Hotel ya bei mbaya duniani

pilau

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
1,595
Reaction score
451


Bei ya chini chumba kimoja dola 1,000 bei ya juu dolla 28,000 kwa usiku mmoja DUBAI nyota 7 pekee duniani
 
Bwana pilau leo naona umekuja na topic tofauti,naomba nichangie kidogo maana nilifanya kazi kwenye hiyo hotel kwa miaka mitatu jina lake ni Burj al arab,yaani ni kama story ya kutunga hapo nilikutana na kila aina ya watu,huo kama ungo unaouona hapo juu pichani sio ungo ni helipad(kiwanja cha helicopter ambazo baadhi ya wageni wanazitumia,kuna baa inauza wine mpaka uae dh 40000 ambayo ni kama tsh 16.5ml na watu wanakunywa!!!Naomi campell alifanya birthday yake mwaka juzi alifunga hotel yote alialika rafiki zake tu!!nakumbuka siku moja kuna m russia alikuwa anaishi hapo kwa siku kama sita siku aliyoondoka alisahau pesa kwenye safe box,baada ya kuwaita security na kufungua tulikuta dola 50,000/ hii ni zaidi ya milioni 75 za tz lakini ajabu tulipompigia simu alisema amesahau kwamba alikuwa na kiasi hicho cha pesa.Nakumbuka wakati nafanya pale kuna mtanzania alikuja kupumzika na familia yake!!!pia hiyo hotel inaingiza pesa nyingi sana kwa watu wanaokuja kuingia na kupiga picha kipindi kile ilikuwa Tsh 50,000/cha ajabu kuna bwana mmoja anakaa mle ndani tangia mwaka 2004.
 

Chumba bei nafuu kabisa kiasi gani?
 
Chumba bei nafuu kabisa kiasi gani?

umeambiwa dollar za kimarekani elfu moja i.e USD 1,000 * 1,620 =1,620,000 kwa usiku mmoja bei ya chini mkuu
 


Bei ya chini chumba kimoja dola 1,000 bei ya juu dolla 28,000 kwa usiku mmoja DUBAI nyota 7 pekee duniani

Mwaka juzi ulivoenda ulilala chumba namba ngapi Mkuu pilau? ha ha ha ha....
 
Bei ya chini chumba kimoja dola 1,000 bei ya juu dolla 28,000 kwa usiku mmoja DUBAI nyota 7 pekee duniani

Wewe Pilau - data zako zina walakini - bora ungesema is among the most expensive hotel suite duniani - lakini wewe unasema ni pekee?!

Vipi kuhusu Royal Penthouse Suite, Hotel President Wilson, Geneva ambayo Kwa usiku mmoja mtu analipia chumba kwa US$65,000 per night

Hebu fuatilia hata hii link ya CNN:

http://edition.cnn.com/2011/09/01/travel/expensive-hotel-suites-cnngo
.
 
Itabidi ukitaka kupiga picha eneo hilo ununue kamera inayozoom vizuriiiii uzoommmm we hadi uipate ndo upige picha hizo 50,000 za kupigia picha noma kutoa hahaha
 

Si unajua watu wanamajonzi ya Gesi na mabomu ya Mtwara nikaona ngoja nizuge usawa huu
 
Mc Foyer nasikia alifanya booking kwa ajili ya fungate,
akashangaa kutaarifiwa kua vyumba viko booked tayari hadi 2015.

Huyu mama mmiliki wa Burj al Arab ni mke wa mfalme au ni nani? msaada Mkuu lucky sabasaba
 
Last edited by a moderator:
ikajua mtakuwa mmesema kaburi ndo most expensive. Ukiangalia bei ya kaburi pale kndoni, halafu halina dirisha, umeme wala ac! Tiles inabidi uweke mwenyewe na hawafanyi renovation! Kha.

(nnawaza kimaskini hadi najionea huruma)
 
Mc Foyer nasikia alifanya booking kwa ajili ya fungate, akashangaa kutaarifiwa kua vyumba viko booked tayari hadi 2015.Huyu mama mmiliki wa Burj al Arab ni mke wa mfalme au ni nani? msaada Mkuu lucky sabasaba
Hii hoteli (Burj al arab) ilijengwa miaka ya 1990s na ikafunguliwa rasmi 1999,cost ya kuijenga ilikuwa $650 milioni sasa kwa wakati huo mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2006 ilikuwa ktk top five expensive hotels in the world..Hii ilikuwa logo ya dubai kabda hawajajenga gorofa refu kuliko yote duniani linaloitwa Burj khalifa,unaona majengo ya waarabu wanayaita Burj maana yake ni Tower kwa kiingereza..pia kwa sasa kuna hoteli ambazo ni more expensive iliyopo abu dhabi (Emirates Palace)hapo burj kuna international prostitute ambao wanaendesha ferrari nilipoulizia cost zao nikaambiwa $7500 per night!!!lakini kuna wajomba wanaona ni bei ya kawaida..Jengo lilijengwa na Jumeirah group of company ambalo mmiliki wake ni sheikh mohammed bin Rashid al maktom...king muswati wa swazland kila mwaka lazima aende hapo na uwa ana book nusu nzima ya hoteli..kwa kuongezea ni kwamba hapo ni rahisi sana kupata kazi kama ukijua vizuri jinsi ya ku apply si lazima uwe umesomea hoteli hapo kuna kazi ya kozi zote kuanzia IT..accounts..engineering..hoteliers etc jaribu www.jumeirahgroup.com ikifunguka click careers..all the best
 
Last edited by a moderator:
Bwana pilau leo naona umekuja na topic tofauti,naomba nichangie kidogo maana nilifanya kazi kwenye hiyo hotel kwa miaka mitatu jina lake ni Burj al arab,yaani ni kama story ya kutunga hapo nilikutana na kila aina ya watu.

Kwanini ukaacha kazi kwenye sehemu inayolipa mshahara mkubwa kiasi hicho,kuna mdau kasema $15000
 


Bei ya chini chumba kimoja dola 1,000 bei ya juu dolla 28,000 kwa usiku mmoja DUBAI nyota 7 pekee duniani

Mkuu hiyo Hotel inazidiwa bei na Hotel za hapahapa Bongo, for sure its not THE MOST expensive, it is ONE OF THE VERY EXPENSIVE HOTELS in the World!! Btw, kwa wenye pesa zao ni sehem nzuri sana, lakini si nzuri kama Hotel ya Mkuu kule kwenye twiga wetu, hewa safi, usiku unabembelezwa na sauti za ndege na upepo mwanana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…