Hospitali ya Taifa Muhimbili yatoa ufafanuzi hoja ya Mdau kuhusu "Huduma zake ni janga kwa Wagonjwa"

 Hospitali ya Taifa Muhimbili yatoa ufafanuzi hoja ya Mdau kuhusu "Huduma zake ni janga kwa Wagonjwa"

imagine, upo kwenye familia, mkaamua mnunue kitendea kazi, mkakipata kwa juhudi za kila mmoja. au mmepata msaada. hivi, mkiamua kukitumia bila kuchajiana mtakula hasara gani? MRN, citiscan, exray, ultrasound etc mkizinunua au kupewa msaada, kwanini mnalipisha hela kubwaaa? MNR ni zaidi ya milioni wakati ilinunuliwa na pesa za kodi zetu. mtapungukiwa nini siku moja mtu aende hospitali asikie ultrasound bure, MRN bure, kumwona daktari bure kwa sababu ni mali za umma wa watanzania, ni mali zetu, na watanzania wenyewe ndio sisi. mtapungukiwa nini? au ninyi ndio wapenda kuchangishachangisha mtu akipata kitu bila kuchangia mnaumia kweli kweli.
MRN ni nini? Au unamaanisha MRI?
 
Umeandika vitu viwili;
1. Rushwa ,ufisadi na wizi wa Kodi za wananchi
i.e. nakubaliana Hilo endapo vitendo hivyo vitakomeshwa pesa nyingi sana itaokolewa na itasaidia katika upatikanaji wa huduma Bora kwa gharama nafuu au Bure kabisa kama ilivyokuwa enzi za utawala wa awamu ya kwanza.

2. Umeandika ulipoishi ughaibuni kama mmataifa mlipata huduma.za afya Bure hapa Mkuu naomba tutofautishe nchi za ughaibuni na zetu huku Dunia ya tatu huko ughaibuni wao wanajitosheleza na bajeti zao kwa 100% wakati huku kwetu bado bajeti zetu na ukusanyaji WA Kodi ni 40% to 60% vyanzo vyetu vya mapato vimegota,sio rahisi Tena tukawa na uwezo wa kutoa huduma Bure mpaka tutakapomesha wizi wa pesa za Kodi ,kuongeza vyanzo vya mapato na wananchi tukawa na.moyo wa kuchangia Kodi na ushuru kama.watu wa ughaibuni Walivyozoea.
Ukiona mtu mmoja ana bilioni 100 alizoiba serikalini, au njia haramu, jua amewanyima na kuwakwamisha watu zaidi ya 1000 fursa za elimu, ajira, maji, umeme, makazi nk. kwa mgao angalau wa milioni 100 kwa hao watu 1000. Kinyume chake anasifiwa mtu mmoja aliyejilimbikizia mali bila kujali wengine wameathirika kiwango gani.
 
Mkuu sekta ya afya ni Pana sana Ina matibabu,Kinga na tafiti vyote vinahitaji pesa tukitaka huduma za Bure haiwezekani ikawa Bure labda iwe huduma zitolewe kwa bei nafuu sana. Naipongeza. hospital ya kisarawe iliyopo mkoani Pwani huduma pale zinatolewa ni za kibingwa kwa wananchi wengi wa mkoa wa Pwani wengi kutoka manerumango, chole,vikumbulu,Malui ni maskini kweli kweli lakini wanada ikiwa kupata matibabu kwa gharama nafuu sana.

Tunaposema matibabu yanaendana na Kinga na tafiti nani atagharamia hizo kinga na tafiti au tukae tukiwategemea wafadhili .

Hiyo mitambo inaharabika pesa ya service itoke Tena serikalini hapana ,inabidi tukubali matibabu yatolewe kwa kulipia kiasi sio hicho kopimo unaambiwa laki SITA operation unaambiwa milioni na nusu ,kitanda elfu hamsini hapana Kwa hospitali za serikali hizo ni bei za hospital binafsi ambazo hazipati msaada wowote kutoka serikalini.
kama za bure hakuna, ziwepo za bei nafuu. na swali ni je, kwani unagarimia kitu gani kwenye mashine ambayo tumenunua sisi wenyewe kwa kodi zetu, au unacharge umeme? kwa sababu kama ni wafanyakazi wapo umeshaajiri, umewaletea mashine waifanyie kazi na hata isipokuwepo watafanya tu kazi na mshahara wataupata uleule. kwanini basi hata vipimo viwe bure, ili mtu akijua tatizo umwambie sasa akajipange kununua dawa (tukijua dawa umejumua kiwandani ila mashine haujajumua), akili ya kawaida kabisa isiyohitaji kwenda shule. lipisha watu kile ulichojumua kufanyia biashara kama vile dawa, ila mashine ambayo tumenunua kupima kujua ugonjwa ili utuungishe dawa inakuwaje unacharge? na hapohapo serikali iwe inatoa pesa nyingi tu na kuwalipa mishahara toka kwenye mfuko mwengine (kama ndio hivyo).
 
