Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kulalamikia gharama wanazotozwa wahitaji wa huduma ya Ambulance katika Hospitali ya Mkoa Shinyanga, kumsoma Mdau bonyeza hapa ~ Gharama za “Ambulance” Shinyanga ni mateso kwetu walalahoi Uongozi wa Hospitali umetoa ufafanuzi.
TAARIFA INAYOSAMBAA MTANDAONI DHIDI YA HUDUMA YA GARI LA WAGONJWA (AMBULANCE) HOSPITALI YA RUFAA YA MКОА SHINYANGA
Kumekuwa na taarifa inayosambaa mtandaoni ya Juni 29, 2024 ikisomeka kwa kichwa cha habari "Gharama za Ambulance Hospitali ya Mkoa ni mateso kwa walala hoi".
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Shinyanga inapenda kuujulisha umma kuwa taarifa hiyo haina ukweli kwa kile kilichochapishwa.
Katika muongozo wa huduma ya rufani kunatoka sehemu A kwenda B, unaelekeza mgonjwa kuchangia gharama za mafuta na siyo kulipia gharama za gari.
Pili, Hospitali huwezesha kutoa gari, dereva na mtaalamu ambaye hujumuika ili kutoa huduma kwa mgonjwa wakati wa safari husika, kwa maana pande zote mbili zinachangia (Cost Sharing).
Hivyo, si kweli kuwa pindi inapotokea kuna wagonjwa (zaidi ya mmoja) kila mmoja anachangishwa shilingi 250,000/= kama ilivyochapishwa na Mtandao wa Jamii Forum, na badala yake pande mbili huchangia kwa ajili ya gharama za mafuta (lita 65) za kwenda na kurudi ambapo hata gharama ya 250,000/= haijawahi kufika, na risiti hukabidhiwa kwa mteja.
Aidha, katika kujali hali ya mteja kulingana na hali yake kiuchumi, Hospitali huwezesha gharama zote kama mgonjwa hajiwezi, lakini pia kuna ambao huchangia kiasi kidogo kulingana na hali zao za kiuchumi.
Uongozi wa Hospitali unawahakikishia wananchi wa Mkoa wa Shinyanga na watanzania kwa ujumla, utaendelea kusimamia huduma bora ambazo zinatolewa na kufuata miongozo yote iliyowekwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya.
Vilevile, uongozi wa Hospitali umesikitishwa na Habari hiyo kwani inaleta taswira hasi na nia ovu ambayo inachafua taswira ya Hospitali na Serikali kwa ujumla.
Tunatoa rai kwa vyombo vya habari kuhakikisha vinafika fuata miongozo na miiko inayo simamia taaluma husika kwa ajili ya kupata taarifa rasmi (balanced story) ili kufikisha taarifa sahihi kwa umma.
George M. Mganga AFISA HABARI
TAARIFA INAYOSAMBAA MTANDAONI DHIDI YA HUDUMA YA GARI LA WAGONJWA (AMBULANCE) HOSPITALI YA RUFAA YA MКОА SHINYANGA
Kumekuwa na taarifa inayosambaa mtandaoni ya Juni 29, 2024 ikisomeka kwa kichwa cha habari "Gharama za Ambulance Hospitali ya Mkoa ni mateso kwa walala hoi".
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Shinyanga inapenda kuujulisha umma kuwa taarifa hiyo haina ukweli kwa kile kilichochapishwa.
Katika muongozo wa huduma ya rufani kunatoka sehemu A kwenda B, unaelekeza mgonjwa kuchangia gharama za mafuta na siyo kulipia gharama za gari.
Pili, Hospitali huwezesha kutoa gari, dereva na mtaalamu ambaye hujumuika ili kutoa huduma kwa mgonjwa wakati wa safari husika, kwa maana pande zote mbili zinachangia (Cost Sharing).
Hivyo, si kweli kuwa pindi inapotokea kuna wagonjwa (zaidi ya mmoja) kila mmoja anachangishwa shilingi 250,000/= kama ilivyochapishwa na Mtandao wa Jamii Forum, na badala yake pande mbili huchangia kwa ajili ya gharama za mafuta (lita 65) za kwenda na kurudi ambapo hata gharama ya 250,000/= haijawahi kufika, na risiti hukabidhiwa kwa mteja.
Aidha, katika kujali hali ya mteja kulingana na hali yake kiuchumi, Hospitali huwezesha gharama zote kama mgonjwa hajiwezi, lakini pia kuna ambao huchangia kiasi kidogo kulingana na hali zao za kiuchumi.
Uongozi wa Hospitali unawahakikishia wananchi wa Mkoa wa Shinyanga na watanzania kwa ujumla, utaendelea kusimamia huduma bora ambazo zinatolewa na kufuata miongozo yote iliyowekwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya.
Vilevile, uongozi wa Hospitali umesikitishwa na Habari hiyo kwani inaleta taswira hasi na nia ovu ambayo inachafua taswira ya Hospitali na Serikali kwa ujumla.
Tunatoa rai kwa vyombo vya habari kuhakikisha vinafika fuata miongozo na miiko inayo simamia taaluma husika kwa ajili ya kupata taarifa rasmi (balanced story) ili kufikisha taarifa sahihi kwa umma.
George M. Mganga AFISA HABARI