Hotuba ya Zitto ya uhamasishaji Busanda - "Ni zaidi ya uchaguzi"

Hotuba ya Zitto ya uhamasishaji Busanda - "Ni zaidi ya uchaguzi"

Nani ni nani Busanda?

  • CHADEMA

    Votes: 80 93.0%
  • CCM

    Votes: 2 2.3%
  • CUF & UDP

    Votes: 4 4.7%

  • Total voters
    86
OOOh my God, what a speech!

Kwa kweli hotuba ni nzuri sana, Lugha yake ni nyepesi na ya moja kwa moja na imeandaliwa. Hotuba hii ina mvuto na imetawaliwa na hoja bila kusahau data.

Nacho shangaa ni njisi ambavyo mpaka sasa thanks zimekuwa chache sana (9) kwa hotuba nzuri kama hii na watu takribani 400 wameiona

Kutoa ni moyo usambe ni utajiri.

Unadhani kila mmoja wetu yupo hapa kuchochea maendeleo ya kweli??
Wengine wapo hapa kuangalia upepo wa kuwaminya mbavu unaelekea wapi na pale wapatapo mwanya hawasiti kuingiza hoja za kuvuruga vichwa vya watu na mwenendo wa hoja.

Ili kutoa thanks shibe ya mawazo inahitajika
 
...siamini kama hawa wananchi watawachagua CCM!
 
Zitto amwaga sumu

  • Wabunge CCM wamenufaika na EPA
  • Wanaopinga wanafanya hadaa
  • Makamba aja juu: Huyo Kagoda nani?

Mwandishi Wetu, Dar na Mwanza Mei 13, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo


WABUNGE wa Chama cha Mapinduzi (CCM) si wasafi kwa vile ni wanufaika wa mbinu chafu zilizowaingiza bungeni, zikiwamo fedha zilizoibwa kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), imeelezwa.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, aliyaeleza hayo, wiki iliyopita, wakati akihutubia katika mkutano wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Busanda, Geita, mkoani Mwanza.

Akihutubia mkutano huo Jumapili iliyopita katika eneo la Katoro, Zitto, ambaye mwenyewe ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, alidai kwamba wabunge wote wa CCM wamepata ubunge kwa kumegewa Sh. milioni tano kila mmoja, fedha zilizoibwa kutoka BoT kupitia EPA.

“Asiwadanganye mtu kwamba ndani ya CCM kuna kiongozi mwenye ujasiri wa kupambana na ufisadi. Maana wameanza kujitokeza baadhi ya wabunge wa CCM eti wakijifanya na wao wana uchungu na nchi hii. Eti na wao wanapambana na ufisadi. Waulizeni walikuwa wapi miaka yote hii nchi ikiuzwa?

“Leo baada ya CHADEMA kuhamasisha umma kwa kupinga ufisadi, nao kwa aibu ya kuogopa kuzomewa ndiyo wanachukua ajenda za CHADEMA ili nao wasionekane mafisadi. Mimi nawaambia, hakuna kiongozi safi ndani ya CCM. Wabunge wote wa CCM walishinda Uchaguzi Mkuu kwa takrima.

“Vita dhidi ya ufisadi ni vita takatifu. Haiwezi kufanywa kwa unafiki. Wala kwa hawa ninaowaita walokole wa vita dhidi ya ufisadi. Mimi nawaambia wabunge wote wa CCM walipewa shilingi milioni tano ambazo ni sehemu ya fedha za ufisadi zilizochotwa BoT kupitia kampuni ya kifisadi ya Kagoda. Waulizeni wakija. Maana wakati walitumia fedha za ufisadi wa Kagoda, leo wanajifanya wanapinga ufisadi,” alidai Zitto.


Baadhi ya wabunge wa CCM waliozungumza na Raia Mwema kati ya juzi Jumatatu na jana Jumanne, kuhusiana na madai hayo ya Zitto ya kutumia fedha za EPA, walikanusha kupokea fedha zozote zenye uhusiano na zilizoibwa BoT kupitia EPA, lakini wengine wakasema waliwahi kupewa fedha za kuwasaidia kutoka Makao Makuu ya CCM kupitia ofisi za mikoa husika.

“Sijui chochote kuhusu hilo. Kama kweli kulikuwa na hizo fedha chafu, basi, mimi sikupata na wala sikusikia kuhusu mgawo huo,” alisema Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela ambaye alipoulizwa kama kweli vita dhidi ya ufisadi wanashiriki kwa unafiki na kwamba walikuwa wapi siku zote aliongeza kwa kujibu;

“Hizo ni siasa tu. Hakuna kingine hapo, vita hii ni ya kila Mtanzania mwenye uchungu na nchi yake bila kujali itikadi. Kwenye CCM tumetamka kabisa katika Ilani yetu ya uchaguzi kwa hiyo kwa upande wangu hakuna unafiki na hata baadhi ya wenzangu katika CCM.”

Mbunge wa Sumbawanga, Paul Kimiti, alipoulizwa kama aliwahi kupata mgawo wa fedha za EPA alisema: “Sikupata na pia sikuwahi hata kupewa msaada wowote wa fedha. Niliwahi kusikia tuhuma hizo za mgawo wa fedha za EPA kwa kusoma magazeti tu, kwa hiyo kama ni kweli basi mimi sikupata.”


Lakini Mbunge wa Kishapu, Fred Mpendazoe, alikiri kupata msaada wa fedha wa Sh milioni mbili kutoka Makao Makuu ya CCM kupitia ofisi ya CCM Mkoa wa Shinyanga, fedha ambazo alisema aliziomba ili kumudu kukamilisha nyongeza ya siku za kampeni baada ya kufariki dunia kwa aliyekuwa mgombea mwenza wa CHADEMA, Rajabu Jumbe, ambaye kifo chake kilisababisha muda wa kampeni za uchaguzi kuongezwa.

