Kuhusu hilo la kujiuza sio uchunguzi wa kina unatakiwa ufanywe kwa sababu ni kashfa mbaya sana.
Kwa uzoef nlionao japo sijafanya uchunguzi wa kina wadada weng wa dodoma hujifanya wanasoma udom.
Yan wanachukulia uanachuo km cheo au sifa kwao na machangudoa nao hujitambulisha km wanachuo ili wapate soko.
Pia hata wewe kwa akili yako unaweza kufikiria km je?
Mwanachuo anayepokea bum la 7500 kwa siku au hata asie nalo anaweza kujiuza kwa shl 500?
*Acha uzushi wako hapa.
Waliosema UDOM wanachuo wanajiuza mpaka kwa shilingi Elfu moja au mia tano ni wakuu wenu wa chuo, Viongozi wa Serikali ya wanafunzi, wahitimu wa mwaka huu na baadhi ya wanachuo wa UDOM tena kupitia vyombo vya habari(Tv, Radio, magazeti) hususani vya serikali.
*Kuhusu ''Boom'' kuwa 7500/= kwa siku sio issue kabisa, kwa sababu;
1/Sio wanachuo wote wanapata mkopo, hivyo kujiuza inaweza kuwa ndio mbadala.
2/Pamoja na kupata ''Boom'' bado mwanachuo ana mzigo mkubwa wa kulipa sehemu ya Ada.
3/Wanachuo wengi wanalalamika kuwa 7500/= wanayopata kama ''Boom'' ni ndogo sana hivyo haiwatoshi kabisa.
4/Kutokana na maisha ya anasa na starehe wanachuo wengi huwa wanaishiwa pesa mapema sana na hivyo wanaona kujiuza ndio suluhisho rahisi.
*Kuhusu 500/= kuwa ni pesa kidogo kwa mtu kama mwanachuo, bado si kweli.
Katika Uchumi thamani ya pesa inategemea nguvu ya soko(Supply and Demand) malaya yuko tayari kupigwa Chapchap kwa 500/= na watu 10 kwa siku ili akusanye shilingi 5000/= kwa usiku mmoja.
Lakini usisahau kuwa Simba akizidiwa hula hata majani.....