Hotuba ya Rais Karume kwenye Sherehe za Mapinduzi Zanzibar:The Best Ever!

Katika hili la makubaliano kati ya Rais Karume na Seif Hamad, nahisi kuna siri kubwa sana. Naona makubaliano yao yamewaunganisha sana kiasi ambacho hakikutegemewa. Natumaini wataendeleza ushirikiano wao. Uchaguzi Mkuu wa ZNZ, mwaka huu nadhani hautakuwa na fujo hata kidogo.

Tuliyaona haya Kenya pia na ikawa vizuri kabisa. Sasa Mzee Moi anaishi kwa raha mustarehe.
 
Hivyo lini umewasikia wale kule (Zenj) kupigia kelele -hata huo mchele wenu wa Kyela. Si wanakuja na kuununua (kwa mujibu wa taratibu za biashara)

Nafikiri Pakacha hujui hata maana ya Muungano, muungano si kwamba utakwenda Kyela kuchukua mchele wao bure ulitegemea watu wa Kyela wakulishie watoto wako kwa mgongo wa muungano wacha uvivu ndugu yangu ndiyo maana umesema dhahabu ikienda hazina wanapata majeshi tu kwani hujui majeshi ni ya muungano.
 
Dondoo Muhimu:
  1. Kwa ujasiri mkubwa na lugha ya kistaarabu sana, ameyaomba gesi na mafuta yao, yawe yao, kama ilivyo bara na dhahabu yetu.

Tuwaachieni jamani mafuta yenyewe yako wapi, kama ni gesi huku bara ndio kama kiwandani ipo kibao, tusijekuwaudhi waasisi wa taifa letu kwa kitu kidogo, kama yapo kweli acha yawaendeleze na wao, tusije kuwa kama Nigeria au Angola bure.
 

Let us hope.
Kweli tuombe iwe hivyo maana ukifika wakati wa uchaguzi utawaona ndugu zetu hawa wanavyopata shida siyo siri utadhani ni watu wa nchi mbili tofauti wakati mwingine baba anaweza kuwa CCM mama CUF lakini mambo wanayofanyiana kweli yanasikitisha.

Kama kweli Karume na Seif wana dhamira ya kweli ni wa kuungwa mkono na mimi nitalaani mtu yeyote anayewabeza ina maana huwa anafurahia yanayotokea watu wakiteseka kwa kisingizio cha itikadi tofauti what is itikadi mbele ya utu?
 
umeme,maji safi hivi ndio mapinduzi halisi kwa wazanzibar....mambo mengi ya amani na upendo yatakuwepo....leo tuko gizani sijui kama kuna taifa kama ili hapa ulimwenguni.....tuonaomba zanzibar ya uhakika kwa maendeleo sio inayorudi nyuma.
 
Kuna hadithi moja nilisimuliwa, Mwanamme mmoja alifikishwa mahakamani kwa kosa la kumvunja mkono mke wake, kisa walikuwa na mpango wa kufuga bata walikubaliana mambo yote lakini ubishi ukawa nani wa kuzoa mavi ya bata kila asubihi mwanamke alikataa kata kata kuzoa ndiyo kisa cha kuvunjwa mkono wakati hata mtaji wenyewe walikuwa hawana.

Kwa hiyo tusigombanie mafuta ambayo hatuna uhakika nayo tuimarishe mambo yaliyopo kwanza ambayo ni mengi hata Rais mwenyewe alishasema hawezi kuzungumzia kitu ambacho hakipo kwa sasa.
 


Haya ni mawazo ya kutaka kubebwa daima. Hayo majeshi, mapolisi wanalinda usalama wa bara peke yake? Hivi Zanzibar ikivamiwa mnategemea nani atakayewapigania? Hayo maubalozi hayawakilishi Zanzibar? Wazanzibari wengi tu wameelimishwa bara wakati amabapo elimu ilikuwa bure. Hakuna siku waliambiwa wachangie kwa sababu pesa yao ya karafuu haiingii katika kasma ya wizara ya elimu ya bara. Wangapi walisoma na wanaelndelea kusoma katika vyuo vikuu vya serikali vilivyo bara. Mbona hawadaiwi ada ya ziada kwa sababu nchi yao haichangii kwenye bajeti ya elimu ya juu? Miaka yote hii Tanesco imekuwa ikiwauzia umeme zanzibar kwa bei ya kutupa. Na pamoja na hayo Zanzibar imekuwa hailipi. Sasa mnadhani hiyo tofauti kati ya gharama halisi ya umeme na hiyo inayouziwa Zanzibar inabebwa na nani kama siyo SMT? Ubavu wa kuisamehe Zanzibar madeni yake yaumeme iunatokana na mazao na mdini yanayozalishwa bara. Lakini yote haya hamuoni, mnakzania kuwa hamfaidiki na madini na mazao ya bara!

Misaada haitolewi kwa malengo ya SMT peke yake. Mara nyingi hii huongozwa na malengo ya nchi zinazotoa misaada hiyo. Kama Zanzibar haimo katika dira lao basi hakuna kitu ambacho SMT inaweza kufanya. Hakuna nchi inayotoa pesa na lkuiachia nchi inayopokea total freedom ya kufanyia na kuzitumia inapotaka. Kama historia ya Zanzibar katika matumizi ya fedha za misaada ni mbovu kamwe haitapewa. Serikali ya Norway ilimwaga pesa Zanzibar kusaidia sekta ya umeme bila mafanikio ya maana. Pesa zimemwagwa kuborosha bandari ya Zanzibar na matokeo yake wote tunayaona. Hapana, utu uzima ni kukubali responsibilities na si kudai kupewa tuu. Na wenzangu mnaowatetea hawa ndugu zetu hamuwatakii mema maana mnataka wabaki tegemezi. Mwanzo mzuri ungekuwa wao wadai kutoa mchango wao unaoendana na ukubwa wa uchumi wao katika bajeti ya taifa letu. Wakikubali na kufanya hilo, basi hayo mafuta na gesi ambayo hayajapatikana wakae nayo!

