Uchaguzi 2020 Hongera Tundu Lissu, kazi umeimaliza

Uchaguzi 2020 Hongera Tundu Lissu, kazi umeimaliza

SN.BARRY

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2012
Posts
4,038
Reaction score
8,929
1. Umemuonyesha Magufuli na Ndugai ukuu wa Mungu. Umepona, umerudi na watanzania wote wameshuhudia kuwa Mungu ni mkuu sana.

2. Wale waliokupiga risasi, wakazuia usitibiwe, wakakunyima mshahara na kukuvua ubunge sasa wanatakiwa kutubu mbele za Mungu na mbele za watanzania.

3. Umemuonyesha Magufuli na waliokuwa wanamdanganya kuwa upinzani umekufa kuwa watanzania sio wajinga. Upinzani upo kwenye fikra za watu. Upinzani hauwezi kuondoka kwa maagizo kutoka juu au kwa kutumia polisi na TISS.

4. Umeweza kuzunguka mikoa kadhaa kutoa elimu ya uraia na umeona jinsi muitikio wa watu ulivyo mkubwa. CCM imechokwa.

5. NEC, Polisi na TISS hawatakutangaza kuwa umeshinda. Ila ukweli utabakia kuwa Magufuli hata akitumia mabavu bado atakuwa sio rais halali wa watanzania. Atakuwa rais halali wa NEC na Polisi ila sio watanzania.

6. Hata kama wakikuzuia kufanya kampeni kuanzia leo bado wataonekana wajinga na waovu. Watanzania wanataka haki na uhuru.

7. Kanda ya ziwa wamemuonyesha magufuli kuwa siasa chafu za ukabila hazitakiwi Tanzania huo ni ujumbe tosha. Kama ana akili timamu atabadilika.

NEC WATANGAZE AU WASIKUTANGAZE BADO UTABAKIA KUWA MSHINDI.
wale waliosema uzikwe ndani ya siku tatu bado hawaamini macho yao.
 
Yahya Jammeh wa Gambia aliondoka pamoja na syndicate yake yote ya roho mbaya mkuu.
Hao Tiss,Police, NEC hawataweza kushindana na nguvu ya wakati raia wakiamua.
Nina hakika Jwtz hawatajiingiza kwenye huu mchezo mchafu wa ccm coz ni taasisi imara na makini sana tunayojivunia mpaka sasa.
 
Yahya Jammeh wa Gambia aliondoka pamoja na syndicate yake yote ya roho mbaya mkuu.
Hao Tiss,Police, NEC hawataweza kushindana na nguvu ya wakati raia wakiamua.
Nina hakika Jwtz hawatajiingiza kwenye huu mchezo mchafu wa ccm coz ni taasisi imara na makini sana tunayojivunia mpaka sasa.
Dawa ni kuingia mtaani tukisubiri tume huru hakuna lolote.
 
1. Umemuonyesha Magufuli na Ndugai ukuu wa Mungu. Umepona, umerudi na watanzania wote wameshuhudia kuwa Mungu ni mkuu sana...

Ongeza na kwamba:-

1). Wakazuia asiombewe kana kwamba wanakaa kwenye call center ya Mungu!.

2). Wakazuia watu wasivae hata Tshirts zilizoandikwa "Tumwombee Lisu".

3). Wakakunyima mishahara ili kufanya familia yako na wewe mpotee kabisa wakasahau kwamba Mungu hulisha ndege wa angani na huvalisha maua ya kondeni.

Sasa:-

Tundu Lisu hakikisha una team ya watu wenye mahusiano sahihi na Mungu ili waendelee kukuombea katika kipindi hiki cha utimilifu wa Neno.
 
Magufuli na genge lake hawatakiwi . CCM imekwishagonga ukuta , ni bora wakakimbilia Msumbiji au Zimbabwe wakatuachia nchi yetu.

Wanajaribu kulazimisha vitu visivyolazimishika , ni UJINGA TUU NA KUZIDISHA UJINGA

Watu wamechoka kusifia mafisi haya , yakimbie tujenge nchi
 
Nilikuwa sijawahi kumuona Lissu ila juzi nilimuona kumbe jamaa ni mtu simpo sana ila ni mtu ambaye yuko in serious business na anaipenda kazi hapendi utani utani wa mademu kama yule wa upande wa pili, pia nilibahatika kucheza nae goma la Bob Marley One Love
 
Ongeza na kwamba:-

1). Wakazuia asiombewe kana kwamba wanakaa kwenye call center ya Mungu!.

2). Wakazuia watu wasivae hata Tshirts zilizoandikwa "Tumwombee Lisu".

3). Wakakunyima mishahara ili kufanya familia yako na wewe mpotee kabisa wakasahau kwamba Mungu hulisha ndege wa angani na huvalisha maua ya kondeni.

Sasa:-

Tundu Lisu hakikisha una team ya watu wenye mahusiano sahihi na Mungu ili waendelee kukuombea katika kipindi hiki cha utimilifu wa Neno.
Kweli mkuu haya mambo yanaumiza sana. Hawa mashetani ndio huwa wanaenda kanisani na kukaa siti za mbele. Aibu sana kwa kanisa la Tanzania.
 
Back
Top Bottom