“Mimi niliwahi kupewa Sh milioni mbili ambazo niliwasilisha maombi yangu katika Halmashauri ya Mkoa ya CCM. Fedha hizo zilitoka Makao Makuu ya CCM. Sasa hili ni jambo la kawaida siwezi kujua zaidi chanzo cha fedha hizo, lakini naamini hapakuwa na kasoro yoyote.

“ Unajua mara baada ya kufariki kwa mgombea wa CHADEMA fedha ziliniishia. Nikalazimika kuomba msaada katika chama changu na nilizitumia kwa kujaza mafuta na kufanikisha ziara za kampeni. Kwa hiyo nasema fedha zilizosambazwa zilitoka katika chama, na si rahisi kujua zilitoka EPA…Sijui source ya fedha hizo,” alisema Mpendazoe.


Alipoulizwa kuhusu kile kinachodaiwa ni unafiki wa baadhi ya wabunge wa CCM kujitambulisha kuwa wako msitari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi, Mpendazoea alisema: “Hatuna unafiki wala mchezo katika suala hilo. Tumeanza siku nyingi na matokeo yake ni pamoja na utafiti wa kisomi wa REDET kueleza kuwa Bunge ni chombo chenye imani kubwa ya wananchi kuliko hata Serikali.”

Mbunge wa Bukombe, Emmanuel Luhahula, naye alisema: “Kinachojulikana ni kwamba fedha za kusaidia baadhi ya wabunge zilitoka kwenye chama na kutumika katika shughuli za kwenye chama, hili si jambo la ajabu na hata vyama vingine vinatumia fedha kutoka kwenye vyama vyao.

“Zipo rumours (minong’ono) kwamba kuna fedha za EPA lakini mimi sifahamu hilo. Labda uwaulize wabunge wengine wenzangu,” alisema mbunge huyo.


Naye Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba alisema hivi alipoulizwa na Raia Mwema kuhusu madai hayo: “Unajua wewe hapa unazungumza na mtu mkubwa sana, halafu msomi, na hivyo tumia akili. Mimi na wenzangu katika CCM tulikwisha kuwahi kusema hatujui mambo ya Kagoda hapa.”

Aliongeza Makamba: “Tulikwisha kusema Kagoda haina uhusiano wowote na CCM, na wala wamiliki wake hatuna uhusiano nao. Sasa hizo habari zako zinatoka wapi?”

Hii si mra ya kwanza kwa Kampuni ya Kagoda kuhusishwa na wizi wa fedha za EPA na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005. Kampuni hiyo pekee inadaiwa imechota zaidi ya Sh. bilioni 40 kutoka akaunti ya EPA, na imekuwa ikihusishwa na watu ndani ya CCM na serikali lakini mara zote CCM imekuwa ikikanusha kuhusika nayo na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya kampuni hiyo.

Tayari wahusika wa kampuni kadhaa zinazotuhimiwa pia katika wizi wa EPA wamekwisha kufikishwa mahakamani, wengi wakiwa ni wale ambao mazingira ya uchotaji wao yanadaiwa hayatofautiani kabisa na Kagoda.

Wizi wa fedha za EPA kwa kipindi cha mwaka mmoja tu 2005/2006 uliokaguliwa umeigharimu Serikali sh bilioni 133, kati hizo Sh bilioni 90 zikiwa ni zile ambazo wakaguzi wa ndani na wa nje wamebainisha kwamba zilichukuliwa katika mazingira ya kijinai na wahusika wakiwamo wa Kagoda wanastahili kuchukuliwa hatua huku Sh bilioni 43 zikielezwa kuhitaji uhakiki wa kimataifa.

Katika hatua nyingine, Zitto alisema kwenye mkutano huo wa kampeni kuwa uchaguzi mdogo wa ubunge wa jimbo la Busanda ni muhimu si tu kwa wakazi wa eneo hilo, bali Watanzania kwa ujumla.

“Uchaguzi huu ni sawa na kura ya maoni ambayo katika nchi nzima nyie watu wa Busanda ndiyo mmepata fursa hii ya kujibu. Mmepata fursa ya kuwaambia watawala tarehe 24, Mei mwaka huu kama mnakubaliana na mwenendo huu wa watawala au hamkubaliani. Mnaridhika au hamridhiki.

“Hii ndiyo maana ya uchaguzi huu. Ni uchaguzi wenu wakazi wa Busanda. Sisi tumekuja kuwawezesha tu. Tumekuja kuwaunga mkono mfanye maamuzi sahihi kwa niaba ya Watanzania wengine ambao hawakupata fursa hii.

“Nimesikia hapa mji mdogo wa Katoro, ambayo ni makao makuu ya jimbo, hamna umeme. Hamna tofauti na Kasulu wala Kibondo mkoani Kigoma. Madhara ya kukosa umeme si tu kwa wenye uwezo wa kuwa na umeme kukosa umeme, hali hii inasababisha gharama za maisha kuwa juu, kwa sababu gharama za uzalishaji zinakuwa juu.

“Tulifanya utafiti Dar es Salaam kwa vijana vinyozi. Umeme ukikatika wakawasha jenereta wanatumia shilingi 68,000. Lakini wakitumia umeme wa TANESCO wanalipia shilingi 8,000 tu. Maana yake kwa kutumia umeme wa jenereta wanapata hasara ya ziada ya shilingi 60,000. Hii ni tafiti iliyofanywa na Kamati ya Bunge. Kwa hiyo si Katoro tu. Nchi nzima ni tatizo.

