Hot story

Hot story

Hapa Eddy ndio kafikia mwisho naona
 
Mwenye nayo yoyote atume jamani hamna tuzo humu so hakuna ulazima wa kua na single source
 
*****SORY MADAM*****(31)
AGE.........................................................
...........18+
WRITER......................................................
......EDDAZARIA G.MSUL
WALIKE NA RAFIKI ZAKO KULIKE HII
PAGE.ASANTE
ILIPOISHIA
Emmy akanikaribisha kwenye sehemu anayo ishi
ambayo yenye vitu vingi vya dhamani ya hali ya
juu.Taratibu Emmy akaanza kuvua nguo zake
moja baada ya nyingine na kunifanya nibaki
nikiwa nimemshangaa kwani sikujua ana maana
gani na imekuwaje amevua nguo mbele yangu na
kubakiwa na chupi wakati mimi na yeye hatuna
mahusiano ya namna yoyote
ENDELEA
Emmy akachukua taulo na kujifunga kisha
akaingia bafuni na kuniacha mimi nikiwa
nimekaa kwenye sofa nikiyatadhimini mazingira
ya ndani kwake.Baada ya muda kidogo Emmy
akatoka bafuni
“Umeshindwa hata kuwasha Tv?”
“Ahaa hakuna tatizo sana”
“Ok ngoja nivae nguo tuelekee hospitalini
ukamuone mama”
“Sawa”
“Ila unajua wodi aliyo lazwa?”
“Hapana siijui”
“Ok basi tutajua huko huko”
Emmy akaingia ndani kwake na akatoka akiwa
amevalia mavazi mazuri kiasi kwamba tama za
mapenzi zikaanza kunitawala na kujikuta
nikimtazama Emmy kwa macho ya matamanio
“Eddy twende zetu”
“Mmmmm”
“Twende zetu mbon unanishangaa?”
“Ahaa hakuna kitu”
Nikanyanyuka na nikatangulia kutoka nje ila
kutokana na baridi kali ikanilazimu kumuomba
Emmy koti na akarudi ndani na kunichukulia koti
lake kubwa na sote tukaingia kwenye Lifti na
kushuka chini gorofani.
“Twnde huku kwenye maegesho ya magari”
Tukafika sehemu yenye maegesho ya magari
mengi na Emmy akafungua gari moja na
kuniomba niingie.Safari ikaanza huku kila mmoja
akiwa kimya ndani ya gari ila Emmy akaamua
kuvunja ukimya
“Hivi Tanzania wewe unafanya kazi?”
“Mimi ni mwanafunzi wa A leve bado”
“Ohh kumbe unasoma?”
“Ndio”
“Kombi gani?”
“PCB”
“Mungu wangu PCB wewe....Mbona unaonekana
kama HKL?”
“Hahaa PCB halisi...Aafu mbona ndege leo
imetua kwenye uwanja wa Maputo international
airport imekuwaje kutokana tumetua
Mozambique?”
“Ndege ilipata itilafu kwa watu kama sisi tunao
jua ndio tumegundua hilo ila ukiwa ni mgeni
huwezi kujua kama ndege imeshindwa kuendelea
na safari”
“Sasa si wangetulipa fidia kwa kwa abiria
inakuwaje ndege inakuwa haina uwezo wa
kumaliza msafara wake?”
“Mimi niliamua tuondoke kutokana wewe
umeseme unahitaji kumuona mama yako ila kwa
walio baki wakisubiria ndege kutengenezwa
watakuwa wamelipwa fidia na kama siku
ukiondoka utakwenda kupanda ndege uwanja wa
kimataifa wa Cape town”
“Sawa”
Safari ya kwenda hospitalini haikuchukua muda
sana hii nikutokana na wingi wa barabara nyingi
zinazo punguza msongamano wa magari.Tukafia
hospitalini na moja kwa maja Emmy akaenda
kwenye katabu kinacho onyesha orodha ya
wagonjwa waliopo hapa hospitalini na nikamtajia
jina la mama kishha akatumi kama dakika tano
kulitafuta na akalipata
“Kumbe mama yako ni waziri?”
“Ndio”
“Twende ukamuone”
“Moja kwa moja tukealekea kwenye chumba
alicho lazwa mama na kabla hatujaingia
nikamkuta askari mmoja akiwa amesimama nje
ya chumba alicho lazwa mama
“Hamuruhusiwi kuingia humu ndani nyinyi ni
kina nani na munahitaji nini?”
“Mimi naitwa Dokta Emmy Samson na
mfanyakazi wa hii hospitali”
“Naomba kitambulisho chako”
Emmy akatoa kitambulisho chake na kumpa
askari aliye simama mlangoni na akakisoma kwa
muda kisha akamrushu Emmy kuingia ndani na
mimi nikataka kuingia ndani ila akanizuia kuingia
“Na wewe ni nani?”
“Mimi ni mtoto wa huyo mama huko ndani?”