Baada ya Wanachama wa JamiiForums.com kuandika hoja zinazoitaja Hospitali ya Muhimbili - Mlonganzila kuwa na gharama kubwa na changamoto nyingine za kiutendaji, taasisi hiyo imetoa ufafanuzi. Kusoka hoja za Wadau bofya hapa chini:

~ DOKEZO: Serikali iimulike hospitali ya Mloganzila, Huduma zake ni janga kwa wagonjwa na ndugu wanaouguza pale
~ Gharama za Kujifungua Hospital ta Taifa Muhimbili MNH (Mloganzila) ni kufuru
UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ILIYOCHAPISHWA NA MTANDAO WA JAMIIFORUMS KUHUSU HUDUMA ZA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI-MLOGANZILA

DAR ES SALAAM: NOVEMBA 22, 2024
Mtandao wa JamiiForums umechapisha taarifa yenye kichwa cha habari "Serikali limulike Hospitali ya Mloganzila, huduma zake ni janga kwa wagonjwa na ndugu wanaouguza." Kutokana na taarifa hiyo, Uongozi wa Hospitali unapenda kutoa ufafanuzi ufuatao;

1. Wagonjwa 20 hadi 25 kufariki kwa siku
Miaka ya hivi karibuni hadi Novemba 21, 2024, idadi ya wagonjwa wanaoonwa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeongozeka kutoka wagonjwa wa nje 400 hadi 1,000 kwa siku na idadi ya wagonjwa waliolazwa wodini wakati wote imeongezeka kutoka 200 hadi 400 kwa siku. Hii ni kutokana na uboreshaji mkubwa wa mifumo na huduma uliofanywa hospitalini hapo na hatimaye kuvutia wananchi wengi kuitumia hospitali hiyo.

Idadi ya wagonjwa wanaofariki kwa siku hospitalini hapo kutokana na sababu mbalimbali ni kati ya wanne (4) hadi sita (6) kati ya wagonjwa 400 waliolazwa na siyo 20 hadi 25 kwa siku kama ilivyoelezwa katika taarifa iliyochapishwa na JamiiForums.

2. Kutoa taarifa za mgonjwa
Ni kinyume na maadili ya kitabibu kwa mtoa huduma kutoa taarifa za mgonjwa bila ridhaa yake na kwa wale ambao hawajiwezi taarifa hutolewa kwa ndugu aliyeandikishwa au kupewa idhini ya kupokea taarifa hizo (next of kin). Ndugu wengine wanaopenda kufahamu taarifa za mgonjwa wanazipata kutoka kwa mgonjwa mwenyewe au ndugu aliyeandikishwa endapo watapenda kufanya hivyo. Tutaendelea kusimamia jambo hili.

3. Gharama za matibabu kuwa juu
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila inapokea na kuhudumia makundi manne ya wagojwa ambayo ni wagonjwa wa bima, wanaolipa fedha taslimu, wagonjwa wa rufaa wanaochangia huduma na wagonjwa wa msamaha. Mwaka wa fedha 2023/2024, Hospitali imetoa huduma kwa njia ya msamaha zenye thamani ya TZS. 3.9 Bil na kwa robo mwaka wa fedha 2024/2025 huduma zenye thamani ya TZS. 970 Mil zimetolewa kwa wananchi wasiokuwa na uwezo.

Ikumbukwe kuwa, Hospitali hii ni ngazi ya nne (ngazi ya juu) ya utoaji huduma nchini, hivyo teknolojia ya huduma za uchunguzi na matibabu imebalidika kutoka za kawaida kwenda kwenye ngazi za ubingwa bobezi ili kumpa mgonjwa matibabu stahiki. Endapo kuna mgonjwa ana changamoto ya malipo utaratibu wa hospitali uko wazi kupitia Huduma za Ustawi wa Jamii.

