Hospitali 10 kujengwa Unguja, Pemba

Hospitali 10 kujengwa Unguja, Pemba

Ferruccio Lamborghini

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2020
Posts
1,667
Reaction score
2,595

Hospitali 10 kujengwa Unguja, Pemba

HOSPITALI 10 zitajengwa Unguja na Pemba ndani ya kipindi cha miezi sita, hatua itakayoboresha kwa kiwango kikubwa huduma za afya Zanzibar.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Wazee, Nassor Ahmed Mazrui wakati akiwapa taarifa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuhusu ujenzi wa hospitali hizo ambazo zitajengwa kwa fedha za mkopo wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kwa ajili ya kupambana na ugonjwa wa Covid-19.

Alisema tayari mchakato wa ujenzi wa hospitali hizo umekamilika, ambapo jumla ya kampuni nne zimeshinda zabuni ya ujenzi. “Hospitali hizo zitajengwa kwa kuzingatia kiwango cha ubora wa hali ya juu na pia kusimamiwa na Wakala wa Bodi ya Majengo iliyopo chini ya Serikali ya Zanzibar.”
‘’Nataka niwajulishe wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwamba, ujenzi wa hospitali 10 Unguja na Pemba utatekelezwa na fedha za ahueni ya ugonjwa wa Covid-19 ambazo ni mkopo wa IMF na sasa tunasubiri kuanza kazi katika kipindi cha miezi sita,’’ alisema.

Alizitaja kampuni zitakazofanya kazi ya ujenzi wa hospitali hizo ni Rans ambayo itajenga Hospitali ya Mwera, Pongwe, kampuni ya China ya CRJE East Afrika ambayo itajenga Hospitali za Chumbuni, Magogoni na Mbuzini.
Alisema kampuni iliyopewa jukumu la kujenga Hospitali ya Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja ni Quality Building Contractor, wakati kampuni ya WCEC itajenga Hospitali ya Pangatupu Mkoa wa Kaskazini Unguja.
’Hospitali zitakazojengwa tutahakikisha zinafikia kiwango na ubora wa hali ya juu ili ziweze kudumu muda mrefu kwa ajili ya kizazi kijacho ambapo tutakuwa tukifuatilia ujenzi kwa karibu sana,’’ alisema.
 
Unaongeza hospitali wakat hizi zilizopo zinapumulia machine, hospitali ya serikali haina hata kifaa cha kupimia pressure( shinikizo la damu) ukienda unaambiwa ukapime private sikuambii hivyo vipimo vingine!!! Ilitakiwa hizo pesa ziboreshe hizi zilizopo kwanza, hospitali sio majengo tu Bali Ni vifaa, dawa pamoja Na wahudumu wenyewe.
 
Unaongeza hospitali wakat hizi zilizopo zinapumulia machine, hospitali ya serikali haina hata kifaa cha kupimia pressure( shinikizo la damu) ukienda unaambiwa ukapime private sikuambii hivyo vipimo vingine!!! Ilitakiwa hizo pesa ziboreshe hizi zilizopo kwanza, hospitali sio majengo tu Bali Ni vifaa, dawa pamoja Na wahudumu wenyewe.
Mpaka atakapo maliza muda wake Hangaya, nako huko Zenji kutakuwa KI-CHATOCHATO!
 
Mkopo huo ni upi, ule wa raisi wao aliowapa au mama yao keshachukua mwingine kwa jina la KUUNGANA?
 
Yaani ni ZANZIBAR TU, akiwa huku bara anahamasisha tu lakini kujenga hajengi.

Kaskazini ndio kabisaa.
 
Back
Top Bottom