“Mbona hatuna maelezo ya aina yoyote
kuhusiana kama mgonjwa ana mtoto?”
“Mimi ni mwanaye unadhani nitafunga safari
kutoka Tanzania hadi hapa nije kujipendekeza
kwa mama yangu?”
Nilizungumza kwa hasira kiasi kwamba watu
walipo karibu na eneo la mlango wa kuingia
kwenye chumba alicho lazwa wakaanza
kunishangaa
“Eddy kuwa mpole ngoja nikamuone mama”
“Kijana ninakuoma usimame mbali na hili enoa la
sivyo nitakuitia walinzi waje wakutoe”
“Eddy tafadhali nakuomba uwe mpole
nitazungumza na mama na utamuona tu”
Nijaitahidi kutulia hasira zangu na kusimama
pembeni kidogo na chumba alicho lazwa mama
huku sura yangu ni kiwa nimeikunja.Emmy
akaingia ndani ya chumba na baada ya muda
akatoka na kumnong’oneza askari kisha kwa
ishara Emmy akaniita na nikanyanyuka kwa
haraka hadi sehemu waliyo simama kisha askari
akaniruhusu kuingia ndani.Macho yangu
yakatizamana na mama ambaye kwa muonekana
hali yake sio nzuri sana japo nimemkuta
amaekaa kitako kwa mwendo wa haraka
nikamfwata mama na kumkumbatia huku
machozi yakinimwagika
Tukabaki tumekumbatiana na mama ndani ya
dakika kadhaa kisha nikamuachia na kuiona sura
yake ikiwa imelowana kwa machozi mengi,Mama
akanishika mashavuni na kunibusu kwenye paji la
uso huku akinichunguza sehemu mbali mbali za
mwili mwangu na kunifanya nizidi kububujikwa
na machozi
“Eddy ni nini kilicho kupata mwanagu?”
Mama aliniuliza huku akiwa anabubujikwa na
machozi kiasi kwamba nikashindwa kulijibu swali
lake hadi ndani ya dakika tano ndipo nikaanza
kumuadisia kila kitu kilicho tokea na jinsi baba
alivyo nifanyia kiasi kwamb hadi ninamalizia
nikamshuhudia Emmy akiinama chini huku
akitokwa na machozi.
“Eddy mwanagu nakuomba unisamehe”
“Nikusamehena nini mama?”
“Eddy najua siku zote ulikuwa unahitaji kujua
ukweli juu ya baba yako na mimi nikawa
nimekuficha ila....”
“Mama nimesha lijua hilo kuwa pacha wa baba
ndio baba yangu”
“Nani amekuambia hivyo?”
“Mama dunia haina siri tena hili swala
nimeambia na mtu baki kabisa tena ni muandishi
wa habari”
“Basi Eddy tuliache hilo mwanagu kwa maana
unazidi kunipa uchungua katika hilo”
Ikanibidi nibadilishe mada ya kuzungu na
kuzungumza na kuanza kupiga story za kupoteza
mawazo hadi mama na Emmy wakaanza kucheka
ila sikumuambia mama kuhusiana na swala la
shule yetu kuingia kwenye matatizo.
“Emmy hapa ni wapi kwenye choo?”
“Ukitoka hapo nje mkono wako wa kushoto
utaona milango miwili imeandikwa toilet”
“Ahaa powa”
Nikatoka nje na kumkuta askari akiwa
amesimama mbali kidogo na chumba
akizungumza na simu akionekana akiwa na
mazungumzo ya siri ikanibidi kulitega sikio langu
kwa umakini kusikiliza ni kitu gani anacho
kizungumza
“Ndii si nimrefu kiasi na mwili wake umejazia
kidogo?”
“Basi amefika hapa kama lisaa lililo pita”
“Amekuja na mwanamke fulani ambaye hapa ni
ndakatari”
“Basi panda ndege uje kwa maana inavyo
onekana mipango yote itakwenda kuharibika”
“Sawa Mr Godwin”
Nikajikuta hata hamu ya kwenda kujisaidi haja
ndogo ikakata na kabla hajaguka nikaingia ndani
huku nikiwa ninawasiwasi hadi mama
akanigundua kwa haraka
“Una tatizo gani mwanangu?”
“Mama hivi huju mlinzi mumemtoa wapi?”
“Kwa nini?”
“Wewe nijibu?”
“Huyo amekwa na ubalozi wa Tanzania uliopo
hapa nchini”
“Unauhakika kweli ni mwema?”
“Ni mwema kivipi?”
“Au kuna siku ambayo baba alisha wahi kuja
hapa”
“Hajawahi kuja hapa na wala hatambui kama
nipo hapa”
“Sawa”
Nikatoka nje na kumkuta mlinzi akiwa
amesimama kwenye sehemu ambayo tulimkuta
kwa mara ya kwanza na akaniangalia kwa jicho la
kuiba na mimi moja kwa moja nikaelekea chooni
na kumaliza haja yangu kisha nikarudi huku
moyoni mwangu nikiwa na wasiwasi kiasi
kwamba nikakosa amani kabisa ya kukaa ndani
ya chumba alichopo mama na Emmy.
