Hongera timu ya watu Simba kwa mapato makubwa uwanja wa taifa

mpimamstaafu

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
4,445
Reaction score
4,707
Hakika Klabu ya Simba ni kipenzi cha Watu,pamoja na kuhamasisha Simba Day kwa siku 3,sherehe kufanyika siku ya kazi Watu wenye Simba yao wakaujaza Uwanja wa Taifa na kuingiza jumla ya Sh.380 Mil.huku Timu ya Wananchi YANGA pamoja na makelele mengi wakaingiza Sh.280 Mil.Watanzania Simba ina Watu sio Wananchi.
 
Jobless hoyeeeee
 
Hayo mamilioni ulikabidhiwa wewe ukayahesabu au umesikia tu?
 
Mtani mnakoelekea ndio mtafanya tuzidi kuamini ile kauli ya Rage (Mbumbumbu Fc) mana kila jambo kwenu ni habari. ๐Ÿ™ˆ

Wacha nigange ya Township Rollers Mtani. ๐Ÿšถโ€โ™‚๏ธ๐Ÿšถโ€โ™‚๏ธ
Mliingiza watu 48 elfu takwimu zetu umeziona hukooo?
Yani ningekuwa mpana ningejikata mara mbili ili tuujaze kabisa
 
wangekuwa jobless wangekuwa na hela za kiingilio ,ameingia mpaka PM,acha chuki mkuu Simba ni timu ya Watu
 
Mtani mnakoelekea ndio mtafanya tuzidi kuamini ile kauli ya Rage (Mbumbumbu Fc) mana kila jambo kwenu ni habari. ๐Ÿ™ˆ

Wacha nigange ya Township Rollers Mtani. ๐Ÿšถโ€โ™‚๏ธ๐Ÿšถโ€โ™‚๏ธ

Wananchi ndo first time lakini tumeshine balaa

Je tukifanya mara ya pili.....tuta-perfom wonders
 
Mkuu punguza Hasira Simba ni Big Club ,niliwaagiza TFF wahesabu
Kama kubwa mbona sponsorship deal zenu pesa ndogo? Jersey 600 m miaka miwili..Mo anaichafua Jersey kwa matangazo yake kwa 400m tu mwaka mmoja... Sportpesa tunajua Yanga wanapewa zaidi
Sasa Yanga Sportpesa 1.1B,Taifa gas 1B na GSM Jersey 1.3 B..jumla 3.4B..endeleeni kupiga kelele Yanga masikini
 
Mbona mnashindwa kuwalipa wachezaji mishahara yao
 
Afu bado mnatembeza bakuli,
IGA ufe, this is the next level
 
Lipeni mishahara Yondan ,Dante wanafamilia wakililia malipo yao mnawaona wabaya ,lipeni
 
Endelea kujidanganya ... GSM kachukua tenda ya utengenezaji wa jersey na vifaa kwakupitia lebo ya yanga mfano .. zitatoka kofia zenye lembo ya yanga t shiart saa za mikono.. nk so yanga imepewa B 1.3 ... uhlsport Dubai hawa wanatengeneza Jersey za simba tuu ... tena hiyo . 600 m sipesa ndugu ni Jersey zenye samani ya hilo pesa zikiuzwa wanagawana faida mtaji ni wa uhlsport .... kwaufupi .. alicho kuwa anakitaka manji nakumnyima Leo yanga wamempaa GSM kirahisi tu kisa njaa tu kumpa mamlaka GSM kutumia nembo ya yanga kwenye biashara yeye kawa yanga 1.3 B .... basi....
 
Wana nchi... Wenye nchi... Ccm ina wenyewe wana nchi[emoji100][emoji100][emoji100][emoji100][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Harafu wanayanga tumebarikiwa huwa hatuongei sana, ni vitendo tuu ndio manatumechukua ubingwa mara nyingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