Hotuba ya mwisho aliyoindika Muammar Gaddafi

Hotuba ya mwisho aliyoindika Muammar Gaddafi

Na wale wahanga wa ndege (zaidi ya 250) ktk anga la Lockerbie mbona huwaonei huruma. Roho zisizo kuwa na hatia ziliteketezwa kupitia mkono wa huyu Gaddafi.
Unajua alichowafanyia wanafunzi wa University mnamo 1976? Na Wakurdi je?
Gaddafi squad special kwa kunyonga watu ulishawahi kuisikia?
Kwanini usiwasikitikie Watz wenzako waliokufa 1978/79 kupitia kwa huyu Gaddafi pale alipomsaidia Nduli Iddi Amini kuipinga Tz?
gaddafi had to help amin, kwa sababu tanzania ambayo ni nchi yako wewe ilivamia uganda mara 2, na mara zote hizo watu walikufa,maelfu, uganda haikuwahi kuivamia tanzania,
na kosa hilo la kuivamia uganda lilisababisha wazee enzi hizo pamoja na watoto wadogo wasio na hatia wateseke na njaa huku tanganyika
 
Hii hotuba inagusa/inatoa funzo kwa wenye akili
 
Kosa lake kubwa ni kujiona yeye ndiye anayestahili kuwa kiongozi wa libya pekee

Hili lilikuwa kosa kubwa sana ambalo hakulijua au alilijua akalipuuzia

Ni bora angeachia madaraka akamwachia mwingine, ungekuta mpaka Leo anadunda tu.
Yani mnalishwa upumbavu na mataifa ya magharibi na nyie mnashiba? Kweli tuna safari ndefu.........

Hivi baba yako(kiongozi) akiwa anakupa elimu bure, miundombinu bora/ afya bure, chakula maji na misaada mbalimbali.....

Then unakaa baada ya muda unasema baba huyu simtaki nataka baba mwingine....Hii ndiyo sababu walibia wanajuta hadi dunia iishe kwa kudhani kwamba maana ya demokrasia eti ni kibadilisha kiongoz kila miaka mitano

Hivi unajua malkia ana nguvu na maamuzi Uingereza?

Mbona hao tunaowaita wastaarabu wa demokrasia hawamtoi malkia ukafanyika uchaguz wa malkia mwingine?

Kwani urusi haijaendelea?

Mbona rais Putin wa Russia yupo kwa miongo kadhaa na bado nchi ina uchumi wa kutosha?

Kwa nyie mnaoamini (kama mlovyomezeshwa) kwamba demokrasia ni kukaa miaka mitano na kuachia mwingine...kama ingekua hivyo nchi yetu ingekua kama marekani mana huo ndio utaratibu wetu kwa miaka mingi sasa
 
gaddafi had to help amin, kwa sababu tanzania ambayo ni nchi yako wewe ilivamia uganda mara 2, na mara zote hizo watu walikufa,maelfu, uganda haikuwahi kuivamia tanzania,
na kosa hilo la kuivamia uganda lilisababisha wazee enzi hizo pamoja na watoto wadogo wasio na hatia wateseke na njaa huku tanganyika
Cha kusikitisha hapa ni kwamba stori za gadafi watu huzipata kutoka kwenye vyombo vya kipropaganda vya kimagharibi kama CNN BBC amnestry internaional e.t.c

Hivi ndio huuaminisha ulimwengu kua gadafi alikua dictator na muuaji na watu wakaamini hizi information zilizopakwa cosmetics
 
Cha kusikitisha hapa ni kwamba stori za gadafi watu huzipata kutoka kwenye vyombo vya kipropaganda vya kimagharibi kama CNN BBC amnestry internaional e.t.c

Hivi ndio huuaminisha ulimwengu kua gadafi alikua dictator na muuaji na watu wakaamini hizi information zilizopakwa cosmetics
ndio tatizo la mtu mweusi huwa hana taratibu ya kuchunguza
mobutu aliipa amani na maendeleo nchi yake kadiri alivyoweza huku akijichukulia vi pesa kidogo mara moja moja huku zingine akipata kwenye investments zake,ila vyombo vya habari vya ulaya vikawaaminisha watu kuwa ana utajiri wa zaidi ya 15 billion usd, ila alivokufa wamefatilia hawajakuta zaidi ya 40 million usd
 
Mwanadamu anataka uhuru wa kuchagua na kuchaguliwa,na kukaa miaka mingi kwenye uongozi haimaanishi kuwa yeye ana akili nyingi kuliko wengine....angeachia mapema wakati vuguvugu ndio imeanza si ajabu mpaka leo hii angekuwa anaishi.
 