“Emmy nakuomba mara moja nje?”
“Kwema?”
“Kwema tuu wewe ninakuomba”
Emmy akatoka na nikamshika mkono hadi
sehemu iliyo tulia ambayo si rahisi kwa askari
kuniona
“Hivi tunaweza kumuhamisha mama hospitali?”
“Kwanini?”
“Nijibu kama kuna uwezekano wa mama
kuhamishwa hospitali ua hakuna?”
“Uwezekano upo ila ni hatua zahadi yeye
kuhamishwa kwenda hspitali nyingine ni ndefu
kwa maana hapa ameletwa na serikali ya
Tanzania....Ila ni kwanini unahitaji ahamishe
kuna nini?”
“Nafsi yangu imekosa amani kabisa juu ya mama
kuendelea kuwa katika hospitali hii”
“Wasi wasi wa nini wakati hapa maaskari
wamejaa wengi na hakuna mtu atakaye weza
kumdhuru mama na mimi leo nitakaa naye siku
nzima humu ndani”
“Emmy ninaamini hujui kwa undani hali ya
familia yangu pale umesikiliza mamaneno
machache wewe mwenyewe umejikuta ukitokwa
na machozi sasa sihitaji uweze kulia zaidi ya pale
ulivyo kuwa unalia?”
“Kwa nini unakuwa unananificha kwa kitu
ambacho wewe unakihisi?”
“Kwa sasa huwezi kunielewa ila utanielewa”
Nikaachana na Emmy na kwenda chumbani kwa
mama na kumkuta akiwa anazungumza na
madakatari wawili ambao wamejifunga vitambaa
vya kijani usini vinavyo fanana na nguo zao
walizo zivaa baada ya kuniona mimi wakaniomba
nisubiri nje kwa muda.Kusema ukweli nafsi na
moyo wangu vikajikuta vikishindwa kuchukua
maamuvu ambayo madakatri wameniomba
nitoke.Emmy akaingia na akaonekana
kuwashangaa madaktari hawa ambao
wamejifunga vitambaa jambo ambalo ni tofauti
sana kwa madaktari tunao waona kwenye hii
hospitali wakiwa wameziacha sura zao wazi
“Nyinyi ni kina nani?”
Madaktari wakatazamana kisha mmoja
akajikoholesha kisha akaanza kuzungumza kwa
sauti ya kujiamini
“Sisi ni madakatari maalumu tumetumwa na
serikali ya Tanzania kuja kuzileta dawa ambazo
zinamsaidia muheshimiwa waziri katika kupona”
“Ngoja mumesema kuwa mumetoka wapi?”
“Tanzania?”
“Dawa mumetumwa na nani?”
“Na wizara ya afya”
“Hivi nyinyi kama hizo dawa mungeziona zina
faida sana si munge mpa mama yangu tangu siku
akiwa yupo Tanzania akiwa anaumwa”
“Hizi dawa kwa hapa hatuna tumeziacha ofisini”
“Basi nendeni mukazilete”
Madakatari wakaanza kubabaika kiasi kwamba
sote tukabaki tukiwatazama kwa macho makili na
hata walivyo toka hawakuga kiasi kwamba
wasiwasi wangu ukaanza kupata jibu kwamba
kuna mkono wa baba katika swala hili.
“Mama ninahitaji tuhame hospitalini kwa maana
baba anatufwatilia na nisipo angalia ninaweza
kufa”
“Kweli mwanangu?”
“Basi ngoja nikaonane na daktari mkuu nitakuja
muda sio mrefu”
Emmy akatoka ndani ya chumba na kutucha
mimi na mama huku akili yangu ikiwa na kazi ya
kupanda nini cha kufanya kuweza kumtorosha
mama katika hospitali hii.Baada ya nusu saa
Emmy akarudi akiwa ameongozana na daktari
mmoja wa kuzungu ambaye ni mtu wa makamo.
“Mama huyu ndio mkuu wangu wa hapa kazini”
Daktari mkuu akaanza kutupa mipango ya
kufwata ili tuweze kumuhamisha mama katika
hospitali hii jambo ambalo kwa mtazamo
linachuku muda mrefu wa siku kama mbili kwani
nilazima kibali kiweze kutoka katika serikali ya
Tanzania na kipitie katika ubalozi wa Tanzania
ndipo mama aweze kuhamishwa
“Basi tutabubiria hadi kesho”
“Mama Hadi kesho una uhakika na kitu unacho
kizungumza?”
