Betterhalf
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 2,882
- 2,560
Habari za jioni wadau.
Naipenda Simba SC na kwa yaliyojiri wiki hii, nitaendelea kuipenda zaidi na zaidi.
Kwa wafuatiliaji wa michezo, hususan soka, hakuna asiyejua ukongwe wa klabu ya Simba.
Iliasisiwa 1936 wakati huo ikiitwa Sunderland.
Hii inaifanya iwe na umri wa miaka 81.Kwa kipindi chote hicho, imeweza kufanya mengi mazuri ingawa haijafikia mafanikio kama ya TP Mazembe,Al Ahly, Esperance, Enyimba,Asante Kotoko na nyinginezo za mfano huo.
Lakini, ninaona nuru mpya kupitia hatua ya maamuzi ya kubadilisha mfumo wa uendeshaji kutoka ule uliozoeleka kwenda mfumo wa hisa.
Sina utaalam sana,lakini naamini timu itakuwa kibiashara zaidi na hivyo kujiuza zaidi kwenye masoko ya ndani na nje ya hisa.
Hali hii, itasababisha timu kujiendesha kwa faida,kulipa wachezaji na waajiriwa wengine kwa wakati, uhakika na haraka pasipo na ubabaishaji.
Rai yangu kwa wana Simba wote, kama tulivyoridhia muundo mpya,pia tuyapokee mabadiliko kwa kushiriki kuyasema mazuri ya mfumo mpya huku tukiyafanyia kazi mapungufu kwa njia sahihi badala ya vurugu.
Pia, naamini muundo mpya lazima utaziba mirija ya ujanja ujanja ambayo iliwanufaisha baadhi huku timu ikipoteza mwelekeo; kwa hali hiyo tujitahidi kutafuta njia nyingine za kujikimu badala ya kuiandama klabu na viongozi au watendaji watakaobeba dhamana ya kutuvusha.
Nitumie fursa hii kuwapongeza wanachama,mashabiki,wapenzi,viongozi,TFF,BMT, Wizara na serikali kwa ujumla kwa kubariki mabadiliko haya chanya kwa maendeleo ya michezo Tanzania, Afrika mashariki na Afrika kwa ujumla.
Nitumie makala hii pia,kuziomba timu nyingine ziige haya ili kuwatendea haki wanamichezo wanaziunga mkono timu zetu.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Simba SC.
Wakatabahu,
Nawasilisha.
The Great Gatsby
Naipenda Simba SC na kwa yaliyojiri wiki hii, nitaendelea kuipenda zaidi na zaidi.
Kwa wafuatiliaji wa michezo, hususan soka, hakuna asiyejua ukongwe wa klabu ya Simba.
Iliasisiwa 1936 wakati huo ikiitwa Sunderland.
Hii inaifanya iwe na umri wa miaka 81.Kwa kipindi chote hicho, imeweza kufanya mengi mazuri ingawa haijafikia mafanikio kama ya TP Mazembe,Al Ahly, Esperance, Enyimba,Asante Kotoko na nyinginezo za mfano huo.
Lakini, ninaona nuru mpya kupitia hatua ya maamuzi ya kubadilisha mfumo wa uendeshaji kutoka ule uliozoeleka kwenda mfumo wa hisa.
Sina utaalam sana,lakini naamini timu itakuwa kibiashara zaidi na hivyo kujiuza zaidi kwenye masoko ya ndani na nje ya hisa.
Hali hii, itasababisha timu kujiendesha kwa faida,kulipa wachezaji na waajiriwa wengine kwa wakati, uhakika na haraka pasipo na ubabaishaji.
Rai yangu kwa wana Simba wote, kama tulivyoridhia muundo mpya,pia tuyapokee mabadiliko kwa kushiriki kuyasema mazuri ya mfumo mpya huku tukiyafanyia kazi mapungufu kwa njia sahihi badala ya vurugu.
Pia, naamini muundo mpya lazima utaziba mirija ya ujanja ujanja ambayo iliwanufaisha baadhi huku timu ikipoteza mwelekeo; kwa hali hiyo tujitahidi kutafuta njia nyingine za kujikimu badala ya kuiandama klabu na viongozi au watendaji watakaobeba dhamana ya kutuvusha.
Nitumie fursa hii kuwapongeza wanachama,mashabiki,wapenzi,viongozi,TFF,BMT, Wizara na serikali kwa ujumla kwa kubariki mabadiliko haya chanya kwa maendeleo ya michezo Tanzania, Afrika mashariki na Afrika kwa ujumla.
Nitumie makala hii pia,kuziomba timu nyingine ziige haya ili kuwatendea haki wanamichezo wanaziunga mkono timu zetu.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Simba SC.
Wakatabahu,
Nawasilisha.
The Great Gatsby