Damu nyeusi hua hairidhiki hata uinyweshe balimi itataka Heineken Na ukiipa Heineken itataka bingwa Na matap tap
Kumbuka sisi binadam asili yetu hatupendi kutawaliwa ndio maana hata Mungu ametuacha huru tuamue sisi wenyewe kati ya njia ya uzima na njia ya uharibifu.

Tatizo Gaddafi hakusoma nyakati, utafikiri hakuna viongozi bora kama yeye ndani ya Libya hilo ndiyo kosa kubwa alilolifumbia macho na masikio.
 
Hebu tumia akili kidogo. Hivi hata ingekuwa ni wewe unapata vitu vyoye hivyp kutoka kwa kiongozi aliyepo madarakani ungetamani aondoke?
Mimi binafsi sipendi kutawaliwa, ni heri Nile ugali kwa maharagwe yaliyooza kwa uhuru na amani kuliko kula wali nyama kwa masimango.

Nikweli walibya walipewa huduma bora lakini ilikua ni "shut your mouth" kitu ambacho si asili ya mwanadam kuto kuwa huru.
 
Labda wewe. Walibya sas wanamtamani gadafi. Wanashindwa hata kutoka nje kufanya shughuli za maendeleo
Mimi binafsi sipendi kutawaliwa, ni heri Nile ugali kwa maharagwe yaliyooza kwa uhuru na amani kuliko kula wali nyama kwa masimango.

Nikweli walibya walipewa huduma bora lakini ilikua ni "shut your mouth" kitu ambacho si asili ya mwanadam kuto kuwa huru.
 
Kosa lake kubwa ni kujiona yeye ndiye anayestahili kuwa kiongozi wa libya pekee

Hili lilikuwa kosa kubwa sana ambalo hakulijua au alilijua akalipuuzia

Ni bora angeachia madaraka akamwachia mwingine, ungekuta mpaka Leo anadunda tu.
Mi naona hata bora angemtengeneza mtu wake akampachika pale. Shida ya viongozi wa Africa kukatalia madarakani.
 
Kosa kubwa la Gaddafi alitaka kuipindua dollar . Alitaka itafutwe currency mbadala au waitumie dhahabu kwenye biashara za kimataifa
View attachment 1123851View attachment 1123850

HOTUBA YA MWISHO ALIYOIANDIKA QADAFFI

QADAFFI ANAANZA HIVI:

"Kwa jina la Mwenyezi Mungu (Allah), Mungu mpaji, na mwenye rehema..
..

Kwa miaka takribani 40 ama ilikuwa zaidi sikumbuki. Nachokumbuka ni kuwa nilifanya kila nilichoweza kuwapa watu wangu nyumba, hospitali na shule. Na kila walipohisi njaa niliwapa chakula. Niliifanya Benghazi kutoka jangwa kuwa ardhi nzuri ya kilimo.

Nilisimama imara dhidi ya Ronald Regan (Rais wa zamani wa Marekani), alipomuua binti yangu niliyemuasili. Alikua anajaribu kuniua mimi lakini akamuua yule binti yatima masikini. Niliwasaidia kaka na dada zangu waafrika fedha kupitia AU.

Nilifanya kila nililoweza kuwafanya watu wangu waelewe maana halisi ya demokrasia; ambapo watu wa tabaka la chini niliwapa madaraka.
Lakini hawakuridhika. Hata aliyekuwa na nyumba ya vyumba kumi, nguo mpya, na fanicha nzuri, hakuridhika. Alihitaji zaidi.

Kwa jinsi walivyokuwa wabinafsi walihitaji zaidi. Hivyo wakawaambia Marekani kuwa wanataka "demokrasia" na "uhuru". Hawakujua kuwa "demokrasia" waliyoitaka ilikua ni mfumo wa unyonyaji ambapo mbwa mwenye nguvu zaidi huwala mbwa wadogo.

Walikua hawasikii wala hawaoni. Walitaka "demokrasia". Wakasahau kuwa hata Marekani hakukuwa na huduma za afya za bure, dawa bure, elimu bure na chakula cha bure. (Huduma hizi za bure zilipatikana Libya tu).
Nchini Marekani mtu masikini/fukara hana cha bure. Labda awe ombaomba au avuje jasho kuhemea.