“Eddy kila kitu kinakwenda kwa mpangilio wa
kiserikali na ukisema uende wewe kama wewe
itakuwa ni shida kumbuka kuwa mimi serikalini
nina mamlaka na ninachukuliwa kama kiongozi
kwahiyo nakuomba uwe mvumilivu mwanangu”
“Mama..”
“Eddy nielewe......Sawa daktari nimekuelewa
nyinyi fanyeni hizo hatua na mukihitaji msaada
wangu tutashirikiana”
“Sawa”
Emmy na daktari mkuu wakatoka nje na
kutuacha mimi na mama huku nikiwa
ninamipnago mingine ya kuto kumshorikisha
mama.Emmy akarudi ndani na kukaa pembeni ya
kitanda alicho lala mama
“Eddy unaoenekana wewe ni mbishi sana”
“Huyo mwanangu nimesha mzoa ila ana ugonjwa
wa hasira kiasi kwamba akiwa anabishana na mtu
huwa hapendi kushindwa”
“Mama achilia na ugonjwa wa hasira ila kuna
hatari ipo mbele yako sasa nyinyi endeleni
kuniona kuwa mimi sifai”
Tukaendelea kukaa hadi mida ya saa moja usiku
nikamuomba Emmy kunielekeza ni wapi ninaweza
kupata sehemu yenye benki ya Backryas na
akanielekeza na haikuwa mbali sana na sehemu
hospitali ilipo
“Niwachukulie chakula gani?”
“Mimi nina chakula changu maalumu huwa
ninaletewa na madakatari wa hapa?”
“Emmy?”
“Mimi niletee keki na soda ya kopa ya koka”
Nikatoka na kumkuta askari akiwa anatembea
tembea huku na kule akionekana akisubiria kitu
fulani kwa hamu
“Hivi zamu yako wewe inabadilika saa ngapi?”
“Nani mimi?”
“Kwani hapa nina ongea na nani?”
“Mimi zamu yangu inabadilika saa nne usiku”
“Ahaa powa”
Nikaachana na askari na kwenda sehemu aliyo
nielekeza Emmy na kukuta ATM ya benki ya
Backrays na kuchukua pesa kiasi zitakazo
nisaidia katika matumizi madogo ya hapa Africa
kusini.Nikaingia kwenye mgahawa uliopo karibu
na hospitali na kuagizia chakula ambacho
nitaweza kukila na nikatafuta sehemu ambayo
ninaweza kuuona mlango wa kuingilia katika
hospitli na kabla sija letewa chakula nikaona
taksi ikiwa imesimama kisha nikamshuhudia
baba akishuka ndani ya gari akiwa ameongozana
na wanaume wawili na katika taksi nikamuona
Sheila akiwa amekaa siti ya nyuma.Kwa haraka
nikanyanyuka na kutoka nje ya mgahawa na
kutokana na magari mengi ikanilazimu kuvunja
seheria za barabara na kujikuta nikivuka kwa
haraka barabara na kabla sijamalizia nikashtukia
nikikumbwa na gari lililo nirusha na kuangukia
pembeni ilipo simama taksi aliyopo Sheila
ITAENDELEA
 
*****SORY MADAM*****(32)
AGE..........................................18+
WRITER...................................EDDAZARIA
G.MSULWA
WAALIKE RAFIKI ZAKO WALIKE HII
PAGE,ASANTENI SANA
ILIPOISHIA
Kwa haraka nikanyanyuka na kutoka nje ya
mgahawa na kutokana na magari mengi
ikanilazimu kuvunja seheria za barabara na
kujikuta nikivuka kwa haraka barabara na kabla
sijamalizia nikashtukia nikikumbwa na gari lililo
nirusha na kuangukia pembeni ilipo simama
taksi aliyopo Sheila
ENDELEA
Nikatulia chini kwa muda na kumuona Sheila
akifungua mlango kwa haraka na kushuka ndani
ya gari na akaonekana kunishangaa baada ya
kunijua ni mimi,nikajaribu kujinyanyua ila
nikajikuta nikishindwa kutokana na mguu wangu
mmoja kutawaliwa na maumivu makali.Nikastuka
baada ya kugundua mguu wangu wa kushoto
umevunjika japo kichwani na mikononi
nimepatwa na michubuko iliyosababishwa na
kuaanguka na kuserereka kidogo kwenye
barabara ya lami.Sheila akaoanekana kupigwa na
bumbuazi kwani hakuzungumza kitu cha aina
yoyote zaidi ya kubaki akinitazama hadi watu
walipo anza kukusanyika na kuwaomba wauguzi
wa hospitalini kunisaidia,
Nikawawekwa kwenye machela na kuingizwa
ndani pasipo Sheila kuzungumza kitu cha aina
yoyote kwangu,Nikaingizwa kwenye moja ya
chumba ambacho ni chaupasuaji na kwa haraka
nikachomwa sindano za ganzi kwenye mguu wa
kushoto ambao umevunjika na kawanipaka
mafuta kisha wakamipitishia kifaa maakumu
kinachotoa mwanga mwekundu wenye miyonzi
mikali huku dakitazama picha inayopita kwenye
Tv ndogo iliyopo ndani ya hiki chumba wakaona
ni sehemu ya ambayo mguu umevunjika na
wakaanza kazi ya kunihudumia
Ndani ya lisaa moja wakamaliza upasuaji wao na
kunifunga bandeji kubwa kisha majeraha madogo
madogo wakayapaka dawa kisha wakanihamishia
kwenye wodi kitu ambacho ninakiona ni
chatofauti ni huku kufanyiwa upasuaji pasiopo
kuchomwa sindano ya usingizi.Sikuweza kupata
rafiki wa kunijulia afya yangu na kitu kinacho
niumiza sana akili yangu ni jinsi hali ya mama
ilivyo na kingine sikujua kama ameweza
kusalimika mikononi mwa baba ambaye ndio
amekuwa adui yetu namba moja kwenye familia
yetu.Sikua ya kwanza ikakatika huku nikiwa sijui
kitu kinacho endelea ila zaidi nikawa
ninahudumiwa na kupewa chakula na wauguzi wa
hospitalini.
