Hongera Rais Magufuli, umeona mbali kwa kuanzisha Wizara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano

Hongera Rais Magufuli, umeona mbali kwa kuanzisha Wizara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano

dndagula

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2016
Posts
1,602
Reaction score
1,650
Katika zawadi nzuri aliyotupatia Rais na Serikali ya muhula huu wa awamu ya Tano ni kuanzisha wizara inayosimamia TEHAMA. Uchumi wa dunia na wa nchi yetu unabebwa na TEHAMA kutokana na sababu zifuatazo:

1. Mawasiliano ya kibiashara, kimalipo, ukusanyaji mapato, maduhuli,matangazo ya kibiashara, mahospitalini, mashuleni, utafiti, hali ya hewa,anga, majini, usalama wa raia nk sasa hivi ni ya kidigitali.

2. Kwa ujumla maisha yetu duniani yanaendeshwa na TEHAMA kuliko kitu kingine chochote.

3. Ushindani wa kiuwekezaji kikanda na kidunia unawezeshwa na teknolojia ya habari.

4 uendeshaji wa serikali na sekta binafsi ni TEHAMA.Tumeshuhudia e-governments na e -industrial and hotel managements.
Kwa msingi huo wizara hii itahitaji kuwa na uwajibikaji wa hali ya juu ili.

1.kulinda mahitaji ya walaji na watumiaji wa teknolojia ya habari

2. Nidhamu na usahihi wa teknolojia hii kwa mazingira yetu

3. Unafuu wa gharama za matumizi ya teknolojia hii

4.ufanisi

5. Uwekezaji wa Mkonga wa mawasiliano wenye kasi kubwa inayotakiwa kwa internet nk. Uliopo uendelee kusambazwa maeneo yasiyofikiwa. Watanzania zaidi ya milioni 15 wanatumia inteneti lakini pia zaidi ya milioni 30 wa simu za mikononi.

6. Kushirikiana na polisi nk Kupambana na makosa ya kimtandao kiufundi.

7. Elimu na kuzalisha wataalam wengi zaidi wa TEHAMA. Ikibidi hata kuanzisha Bodi ya ithbati au kitaaluma ya wana TEHAMA kama ilivyo kwa bodi za wahasibu, madaktari, walimu, mainjinia nk ili kudhibiti taaluma hii.

8. Iwepo program ya kufundisha TEHAMA kuanzia elimu ya msingi hadi chuo kikuu nk.

9. Kuanzisha mpango wa TEHAMA vijijni ili kuwafikishia huduma hii wananchi popote walipo. Teknolojia hii kwa sasa inaonekana kuwa ni muhimu sana kijijini kwa kupashana habari na mawasiliano ya haraka katika uzalishaji. Watu wengi wana simu za mikononi hata bibi wazee kabisa, walemavu nk.

10. Kuzidi kupunguza kodi na ushuru wa forodha kwenye vifaa vya TEHAMA.

Tunamtakia mema waziri Ndugulile kwa kupewa wizara hii nzito na matumaini ya watanzania wakati tukielekea uchumi wa juu. Kama ulivyosema DIJITALI ni uchumi na ni "software" ya maendeleo jadidi. Hongera waziri heri ya Mwaka Mpya.
 
Kwani haya hayakua tunayafanya kabla? Wizara imwanzishwa kudhibiti kwa karibu zaidi uhuru wa watu kuongea na kutoa maoni... na sio hizi hadithi zako
Thibitisha unayoyasema. Vinginevyo huna ushahidi nyamaza!
 
Weka namba ya simu ili tukupe uteuzi.
 
Hii wizara washirikiane na wizara ya fedha kuwezesha kufanya miamala haswa kuweza kupokea fedha kutoka payment gateway kama PayPal na zinginezo. Itawasaidia sana wajasiriamali
 
Sheria ya mtandao na mawasiliano na habari ipitiwe upya ili kuondoa vikwazo na ukiritimba kwa mwananchi kujitafutia habari ,teknolojia,maendeleo na fursa za kujikwamua kiuchumi.
 
Wizara hii ndiyo ile inayotaka wanaotumia Drone kupiga picha waende wakasomee? Je, ndiyo hii inayosema fundi simu wakasome wapewe cheti bila hivyo ni vishoka?
 
Katika zawadi nzuri aliyotupatia Rais na Serikali ya muhula huu wa awamu ya Tano ni kuanzisha wizara inayosimamia TEHAMA. Uchumi wa dunia na wa nchi yetu unabebwa na TEHAMA kutokana na sababu zifuatazo:

1. Mawasiliano ya kibiashara, kimalipo, ukusanyaji mapato, maduhuli,matangazo ya kibiashara, mahospitalini, mashuleni, utafiti, hali ya hewa,anga, majini, usalama wa raia nk sasa hivi ni ya kidigitali.

