Hongera Rais kwa kuimarisha demokrasia nchini. Hakuna TV yoyote ingeruhusiwa kurusha mkutunano wa CHADEMA

deblabant

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2022
Posts
2,650
Reaction score
4,065
Kwa kweli Rais anastahili pongezi kuliokoa taifa hili. Kipindi kile upinzani ulikuwa kama uko ukimbizini. Jamaa alikuwa katili zodi ya Adolf Hitler.

Nakumbuka mpaka akina Boni Yai walivuliwa Umeya kibabe kisa wapo upinzani ili wasalende. Hata Mwita naye akavuliwa kibabe Umeya kisa yupo CHADEMA.

Kipindi kile ikitikea kuna tv au radio au blog yoyote ikirusha mikutano ya upinzani ama wamiliki wanatekwa au inafungiwa moja kwa moja.

Nakumbuka kulikuwa na mkutano wa CHADEMA kama wa leo pale Mlimani city, bwana mdogo Pplepole aliwapiga mkwara mzito Azam tv kurusha mkutano ule baada ya hapo wakapotea hewani.

Kwa kweli mama umeiokoa nchi hii. Hongera sana
 
Sasa hapo mama Anasifiwa nini?

Kwa sababu vyombo inabidi viwe huru hata hio tbc
 
na sasa maridhiano yanashuka kwa jamii hii falsafa ya mama inazidi kutupa mwanga chama cha mapinduzi ndio baba wa demakrasia ulimwenguni katika karne hii
 
Na mama ndio amewalipia Matangazo yt Kwenye vyombo vyote vya habariii🤪🤪🤪🤪
 
Hawa ndio wale wafu wa Mzee Kenyata.
 
Enzi za JK mambo yalikuwa hivi, ngosha colonialism ndo ilivurunda.
 
Wewe ni MJINGA,

Yaani Rais amekuwa mhariri, Mkurugenzi wa vyombo vya habari vyote, mmiliki wa vyombo vyote vya habari???

Watanzania tutaacha lini ujinga huu??

Hata hiyo TBC siyo Mali yake ni Mali ya umma inaendeshwa kwa kodi zetu!!!

Punguza UCHAWA 🤣🤣🤣🤣
 
Jpm yeye alizuia kabisa visiripoti issues zote za upinzani vikabaki vinamuimba yeye tu. Mama anajitahidi sana
 
Wewe ni chawa mpya au mzeefu ,tuanzie apo kwanza
 
Na mama ndio amewalipia Matangazo yt Kwenye vyombo vyote vya habariii🤪🤪🤪🤪
YAANI Hii Tanzania Ina Uchawa
Chama Kinalipa Pesa Kurusha Hayo Matangazo
Vituo Vya Television Vinafanya Biashara Vinapewa Pesa
 

🚮🚮🚮🚮 rubbish
Aisee
 
Samia mitano CCM daima
 
na sasa maridhiano yanashuka kwa jamii hii falsafa ya mama inazidi kutupa mwanga chama cha mapinduzi ndio baba wa demakrasia ulimwenguni katika karne hii
Chama cha fomu moja😂😂😂 Nimecheka vibaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…