Wiki moja ikakatika na hali yangu ikaendelea
kuwa nzuri zaidi na nikaanza kufanyishwa
mazoezi ya kutembea na siku hii nikamuomba
muuguzi kunipeleka kwenye sehemu kilipo
chumba alichomo mama na hakusita na kwa
mwendo wa taratibu tukafanikiwa kufika ila
sikuweza kumpata mama na ikanibidi kumuuliza
muuguzi huyu kwa lugha ya kingereza
“Hivi huyu mama humu ndani amekwenda wapi?”
“Mama yupi?”
“Kuna mama waziri ambaye alilazwa humu
chumbani”
“Sijajua labda tukaulize sehemu zenye rekodi ya
wagonjwa kwa maana mimi sihusiki katika kitngo
hichi na kama unavyo iona hospitali yetu ilivyo
kubwa siwezi kuwajua wagonjwa wote”
“Sawa dada yangu basi nakuomba unifikishe hiyo
sehemu wanayo angalizia orodha ya wagonjwa”
Cha kumshukuru Mungu huyu nesi hana makuu
zaidi ya alicho kifanya ni kunipeleka hadi sehemu
wanayo angalizia idadi ya wagonjwa walipo
kwenye hospitali hii na kadri tunavyo litafuta
jina la mama kwenye kumputer yao hawakuliona
na ikanibidi niweze kuuliza jina la daktari Emmy
na jibu nililo lipata kutoka kwa mfanyakazi wa
ofisi hii ya takwimu za hospitali likazidi
kunichanganya
“Hapa hospitalini kwetu hatuna jina la daktari
anaye itwa Emmy na dokta anaye anziwa na
herufi ya E ni mwanaume na anaitwa Emmanuel”
“Kweli huyo daktari hayupo....Mbona ana hadi
kitambulisho na kitambulisho kinacho
muonyesha kuwa yeye ni daktari wa hii
hospitali?”
“Wewe ulikutana naye wapi?”
“Tanzania na nikapanda naye ndege moja hadi
hapa”
“Mmmm hapa mulikuja lini?”
“Kama wiki moja iliyo pita”
“Ngoja kwanza”
Msichana anayehusika na maswala ya takwimu
akanyanyua mkonga wa simy ya mezani kisha
akaminya baadhi ya namba na kuiweka simu
yake sikioni
“Kiongozi ninashida moja ninakumba unisaidie”
“Kuna tatizo limejitokeza la hawa madaktari feki
kuendelea kuivamia hospitali yetu na
wanaendelea kufanya matukio ya ajabu”
“Basi ninakuja sasa hivi”
Akakata simu na kuniomba niogonzane naye
huku nesi anaye nifanyisha mazoezi akinishikilia
vizuri na tukaingia kwenye lifti na ikatupeleka
hadi gorofa ya tatu na tukaingia kwenye chumba
ambacho nikakuta tivi nyingi ndogo ndogo
ambazo idadi yake kwa haraka haraka zinaweza
kufika hamsini na kila Tv inaonnyesha sehemu
yake na nikagundua zinaonyesha picha za kamera
za ulinzi zilizo fungwa ndani ya hii hospitali
“Una rekodi za wiki nzima?”