“Kwa hiyo unaona thamani ya kura yako ilivyo kubwa. Kura yako ina thamani ya mabilioni. Lakini leo tunasikia CCM wanapita wanawahonga watu shilingi elfu mbili, tatu, nne, tano. CCM inajua bei za wateja wake. Ukiwa mjanja mjanja kidogo inakupa hata 10,000. Ukiwa hujui kitu kabisa inaweza kukupa hata shilingi mia moja. Lakini wote hawa ni wajinga, tofauti yao ni bei za ujinga wao.

“Ukiuza shahada yako maana yake unahujumu maendeleo ya Taifa lako. Unahujumu maisha ya watoto wako. Lazima mjiulize kwa nini mtu akupe pesa kukuzuia usipige kura? Watoto wenu hapa wanasoma shule za kata zisizo na walimu, vitabu, wala maabara kwa sababu mnakosea kupiga kura,” alisema.


Harakati za kampeni Busanda zinaendelea na vyama kadhaa kila kimoja kimesimamisha mgombea, vyama hivyo ni CHADEMA ambacho mgombea wake ni Finias Magesa, CCM mgombea wake Lolensia Masele, Beatrice Lubambe wa United Democratic Party (UDP) na na Oscar Ndalahwa wa Civic United Front (Chama cha Wananchi -CUF).
 
Kweli hotuba ni nzuri sana. Big up guys you are the one for the change. U have my support!
 
