Hongera Ummy Mwalimu kwa Utendaji kazi wako usikivu wako

Hongera Ummy Mwalimu kwa Utendaji kazi wako usikivu wako

JAY THE SON

Member
Joined
Nov 26, 2017
Posts
43
Reaction score
33
1623734348907.png
Nianze kwa kukusalimu kwa salamu nzuri inayohamasisha ufanyaji kazi katika hali na juhudi kubwa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania".

Siandiki bandiko hili nikitarajia ujira wowote katika kuandika haya na wala siandiki hili kwa kuwa tunatokea Tanga tena mwahako bali naandika kama raia mwema ninayetambua na kuheshimu uchapakazi wako na ifikie mahali tutambue na kuwatia moyo viongozi wanaochapa kazi kwa moyo kwa maslahi mapana ya nchi yetu.

Utendaji kazi wako usikivu wako kasi yako katika kufika katika maeneo yenye changamoto yanazidi kukuongezea sifa za utandaji kazi ulianza vyema na kufanya kazi nzuri chini ya wizara ya afya, wizara ya ofisi ya makamu wa rais mazingira japo hukukaa sana na sasa wizara ya ofisi ya rais Tamisemi ninayo matumaini makubwa kuwa utafanya mambo makubwa na mazuri zaidi mungu akusimamie na kukutetea zaidi mie kama sehemu ya vijana wa tanga na mtanzania kwa ujumla kutojilaumu dhidi ya kura zetu tulizopiga kukuchagua wewe na viongozi wengine kazi iendelee na unayoyafanya yaendelee kwa viongozi wengine ukizingatia safari yako ni wazi bado ni ndefu katika kutumikia nchi yetu.

Zaidi ya yote wanna tanga mjini tunakuunga mkono tupo pamoja nawe na tutakuombea zaidi chapa kazi mbegu unayoioanda leo itkuja kumea na kuzaa matunda mema kwa vizazi vijavyo na vyaleo.

Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
 
Ummy Mwalimu achana na Mitandao hii na Kujipigia ' Promo ' kwa ID's tofauti tofauti hapa Jamvini hebu fanya Kazi ya nchi katika Dhamana uliyopewa na Rais Samia, kwani utasababisha sasa tunaojua ' Siri ' zako na ' Aliyeondoka ' tufunguke nazo zaidi hapa. Fanyia Kazi huu Ushauri wangu tafadhali.
 
Ndiyo maana Tanga mmejaa mafukara haswa, hapo utakuta waarabu na wachaga ndiyo wanamiliki pesa nyie mnacheza bao pekee sababu ya ujinga wenu.
 
Ummy Mwalimu achana na Mitandao hii na Kujipigia ' Promo ' kwa ID's tofauti tofauti hapa Jamvini hebu fanya Kazi ya nchi katika Dhamana uliyopewa na Rais Samia, kwani utasababisha sasa tunaojua ' Siri ' zako na ' Aliyeondoka ' tufunguke nazo zaidi hapa. Fanyia Kazi huu Ushauri wangu tafadhali.
Sawa, umemtuliza mtu Kama namuona vile
 
Hongera sasa dada Ummy. To me you are the best lady leader ever! This is since Mwendazake regime. Una utu sana, hata mwendazake aliposema anafuatilia message zako WhatsApp hukujali bali uliendelea kuchapa kazi, hasa kipindi cha Corona.

Naomba hiyo picha upande wako wa kulia iondoke, siipendi hata kuiona. Tumeumizwa sana na uwepo wake. ndugu zetu wamekufa na wengine wapo magerezani eti walimkashfu yeye, kwa kubambikizwa tu ili watu wapate cheo.
 
Ummy Mwalimu achana na Mitandao hii na Kujipigia ' Promo ' kwa ID's tofauti tofauti hapa Jamvini hebu fanya Kazi ya nchi katika Dhamana uliyopewa na Rais Samia, kwani utasababisha sasa tunaojua ' Siri ' zako na ' Aliyeondoka ' tufunguke nazo zaidi hapa. Fanyia Kazi huu Ushauri wangu tafadhali.
Ummy anafanya kazi kweli na anajituma sana. Kazi aliyofanya ya kuruhusu uhamisho na kuweka ratiba maalum basi nampigia Salute na nitamuheshimu sana maana wengi walikuwa wahanga na issue ya uhamisho. Uhamisho ni haki ya mtu lakini ilikuwa lazima utoe pesa chini ya Engineer Nyamhanga. MNYONGE MNYONGENI LKN HAKI YAKE MPENI.
 
Back
Top Bottom