“Ndio ninazo”
“Ninaomba utuwekee za siku saba za nyuma”
Jamaa anaye onekana ndio muongozaji wa
kamera za humu hospitali akaigeukia Tv moja
kubwa kama nchi 32 kisha akachuku CD ndogo
na kuziingiza kwenye deki ndogo na tukaanza
kuangalia video zilizo chukuliwa ndani ya wiki
moja na nikajikuta nikinyoosha kidole changu
kwenye moja sehemu hii ni baada ya kujiona
nikiingia hapa hospitalini siku ya kwanza nikiwa
na Emmy na kumfanya jamaa kuisimamisha
sehemu hii kisha akaisogeza kwa ukubwa kiasi
(ZOOM) na kuiangalia sura ya Emmy ambaye
alizidi kunichanganya baada ya kumuona dada
wa ofisi ya takwimu akitingisha kichwa huku
akiibenua midomo yake
“Mmmm hatuna daktari kama huyu”
“Kaka hembu peleka mbele”
Jamaa akairuhusi CD kutembea na kuanza
kuangalia picha za mbele na kujiona nikiingia
ndani ya chumba alichokuwa mama kipindi
ninatoka kuzungumza na Emmy baada ya kuanza
kuhisi hali ya ajabu,Video ikamuonyesha Emmy
akizungumza na askari ambaye alikuwepo pale
mlangoni kisha yeye akaingia ndani huku
akiitazama camera ya ulinzi iliyokuwepo juu.
“Hii ni Camera namba 38 ngoja niweke video
zake kwani huu ni mkanda wa jumla”
“Sawa fanya hivyo”
“Na huyo askari hapo ni wa hapa?”
“Askari huyo aliletwa na ubalozi wa Tanzania
kumlinda huyo mama.....Kwani wewe huyo
mama ni nani yako?”
“Mama yangu mzazi”
Jamaa akaito CD aliyokuwa ameiweka kwenye
deki kisha akatafuta CD nyingine ndogo na
kuuweka kwenye deki yake na tukaendelea kuona
matukio yaliyo endelea eneo la nje ya chumba
alicho lazwa mama baada ya mimi kuondoka
kuelekea banki.Tukamuona askari akipewa soada
ya kopo na Emmy na akaianza kuinywa baada ya
Emmy kuingia ndani na baada ya muda
akaonekana kama anaumwa na tumbo na
akandoka katika eneo la nje ya chumba akielekea
sehemu vilipo vyoo na baada ya muda kidogo
mlango ukafunguliwa na kumshuhudia Emmy
akiwa amevalia koti la kidaktari akikisukuma
kitanda cha mama huku mama akiwa amefumba
macho yake na kulala kama mtu aliye poteza
fahamu
Mapigo ya moyo yakazidi kunienda mbio huku
nikiema kwa hasira na kujikutani nikiyang’ata
meno yangu kwa hasira kiasi kwamba nikatamani
nipone kwa haraka ili niweze kumsaka Emmy
sehemu yotote akatakayo kuwepo nchini Afrika
kusini.Nikashusha pumzi huku nikiwa macho
yangu yamebadilika na kuwa mekundu na
kujikuta nikikitazama kioo kilichopo ndani ya
chumba hichi kinacho nionyesha vizuri sura
yangu na kila mtu akabaki akinitazama kwa
umakini pasipo kuzungumza kitu chochote
“Hemu rudisha hiyo CD ya kwanza”
Jamaa akairudisha CD ya kwanza na kipelea
mbele kidogo na kumuona Emmy akimuingiza
mama ndani ya gari la wagonjwa huku
akisaidiana na watu wawili ambao niliwaona
wakishuku na baba huku nao kwa sasa wakiwa
wamevalia makoti meupe wakionekana kama
madaktari.
“Kaka hembu simamasha kidogo hape na zoom
kwenye kioo cha dereva wa hilo gari”
Jamaa akafanya kama nilivyo muagiza na
akaikuza picha ya dereva na kugundua ni baba
japa amevalia miwani huku akiwa amebandika
ndevu za bandia na kumfanya aonekane kama
mtu wa makamo
“Kwani Flora ina maana hawa jamaa sio wafanya
kazi wa hii hospitali?”
“Ndio”
“Mbona wanavitambulisho kwa maana mimi hili
tukio linatokea sikustushwa kwa maana ni jambo
la kawaida kwa wagonjwa kuhamishwa hapa
hospitalini kwetu”
Nikamshuhudia Flora ambaye ndio muhusika
kwenye ofisi ya takwimu akikuna kichwa pasipo
kuzungumza kitu cha aian yoyote.
“Je daktari wenu mkuu yopoje?”
“Yupoje kivipi?”
“Yaani muonekano wake?”
“Ni mweusi kiasi kiasi na sasa yupo Captown
kwenye kikao cha madaktari wakuu hapa nchini”
“Mbona alikuja mzee wa kizungu huyo dada
akasema ndio daktari mkuu?”
“Mmmm atakuwa amekudanganya kwani ni wiki
ya pili daktari mkuu yupo kwenye kikao cha
madaktari kama nilivyo kuambia hapo awali”
Sikuwa na lakuzungumza zaidi ya kuumiza
kichwa ni jinsi gani ninaweza kumpata mama
yangu na moja kwa moja nikajua ametekwa na
baba na sikujua ni wapi alipo mpeleka.
