Hosea Chamba (mwanasheria wa Simba) unaharibu image ya timu.

Hosea Chamba (mwanasheria wa Simba) unaharibu image ya timu.

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Naandika nikijua wasio na ABC ya sheria wanitupia mishale lakini sijali. Lakini Kwa mara ya Kwanza tunashuhudia Migogoro ya usajili ya mwaka 1994 ikirejea 2024 Kwa timu ya Simba kuwa na mwanasheria anayetafuta Kwanza maslahi binafsi kabla ya maslahi ya timu. Migogoro ya Mohamed Mwameja na Kenneth Mkapa kusaini huku na huku imepata copy 2024 kwenye mkataba wa Kagoma. Lakini pia Mikataba ya Valentino Mashaka na Awesu Awesu ni Sawa na kumtuma Mtoto akaibe kwao Bahati mbaya alikamatwa unajifanya hujui, muulizeni mwenyewe.
Migogoro ya Aina hii ilizoeleka Yanga Hadi likawa tusi kwao na kutakiwa kwenda kujifunza Simba. Lakini safari hii mwalimu ndo kafanya wonders Kwa 4in1.
Kisheria haya ni madhaifu Makubwa ya mwanasheria. Ni wakati wa viongozi wa Simba kuangalia Mtu mwingine makini wa kufanya kazi hiyo adhimu badala ya huyu anayewapaka mafuta Kwa mgongo wa chupa huku akijua timu inaumia. Nachelea kusema kuna percent anapokea si bure.
 
Kabisa sijajua why...hivi vitu vimejitokeza kwa sasa...au atakua utopwile huyo..
 
Mtoa post umesema ukweli kuwa hujui Sheria na sio kosa lako. Hao ni wachezaji halali wa Simba. Mwanasheria wa Simba hausiki na mgogoro wowote hapo!
 
Mtoa post umesema ukweli kuwa hujui Sheria na sio kosa lako. Hao ni wachezaji halali wa Simba. Mwanasheria wa Simba hausiki na mgogoro wowote hapo!
Mwanasheria hana shida ila mmesahau kwenye usajili mme mrudisha Magori ambaye ni Version ya zamani kabisa katika mpira wa kisasa.
Yeye Magori Bado ana amini katika mfumo wa kizamani wa timu kubwa Simba na Yanga kubebwa na Tff katika migogoro ya wachezaji wa timu ndogo.

Kwa namna Simba ilivyo ingia kwenye migogoro ya kupora wachezaji wenye mikataba na kuwachezesha inakiwa watandikwe rungu na Tff ni mambo ambayo kwasasa ni Ngumu kutokea uko Duniani.
 
Nadhani Kagoma na Velentino suala lao limeisha. Leo mmoja alikuwa benchi mwingine kacheza. Imeisha hiyo.

Simba ilikuwa aggressive sana safari hii kwenye kuchukua wachezaji, migogoro ilikuwa haiepukiki. Nia ilikuwa ni kuondokana na ile hali ya misimu ya karibuni ya kumtamani mchezaji na kumkosa, mbaya zaidi anaenda upande wa pili. Naona ya Mpanzu tu ndiyo ilishindikana.
 
Nadhani kila mtu abaki kwenye nyanja yake aachane na mambo asiyoyajua. Mtoa mada nadhani ni kinyozi aachane na Sheria ajikite kukata nywele akishindwa hata nyasi.
Yan mkataba wa mchezaji na timu yake kabla iwe na kipengele endapo timu hiyo timu ikishuka daraja mchezaji anakuwa huru (automatic contract termination) halafu timu nyingine imsajili halafu uje kulaumu timu iliyomsajili 😂😂 endelea kunyoa mkuu
 
Mwanasheria hana shida ila mmesahau kwenye usajili mme mrudisha Magori ambaye ni Version ya zamani kabisa katika mpira wa kisasa.
Yeye Magori Bado ana amini katika mfumo wa kizamani wa timu kubwa Simba na Yanga kubebwa na Tff katika migogoro ya wachezaji wa timu ndogo.

Kwa namna Simba ilivyo ingia kwenye migogoro ya kupora wachezaji wenye mikataba na kuwachezesha inakiwa watandikwe rungu na Tff ni mambo ambayo kwasasa ni Ngumu kutokea uko Duniani.
Dogo unaelewa unazungumza? Kwa taarifa yako, siku hizi ujanja ujanja wa zamani haupo! ITC za wachezaji zipo TFF kihalali zikiwatambua ni wachezaji halali wa Simba. Na ndio maana HAKUNA. Narudia tena, HAKUNA mahali Simba inatuhumiwa kiusajili mchezaji bila kufuata utaratibu. Ni kesi aidha dhidi ya timu walizotoka au dhidi ya mchezaji husika. Simba na Magori wanahusikaje hapo Dogo?
 
Back
Top Bottom