tatizo la kukojoa, sasa ipo hivi huyu mtoto mzazi wake akiacha kumpigisha tungi hio hali inapungua hakojoi wala kifua hakibani ila kuna muda anaanza kumpigisha tungi sana sana konyagi chupa ndogo kubwa zimejaa kwenye fridge watoto kila wakifungua fridge wanazikuta na muda mwingine wanataka wanywe nae maana ananywea nyumbani sometimes kwa hio hali inakua mbaya mtoto analala kwa tabu sana unaweza kumhurumia kifua km kimepasuka eksozi anavyokoloma km kifua kimetoboka na anajikojolea mbaya zaidi ni mtoto wa miaka 8 tu, mzazi unamnyweshaji mtoto pombe kali? Mboni wazazi mnapenda kutesa watoto, mtoto na pombe kali wapi na wapi?
Huu ni ukatiri kwa watoto ningeomba Muheshimiwa Waziri na mamlaka zinazohusika na Watoto wajaribu kuwaasa wazazi wenye tabia km hizi waache mara moja kuna wazazi ni vichwa vibovu kabisa