Tarehe ya Mei 09, 2009 baada ya maandamano makubwa yaliyotanguliwa na Bango
> lenye ujumbe “ Karibu Zitto Kabwe, Karibu Obama wa Tanzania, Mwongoze
> Magessa Bungeni, huku mbele yake wakiwa vijana waliobeba jeneza
> lililozungushwa kitambaa cha kijani katika kata ya Katoro ambayo ndio kata
> yenye wapiga kura wengi takribani asilimia thelathini ya wapiga kura wote wa
> jimbo la Busanda.
>
> “ Leo ni furaha isiyo kifani kwa maandamano na mahudhurio makubwa kiasi
> hiki. Umati huu mkubwa unanikumbusha Mkutano wangu mkubwa wa kwanza kuwahi
> kufanya, Mkutano wa Jangwani niliofanya viwanja vya Jangwani baada ya
> maandamano marefu ambapo watu takribani laki mbili waliandamana na
> kukusanyika viwanja vya Jangwani mwezi Agosti 2007 wakipinga uamuzi wa
> wabunge wa chama cha mafisadi-CCM, kunisimamisha ubunge baada ya kuwashinda
> kwa hoja, katika mjadala uliohusu mkataba mbovu na wakifisadi wa Buzwagi.
>
> Ni imani yangu mahudhurio haya tafsiri yake ni imani yenu kwa mgombea wetu
> Finnias Maggesa. Ni imani yangu kuwa Busanda na Katoro hamtatuangusha.
> Viongozi wenzangu waliotangulia kuhutubia wamezungumzia matatizo mengi
> yanayolikumbuka taifa letu, matatizo ambayo kwa miaka 48 utawala wa CCM
> umeshindwa kuyatatua.
>
> Mtakumbuka matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2005 kwa kura halali na zisizo
> halali yalikipa CCM ushindi wa wabunge 274 na CHADEMA wabunge 11.Lakini kwa
> kipindi cha miaka mitatu, wabunge 11 wa CHADEMA tumeweza kuhakikisha masuala
> mengi muhimu kuhusu mwenendo wa Taifa letu yanajulikana kwa Umma. Bila
> CHADEMA watanzania wasingejua ufisadi wa Buzwagi, EPA wala ufisadi wa
> Richmond uliosababisha serikali ya awamu ya nne kuanguka. Nasema kuanguka
> kwasababu kikatiba waziri mkuu ndio mwenye serikali. Kwahiyo serikali hii ni
> ya awamu ya nne na nusu.
>
> Wananchi wa Busanda, Ingawa tupo wabunge 11, lakini CHADEMA tupo makini
> kukabiliana na utawala huu mbovu chini ya uongozi mahiri wa Naibu Kiongozi
> wa kambi ya upinzani bungeni,na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dr Willibrod Slaa.
> Hii ndio sababu kwanini tunaomba mtuongezee mpiganaji wa 12, ambaye si
> mwingine bali kijana wenu, msomi wetu, mwenye sababu za kutosha kwa
> mapambano haya, Finias Magessa.
>
> Ndugu zangu wa Busanda, Uchaguzi huu sio uchaguzi wa Ilani za vyama.
> Uchaguzi wa Ilani za vyama ulikuwa mwaka 2005, ndipo vyama viliomba kura kwa
> Ilani , na CCM ikapata asilimia 86 ya wabunge pamoja na Urais. Mwenendo wa
> serikali ya CCM wote mmeouna. Wanasikitisha na kukatisha tama wananchi. Ndio
> maana ninawaambia, Ilani ya CCM ni ileile, kama kwa kuwapa wabunge zaidi ya
> 200 pamoja na Urais wameshindwa kuwatumikia, mnadhani mkichagua mbunge huyu
> mmoja wa CCM atabadilisha kitu? Ataongeza nini kama wenzake zaidi ya 200
> wameshindwa ? Jamani CCM hawana nyongeza ya Ilani! Ni hivi hivi! Ndio maana
> ninawaambia kwamba uchaguzi huu ni muhimu sana sio tu kwa nyie wakati wa
> Busanda, bali watanzania kwa ujumla. Ni kipimo. Ni kura ya maoni ambayo
> katika nchi nzima nyie watu wa Busanda ndio mmepata fursa hii ya kujibu.
> Mmepata fursa ya kuwaambia watawala tarehe 24, Mei mwaka huu kama
> mnakubaliana na mwenendo huu wa watala au hamkubaliani. Mnaridhika au
> hamridhiki.
>
> Ukipigia kura mgombea wa CCM Mei 24, tafsiri yake ni kwamba unaridhika na
> mwenendo wa utawala wa CCM, na ukipigia kura CHADEMA maana yake ni kwamba ni
> unatuma ‘signal’ kwa watawala wetu kuwa hauridhiki na mambo yanavyokwenda
> katika nchi yako.
>
> Ndugu zangu wa Busanda, labda nyie hamkumbuki CCM inatupeleka awamu mmoja
> hadi nyingine. Kwa mujibu wa taarifa ya Hali ya Umasikini na Maendeleo
> nchini, Mwaka 2005, Tanzania ilikuwa na wananchi ambao ni fkara milioni 11,
> yaani hawa wanaishi chini ya dola moja kwa siku. Yaani mapato yao ni chini
> ya ya shilingi 1300 kwa siku.
>
> Rais Jakaya Kikwete alipokuwa kwenye kampeni aliahidi maisha bora kwa kila
> mtanzania. Na CCM ikaahidi kwenye ilani yake kwamba itapunguza idadi ya watu
> hawa masikini kabisa kwa asilimia 50%. Leo mwaka 2009, mwaka mmoja kabla ya
> mwaka wa uchaguzi 2010, Taarifa ya Hali ya umasikini inaonesha kuwa idadi ya
> watanzania wanaoishi chini ya kipato cha dola moja(shilingi 1300) kwa siku
> wameongezeka badala ya kupungua, na sasa wamefikia milioni12.7. Umasikini
> unapungua, au unaongezeka?
>
> Hili ndilo Busanda mnalo Mei 24. Ukipigia kura CCM maana yake unakubaliana
> na mwenendo wa serikali ya CCM uliosababisha idadi ya masikini kuongezeka
> mwaka hadi mwaka. Leo mwaka 2009 masikini kabisa wameongezeka kufikia
> milioni 12.7 kutoka milioni11 mwaka 2005. Maana yake katika miaka 3 CCM
> imeongeza idadi ya watu masikini kabisa milioni moja na laki saba.. Kwa
