Hongera Serikali ya CCM kwa ujenzi wa barabara zote za Mwananyamala, kura zetu mtazipata 2025

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Kwa niaba ya Wazawa wa mwananyamala nichukue fursa hii kuipongeza serikali ya CCM kwa ukarabati mkubwa wa barabara zote unaoendelea kuanzia Vijana hostel na mzunguko wote Komakoma, A nyamala, Manjunju, Kwa mama Zakaria Peace Kwa kopa, Magengeni, Hospitali na kurudi pale A nyamala kwa mzee Lutangilo Ng'ondya!

Mungu ni mwema wakati wote!
 
Vipi wazee wako huko kijijini wanasemaje kupanda kwa Bei ya mbolea,petrol, cement , tozo nk,au watakula barabala za mwananyamala?
Machame wazee hawana matatizo bwashee!
 
John wewe ni mkazi wa mwananyamala ipi, kwani nami jirani yako tujuane
 
Jambo la kheri
 
Baada ya barabara agawe na khanga za chama kila mtaa wa Mwananyamala
 
Vibaka wa uchaguzi wanapoanza kujipa matumaini kuelekea 2025.
 
Ukisema bara bara zote ina maana mwananyamala yote ina lami
Mbona mitaa ndani akiba Bank,ipole Street,mitaa ndani ya makoma hkuna lami

Ova
 
Kwahiyo ulitaka tuendelee kula vumbu kisa tu bibi zako wa huko maporini?
Hapa ni jijini lazima tupendelewe
Vipi wazee wako huko kijijini wanasemaje kupanda kwa Bei ya mbolea,petrol, cement , tozo nk,au watakula barabala za mwananyamala?
 
Waikumbuke na ya kuelekea mahakamani kutokea kwa dr. Mvungi. Mahakama nzuri kama money heist lakini barabara ina mti katikati.
 
Ukisema bara bara zote ina maana mwananyamala yote ina lami
Mbona mitaa ndani akiba Bank,ipole Street,mitaa ndani ya makoma hkuna lami

Ova
Bwashee muhimu ulikuwa ni huo mzunguko kwanza.

Halafu upande ule wa komakoma Kanisa Anglican barabara kibao zina lami!
 
Bwashee muhimu ulikuwa ni huo mzunguko kwanza.

Halafu upande ule wa komakoma Kanisa Anglican barabara kibao zina lami!
Mm kwangu mitaa ya garden lami ilipita
Ila baharia rubama analalamika mitaa yao upande ule mbona wanasahulika
Aise kwa diwani songoro lami itamfikia
Kule😂😂 buibui kushuka chini

Ova
 
Waambie watukumbuke na HUKU MPWAPWA NA KIBAKWE TUNAUMIA MIGONGO WENZAO NA HAYA MASHIMO!!
 
Mm kwangu mitaa ya garden lami ilipita
Ila baharia rubama analalamika mitaa yao upande ule mbona wanasahulika
Aise kwa diwani songoro lami itamfikia
Kule😂😂 buibui kushuka chini

Ova
Awamu inayokuja ndio mitaa ile ya Bui bui kwa mzee Kiaratu hadi Kambangwa .

Pia MK kwenda kuibukia Manyanya!

Bwashee karibu CCM
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…