Hotuba ya Zitto ya uhamasishaji Busanda - "Ni zaidi ya uchaguzi"

Nani ni nani Busanda?

  • CHADEMA

    Votes: 80 93.0%
  • CCM

    Votes: 2 2.3%
  • CUF & UDP

    Votes: 4 4.7%

  • Total voters
    86

Sasa ulikuwa na maana gani kusema


This is more of a statement of fact than anything else.
 
Sasa ulikuwa na maana gani kusema



This is more of a statement of fact than anything else.

My apologies for the statement. I never saw or heard any where Mbowe say he will step down. Since you have the info you should give us a source of when & where he said that so we can all know. Otherwise if he really did say that sikum sikia & I'm sorry for that.
 
OOOh my God, what a speech!

Kwa kweli hotuba ni nzuri sana, Lugha yake ni nyepesi na ya moja kwa moja na imeandaliwa. Hotuba hii ina mvuto na imetawaliwa na hoja bila kusahau data.

Nacho shangaa ni njisi ambavyo mpaka sasa thanks zimekuwa chache sana (9) kwa hotuba nzuri kama hii na watu takribani 400 wameiona
https://www.jamiiforums.com/members/zungu-pule.html
 
Last edited:
Tatizo watu Mnadhani Rais ni mtu mmoja, si ki hivyo jamani. Rais Ndo serikali yenyewe huyo mtu anaekalia kiti hicho yeye ni director tu lakini watendaji wakiwa wabovu hata akikaa nani hatoweza kitu kama watendaji wake watamkwamisha tu. Siamini kuwa Mbowe ni failure hivyo mnavyoamini wengi wetu, niaminivyo mimi, Mbowe ana anacheza nafasi kubwa sana kufanikisha utendaji wa hao 11 bungeni na ndo maana wanaweza kuwa na nguvu kiasi hicho. Nimekuwa nikisikiliza hotuba za kampeni 2005, hata mdahalo wa JK na Mbowe, Mbowe alikuwa juu na alifanya vizuri, tatizo lilikuwa ni ule muitikio wa watanzania kama kawaida si wepesi kumwamini mtu kwa haraka, pili Mbowe hakuwa na Muda wa kutosha kuonesha makali yake kama wanavyoupata Zito na timu yake sasa. Hata Dk Slaa Uwezo wake umeonekana sana kwenye hii vita ya Awamu ya Nne.

Kimsingi watanzania hawakuwa na chaguo la kuaminika katika kiti cha Urais kupitia Upinzani kabla Mbowe hajaibuka huko alikotokea na kuigeuzia kibao CCM na kufanya Uchanguzi japo ukachangamka na watu wakaiona chadema.

Mbowe amekuwa sababu kubwa ya watu kuitizama chadema. Nawashangaa watu wanavyosema hapa kuwa mbowe si chochote. Kumbukeni ni Mbowe huyo huyo mnaemdhiaki ndo anakiongoza chama mnachotaka kitawale na yeye ndo amekifikisha hapa kilipo akisaidiana na timu ya wapiganaji 11 wakali waliopo Bungeni.

jamani tusiwe wepesi wa kusahau na wazito wa kukumbuka. Mbowe bado ni mtu Muhimu sana, kuiongoza Chadema. Chadema chini ya uongozi wake imepitia magumu mengi na bado imesimama sioni kwanini watu waseme hafai.

Huyu Zitto leo akigombea Urais atashindwa vibaya na hapo ndo itakuwa mwisho wake. time for him to race for president sit not yet. Watanzania Muwaonavyo sivyo walivyo. Anakufurahia kwa nje ndani anakutukana. Zitto anahitaji another 5yrs ya kuonesha stability then atleast 2015 ndo afikirie kinyang'anyiro cha urais.

This time they have to give another chance to Mbowe, na sisi tumuunge mkono tukiamini kazi nzuri aloionyesha kama mwenyekiti wa chama kwa kipindi chote cha uongozi wake; itaonekana katika kuiongoza serikali pia.

Si busara kabisa kwa sasa ku take risk ya kumtumia Dr Slaa au Zitto kwenye kiti cha Urais maana kwa hali ilivyo bado watanzania wengi sana wanaamini Kikwete anaweza. Bora wanajeshi hao warudi tena Bungeni wakaongeze Nguvu za uzoefu kwa hao wengi wapya tutakaowaongeza. Ni bora kwa sasa ku risk kiti cha urais kwa kumpambanisha Mbowe tena na Mtani wake Kikwete. Wakati huo huo kujihakikishia uimara Bungeni.