> mwenendo huu, Je kufikia kipindi cha uchaguzi wa 2010 watanazania wangapi
> watadumbukia kwenye shimo hilo la masikini kabisa? Milioni3? 5?.
>
> Hii ndio maana ya uchaguzi huu. Ni uchaguzi wenu wakazi wa Busanda. Sisi
> tumekuja kuwawezesha tu. Tumekuja kuwaunga mkono mfanye maamuzi sahihi kwa
> niaba ya watanzania wengine ambao hawakupata fursa hii. Mkichagua CCM
> mtakuwa mmewaangusha watanzania. Watanzania wana imani kubwa na nyie
> mliochaguliwa na Mungu kupiga kura hii ya maoni!
>
> Hebu fikiria wewe Baba na Mama wa Busanda. Mwaka 2005, katika kila wanawake
> 100,000, wanawake 520 walifariki dunia kutokana na matatizo ya ujauzito, Leo
> mwaka 2009, wanawake 527 wanafariki kutokana na matatizo ya ujauzito,
> matatizo ambayo msingi wake ni huduma duni za afya. Takwimu hizi maana yake
> nini? Maana yake katika kila lisaa limoja la Tanzania chini ya utawala wa
> CCM mwanamke mmoja anafariki dunia kutokana na matatizo ya ujauzito
> yanayosababishwa na serikali kutojali wanawake wan chi hii, na zaidi
> wanawake wa vijijini kama Busanda.
>
> Hebu fikirieni ninyi wazazi na wakazi wananchi kwa ujumla. Mwaka 2005,
> katika kila watoto 1000, watoto 114 walipoteza maisha kwasababu ya matatizo
> ya uzazi, leo mwaka 2009, watoto 112 wanafariki dunia kwa matatizo hay
> ohayo. Tarehe 24 Mei unapokwenda kupiga kura maana yake unakwenda kujibu
> swali hilo. Ukimpigia kura Magessa wa CHADEMA maana yake unapinga watoto
> wasio na hatia kuendelea kufriki dunia kwasababu zinazotibika kabisa. Na
> ukipigia kura CCM maana yake unakubaliana na mwenendo wa vifo vya watoto
> wasio na hatia kama hivi.
>
> Sisi CHADEMA tunaomba utupigie kura katika uchaguzi huu ili watawala
> washituke, wajirekebishe. Wajue kwamba watanzania haturidhiki na mwenendo
> huu wa umasikini na vifo. Wewe mwananchi ukiipigia CCM kura hawatajua kama
> kuna tatizo, hawatajua kama wananchi wanaumia. Hawatajirekebisha.
>
> Hali ya Taifa hili ni mbaya sana. Na tusipoangalia, Taifa hili tutalipeleka
> shimoni kabisa. Tangu mwaka 2007, Asilimia 38% ya watanzania wamedumaa akili
> kutokana na lishe duni. Maana yake nini? Maana yake katika kila watanzania
> 100, watanzania 38 wamedumaa akili, hawafikiri vizuri kutokana na lishe
> duni. Lishe duni ni ‘indicator’ ya ufukara. Kama madiwani wa CCM ni
> watanzania wa kawaida, basi katika kila madiwani 10, madiwani 4 wamedumaa
> akili. Au katika kila wabunge 10( wa CCM lakini), wabunge 4 wamedumaa akili
> kama wanatoka familia za kawaida. Hivyo hivyo kwa mawaziri wa serikali ya
> CCM, kwamba inawezekana katika kila mawaziri 10, mawaziri 4 wamedumaa akili.
> Pengine ndio sababu wamekuwa wanasaini mikataba mibovu ya kifisadi.
>
> Kwahiyo tarehe 24, Mei, Ukichagua CCM, maana yake ni kwamba unaunga mkono
> mwenendo wa serikali ya CCM kusababisha watanzania 4, katika kila watanzania
> 10 wawe waendelee kudumaa akili. Na ukimpigia kura Magessa wa CHADEMA, maana
> yake ni kwamba, unapinga , unakasirishwa na mwenendo huu. Jamani taarifa
> hizi hatuzitungi sisi! Wala hatuziandai sisi. Ni taarifa za serikali.
> Ukisoma taarifa ya serikali ya Hali ya Umasikini na Maendeleo nchini (Pverty
> & Human Development 2007).
>
> Haya ndio maswali CCM wakija muwaulize, ingawa sidhani kama watafanya
> mikutano ya hadhara mana nimesikia wanaogopa sana kuzomewa kwa uzembe na
> ufisadi wa serikali yao.
>
> Nimesikia hapa mji mdogo wa Katoro, ambayo ni makao makuu ya jimbo hamna
> umeme. Hamna tofauti na Kasulu wala Kibondo mkoani Kigoma. Madhara ya kukosa
> umeme sio tu kwa wenye uwezo wa kuwa na umeme kukosa umeme, hali hii
> inasababisha gharama za maisha kuwa juu, kwasababu gharama za uzalishaji
> zinakuwa juu.Tulifanya utafiti Dar es Salaam kwa vijana vinyozi. Umeme
> ukikatika wakawasha jenereta wanatumia shilingi 68,000. Lakini wakitumia
> umeme wa TANESCO wanalipia shilingi 8000 tu. Maana yake kwa kutumia umeme wa
> jenereta wanapata hasara ya ziada ya shilingi elfu sitini. Hii ni tafiti
> ilifanywa na Kamati ya bunge. Kwaiyo sio Katoro tu. Nchi nzima ni tatizo.
>
> Nilazima watanzania tutafakari kama tunakokwenda ni sahihi au la! Na tufanye
> maamuzi. Wakati tunapata uhuru, Asilimia 15 ya watanzania walikuwa na
> Umeme.Leo ikiwa ni miaka 48 ya Uhuru, watanzania wanaopata huduma ya umeme
> hawazidi asilimia 12. Maana yake katika nchi hii yenye umri wa miaka 48 ya
> uhuru, katika kila nyumba 100, ni nyumba 12 tu ndizo zenye umeme, ilhali
> wakati wa uhuru, katika kila nyumba 100, nyumba 15 zilikuwa na umeme.
>
> Kwahiyo ukienda kupiga kura tarehe 24, Mei, unapaswa kujiuliza kama
> unakubaliana au hukubaliana na mwenendo huu. Ukichagua CCM maana yake
> unaridhika kuona kwamba wakati miaka 48 iliyopita watanzania walikuwa na
> huduma ya umeme ilikuwa 15, ni sawa, na sio tatizo kwa leo Tanzania huduma
