Hongera ndugu zetu Waislamu. Wakristo tujifunze kwa hili kutoka kwa ndugu zetu

musicarlito

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2020
Posts
368
Reaction score
556
Wasalaam

Ndugu zetu waislamu wameanza mwezi mtukufu tangu tar 2...wanatimiza moja kati ya nguzo muhimu katika imani yao

Chanda chema huvishwa Pete...tangu wenzetu wameanza mwezi mtukufu,mwamko unauona ni mkubwa sana,watu wa kada mbalimbali,wakubwa kwa watoto,hata wale tunaowaweka kwenye makundi hatarishi kama wahuni,nao wakionekana kujitahidi...heko

Wakristo tunaanza Mfungo Jtano ya majivu ya wiki hii (hasa wakatoliki)
Ajabu muitikio wa kufunga huwa mdogo...huwa tunasingizia kufunga sio mpaka chakula kufunga ni matendo mema...sote tunajua kufunga ni namna tunayouadhibu mwili kwa kuukatalia vikali katika yale ambayo ungedai ni haki yake kama...vyakula,vinywaji,ashki,mazoea tunayoyapenda mfano burudani na michezo

Haya wakati mwingine yametusonga kiasi tumekosa tafakari kwa Mungu...mungo husaidia waliowahi kufunga mashahidi

Tusifunge pale tunapokuwa tumebananishwa na hali ngumu kama uchumi,maradhi na kadhia mbali mbali kubwa au ndogo

Tuweke uwe ni utaratibu wa kujiunganisha na Mungu...kumbuka pamoja na dini zetu...bado binadamu anatakiwa ku connect kwa namna ya pekee na Mungu wake

Hongera waislamu wakristo tuige na tubadilike

NB:Shetani akimghiribu mtu anampa na kisingizio kuhalalisha ughiribu wake...wako watakuja na hoja...ooh waislamu hawafungi wanabadili ratiba ya kula...owk basi ninyi mnajua kufunga...tuwaoneshe wenzetu

Ukweli funga yao ni nzuri na Mungu anaipokea
 
Tukisema ukweli bila kua na upendeleo, kipi katika masuala ya dini, wa kristo wamezidi hao wavaa kobazi (waislamu)

Kwenye mazishi wako excellent kwenye ndoa hata masikini muislamu ana oa, kwenye ibaada wana swali mara tano kwa siku, kwenye kutoa zakat masikini hujaa nyumba zao za ibaada kwa sababu wana jua wanatoa pesa na chakula, likija suala la kufunga mwezi wao hata muislamu mlevi mvuta bagi atafunga au atajificha,

je sisi wakuristo hao watu tuna wazidi nini kwenye dini? Au tuseme dini yao ina uhalisia na ukweli.
 
Hoja Mfu huwezi lazimisha au shawishi watu kufuata imani nyingine kisa kufunga. Kila mtu anafunga kwa imani yake.
 
Usisahau na kitimoto a.k.a mbuzi katoliki yetu imeanza kudoda..!!
 
Ieleweke kwamba, Kwaresma sio miongoni mwa shughuli za Kikristo, hilo ni tamko la Roman Catholic kwa mujibu wa utaratibu wao, hakuna popote kwenye Biblia utakutana na hicho kitu, waislamu wao, mwezi wa Ramadan ipo kwenye vitabu vyao tofauti na kwaresma. Kwa Wakristo hakuna siku au mwezi maalumu ya kufunga, wanao fungal siku 40 wapo wengi, siku 30 au 21 kama zinavyo onekana kwa manabii kama Daniel nk. Unafunga kulingana na hitaji lako au la kanisa au taifa, I can assure you, Wakristo funga yao ni ngumu kuliko hi ya Waislam au hi ya Kwaresma, kipindi cha uchaguzi specifically Wakristo huaga wana mlilia sana Mungu wao kuhusu amani, Wakatoliki pia wana kitu inaitwa NOVENA, waislamu hawawezi hizo funga za Wakristo, na hutasikia wakiomba excuse makazini kwao wala favor sijui ya bei za vyakula, wao na Mungu wao.
 
Nijuavyo ni kwamba wakristo huwa tunafunga ila si Kwa kujitangaza ndivyo biblia inavyotuambia
Mathayo 6:16-18 inasema "Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso; ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi".
 
Hujui maana ya mfungo wewe. Wala sio mkristo wewe, hivyo nyamaza
 
Mwili unaweza ukaongea vingine, roho ikaongea vingine. Kufunga kuunganishe mwili na roho. Ukifunga halafu hela uliyoiokoa unaiweka katika akiba uje uitumie baadaye, huko ni kubana matumizi. Unatakiwa ufunge ili utafakari hao wanaokosa siku zote huwa wanakuwa katika hali gani. Funga hata kupanda gari lako, kama ni karibu tembea, kama ni mbali panda usafiri wa umma. Hela utakayookoa ipeleke katika jamii zenye mahitaji, usiweke akiba uje kununulia simu au kitu cha ziada
 
Naunga mkono hoja yako.
 
Kufunga ni siri ya mtu,siyo mpaka kuku ajue kuwa umefunga huko ni kushinda njaa,waabudu wa kweli wanafunga zaidi ya wale wanaojitangaza na hutasikia wakijitapa kuwa wamefunga.
 
Ongezea na wanasali kwa utulivu hawana mambo ya sebene kama la yesu ibadani, wala kukata viuno ibadani, Wala mapaja nje, Wala kuchanganyika na wanawake, wanavaa stara. Nk
 
Hivi Biblia inasema nini kuhusu kufunga kabla ya Easter?
  • Matayo 6:16–18.
  • Matayo 9:14–15
  • Joel 2:12–13
 
Isaya 58:6-7 Je! Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira? Je! Siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako, na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? Umwonapo mtu aliye uchi, umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe?
 
Reactions: I M
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…