Hotuba za Mikutano ya Hadhara: Mpaka sasa Mnyika anaongoza akifuatiwa na Heche

Hotuba za Mikutano ya Hadhara: Mpaka sasa Mnyika anaongoza akifuatiwa na Heche

Master Legendary

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
576
Reaction score
876
WanaJamvi nimefuatilia Hotuba za Mikutano yote ya hadhara iliyofanyika baada ya Mama Samia kuifungua.

Kwa maoni yangu mpaka sasa Mnyika anaongoza kwa kutumia nafasi hizo vizuri. Ukimuangalia kwa muda mchache anaopewa anaongea point tupu na kugusa mambo ya Msingi ikiwemo Katiba Mpya, Maisha ya Wananchi, Chadema Digital, Uchaguzi.

Pia amefanikiwa kujua hadhira iliyoko mbele yake inataka nini, mfano alivyokuwa Tarime alizungumza mambo ya Msingi sana kuhusu hatma ya Uchumi wa Madini na Wananchi wa Tarime na alimwaga madini tupu, hii ilinigusa sana.

Baada ya huyo ni Heche, Kamanda wa anga baada ya kuchemka Mwanza nimeona kaimprove kidogo Musoma ila bado.

Ni mtazamo wangu tu masela msijenge chuki, bado nafuatilia ntaendelea kutoa updates.
 
CCM mnatakiwa kuchangia hoja siyo kutoa misifa kama mnavyoshindwa kuongelea uhai wa nchi hii mkabaki kumsifia rais sababu hamna.
 

Ngwear FT Mirror - Maskini WENZANGU


Intro: cowwizy ,ybm

Verse 1:
wachache ndo wanaishi wengi wetu ma escorts,
twiga wanapanda pipa hata bila ya passports,
mikoa mingi bado haina hata airports,
zaidi ya migodini madini kuya export,
bila ya wazawa kufaidika,
ndo mana wazanzibara wamechoka kutanga na nyika,
big up Mandela leo South sio Africa,
waliotangulia kupata uhuru bado wanapigika,
bidhaa zilizo expire kutubambika,
meli zinazidi zama wengi daily tunawazika,
wenye hali duni ndo tunao athirika,
wao ma vx yao ni special order uhakika,
tutalia machozi ya damu mpaka yata form bahari,
na tutaogelea wenyewe na watu hawajali,
leta mgomo baridi uijue serikali then muulize Ulimboka umuhimu wa Madaktari let's go

Chorus
(bado nalia tu na Tanzania yangu/kweli mali ni nyingi wale wachache wenzangu/me nalia na masikini wenzangu/eeh baba Mungu sikia kilo changu/issue is harder tuna suffer/sikia kilio changu/issue is harder tuna suffer/me nalia like..........)

Verse 2:
viongozi wa siasa kama viongozi wa dini,
mengi wanaongea coz silaha yao ni ulimi,
mh.spika Tanzania huru inazidi zeeka tayari ni miaka 50,
mengi mmetuahidi pia ahadi ni deni,
pia tunatambua umuhimu wa UN,
kupinga h.I.v,umaskini na rushwa and,
mabilioni yanayotumika kwa campgain,
kama za kupinga unyanyasaji wa watoto,
zisiishie kwenye promo na kuwalisha bado ndoto,
ishu sio kutupiana maneno bungeni,
bali watoto watoke mtaani warudi shuleni
,mkulima shambani anahitaji usafiri wa treni,
nyie piteni angani mazao yake muuzieni,
mpeni bei nzuri aweze mudu zaidi ya trector,
ni mawazo tu DIC usione nakuTATOR

(chorous)

Verse 3.
Tanu ilifanya kazi kubwa 61,
solution sio labda nchi wachukue upinzani,
bali mtanzania wa chini anaishi maisha gani,
watu wanakufa kwa njaa iweje tujivunie amani,
ni mengi tu mazuri yamefanyika mpaka sasa,
ila naamini bado tungekuwa mbali(hivi babu wa Loliondo nae inawezekana tu ilikuwa ni siasa)NO !(Lakini iko wapi hii kaburi ya Balali !?) Men ! Jibu unalo so usiulize swali,una dini ?
Mkristu sali na Muislam swali coz,
bado tunaishi ki mungu mungu,
Baada ya m weka z usikie kizungu zungu jinsi ukoloni unafanya mambo mpaka leo,
kuongoza jamii sio kumtawala mkeo,
najiuliza maisha yangekuwaje bila mziki,
hivi mtaani ingekuwa vp ? Ingekuwa mziki ...

(Chorous)

outro yeah chamber squad baby,one love,Tanzania,Muro jr I see ya ......
Till fade
 
Mimi nimefurahishwa zaidi na wazungumzaji ambao ni wenyeji wa maeneo husika.

Kwa mfano, Tarime yuko jamaa anaitwa Bashir Ally Mwenyekiti wa Cdm Tarime Mjini ni mpangiliaji hoja mzuri sana na nimeanza kumuona majuzi.
 
Back
Top Bottom