Hongera Waziri Mkuu kwa kuagiza mmiliki wa jengo akamatwe, tamaa imemponza

Hongera Waziri Mkuu kwa kuagiza mmiliki wa jengo akamatwe, tamaa imemponza

Leonel Ateba Mbinda

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2023
Posts
644
Reaction score
2,695
Naishukuru sana serikali kwa kuchukua hatua dhidi ya mmiliki wa jengo, naomba kuisaidia Jeshi la Polisi kuendelea kusaka taarifa zaidi za tukio hilo lakini kinachosemwa pale kariakoo na watu mbalimbali kisipuuzwe.

Mimi nimesikia watu wakisema kuwa mmiliki wa jengo hilo alifanya tamaa, kwamba alipoona gorofa limejaa wateja na hakuna pa kupangisha alianza mipango ya kujenga stoo nyingine za kuhifadhia mizigo underground, kwahiyo wakati wanachimba chini ili kujenga jengo lingine underground mafundi wakawa wanachimba hadi kwenye nguzo, hivyo nguzo zilishake kutokana na uchimbaji usiokuwa na maarifa, madhara yake ndio haya tunayoyaona leo.

Kazi kubwa imefanywa na serikali kuokoa maisha ya watu lakini uzembe wa aina hii usivumiliwe, tuendelee kuokoa maisha ya watu, hawa wajinga wajinga wengine wanaoleta siasa katika maisha ya watu tuwaache waendelee na ujinga wao.

Nakupongeza sana RC Chalamila. Waziri Lukuvi kwa kazi kubwa mnayoendelea kuifanya, hii sio siasa hapa kama Taifa tumepata msiba mkubwa, uchunguzi uendelee kufanyika na taarifa za wadau mbalimbali ziendelee kufanyiwa kazi, vyombo vyetu vya usalama naviamini viko kazini na damu za waliopoteza maisha hazitoenda hivi hivi.

Yote kwa Yote namshukuru Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa maelekezo ya kiserikali ili kutoa faraja kwa wananchi wote waliopoteza ndugu zao.

Mwisho, kesho ni Do or Die uwanja wa TAIFA, LAZIMA TWENDE MOROCCO.
 
Wabongo tuna laana. Haya ''maigizo''. mbona hufanywa kila linapotokea tukio kama hili? Kuna tofauti kati ya kuagiza na kuigiza.
 
mnashukuru shukuru tu, Huyo mmiliki alipata wapi vibali vya kuanza huo ujenzi wa underground?

Hao maafsa waliotoa hivyo vibali wako wapi?

Je huyo injinia wa majengo aliyeanza kujenga bila tahadhari yuko wapi?
 
Siku zote mbona hakuagiza tokea tukio litokee ndio anaagiza sasa!

GOD BLESS TANGANYIKA
 
Wewe ni fara sana. Kipindi linajengwa Kwa tamaa na mmiliki serikali ilikuwa wapi?
Serikali ni pamoja na hao mafundi waliokuwa wanachakachua, wapangaji wa juu mpaka majirani.

Mazoea ya kupuuzia mambo bila kuyaripoti matokeo ndio hayo, tunavuna tulichopanda...
 
Tamaa mbaya. Ukwepaji wa vibali vya ujenzi na wataalamu wa ujenzi matokeo yake ndio hayo. Tunapotaka kuendeleza ujenzi kwa jengo lililopo tafuta wataalamu wakushauri kabla ya kufanya maamuzi yoyote. N.b mimi ni kanda ya ziwa hivyo L na r msifikirie sana.
 
Andikaa hapo mwenye jengo kashapepea ilaa yule aliyechangishaa pesa Kwenye mtandao anaenda kupewa kesi ya utakatishaji pesaa
FB_IMG_1731931623196.jpg
 
Sijaona sababu ya hizo pongezi zako. Maana hilo jambo liko wazi tu. Na serikali haitakiwi kuishia kwa mmiliki pekee! Badala yake mpaka maafisa ardhi na mipango miji nao wanatakiwa kuwajibishwa.
 
Sijaona sababu ya hizo pongezi zako. Maana hilo jambo liko wazi tu. Na serikali haitakiwi kuishia kwa mmiliki pekee! Badala yake mpaka maafisa ardhi na mipango miji nao wanatakiwa kuwajibishwa.
Mark my words!
Deep down... Mmiliki wa jengo utakuta ana ubia na ccm.
 
Back
Top Bottom