“Tutawasiliana na polisi kuweza kulifwatilia hili
tukio”
“Naombeni mufanye hivyo kwani mama yangu
ndio kila kitu katika maisha yangu kwa maana
nimetoka Tanzania kwa ajili yake na mwisho wa
siku mambo yanakuwa kama hivi”
“Usijali wa hilo”
Nikakaa hospitali zaidi ya wiki nne na nikapona
kabisa mguu wangu na kufunguliwa bandeji nililo
fungwa.Habari za wapi alipo mama kila
nilipojaribu kuwaulizia walio sema
watalishuhulikia wakadai bado askari
wanaendelea na uchunguzi ambao sikujua
utaisha lini
“Kaka gharama zako za hospitalini zimesha
lipiwa”
“Zimelipiwa na nani?”
“Aliye kulipia ni yule aliye kugonga na gari na
yupo nje anakusubiria?”
Nikaanza kujiuliza ni nani huyu aliye ni gonga na
kuwa na moyo wa kujitolea kiasi kwamba
amenilipia gharama zote za ajali yangu wakati
mimi ndio nilikuwa ninamakosa.Nikatoka nje
pamoja na daktari aliye niambia habari hii
ambayo kwangu ni nzuri kiasi japo bado akilini
nimetawaliwa na wazo la wapi alipo mama.
Daktari akanionyesha mzee mmoja aliye valia
koti jeusi la suti na alinipa mgongo kwani
anazungumza na simu,ikatulazimu kumsubiria
amalize ndio daktari amjulishe uwepo
wetu.Baada ya muda akakata simu na kugeuka
na kujikuta nikihamaki kwa kiasi kikubwa kwani
mtu aliyepo mbele yangu anafanana kabisa na
baba yangu ambaye kwa sasa ni adui yangu
namba moja.
“Habari yako kijana”
“Sh...ikamaoo”
Nilipata kigugumizi cha gafla kiasi kwamba mzee
naye akaanza kunitazama kwa umakini huku
akionekana kunichunguza kuanzi kichwani hadi
miguuni.Daktari akatutizama kwa muda na
kuzungumza kitu kilicho tufanya sote tumtimame
“HUYO NI MWANAO?”
HAKUNA aliye lijibu swali la daktari zaidi ya
kukaa kimya kimya na tukageukiana na
kuendekea kutazama na kadri tulivyo zidi
kutazamana ndivyo nilivyohisi ukweli wa maisha
yangu juu ya baba yangu kwani kuanzia macho
pua midomo na sura hakuna kilicho pishana na
mwenzake kiasi kwamba machozi yakaanza
kunilenga lenga huku moyoni mwangu nikijihisi
amani na furaha iliyo kuba tofauti na ninavyo
kuwa na baba yangu gaidi.
“Jina lako ni nani kijana?”
“Eddy”
“Eddy nani?”
“Godwin”
Nikastukia mzee akinikumbatia kwa furaha huku
akicheka kwa kicheko kikubwa cha furaha na
akaninnyanyua juu kidogo na kuanza
kunizungusha kisha akanisimamisha na
kunitazama tena usoni huku machozi ya furaha
yakimwagika na mimi nikajikuta nikiachia basabu
pana
“Dokta nahitaji vipimo vya DNA na huyu kijana”
“Sawa ila inabidi na yeye aridhie”
“Eddy upo tayari kwa hili?”
“Ndio mzee”
Sikuweza kumuita baba moja kwa moja japo
tunafanana kwa asilimia 99(tisini na tisa) ila
nikahofia endapo majibu yatakuwa siyo sijui sura
yangu ningeiweka wapi.Tukaingia kwenye
maabara nzuri na yakisasa kisha tukachukuliwa
damu na kuombwa kusubiri nje.
“Eddy mimi ninaitwa Godfrey nani Mtanzania
japo sasa hivi nina uraia wa hapa Arfrika kusini
hii ni kutokana na kuishi miaka mingi hapa
Afrika kusini”
“Ahaa sasa ni kwanini uliondoka Tanzania
ilikuwaje?”
“Ni historia ndefu sana iliyo nipata hadi kufikia
hapa ni vikwazo na mambo mengi nilipitia ila
ninamshukuru Mungu hadi leo hii nipo salama”
“Ni kitu gani kilicho kupata?”
