DOKEZO Hospitali ya Ekenywa inalazimisha wagonjwa wa NHIF kununua dawa hospitalini kwao

DOKEZO Hospitali ya Ekenywa inalazimisha wagonjwa wa NHIF kununua dawa hospitalini kwao

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kipindi hiki nilikuwa sijasajili bima ya mtoto NHIF.

ila kuna mkuu amelalamika hapankwamba hawapokei NHIF kwa baadhi ya dawa.
Mbona hilo lipo hospital zote hata za serikali aisee, especially dawa za kisukari baadhi unakuta haziwi covered na NHIF. Hata baadhi ya vipimo mtu analazimika kulipia
 
Mbona hilo lipo hospital zote hata za serikali aisee, especially dawa za kisukari baadhi unakuta haziwi covered na NHIF. Hata baadhi ya vipimo mtu analazimika kulipia
Ni kwl lakini hao ikenywa hawataki kukuandikia dawa ukanunuwe inje,

Wanataka lazima ununuwe kwao ambapo dawa ni ghali sn.
Kama hutaki kununuwa basi dawa huandikiwi..
 
Ni kwl lakini hao ikenywa hawataki kukuandikia dawa ukanunuwe inje,

Wanataka lazima ununuwe kwao ambapo dawa ni ghali sn.
Kama hutaki kununuwa basi dawa huandikiwi..
Mkuu,kwa mfumo wa sasa hospital zote zilizo funga mifumo hufanya mawasiliano kwa njia ya mtandao..mgonjwa hatembei na kadi...mwezi wa tisa mwaka huu nilikuwa na mtoto Benjamin mkapa.

Tulimuona daktari wa watoto,aliandika vipimo kupitia computer akavisend Maabara..Kule maabara tulipimwa,majibu walirudisha kwa Daktari kupitia mfumo (computer)..tulirud kwa Daktari,kupitia majibu aliyo tumiwa kutoka Maabara,aliandika dawa kupitia mfumo kwenda dirisha la dawa..ndiko tulipokea dawa.

Nilishuhudia mtu akiomba aandikiwe dawa pale dirisha la dawa,maana yeye alikuwa anatumia cash,hivyo aliishiwa. Aliambiwa aende halafu atarudi,,ila atunze ile namba ya utambulisho na siku aliyo hudhuria hospital.

Tusipende kulaumu private wakati hata serikalini hicho kitu kinafanyika.
 
Hospital za masikio Dar hii zipo kibao
Ni kwl lakini unaweza ukatoka gongo la mboto ukafata hospital tegeta?
Hata kama zipo nyingi ukaribu wa hospital lazima uzingatiwe pia..
 
Hao jamaa ni noma sana aisee,,

Nilimpeleka mtoto wangu kuangaliwa masikio.
Gharama zao ni balaa na nusu.

Kuandikisha kadi 20000/
Kumwona dokta 40000/

Sikio la mtoto niligjaramia 120,000.,

Kutokana na kukamua wanaichi amenunuwa nyumba zote zilizomzunguka..

Iwekwe sheria kali kwa watu ambao hawataki kupokea wagonjwa wa wanachama na NHIF

Tiba ni gharama
 
Kwanza mfamasia haruhusiwi kuandika dawa, hiyo ni kazi ya daktari.

Pili nhif wana mabango kila kona ni haki yako kupiga ulalamikie hilo swala.

Tatu hospitali kubwa zote nhif wameweka wawakilishi wao hivyo unapaswa kuomba kuonana nao.

Nne nhif wana package zaidi ya nane lazima ufahama huduma ambayo kifurushi chako kinapata.
 
Hii nchi sasa kila.mmoja anajimegea keki yake
 
Katika afya kuna huduma kama 3 hivi
1. Ni medical consultation (Ushauri wa kitabubu)...huyu anakusikiliza, anaweza kukuandikia vipimo vya kufanya na unaenda kufanya kwenye maabara yoyote iliyoidhinishwa na unarudisha vipimo. Anakupa ushauri na kukuandikia dawa ambazo unaenda kununua duka lolote la dawa ambalo limeidhinishwa. Utamlipa consultation fees mnamalizana.
2. Huduma ya maabara/vipimo. Huyu anapokea wagonjwa kutoka kwa consultants na kufanya vipimo then ana mrudishia majibu consultant. Unamlipa gharama za vipimo mnamalizana.
3. Huduma ya kuuza dawa a.k.a pharmacy. Huyu hupokea prescriptions (List ya dawa), iliyoandaliwa na consultant. Unamlipa gharama za dawa mnamalizana.
4. Kuna hospitali ambazo hutoa huduma zote hapo juu. Mara nyingi kwa sababu huduma zote hutolewa pamoja anaweza kuwa ameweka punguzo kwenye huduma fulani fulani na mwisho wa siku inakuwa rahisi kuliko kama ungeenda sehemu tatu tofauti, kama nilivyoeleza hapo juu. Pia kwa sababu huduma zote ziko sehemu moja ni inarahisisha huduma kwa mgonjwa na kupunguza usumbufu wa kwenda na kurudi.

Kuhusu bei ya dawa, inategemea na source (chanzo) cha dawa zake. Dawa aina moja zinaweza kuwa na bei tofauti kulingana na brand. Panadol ya Kenya na panadol ya Tanzania bei yake si sawa. Hivyo inategemea na brand anazotumia. Je ni kutoka Ulaya, marekani, India, china, Tanzania au Kenya.

Pia kwa nini hakuandikii dawa ukanunue sehemu nyingine. Ni kwasababu huduma yote anaitoa kama package moja. Ni sawa sawa na hotel ambayo wana uza chakula kwa style ya Bufee...huwezi kwenda kuchukua sehemu ya chakula halafu ukataka ulipe kidogo.

Lakini pia kama utawaeleza kuwa wewe unataka consultation peke yake watakupa gharama.za consultation peke yake ambazo mara nyingi zitakuwa juu kuliko gharama ya package nzima.

Lakini pia hawatoi orodha ya dawa kwa sababu mbali mbali kama kutunza siri za wagonjwa na kulinda afya ya mgonjwa. Hospital zina jukumu la kutunza siri za wagonjwa. Pia akikuandikia dawa ukaondoka nayo unaweza kutumia vibaya. Labda ukanunua dawa nusu dose usipone au ukanunua dawa zisizo na kiwango usipone, au ukapata tatizo lolote la kiafya wakaingia matatizoni.
Ahsante.
 
Hospitali ya Ekenywa wanalazimisha wateja wa Bima hasa NHIF kununua dawa kwao.

Ukienda kutibiwa wanakwambia hii dawa haipo kwenye bima; ukienda Kwa mfamasia ukimuomba akuandikie jina la dawa hawataki. Ukirudi kwa Daktari pia naye anakwambia ukipata pesa njoo uchukue na dawa zao ni ghali sana tofauti na ghar
 
Back
Top Bottom