....Pamoja tutashinda....
 
ndio chadema ina pendwa lakini ina wabunge 11 kwa hiyo lazima muelewe wanahitaji zaidi ya election moja kushinda uchaguzi na mtu kama zito akiwa mwenyekiti sasa hivi itakuwa ni kujiteketeza mwenyewe kisiasa kwa ajili uwezekano wa kumng'oa JK ni mdogo kutokana na hali ilivyo sasa hivi, watu kama mboe ndio watakuwa wanabeba lawama za chadema na itakapofika wakati wa zito chama kitakuwa kimekuwa kikubwa binafsi na mshauri agombee 2015....

watu naona hawampendi freeman kwa ajili ya bilicana, ile ni biashara tu..
mnasema amefail in bussiness na wakati bilicana ina badilika kila wakati, na inapohitaji ukarabati wa nguvu inapata mkwere nina uhakika hawezi hata ku run duka kwa faida sio yeye tu hata waziri wake wa fedha...

pamoja na misukosuko iliyoikumba chadema bado chama kimekuwa na stability na hii iansema mengi juu ya mbowe
 
Endelea,

Obama hakusubiri apate uzoefu. Kavamia hivyohivyo kichwa kichwa.
Mie nshatangaza kuwa MPAMBE wa Slaa huku Sikonge. Tutahakikisha tunatumia ujanja wa JKT na shuleni kuhakikisha tunapeleka ujumbe kwa kila ndugu, jamaa na marafiki. Ni au MBOWE agombee kuwa mbunge na kuongeza nguvu na Slaa pia au UPINZANI wote uwe chini ya SLAA. Mbowe abaki kuwa BOSS wa chama. Akichukua form za URAIS kumsindikiza JK, mie simo.

YES, SLAA FOR PRESIDAA.
 
Hotuba kuntu sana hii.
Nilitamani kumuona Zitto kwenye warsha ya uzinduzi wa AlmuniPortal Deutscheland pale Diamond ila najua alikuwa amebanwa na ratiba za kampeni. Ila angetoa hata sehemu ya hotuba yake pale ingekuwa sooo catching kwani wajomba wa magharibi walikuwepo pale na ingekuwa jukwaa muafaka la kuendeleza ukombozi wa nchi yetu.
 


Umeshasahau alivyokuwa akiipigia chapuo Dowans ... huyu ni fisadi tu, usidanganywe na hayo maneno ... unalambishwa asali ya kisiasa ... wanasiasa ndivyo walivyo ...
 
Hii hotuba imetulia. Nimependa kwa kweli jinsi ulivyopresent hizo data..simple and reflecting the real life. Big up Zitto.
 
Kama zitto ni mla hela za fisadi basi amelaaniwa kwa unafiki usio na mipaka.
Mimi nimeamua kuamini kuwa ana nia ya kupigania nchi, isiongozwe na wafanya biashara matajiri.
Hopefully, hawa G8 vijana wa mujini hawatapata kura za kuwatosha safari ijayo, hawa ndio nawaogopa sana. Maana they are inteligent, na wanawekwa na watu wenye tamaa zisizo na mipaka, pia inabidi tuwategee kuwapo mpaka tufe, kwani wengi ni vijana
 

Usimuwahishe.... Zitto is inspirational and gifted Tanzanian, lakini nadhani Presidency ni institution na sio person!!! Mwachemwache akomae kidogo, urais hautaki haraka

Tusipoteze mapema, watu wakaanza kuzoea zitto kushindwa

Well done Zitto aka D*****
 
 
 
Jamani hotuba ya ZITO ina hoja za uhakika, za ukombozi.

Mtu ukiisoma machozi yatiririka...

Hata hivyo ni watu wachache sana wanaipata, sisi tunaoisoma kila tunapotaka tupo asilimia moja.

Hii Hotuba sio kwa Busanda pekee...

Ichapishwe kwenye gazeti tena, irudiwe mara nyingi. Pia sisi wana JF tuanzishe kijarida cha JF ambapo tutachangia kuchapisha na kugawa bure.

TUKUSANYE MICHANGO, Tuwasambazie watu wengi zaidi. Tuchapishe kijarida coloured ili watu wengi wavutiwe.

Hata hao wanachama wa CCM waliorithi TANU watageuka na kupigia KURA upinzani. MAANA watajua uozo ndani ya ccm. Mtoto wake ananyima Mkopo UDSM au SUA halafu awe mshabiki wa CCM tu?

Iwe ni vijarida ambavyo vitagawanywa hadi vijijini,

Hapa JF tutasikia,tutajadili hoja nzuri sana sa kuchukia ufisadi lakini hatufaidiki kitu. Hoja zetu zinaishia hapa hapa. Sisi tupo kama mia tano au zaidi???

Nashauri hoja nzuri kama za Zito, Kama za mishahara ya wabunge, na nyingine ziwe zijachapishwa weekly na kugawa Tanzania nzima. Tuamshe wananchi wa vijijini, na hivyo wataelewa na kujua haki zao na ukombozi wa Tanzania.
 
Hii hotuba ya Mh. Zito Kabwe ni nzuri sana, sasa sijui Majambazi na Mafisadi wa CCM watajibu nini, ukweli ni kwamba hawana jibu hata moja zaidi ya kutaka kuendelea kuwaongopea, kuwafisadi na kuwaibia watanzania. Hongera sana Zito yaani hapa nimehamasika.

USHAURI WA BURE: Tafadhali Chadema wekeni sehemu ya watu kukichangia chama kwenye website yenu, muwe mnaruhusu watu kuchangia kwa Credit Cards na Paypal ili wengi wetu tulio mbali nyumbani Tanzania tuweze kuwachangia.
 
Ni hotuba nzuri ana ya kiuanamapinduzi kabisa kama wana Busanda wataelewa basi hakuna haja ya kampeni...Magesa kazi kwake kujipanga...ili akatetee watu wake huko bungeni hakuna ubisshi CCM chali kabsa...hawana jipya na ufisadi wao....aibuuuuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…