> ya umeme kuwa asilimia 12.Naukiipigia kura CHADEMA mana yake unatma ujumbe
> kwa watawala kwamba unaumizwa na hali hii. Haukubaliani na hali hii.
>
> Njia pekee yaw ewe mkazi masikini kukataa hali hii ni kukataa kuipigia kura
> CCM. Ni kuipigia kura CHADEMA. Ni muhimu uone kama nafasi hii adimu kuwa
> muhimu sana kwako. Maana uchaguzi huu umefanyika kwasababu ya mipango ya
> Mungu. Na tunao amini katika Mungu, tunaamini kwamba mipango ya Mungu haina
> makosa. Na kila mpango una busara yake. Msituangushe kwakupewa fursa hii
> kabla ya miaka5 kukamilika.
>
> Hali ni mbaya ndugu zangu. Tanzania nzima ina majimbo 232. Lakini ni ninyi
> watu wa Busanda mliopewa fursa ya kuchagua tena kabla ya miaka 5. Nimesikia
> viongozi wa CCM wakipita na kuahidi eti CCM ikishinda uchaguzi huu italeta
> umeme Busanda. Waulizeni walikuwa wapi miaka 48 yote hii. Kama wameshindwa
> kuleta ndani ya miaka 48, watawezaje ndani ya mwaka 1?
>
> Ndio maana sisi CHADEMA tunawaambia watanzania kwamba uchaguzi huu ni kura
> ya maoni , Tunaamini mtachagua CHADEMA ili kuonyesha kwamba hamkubaliani.
> Kuna matatizo mengi sana wilaya hii ya Geita. Kwa mujibu wa taarifa za
> uchumi za mwaka 2006, Geita ni miongoni mwa wilaya tatu masikini kabisa
> Tanzania, ikiwa pamoja na Bunda na Musoma vijijini.
>
> Ninyi wilaya yenu ya Geita, unaozalisha takribani wakia laki tatu na nusu
> kwa mwaka, ambazo ni sawa na bilioni 211 kwa bei ya sasa. Lakini utajiri huo
> hauna tafsiri yoyote kwa maisha yenu. Sisi kwenye Kamati ya Bomani
> iliteuliwa kupitia upya mikataba ya madini nchini tulipendekeza kanuni ya
> kukokotoa mrabaha kwanza ibadilishwe kutoka asilimia tatu hadi 5, lakini
> zaidi hesabu hizo zikokotolewe kutokana na gharama zote za uzalishaji, na
> sio mwekezaji azalishe kasha aondoe gharama zote za uzalishaji kasha ndio
> atupe watanzania asilimia 3 tu ya hilo salio. Kwasababu CCM haina dhamira ya
> kuwasaidia, bado imeendelea kupiga danadana utekelezaji wa Kamati yetu.
>
> Baada ya vuguvugu la kupinga mikataba mibovu liliasisiwa na CHADEMA tangu
> sekeseke la Buzwagi, Leo Geita mnapata dola laki 2 kutoka mgodi wa dhahabu
> wa Geita( Geita Gold Mining-GGM). Kule Tarime, Halmashauri ile chini ya
> Uongozi wa CHADEMA, kwa kuamini kuwa wawekezaji wanatunyonya watanzania
> wakawaida kwasababu ya elimu duni, CHADEMA tuliamua fedha yote ile ipelekwe
> kusomesha watoto bure kwa shule za sekondari. Ni kweli fedha hizi ni kiduchu
> sana, lakini si haba. Sio sawa na kukosa kabisa. Sasa kama Tarime fedha hizi
> zinasomesha watoto. Nyie wilaya ya Geita fedha hizi zinakwenda wapi?
> Zinaishia kwenye warsha, vikao na makongamano ya madiwani.
>
> Yote haya ni matokeo ya utawala dhaifu na usiowajali wa Chama cha
> Mapinduzi-CCM. Kwa mfano, kama Serikali ya CCM ingekubali kuetekeleza
> mapendekezo ya Kamati ya Bomani, Badala ya wilaya zenye migodi kupewa dola
> 200,000. Kila wilaya yenye mgodi ingelipwa dola milioni2 kwa mwaka. Yani
> mara 10 zaidi ya sasa.
>
> Tarehe 24 Mei, ukienda kupiga kura, ukichagua CCM, maana yake unakubaliana
> na utaratibu wa sasa wa CCM kutoa dola laki mbili kwa mwaka kwa halmashauri
> yako badala ya dola milioni mbili kama Kamati ya Bomani inavyotaka unufaike
> na madini. Kura yako ni alama! Ukienda ukampigia kura Magessa, maana yake
> unataka Serikali ya CCM itoe dola milioni mbili badala ya dola laki mbili
> kwa Halmashauri yako.
>
> Kwaiyo unaona thamani ya kura yako ilivyo kubwa. Zaidi ya utu wako, kura
> yako ina thamani ya mabilioni. Lakini leo tunasikia CCM wanapita wanawahonga
> watu shilingi elfu mbili, tatu,nne, tano. Inajua bei za wateja wake. Ukiwa
> mjanja mjanja kidogo inakupa hata elfu kumi. Ukiwa hujui kitu kabisa inaweza
> kukupa hata shilingi mia moja. Lakini wote hawa ni wajinga, tofauti yao ni
> bei za ujinga wao.
>
> Ukiuza shahada yako maana yake unahujuma maendeleo ya Taifa leko. Unahujumu
> maisha ya watoto wako.Lazima mjiulieze kwanini mtu akupe pesa kukuzuia
> usipige kura? Watoto wenu hapa wanasoma shule za kata zisizo na walimu,
> vitabu, wala maabara kwasababu mnakosea kupiga kura.
>
> Kura yako ni muhimu sana. Ukipigia kura CCM maana yake unaunga mkono
> ufisadi. Ukipigia kura CHADEMA maana yake umeamua kuunga mkono harakati za
> uzalendo. CCM haijawi kuwa na huruma baada ya Mwalimu Nyerere.
>
> Wakati kwa kipindi cha miaka 10, tangu mwaka 1997 hadi mwaka 2006, Bunge la
> Tanzania halikuwa limepata hoja binafsi kutoka kwa mbunge yeyote, Hoja
> binafsi ya kwanza ilitolewa na mimi Bungeni, Hoja ya Buzwagi kupinga ufisadi
> katika mikataba ya madini ambapo baada ya kuwashinda kwa hoja, bunge la CCM
> mafisadi waliamua kunisimamisha kazi yangu ya uwakilishi. Na hoja binafsi ya
> pili ni hoja ya ufisadi wa benki kuu iliyowasilishwa na Katibu Mkuu wa
