Hoteli mbili zafungwa Nairobi kufuatia mlipuko wa kipindupindu

Hoteli mbili zafungwa Nairobi kufuatia mlipuko wa kipindupindu

Donatila

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,772
Reaction score
22,598
_96999417_419cc5e5-710c-47a7-aa99-8b15f758bf7c.jpg

Hoteli mbili zimefungwa mjini Nairobi kutokana na mlipuko wa ugonjwa kipindupindu mjini humo.

Wizara ya afya ilitoa amri ya kufungwa hoteli hizo kufuatia watu kadha wakiwemo mawaziri wawili kulazwa hospitalini, baada ya kula chakula kilichokuwa kimepikwa na hoteli hizo mbili.

Watu wanne tayari wamefariki kutoka na ugonjwa wa kipindupindu tangu mwezi Mei na zaidi ya visa 300 vya ugonjwa huo vimeripotiwa.

Waziri wa afya Dr. Cleopa Mailu anasema hoteli hizo mbili zitasalia zimefungwa hadi zitimize viwango vipya vya wizara ya afya.

Wizara ya afya pia ilifuta leseni za sehemu zote za kupika chakula kote nchini, na kubuni jopo litakaloongoza hatua za serikali dhidi ya ugonjwa huo.

Vituo sita vya kutoa matibabu vimebuniwa hasa maeneo ya mabanda mjini Nairobi kuzuia kusambaa kwa ugonjwa wa kipindupindu.

Chanzo: BBC swahili
 
Kipindu pindu Kiangazi!
hahaha Sipati picha ile Jehannam ya Kibera hali ipoje!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Back
Top Bottom