Haikujalisha nilifanya kwa kiasi gani bado hawakuridhika. Lakini wapo waliojua mimi ni mtoto wa Gamal Abdel Nasser, mwarabu pekee halisi na kiongozi wa kiislamu tuliyewahi kuwa nae tangu enzi za Salah-al-Deen.

Wakati Nasser anapigania mfereji wa Suez kwa watu wake nami nilikua naipigania Libya kwa watu wangu. Nilikua najaribu kufuata nyayo zake ili kuwaweka watu wangu huru kutoka kwenye makucha ya wakoloni wanaotuibia.

Lakini kwa sasa niko mateka katikati ya majeshi makubwa ya dunia katika historia. Mwanangu mpendwa mwenye asili ya Afrika, Obama anataka kuniua.
Ili achukue uhuru wetu, achukue haki yetu ya huduma za bure za afya, huduma za bure za elimu, na chakula chetu; na kutuletea mfumo mpya wa kimarekani wa kuiba uitwao "Ubepari"

Lakini wote katika dunia ya tatu tunajua maana yake. Maana yake ni kuwa "washirika" wanatawala mataifa, wanatawala dunia, na watu wanaishia kuteseka.
Kwa hiyo hakuna mbadala kwangu. Lazima niwe na msimamo. Na kama Mungu atapenda nitakufa kwa mapenzi yake.

Mapenzi yake yaliyofanya nchi yetu kuwa na ardhi yenye rutuba, chakula bora, na huduma bora za afya. Mapenzi ya Allah yaliyowezesha tukawasaidia kaka na dada zetu waafrika na waarabu waliokuwa na shida.

Sipendi kufa; lakini kama nitakufa ili kuiokoa ardhi hii, kuokoa watu wangu, na wengine ambao ni kama wanangu; acha nife.!
Acha sauti hii iwe agano langu kwa dunia kuwa nilisimama kupinga uvamizi wa NATO. Nilisimama kishujaa kupinga usaliti wa nchi za magharibi na nia mbaya za kikoloni. Na hapa nimesimama na ndugu zangu waafrika, kaka na dada zangu waislamu kama ngao yangu ya matumaini.

Wakati wengine walipokuwa wanajenga majumba ya kifahari, mimi niliishi kwenye nyumba ya kawaida na kwenye mahema. Siwezi kusahau maisha yangu ya utoto kule Sirte.
Sikutapanya rasilimali za nchi yangu kipumbavu. Na kama alivyokua Salah-al-Deen, kiongozi wetu katika uislamu, nilichukua kidogo sana kwa ajili yangu, na sehemu kubwa niliwapa wananchi.

Watu wa magharibi wameniita "kichaa", "mwendawazimu" lakini wanajua ukweli kuwa mimi si kichaa wala mwendawazimu; ila waache waendelee kudanganya. Wanajua hii ardhi ni huru na haipo kwenye himaya ya kikoloni. Huu ndio msimamo wangu na dira yangu na imekuwa wazi kwa watu wangu.
Nitapambana hadi pumzi yangu ya mwisho ili watu wangu wawe huru. Mwenyezi Mungu atusaidie tubaki waaminifu na tuwe huru.
-- Mu'uammar Qaddafi.
 
Hivi mnavyosema aliandika mwishoni alijua atauawa au kufa kwa namna aliyokufa au!?
 
Hebu tumia akili kidogo. Hivi hata ingekuwa ni wewe unapata vitu vyoye hivyp kutoka kwa kiongozi aliyepo madarakani ungetamani aondoke?
Uhuru wa watu ndio maendeleo ya kwanza mtu kukupa kila kitu kakunyima uhuru ni sawa na kukufuga ni sawa na kuku unampa pumba lkn hawezi toka bandani lazima binadamu wanao tawala wajue kwamba uhuru wa mtu ni jambo la kwanza ktk sector ya maendeleo .uhuru wa kulima na kuuza bidhaaa .sio nilime mm wewe unipangie tarehe ya kuuza na kupata pesa kama tulilima wote wakati wewe unategemea mshahara
 
Nakumbuka akiwa mbele ya Jengo la Ikulu iliyopigwa kombora Usiku...mchana wake aliisoma hotuba hii... Aliondoka kwa msafara wa magari kutokomea na kuanza kusakwa pande zote
 
Back
Top Bottom