“Ni mambo mengi sana yaliyo nipata na hapa sio
wakati muafaka wa kulizungumzia hilo”
Kabla sijamuuliza swali jengine mlango wa
chumba cha maabara kikafunguliwa na akatoka
daktari aliye tuchukua vipimo vya damu na
kutuomba twende naye ofisini kwake ambapo
akatupa mikono huku usoni mwake akiwa na
furaha
“MAJIBU NI ASILIMIA 100 DAMU ZENU
ZINAFANA”
Ikawa ni habari mpya yenye furaha maishani
mwangu kwani siku zote kilio changu ni
kuhusiana na baba yangu.Baba akanyanyuka kwa
fauraha na kunikumbatia huku mkono wake
mmoja akiupiga piga mgongoni mwangu,machozi
ya furaha yakanibubujika na hata wazo la mama
kichwani mwangu kwa wakati huu likafutika
kidogo.Baba akatoa simu yake na kupiga namba
fulani
“Andaa tafrija kubwa na waalike watu wangu wa
karibu kwani nina kitu cha kuzungumza nao”
“Fanya hivyo na ndani ya lisaa nitakuwa hapo
nyumbani”
“Waambie ni saa mbili usiku”
Sikujua baba anatoa maagizo kwa mtu gani kisha
akatoa kitabu kidogo cha kuchukulia pesa na
kuandika kiasi anacho kijua yeye kisha akampatia
daktari na nikaondoka huku nikiwa nimebeba
baasha yenye majibu yetu ya DNA.Tukatoka nje
na kulekea eneo la maegesho ya magari na
dereva aliye valia suti nyeusi akafungua mlango
wa gari aina Astorn Martin na kidogo dereva
akawa ananishangaa.Safari ikaanza huku kila
nilipo tazamana na baba tukajikuta tukitabasamu
ikiashiria ni furaha iliyotawala kati yetu
Geti kubwa likajifungua na mbele yangu kwa
mbali kidogo nikaliona jumba kubwa midhili ya
ikulu na kuna eneo kubwa lenye kila aina ya kitu
cha kuburudika pamoja na bustani kubwa zenye
maua ya kupendeza sana
“Karibu nyumbani mwanangu”
Kwa wingi wa walinzi walioo kwenye eneo hili
hadi nikaanza kuogopa japo ni baba yangu ila
sikujiamini sana juu ya usalama wangu
“Karibu sana nyumbani Eddy”
“Asante baba”
Tukashuka kwenye gari huku macho yangu
yakitazama tazama pande zote za sehemu
tuliyupo.Mlango wa kuingilia ndani ukafungulia
na macho yangu yakakutana na seble
inayoendelea kupambwa na wafanyakazi na
akashuka mama mmoja wa kizungu kwenye ngazi
na kuja kumkumbatia baba kisha akambusu
mdomoni na mama huyo akabaki akinishangaa
“Huyu ni nani?”
“Mwanangu”
Mama wa kizungu akanipa mkono kwa dharau
kisha akaondoka huku akionekana kukasirika kwa
uwepo wangu katika nyumba hii hadi nikajihisi
vibaya
“Eddy mwanangu karibu na jisikie upo huru na
mwenye amani kwa maana hapa ni kwako”
“Asante baba yangu”
Niliitikia kwa sauti ya kinyonge ila moyoni
mwangu nikaanza kuhisi kuna mapambano
yatakayo endelea kati yangu na huyu mama wa
kizungu.Tukaongozana hadi kwenye chumba
kikubwa chenye mali nyingi za dhamani na baba
akanikaribisha kwenye moja ya kiti kilicho
tengenezwa kihalisi na yeye akakaa kwenye
sehemu nyingine
“Una hitaji kinywaji?”
“Hapana”
“Sawa Eddy kwanza ninakuomba unisamehe kwa
kile ulicho kiona pale mlangoni”
“Bila samahani kwani yule ni nani?”
“Yule ni mke wangu wa ndoa ambaye nimefunga
naye ndoa miaka mitano iliyo pita”
“Aaaahaa sasa mbona ameonekana kuchukizwa
baada ya kuniona?”
“Ahaa nahisi hakutegemea kuupata ujio wako leo
kwani hata mimi sikuwahi kumuambia kuwa
mimi nina mtoto”
“Sawa na yeye ume zaa naye?”
“Hapana na sina mtoto mwengine zaidi yake japo
yeye naye ana mtoto wa kike hayupo hapa yupo
Johnsburg anasoma chuo”
“Mama yako hivi hajambo?”
“Siwezi kujiu kama hajambo au anaendeleaje kwa
maana alikuwa yupo hospitalini na amatekwa?”
“Ametekwa na nani?”
“Ametekwa na baba?”
“Ina maana kaka Godwin anaweza kumteka mke
wake?”
“Babahiyo ni historia ndefu sana,na chanzo
kikubwa cha mimi kuja huku ni yeye kwa maana
alikuwa amelazwa kwenye ile hospitali uliyo
nikuta”
“Duu kweli malipo ni hapa hapa duniani?”
“Kwa nini baba?”
“MAMA YAKO NI KATILI SANA TENA ZAIDI YA
SANA JAPO USONI MWEKE NI MWAMA
KUPITILIZA”
Maneno ya baba yakanicha mdomo wazi huku
nikishangaa nisijue ni kwanini amesema mama
yangu ni katili sana
ITAENDELEA
 
ooh my god kila nikianza kusoma napata uvivu ingawa inaonekana ni nzuri

Jmos wakati nimejipumzisha nitasoma
 
Back
Top Bottom