Amandla.........
 

Tunarudia makosa yale yale tuliofanya kwenye Muungano wetu. Huu muafaka ulitakiwa upate baraka za wanachama wa vyama vyote viwili kabla hauja-sainiwa. Ulitakiwa uwe wazi na kila mwanachama ajue nini hasa kilichokubaliwa. Muafaka wa kudumu hauwezi kuingiwa kwa siri kati ya Karume na Maalim Seif peke yao. Utakosa legitimacy. Tumeona tunavyosumbuka na huu Muungano walioingia viongozi wetu bila kutushirikisha wananchi. Bila kuweka wazi makubaliano haya basi yaliyopita yatarudiwa tena. Kwa kufanya hivi, kesho na kesho kutwa hakuna atakayekuwa na uwezo wa kuupindisha kwa manufaa yake bila wananchi kumstukia.

Amandla.........
 
Kweli neema imefunguliwa znz.Karume asigombee, awe mshauri tu.Lakini Shamsi Vuai hafai kabisa bora mara mia naibu waziri wa afrika mashariki ndg. Aboud.
 
Wazanzibari wengi tu wameelimishwa bara wakati amabapo elimu ilikuwa bure.

Hii ni kweli kabisa wakati nikiwa UDSM miaka ya 90 wakati tukigomea posho ndogo wao walikuwa hawahangaiki hawajali kwa sababu walikuwa wameshalipiwa tayari na SMT tena wakicheleweshewa SMZ ilikuwa kali kweli kweli kwa madai wanachangia pato la taifa, wakati fulani ilifika hadi bungeni wakati huo wanachuo wa bara tukijihangaikia wenyewe kupitia Daruso. Chuo kikifungwa wao na wanafunzi wa nje walikuwa wakibaki chuoni hata baadhi ya matangazo ya kufunga chuo yalisomeka 'wafuatao hawahusiki wanafunzi kutoka nje na wale wanaotoka upande wa Tanzania visiwani'
 
..lakini Wazenj si wanakuja huku Tanganyika na wanaweza hata kumiliki mashimo ya dhahabu,tanzanite,etc.

..Mtanganyika kuingia Zenj lazima afanye hivyo akiwa na passport. Wazenj wao wanaingia Tanganyika bila kuulizwa maswali yoyote yale.
 

Exactly Mkuu FM.

Na usiri wa namna hiyo, usiotakiwa kuonekana na wengine, unaweza usilete mafanikio ya kudumu. Ili kuuboresha muungano, ni vyema kila mdau akahusishwa vyema katika kuchambua na kupatia utatuzi matatizo yote yaliyopo katika Muungano wetu.

Nionavyo mimi katika hili ni kwamba, kunaweza kuwepo usiri tu, endapo watakubaliana/wamekubaliana jinsi ya kuachiana madaraka kinyume na taratibu zilizopo. Ni kwa mantiki hiyo, ndio maana naona uswahiba wao umekuwa wa ghafla na mkubwa kwa mshangao wa wengi.
 
Bara hata wapate mafuta kedekede lakini yataishia kwenye mikono ya wahindi na papa wa mafisadi
 

Mrema huyo ni Kibaraka wa CCM sisi tunamfahamu, tumechoshwa na kauli zake kama za mlevi.
 
..lakini Wazenj si wanakuja huku Tanganyika na wanaweza hata kumiliki mashimo ya dhahabu,tanzanite,etc.

..Mtanganyika kuingia Zenj lazima afanye hivyo akiwa na passport. Wazenj wao wanaingia Tanganyika bila kuulizwa maswali yoyote yale.

Hapa unaonekana kuonesha kama huu ni ubaguzi, lakini hii hoja haina mshiko.Chukulia mfano Hong-Kong na wachina wa kawaida.Ukiwa wewe ni mchina wa kawaida kuingia Hong-Kong ni sawa na unakwenda Europe, ni lazima ufanyiwe control za immigration na kila kitu.

Lakini alieko Hong-Kong, anaingia sehemu zengine za China kama kawaida.

Sasa hii sio bahati mbaya, kwani wakiachiwa hao wachina wote watakimbilia Hong-Kong na athari zake zinajulikana.

Sasa na Tanganyika kuwekewa vizingiti Zanzibar ni sawa kabisa, kwani watanganyika wote hawawezi kuingia visiwani humo.Ni sehemu ndogo, na ardhi yake ni ndogo.Watanganyika 0.5Mil tuu wahamie Zanzibar, tayari hiko ni kishindo na visiwani huwezi hata kujamba.


Aidha kwa suala la dhahabu na madini mengine Zanzibar inanufaika vipi?Mie sioni jinsi wanavyonufaika.Hii ni general case ya muungano kuwa unanufaisha Tanganyika tuu na kuiwekea guu Zanzibar isiende mbele wala isifurukute.Bajeti yote ya Tanzania ni kuhusiana na Tanganyika tuu, sijawahi kumsikia JK akisema bajeti hii ni kujengea barabara kule Msuka (North-Pemba).

Sasa FUTA wacha wazenji wale peke yao acheni uroho, kuleni Tanzanite....hamushibi?😀
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…