2. Kwa ujumla maisha yetu duniani yanaendeshwa na TEHAMA kuliko kitu kingine chochote.

3. Ushindani wa kiuwekezaji kikanda na kidunia unawezeshwa na teknolojia ya habari.

4 uendeshaji wa serikali na sekta binafsi ni TEHAMA.Tumeshuhudia e-governments na e -industrial and hotel managements.
Kwa msingi huo wizara hii itahitaji kuwa na uwajibikaji wa hali ya juu ili.

1.kulinda mahitaji ya walaji na watumiaji wa teknolojia ya habari

2. Nidhamu na usahihi wa teknolojia hii kwa mazingira yetu

3. Unafuu wa gharama za matumizi ya teknolojia hii

4.ufanisi

5. Uwekezaji wa Mkonga wa mawasiliano wenye kasi kubwa inayotakiwa kwa internet nk. Uliopo uendelee kusambazwa maeneo yasiyofikiwa. Watanzania zaidi ya milioni 15 wanatumia inteneti lakini pia zaidi ya milioni 30 wa simu za mikononi.

6. Kushirikiana na polisi nk Kupambana na makosa ya kimtandao kiufundi.

7. Elimu na kuzalisha wataalam wengi zaidi wa TEHAMA. Ikibidi hata kuanzisha Bodi ya ithbati au kitaaluma ya wana TEHAMA kama ilivyo kwa bodi za wahasibu, madaktari, walimu, mainjinia nk ili kudhibiti taaluma hii.

8. Iwepo program ya kufundisha TEHAMA kuanzia elimu ya msingi hadi chuo kikuu nk.

9. Kuanzisha mpango wa TEHAMA vijijni ili kuwafikishia huduma hii wananchi popote walipo. Teknolojia hii kwa sasa inaonekana kuwa ni muhimu sana kijijini kwa kupashana habari na mawasiliano ya haraka katika uzalishaji. Watu wengi wana simu za mikononi hata bibi wazee kabisa, walemavu nk.

10. Kuzidi kupunguza kodi na ushuru wa forodha kwenye vifaa vya TEHAMA.

Tunamtakia mema waziri Ndugulile kwa kupewa wizara hii nzito na matumaini ya watanzania wakati tukielekea uchumi wa juu. Kama ulivyosema DIJITALI ni uchumi na ni "software" ya maendeleo jadidi. Hongera waziri heri ya Mwaka Mpya.

Bado sana, tuliachwa ktk Mapinduzi ya mwanzo ya viwanda, hata haya Mapinduzi ya Nne ya Viwanda tayari tumesha achwa mbali boti ya Mapinduzi ya Nne ya Viwanda imetuacha pwani na tunaiona inatokomea mbali baharini na wale "masto-awei" wanjanja walioghamua fursa hii .

Hata mtizamo wa jinsi tunavyozungumzia TEHAMA kutusaidia kuleta mapinduzi ya viwanda inaonesha dhahiri tunaizungumzia kwa wepesi mno na hii inatokana na maono yetu ni mafupi hatuendi zaidi ya kuzungumzia kulipia bili , miamala ya fedha, uber taxi, kuoda chakula au keki toka kwa mama ntilie kwa kutumia simu-janja, kununua tiketi za usafiri n.k

Wakati wenzetu wanatumia TEHAMA kuunda ndege aeroplane kiwandani, kuyeyusha jiwe au mwamba ili kutengeneza kwa haraka injini ya chuma kuendesha viwanda, vyombo vya usafiri, vyombo vya tiba-afya, kurusha roketi za Mawasiliano na vifaa vita n.k

Na mbaya zaidi Mapinduzi ya Nne ya Viwanda vinahitaji kwenda na kubadilisha mfumo mzima wa maisha uwe unaishi mjini au kijijini. Sisi hata Mapinduzi ya Mwanzo ya Viwanda hatukuweza kubadilisha au kugusa wananchi walio wengi ambao wanaishi vijijini. Hii imepelekea "machinga" wengi kuzalishwa vijijini na kuhamia mijini wakati wale wa Dunia ya Kwanza Mapinduzi ya Mwanzo yaliwagusa wa vijijini na hata walipohamia mijini walikuta viwanda vya kuwapa ajira.
 

19 Sept 2017

The Fourth Industrial Revolution: Technology-Driven and Human-Centred


Advances in science and technology must serve all of humanity to its fullest potential. What can the private sector, civil society and public institutions do together today to ensure an inclusive outcome for the future? -
  • Marc R. Benioff, Chairman and Chief Executive Officer, Salesforce, USA
  • - Jay R. Inslee, Governor of Washington, USA -
  • Marianne Eve Jamme, Founder and Chief Executive Officer, SpotOne Global Solutions, United Kingdom; Young Global Leader -
  • Sunil Bharti Mittal, Chairman, Bharti Enterprises, India -
  • Johan Rockström, Executive Director, Stockholm Resilience Centre, Sweden
  • Chaired by - Gillian R. Tett, Managing Editor, US, Financial Times, USA
Source : World Economic Forum
 
Back
Top Bottom