> CHADEMA, Dk Willibrod Slaa, ambayo ilikataliwa na tukaamua kuipeleka kwa
> Umma septemba 15, 2007 , na mpaka leo bado inaisulubu serikali ya CCM.
>
> Tangu sekeske la Buzwagi, Agosti 14, 2007, Hali ya taifa ni tete haijawahi
> kutokea tangu uhuru, na itaendelea kuwa tete mpaka hapo watanzania
> watakapofaidika na rasilimali za nchi yao. Na Tanzania haitafikia hali hiyo
> chini ya utawala wa CCM. Njia pekee ni kuondoa utawala huu uliojaa wezi,
> wasio na uchungu na maisha yaw ewe masikini wa Busanda.
>
> Asiwadanganye mtu kwamba ndani ya CCM kuna kiongozi mwenye ujasiri wa
> kupambana na ufisadi. Mana wameanza kujitokeza baadhi ya wabunge wa CCM eti
> wakijifanya na wao wana uchungu na nchi hii. Eti na wao wanapambana na
> ufisadi. Waulizeni walikuwa wapi miaka yote hii nchi ikiuazwa? Leo baada ya
> CHADEMA kuhamasisha Umma kwa kupinga ufisadi, nao kwa aibu ya kuogopa
> kuzomewa ndio wanachukua ajenda za CHADEMA ili nao wasionekane mafisadi.
> Mimi nawaambia, hakuna kiongozi safi ndani ya CCM. Wabunge wote wa CCM
> walishinda uchaguzi Mkuu kwa takrima.
>
> Vita dhidi ya ufisadi ni via takatifu. Haiwezi kufanywa kwa unafiki. Wala
> kwa hawa ninaowaita walokole wa vita dhidi ya ufisadi.. Nimeambiwa watakuja
> hapa akina Olesendeka, akina Dk Mwakyembe na wenzao. Mimi nawaambia wabunge
> wote wa CCM walipewa shilingi milioni5 ambazo ni sehemu ya fedha za ufisadi
> zilizochotwa benki kuu kupitia kampuni ya kifisadi ya Kagoda. Waulizeni
> wakija. Mana wakati walitumia fedha za ufisadi wa Kagoda, leo wanajifanya
> wanapinga ufisadi. Wapi na Wapi jamani?
>
> Ndio maana nawaambia kuwa uchaguzi huu wa Busanda ni wa kihistoria. Mnayo
> nafasi ya kuamua kuiangusha CCM, mnayo nafasi ya kutukataa. Sisi tupo
> wabunge 11. Lakini kazi tuliyoifanya kwa miaka hii mitatu tunaamini, kama
> mnaipenda nchi yenu mtatuongezea wabunge. Tumpate mpiganaji wa 12, Ndugu
> yangu Finias Magesa. Mkituchagua mtakuwa mmetupa moyo, na itatusaidia
> kuongeza mapamabno zaidi. Lakini mkituangusha mtakuwa mnatuvunja moyo. Ni
> sawa na kutuambia kuwa mapambano yetu dhidi ya ulinzi wa rasilimali za
> madini na vita dhidi ya ufisadi ni kelele tupu.
>
> Tumekuwa tukiwaambia watanzania. Mwenyezi Mungu hakudhmilia nchi hii iwe na
> watu masikini kiasi hiki. Hebu angalieni, Kanda ya ziwa imejaa dhahabu,
> Almasi, Nickeli na Almasi. Kanda ya Magharibi imejaa Shaba, Mafuta na madini
> ya fedha. Kanda ya kati ya ina madini ya uranium yanayotumika kutengenezea
> mabomu ya nuclear, Kanda ya Pwani imejaa gesi na mafuta. Kanda ya kusini
> imejaa makaa yam awe. Kila kanda Mungu ameipa utajiri. Lakini masikini
> wamejaa juu ya ardhi tajiri. Kwanini msichukue hatua? Mimi ninawaambia. Njia
> pekee ya kutoka hapa tulipo kwanza ni kuikataa CCM.Ndio maana ninarudia!
> Uchaguzi huu ni zaidi ya uchaguzi. Ni kipimo kama mnaridhika au hamridhiki
> na mwenendo wa utawala wa namna hii.
>
> Katika uchaguzi wa 2005, CCM waliwaahidi maisha bora kwa kila mtanzania
> kufikia mwaka 2010. Leo ni 2009, mwaka mmoja kabla ya uchaguzi, Wangapi
> maisha bora walau yamepiga hodi kwao? . Mwaka 2005 bei ya kilo ya sukari
> ilikuwa shilingi 600, leo bei ya sukari shilingi 1400. bei imepanda zaidi ya
> mara mbili, Je mapato yenu yamepanda au yameshuka? Bei ya khanga za akina
> mama mwaka 2005, khanga ya India ilikuwa sh 2000. Leo naambiwa hapa Busanda
> khanga ileile inauzwa shilingi 3500. Mfuko wa saruji mwaka 2006 uliuzwa kwa
> shilingi 11,000. Leo mwaka 2009 mfuko wa saruji unauzwa shilingi 21000.
> Mwaka 2006 nauli kutoka kijiji chochote cha jimbo la Busanda kwenda Geita
> ilikuwa ni shilingi 1000 mpaka 2000 tu.
>
> Leo mwaka 2009, nauli zimepanda hadi shilingi 3000. Lazima mjiulize kweli
> mapato yenu yamepanda?. Kweli haya ndio masiha bora mliyotarajia? Wakati
> bidhaa hizi zinapanda bei, mazao yenu ya kilimo kama pamba serikali
> imeshindwa kuzuia yasiporomoke bei. Wakati mwaka 2006 kilo ya pamba iliuzwa
> kwa shilingi 400, leo mwaka 2009, kilo ya pamba inauzwa kwa shilingi 300. Na
> haya ndio maisha bora mliyoahidiwa na CCM. Mapato yenu yanaporomoka, uwezo
> wenu wa kununua unashuka, lakini bidhaa za kununua zinaachwa zipande bei.
>
> Tarehe 24, Mei ukienda kupiga kura , ukichagua CCM maana yake unakubaliana
> na gharama za maisha kupanda. Ukichagua CHADEMA na Magessa maana yake
> unatuma ujumbe kwa watala kwamba hakubaliani na kupanda kwa gharama za
> maisha.
>
> Najua kwamba watawala hawa walioshindwa wamekuwa wakitumia nguvu za dola
> kukabiliana na utashi wa wananchi walioamua kufanya mabadiliko. RPC na OCD
> naomba mnisikilize kwa makini. Mjue kwamba chochote mlichovaa, kuanzia
> kiatu, magwanda ni kodi zetu wananchi. Na labda wananchi mkumbuke kuwa hawa
> polisi, wengi ni watoto wa masikini kama sisi. Ni mgawanyo wa kazi, wengine
