Simba Mkali
JF-Expert Member
- Jan 31, 2012
- 620
- 239
Sijui kama ni sawa au si sawa, msaidizi wangu wa kazi ameniambia kuwa anataka likizo ili aende kwao, hilo kwa roho za kibinaadamu naona ni jambo zuri sana, lakini anataka na mshahara wa mwezi mmoja, nauli na fedha za matumizi ya njiani. Kama vile haitoshi anasema kuwa anapaswa kulipwa fedha za nauli za jamaa yake ambaye amepanga kwenda kumtambulisha huko kijijini kwao, hebu niambieni kuna haki hapa?
hakuna tatizo.fanya kiubinaadamu.mimi house girl ambae anaishi na mama,kila akisafiri kwenda kwao,huwa namlipa hela,za mwezi mzima na huo haufanyii kazi,akirudi mshahara wake unaendelea kama kawaida.huwa namlipa kila baada ya miezi minne kwa mkupuo,ili hela zake afanyie la maana
Kweli kabisa lakini kazini miye nikienda likizo nalipwa mshahara wa mwezi mmoja tu, hakuna marupurupu wala nini,si unajua tena haya makampuni yetu ya watu binafsi.Mzee, mbona hiyo kawaida... kwani wewe ukienda likizo si unapewa hela ya likizo ya kusafirisha wewe na familia ya watoto wanne mpaka kijiji ulichotoka. Tatizo liko wapi hapo ndugu? Kwani mshahara wake wewe unamlipa kiasi gani mpaka uone tabu kumpa hiyo hela ya mwezi mmoja, au unaona atatoroka? kama ni hivyo mpe hiyo hela ila mwambie akutumie mwenzie mwingine kama yeye hatarudi. Hii ni kwakuwa ulisha amua kumruhusu. Au vipi kamanda?