4. Kauli za Watoa Huduma
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeendelea kutekeleza azma ya Serikali ya utoaji huduma bora kwa wananchi. Kauli zisizo na staha kutoka kwa watoa huduma zimepungua kwa kiasi kikubwa. Uongozi wa Hospitali hauvimilii kauli za namna hii. Tumelipokea jambo hili, tutaendelea kulifanyia kazi,

Aminiel Buberwa Aligaesha
MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMΜΑ


Kumbe ni kweli kujifungua ni 1.4 million....!?

Wamama walitakiwa kujifungua Bure Nchi nzima....!
 
Gharama ni kubwa na hazieleweki achen kujibu kisiasa, mnamuandikia mgonjwa bill akiuliza vitu alivyotumia hamna majibu
Hasa kitengo cha dressing Ni majanga matupu!
 
Baada ya Wanachama wa JamiiForums.com kuandika hoja zinazoitaja Hospitali ya Muhimbili - Mlonganzila kuwa na gharama kubwa na changamoto nyingine za kiutendaji, taasisi hiyo imetoa ufafanuzi. Kusoka hoja za Wadau bofya hapa chini:

~ DOKEZO: Serikali iimulike hospitali ya Mloganzila, Huduma zake ni janga kwa wagonjwa na ndugu wanaouguza pale
~ Gharama za Kujifungua Hospital ta Taifa Muhimbili MNH (Mloganzila) ni kufuru
UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ILIYOCHAPISHWA NA MTANDAO WA JAMIIFORUMS KUHUSU HUDUMA ZA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI-MLOGANZILA

DAR ES SALAAM: NOVEMBA 22, 2024
Mtandao wa JamiiForums umechapisha taarifa yenye kichwa cha habari "Serikali limulike Hospitali ya Mloganzila, huduma zake ni janga kwa wagonjwa na ndugu wanaouguza." Kutokana na taarifa hiyo, Uongozi wa Hospitali unapenda kutoa ufafanuzi ufuatao;

1. Wagonjwa 20 hadi 25 kufariki kwa siku
Miaka ya hivi karibuni hadi Novemba 21, 2024, idadi ya wagonjwa wanaoonwa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeongozeka kutoka wagonjwa wa nje 400 hadi 1,000 kwa siku na idadi ya wagonjwa waliolazwa wodini wakati wote imeongezeka kutoka 200 hadi 400 kwa siku. Hii ni kutokana na uboreshaji mkubwa wa mifumo na huduma uliofanywa hospitalini hapo na hatimaye kuvutia wananchi wengi kuitumia hospitali hiyo.

Idadi ya wagonjwa wanaofariki kwa siku hospitalini hapo kutokana na sababu mbalimbali ni kati ya wanne (4) hadi sita (6) kati ya wagonjwa 400 waliolazwa na siyo 20 hadi 25 kwa siku kama ilivyoelezwa katika taarifa iliyochapishwa na JamiiForums.

2. Kutoa taarifa za mgonjwa
Ni kinyume na maadili ya kitabibu kwa mtoa huduma kutoa taarifa za mgonjwa bila ridhaa yake na kwa wale ambao hawajiwezi taarifa hutolewa kwa ndugu aliyeandikishwa au kupewa idhini ya kupokea taarifa hizo (next of kin). Ndugu wengine wanaopenda kufahamu taarifa za mgonjwa wanazipata kutoka kwa mgonjwa mwenyewe au ndugu aliyeandikishwa endapo watapenda kufanya hivyo. Tutaendelea kusimamia jambo hili.

3. Gharama za matibabu kuwa juu
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila inapokea na kuhudumia makundi manne ya wagojwa ambayo ni wagonjwa wa bima, wanaolipa fedha taslimu, wagonjwa wa rufaa wanaochangia huduma na wagonjwa wa msamaha. Mwaka wa fedha 2023/2024, Hospitali imetoa huduma kwa njia ya msamaha zenye thamani ya TZS. 3.9 Bil na kwa robo mwaka wa fedha 2024/2025 huduma zenye thamani ya TZS. 970 Mil zimetolewa kwa wananchi wasiokuwa na uwezo.

Ikumbukwe kuwa, Hospitali hii ni ngazi ya nne (ngazi ya juu) ya utoaji huduma nchini, hivyo teknolojia ya huduma za uchunguzi na matibabu imebalidika kutoka za kawaida kwenda kwenye ngazi za ubingwa bobezi ili kumpa mgonjwa matibabu stahiki. Endapo kuna mgonjwa ana changamoto ya malipo utaratibu wa hospitali uko wazi kupitia Huduma za Ustawi wa Jamii.