> wanakuwa walimu, wengine madkari, wengine polisi, wengine wabunge. Sasa
> kwenda kwenu upolisi kusiwafanye mgeuke tatizo kwa wananchi badala ya
> kuwalinda.
>
> Polisi mnapaswa kukumbuka kuwa ninyi ni watoto wa masikini kama sisi.
> Mkimtesa kijana wa Busanda, basi ujue kwamba na wewe kwenu mdogo wako
> anateswa na polisi mwenzako. Ukimtesa mama wa Busanda hapa, ujue kwamba
> polisi mwenzako anamtesa mama yako huko kwenu. Ukimtesa mzee wa Busanda,
> ujue na wewe wazee wako wanateswa na polisi wenzako huko kwenu.
>
> Polisi wanapaswa kukumbuka ni sisi wabunge tunaojadili na kupitisha bajeti
> zao. Na sisi wabunge wa upinzani siku zote tumekuwa mstari wa mbele kudai
> maslahi bora ya polisi ili kupunguza udokozi wa polisi kwa wananchi masikini
> kabisa, na kuwasababishia usumbufu, na kukosa amani. Hatutaki polisi
> watupendelee, wala watuonee. Wakituonea tutajibu. Wakipendelea CCM
> tutakataa. Polisi wanapaswa kujua leo ni polisi, kesho raia. Hatutaki polisi
> waonee raia, ingawa hatutaki raia wavunje sheria.
>
> Jamani polisi wa Tanzania ndio polisi wanaolipwa kidogo kuliko polisi wote
> katika nchi kumi na mbili za SADC. Nchi zingine kama Malawi ambazo uchumi
> wake unategemea tumbaku lakini polisi wake wanalipwa vizuri kuliko polisi
> wetu, Nchi yenye madini, ziwa, bahari, ardhi yenye rutuba, watu wenye moyo
> wa kufanya kazi na kila aina ya utajiri.
>
> Polisi wanapaswa kufikiria upya kuhusu ukandamizaji wanaoufanya dhidi yetu
> wapinzani maana wao ni sehemu yetu. Wote tumepigika tu! Polisi ndio
> wanaolinda benki kuu, lakini wakati mafisadi yanaingia benki kuu, polisi
> wetu wanapiga ‘saluti’, mafisadi yanaingia yanachota mabilioni ya fedha,
> yanatoka. Polisi wanabaki ni wakukamata vibaka wanaoiba masufuria, mbuzi,
> kuku, na vitu vidogo vidogo. Mapapa na manyangumi yanayohujumu uchumi wetu
> hayaguswi.
>
> Mimi Zitto Kabwe nawambia, sitaki kusikia mtanzania yeyote wa Busanda
> ananyanyaswa na polisi eti kwa sababu ya chama chake.Nikipata polisi mmoja
> anayenyanyasa raia kwa sababu tu ya chama chake, nitamfanyia kazi kama
> nilivyomfanyia Nazir Karamagi. Na nilipokuwa Tarime kwenye uchaguzi mdogo
> niliwaambia polisi kauli kali kwasababu ya ujinga na upumbavu wa baadhi ya
> polisi. Sitarajii yaliyofanywa na polisi Tarime yatajirudia Busanda. Yeyote
> atakaye nyanyaswa na polisi hapa atoe taarifa kwa viongozi wa CHADEMA. Ila
> msivunje sheria.Hatutamtetea yeyote atakaye vunja sheria. Tunataka uchaguzi
> wa amani, tumapate Magessa tujenge taifa hili, Kazi ambayo CCM imethibitisha
> kwa vitendo kuwa wameshindwa.
>
> Tarehe 24, Mei mchague Magessa akutetee wewe mkazi wa Katoro, awatetee
> wakazi wa jimbo la Busanda. Awatetee wakazi wa mkoa wa Mwanza. Awatetee
> watanzania. Mkoa wa Mwanza una majimbo 11, yote mkaipa CCM. Kuna Kikao cha
> Kamati ya mashauriano ya mkoa, RCC, Nani atawatetea kwenye RCC ilhali
> mmejaza wabunge wa CCM humo?
>
> Mimi nawaambia kutoka uvungu wa moyo wangu kwamba, wabunge wa CHADEMA hata
> tufanye kazi namna gain Dodoma, kama hamna ‘mbwa’ mkali Geita, Mwanza,
> mtaendelea kuibiwa tu!. Tunahitaji mbwa mkali ambaye akiona ufisadi kwenye
> Halmashauri, RCC na Serikali kuu aje kuwaambia. Tunahitaji mtu mwenye rekodi
> na tusiye na mashaka kuhusu dhamira yake ya kututumikia. Na katika wagombea
> hawa, hakuna Mwingine isipokuwa Magessa.
>
> Hakuna mtu yeyote wa CCM ambaye akiwa mbunge anaweza kupinga ufisadi wa CCM
> ilhali wabunge wote wa CCM ni zao la ufisadi.. Labda apinge kwa unafiki wa
> makundi ndani ya CCM lakini sio kwa dhamira ya mapenzi ya mtanzania kwa nchi
> yake. Magessa amesoma sekondari Tosa Maganga, Zitto amesoma sekondari
> Tosamanganga. Magessa amesoma shahada ya kwanza na kufanya harakati Chuo
> Kikuu cha Dar es Salaam, Zitto amesoma shahada ya kwanza na kufanya harakati
> Chuokikuu cha Dar es Salaam. Magessa amesoma shahada ya pili Ujerumani,
> Zitto Amesoma Shahada ya pili Ujerumani. Ninawaomba wananchi wa Busanda,
> mpeni nafasi kijana wenu Finias Maggessa. Ninaamini Magessa ni Zitto na
> Zitto ni Magessa.
 
Hii hotuba ya Mh. Zito Kabwe ni nzuri sana, sasa sijui Majambazi na Mafisadi wa CCM watajibu nini, ukweli ni kwamba hawana jibu hata moja zaidi ya kutaka kuendelea kuwaongopea, kuwafisadi na kuwaibia watanzania. Hongera sana Zito yaani hapa nimehamasika.

USHAURI WA BURE: Tafadhali Chadema wekeni sehemu ya watu kukichangia chama kwenye website yenu, muwe mnaruhusu watu kuchangia kwa Credit Cards na Paypal ili wengi wetu tulio mbali nyumbani Tanzania tuweze kuwachangia.

Mkuu majambazi hayana jipya, nasikia yamerudi kwa vibaraka wao polisi kuwambia wakamate pikipiki zilizo kuwa zinatumika katika kampeini, ila nadhani wamechelewa, am sorry to tell them it is too late! hii siyo 2005.
 
Back
Top Bottom