Hotuba yangu jimboni Kigoma

Hotuba yangu jimboni Kigoma

(c) Hajakomaa kisiasa, mkomavu kisiasa kamwe hawasifii mafisadi kwa lolote. Fedha walizoiba mafisadi ni zaidi ya mazuri waliyofanya

Hitimisho: Hotuba hii ni chini ya kiwango na inanufaisha CCM kuliko Chadema. Inaonyesha woga wa Zitto dhidi ya CCM, imeshindwa kuonyesha malengo na mikakati ya Chadema kujipanua katika majimbo mengine, na kibaya zaidi inawashukuru mafisadi ambao hata CCM yenyewe haijawashukuru. Wapinzani tuna safari ndeeeeeeeeeefu.

Hivi kati ya Zitto na CCM nani anamhofia mwenzake?

Na hizi fikira mgando za kukomaa kisiasa nazo tumechoka nazo. Ukweli ni kuwa katika nchi inayoendeshwa chini ya mfumo fisadi kama nchi yetu kukomaa kisiasa kuna maana kuwa compromised kiasi cha kutosha kuonea haya uozo kwa manufaa ya mfumo.....na pia kuna maana ya kuwa tayari kufanya siasa zilipendwa zilizojaa fitina, uadui, majungu, rushwa na uchafu wa kila aina huku tukijidai tunapigania demokrasi na maendeleo...Zitto anatufunza kuwa kuna siasa mbadala wa hizi siasa hovyohovyo tulizoea na hayo ndiyo tunapaswa kuyaona kwa mwanasiasa kijana....

omarilyas
 
Hivi kati ya Zitto na CCM nani anamhofia mwenzake?

Mwenye hofu ni yule anayekuwa diffensive. Karibu hotuba yote Zitto yuko diffensive.

Mwanasiasa anapokuwa diffensive ananufaisha offensive kwasababu offensive ndio anaye determine nini kiongelewe, ndio mana wanasiasa wengi hukwepa au kupindisha maswali ili wageuze diffensive mode kuwa offensive.

Katika hotuba yake Zitto anahofia wana CCM wanaopita jimboni kwake wakisema kwamba maendeleo ya jimboni kwao yameletwa na CMM, na hivyo kufanya hotuba yake mzima kuwa majibu kwa CCM. Unfortunately hao wana CCM anaowajibu ambao wanapita katika jimbo lake hatuwajui, na wanaweza wasijitokeze kumjibu Zitto, as the result, machoni mwa watu inaonekana Zitto ni mwoga wa kivuli chake.
 
Nilichoambulia katika hotuba ya Mh Zitto:

(a) Anahofia upinzani kwenye jimbo lake hasa kutoka ccm na hivyo akaenda kwenye diffensive mode

(b) Akiwa anajaribu utetezi wake hotuba yake ikawa 100% reduced to Zitto vs CMM na sio Chadema vs CCM

(c) Hajakomaa kisiasa, mkomavu kisiasa kamwe hawasifii mafisadi kwa lolote. Fedha walizoiba mafisadi ni zaidi ya mazuri waliyofanya

Hitimisho: Hotuba hii ni chini ya kiwango na inanufaisha CCM kuliko Chadema. Inaonyesha woga wa Zitto dhidi ya CCM, imeshindwa kuonyesha malengo na mikakati ya Chadema kujipanua katika majimbo mengine, na kibaya zaidi inawashukuru mafisadi ambao hata CCM yenyewe haijawashukuru. Wapinzani tuna safari ndeeeeeeeeeefu.

Pole sana MgonjwaUkimwi,

Naona umekuta vitamu vyote vimeisha na wewe kama ulivyoandika UMEAMBULIA. Siku nyingine jitahidi uwahi ili USIAMBULIE.....
 
at least Zitto you are doing something, notable and remarkable! its a good question to ask, what those Mps with 10 or more years in the house have done? its shame on them! Bravo Zotto
 
Mwenye hofu ni yule anayekuwa diffensive. Karibu hotuba yote Zitto yuko diffensive.

Mwanasiasa anapokuwa diffensive ananufaisha offensive kwasababu offensive ndio anaye determine nini kiongelewe, ndio mana wanasiasa wengi hukwepa au kupindisha maswali ili wageuze diffensive mode kuwa offensive.

Katika hotuba yake Zitto anahofia wana CCM wanaopita jimboni kwake wakisema kwamba maendeleo ya jimboni kwao yameletwa na CMM, na hivyo kufanya hotuba yake mzima kuwa majibu kwa CCM. Unfortunately hao wana CCM anaowajibu ambao wanapita katika jimbo lake hatuwajui, na wanaweza wasijitokeze kumjibu Zitto, as the result, machoni mwa watu inaonekana Zitto ni mwoga wa kivuli chake.

Kwa hiyo ulitaka anyamaze ili muendelee kumwaga sumu zenu mlizozoea. Ukweli alichosema ni kidogo hata robo yake haifiki kwa aliyoyafanya chinichini. Tazizo mmezoea ile style ya kuita na kuhonga media kuonyesha kila mnachokifanya kwa mantiki ya kura badala ya utumishi kwa jamii. Hii janja yenu ya kuendesha fitina na upotoshaji mkitegemea mtawashinda maadui zenu kwa kulazimisha ukimya kwa upande wao hazina tija mnapowafanyia watu weny kujua siasa kwa mapana yake.