4. Kauli za Watoa Huduma
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeendelea kutekeleza azma ya Serikali ya utoaji huduma bora kwa wananchi. Kauli zisizo na staha kutoka kwa watoa huduma zimepungua kwa kiasi kikubwa. Uongozi wa Hospitali hauvimilii kauli za namna hii. Tumelipokea jambo hili, tutaendelea kulifanyia kazi,

Aminiel Buberwa Aligaesha
MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMΜΑ


Kwahiyo ikiwa ngazi ya nne, hata vitanda vinaacha kuwa vya kupumzikia, vinageuka vya guest houses
 
Kuna baadhi ya vifaa vya wagonjwa Huwa wanadai hawana! Utatao hela vinunuliwe kumbe vipo! Hutapata risiti kamwe!
Pale ni rushwa rushwa rushwa!
 
kitu ambacho huwa sikielewi kwenye hospitali za serikali ni kwamba, LABDA KAMA HAWAPOKEI FUNGU LA KUENDESHEA HOSPITALI TOLA SERIKALINI. nijibuni maswali haya;

1. hospitali hizi za serikali, zinajiendesha? au zinaendeshwa kwa kodi/bajeti ambayo ni kodi yetu. kama jibu siyo, kwanini?

2. serikali huwa inanunua mitambo mara kwa mara. mfano; mtambo wa MRN, xray na mingine, na vipimo vingine. mitambo hiyo huwa inanunuliwa kwa pesa zinazotokana na kodi za wananchi au na pesa zinazotozwa hospitali?

3. kama jibu namba 2 litakuwa vinanunuliwa kwa pesa za kodi, wanapata hasara gani wakiamua kupima watu bure badala ya kuwalipisha? mashine umepewa na serikali haujanunua wewe au umepewa msaada, unao wafanyakazi wa kila siku uliowaajiri wa kuziendesha, umeme zinatumia wa kawaida hata usipozitumia bili inakuja hat akuongezeka itakuwa kidogo sana, kama mashine hizo ni zetu sisi watanzania, KINACHOWAFANYA MSIPIME WATU BURE NI NINI? mngepata hasara gani? au mna shetani wa kulipisha watu msipolipisha mtu akapata huduma bure mnajisikia vibaya sana? si mali yetu sote, hamjanunua, au mmenunua kwa pesa za kodi zetu, pimeni watu bure, wengi wanakufa kwa kukosa huduma ambazo kodi zao zimenunua vifaa mnavyotumia.

4. serikali, inashindwa nini, kwa pesa hizo samia anabukia kwenye masafari yaliyojaa wasanii wasio na faida yeyote kwa nchi, wanashindwa nini kununua vitendea kazi mahospitalini ili ibaki kwa madaktari kuvitumia kwa watu bure. mnashindwa nini? safari mbili za samia zinanunua MRN moja. hata hizi za mkoani zina garama sana. pesa wanazotumbua na kuiba wangeweza kununua mashine nyingi, na kwa sababu ni za kwetu? tutumie bure, na wafanyakazi tunao tayari hawatalipwa ziada kwa kuendesha mashine za vipimo.

5. mnajisikiaje mtu kwenda hospitali ya umma leo hii, analipia hata ultrasound? au mnataka watu wawe wanakufa tu.
SGR na Air Tanzania si zimrnunuliwa kwa kodi zetu, mbona tunalips nauli ?

unajus X ray au CT scan inahitaji umeme kiasi gani kutoa mionzi au unabwatuka
 
JF inapenyeza sana, naweza sema wanaichukulia serious kuliko twitter x.. kaz nzur mods.
 
da
SGR na Air Tanzania si zimrnunuliwa kwa kodi zetu, mbona tunalips nauli ?

unajus X ray au CT scan inahitaji umeme kiasi gani kutoa mionzi au unabwatuka
hauisaidii jamii kuja hapa kutuuliza sisi tusio madaktari umeme kiasi gani unatumika kwenye xray na CT scan au MRI. na siamini kama serikali inayolipia taifa stars milioni 700, inayotumbua pesa kwa misafari na wizi kibao, itashindwa kulipa umeme. pia, tunatofautiana sana ufahamu mtu kuja kufananisha hospitali na SGR, tafuta mfano mwingine ili ustahili kujadiliana JF chief.
 
Huu mtandao nilikuwa nauchukulia poa Sana kuna siku nilitoa hoja yangu na ikatolewa ufafanuzi na mamlaka ndipo nilipohuheshimu jamii forum safi sana
Baada ya Wanachama wa JamiiForums.com kuandika hoja zinazoitaja Hospitali ya Muhimbili - Mlonganzila kuwa na gharama kubwa na changamoto nyingine za kiutendaji, taasisi hiyo imetoa ufafanuzi. Kusoka hoja za Wadau bofya hapa chini:

~ DOKEZO: Serikali iimulike hospitali ya Mloganzila, Huduma zake ni janga kwa wagonjwa na ndugu wanaouguza pale

~ Gharama za Kujifungua Hospital ta Taifa Muhimbili MNH (Mloganzila) ni kufuru

View attachment 3158867
View attachment 3159477

UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ILIYOCHAPISHWA NA MTANDAO WA JAMIIFORUMS KUHUSU HUDUMA ZA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI-MLOGANZILA

DAR ES SALAAM: NOVEMBA 22, 2024
Mtandao wa JamiiForums umechapisha taarifa yenye kichwa cha habari "Serikali limulike Hospitali ya Mloganzila, huduma zake ni janga kwa wagonjwa na ndugu wanaouguza." Kutokana na taarifa hiyo, Uongozi wa Hospitali unapenda kutoa ufafanuzi ufuatao;

1. Wagonjwa 20 hadi 25 kufariki kwa siku
Miaka ya hivi karibuni hadi Novemba 21, 2024, idadi ya wagonjwa wanaoonwa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeongozeka kutoka wagonjwa wa nje 400 hadi 1,000 kwa siku na idadi ya wagonjwa waliolazwa wodini wakati wote imeongezeka kutoka 200 hadi 400 kwa siku. Hii ni kutokana na uboreshaji mkubwa wa mifumo na huduma uliofanywa hospitalini hapo na hatimaye kuvutia wananchi wengi kuitumia hospitali hiyo.

Idadi ya wagonjwa wanaofariki kwa siku hospitalini hapo kutokana na sababu mbalimbali ni kati ya wanne (4) hadi sita (6) kati ya wagonjwa 400 waliolazwa na siyo 20 hadi 25 kwa siku kama ilivyoelezwa katika taarifa iliyochapishwa na JamiiForums.

2. Kutoa taarifa za mgonjwa
Ni kinyume na maadili ya kitabibu kwa mtoa huduma kutoa taarifa za mgonjwa bila ridhaa yake na kwa wale ambao hawajiwezi taarifa hutolewa kwa ndugu aliyeandikishwa au kupewa idhini ya kupokea taarifa hizo (next of kin). Ndugu wengine wanaopenda kufahamu taarifa za mgonjwa wanazipata kutoka kwa mgonjwa mwenyewe au ndugu aliyeandikishwa endapo watapenda kufanya hivyo. Tutaendelea kusimamia jambo hili.

3. Gharama za matibabu kuwa juu
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila inapokea na kuhudumia makundi manne ya wagojwa ambayo ni wagonjwa wa bima, wanaolipa fedha taslimu, wagonjwa wa rufaa wanaochangia huduma na wagonjwa wa msamaha. Mwaka wa fedha 2023/2024, Hospitali imetoa huduma kwa njia ya msamaha zenye thamani ya TZS. 3.9 Bil na kwa robo mwaka wa fedha 2024/2025 huduma zenye thamani ya TZS. 970 Mil zimetolewa kwa wananchi wasiokuwa na uwezo.

Ikumbukwe kuwa, Hospitali hii ni ngazi ya nne (ngazi ya juu) ya utoaji huduma nchini, hivyo teknolojia ya huduma za uchunguzi na matibabu imebalidika kutoka za kawaida kwenda kwenye ngazi za ubingwa bobezi ili kumpa mgonjwa matibabu stahiki. Endapo kuna mgonjwa ana changamoto ya malipo utaratibu wa hospitali uko wazi kupitia Huduma za Ustawi wa Jamii.

4. Kauli za Watoa Huduma
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeendelea kutekeleza azma ya Serikali ya utoaji huduma bora kwa wananchi. Kauli zisizo na staha kutoka kwa watoa huduma zimepungua kwa kiasi kikubwa. Uongozi wa Hospitali hauvimilii kauli za namna hii. Tumelipokea jambo hili, tutaendelea kulifanyia kazi,

Aminiel Buberwa Aligaesha
MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMΜΑ
 
Back
Top Bottom