Tatizo wengi hamkutegema kuwa Zitto ataamua kuwaondolea uvivu na propaganda zenu hovyohovyo. Imefika wakati hata yule mama yetu SIJAPATA naye ana jeuri ya kusimama na kudai amewafanyia mengi watu wa kigoma zaidi ya Zitto.

Mkae mkijua, sio kila mwanasiasa mtu wa kukurupuka kama MASIHA wenu wasio na sifa wala utashi wa kuwapigania watanzania wafanyavyo. Hayo yote unayoyaona hapo yamekuja baada ya maandalizi na bado dozi itaendelea.

Ushauri; tafuteni mbinu makini kupambana na mwanasiasa makini na sio siasa zenu za uzoefu zilizojaa fitina, uwongo, upotoshaji, ubabaishaji, chuki, hujuma, matusi na mbambo hovyo mengine...
 
its a good question to ask, what those Mps with 10 or more years in the house have done?

Walifika sana shughulini, wakakaa sana na kutoa ofa za kahawa mabarazani, wakaenda sana misibani hata kama hawawajui walikufa ama waliofiwa, wakapiga sana majungu na fitina, wakazungusha sana ofa za mia tano mia tano, wakaropoka sana bungeni kuhusiana na petty issues(major issues hawakuzijua na hata kama wangezijua hawakuwa na kuda wa kujisomea na kujieleimisha masuala ya kitaifa na kimataifa), wakabeba sana smile feki na mengineyo ya aina hiyo....Na hawa ndio aina ya watu baadhi ya wapiga debe wao humu ndani wangependa warudi bungeni kuendeleza nyimbo za kikasuku

Bahati mbaya hata hao wanaowinda kumuondoa Zitto huko bado wanategemea mbinu zao hizo "zilipendwa" kujitengenezea kura
 
Mwenye hofu ni yule anayekuwa diffensive. Karibu hotuba yote Zitto yuko diffensive.

Mwanasiasa anapokuwa diffensive ananufaisha offensive kwasababu offensive ndio anaye determine nini kiongelewe, ndio mana wanasiasa wengi hukwepa au kupindisha maswali ili wageuze diffensive mode kuwa offensive.

Katika hotuba yake Zitto anahofia wana CCM wanaopita jimboni kwake wakisema kwamba maendeleo ya jimboni kwao yameletwa na CMM, na hivyo kufanya hotuba yake mzima kuwa majibu kwa CCM. Unfortunately hao wana CCM anaowajibu ambao wanapita katika jimbo lake hatuwajui, na wanaweza wasijitokeze kumjibu Zitto, as the result, machoni mwa watu inaonekana Zitto ni mwoga wa kivuli chake.

You are wrong!

Kuna wanaosema kwamba "Facts speak for themselves" Hao CCM hatuhitaji kuwajua na wala hatuhitaji waje kumjibu Zitto. Baadala yake wamjibu Zitto kwa matendo..kwa kuwaletea huduma wananchi wa majimbo yao. Cha msingi ni kwamba barabara imejengwa tumeiona. Watoto hao yatima wameenda shule rekodi zipo, viwanja vimepimwa ushahidi upo..sasa hao wanaCCM unaotaka tuwajue..tuwajue kwa lipi? waende wakawasaidie wapiga kura wao...hayo ndo yatakuwa majibu mazuri kwa Zitto siyo kwenda majukwaani kupiga porojo.

Unajua MUNGU ana akili sana..kila mwanadamu alimpa uwezo wa kuchanganua mabaya na mazuri (albeit differently). Kwa hiyo hapa hatuhitaji kupata majibu ya Sanzugwanko wala Serukamba..majibu ni barabara zillizojengwa. Punkt.
 
Hotuba nzuri Zitto lakini utakuwepo uchaguzi ujao?Tuewke wazi, sisi tulio mjuu bado hatujui msimamo wako kaka.
 
Hongera Zitti kwa akzi nzuri katika jimbo lako na Taifa kwa jumla.

kaza mwendo bado mchangooo wako wahitajika zaidi kulikowakati wowotee..

sioni tabu kuwaacknowledge chenge, meghji na mrema kwani wao no viongozi na walifanikisha juhudi zakee...huo ndio uongoziii..

tuachee chuki za kitotoo...
 
Umefanya mengi sana hata katika ngazi ya Taifa na hivyo umefanya uwe model yetu wote Tanzania, Nakuombea kwa Mungu akusaidie sana katika mambo yote Kaka yangu
 
Mimi siyo mwanachama wala shabiki wa chadema lakini huyu kijana ni hazina tunayoitegemea na nina amini wako vijana wengi ambao wakipata nafasi ya uongozi watatufikisha mahala pa kuridhisha.
OMBI
Tuache kulalamika na kuanzia sasa tuhamasishe vijana wa sampuli hii wajitokeze kwenye uchaguzi ujao na tuachane na vizee vinavyotaka kuifa bungeni wakati hawana jipya kwa nchi yetu. ninarudia tena tuache kuangalia chama bali tuangalie aina ya watu wanaofaa kwa nchi yetu. IDUMU TANZANIA
 
Back
Top Bottom