Howo Vs Scania

Hivi hizi HOWO zina nguvu ya kuvuta mzigo kweli au madereva wake huwa wanafanya mapozi wakati wanapanda milima ?maana huwa nazipita kama zimesimama barabarani...
 
Gari zote hizo zina faida yake na hasara pia.kwa ubora ni scania lakini hata hizo faw, howo nazo ni nzuri tena ni economy kwenye fuel na spare zake ni bei ya kawaida tu.

Hapo ni wewe tu na nguvu yako , mchina utapata mpya kabisa lakini scania mara nyingi bongo tunanunua used. Kitu kipya ni kipya tu mkuu itakulipa fadhila kama ikapata mtunzaji mzuri. Na kama mapenzi yapo kwa scania basi nakushauri anza na 320 hutojutia.
 
Ubarikiwe mkuu wangu
 
Nunua Howo kaka acha kusikiliza maneno ya watu ambao wengi nna uhakika hawajawahi fanya hiyo biahsara.

Makampuni mengi makubwa yananunua Howo na yanafanya kazi vizuri sana.

Kama unaanza, nunua Howo mpya kabisa hakikisha unaitunza vizuri tu.
Itakuingizia hela yako bila tatizo. Naongea from experience.
 
Tatizo ya gari ya mchina kama hiyo HOWO sio imara.

Kinachokera zaidi mfano mzuri ukitoka hapo Dar ukifika hapa Tunduma ubavu wote wa kushoto na mkono pamoja na mguu wa kulia utakoma kwa maumivu coz gia zake ni za cable hazitumii upepo (valve) halafu huwezi kuiamrisha ukifanya hivyo ujuage bearing ya kwenye gearbox umeua so chukua scania kama mfuko upo vizuri.
 
Ukikuta scania ipo juu ya mawe jua imefanya kazi miaka mingi wakati huo kumbuka ilikuja ikiwa second hand hiz za kichina zimekuja juzi tu kiukweli sio nzuri.
 
Pole mkuu .Yaani nimecheka na kukuonea huruma .kaka kwani ubavu unaendesha gari kaka ,by the way asante sana mkuu nimeachana na hayo matoy ya hao watu wenye macho madogo mkuu .
 
Kaka mzungu ni mzungu achana na hao wachina OK hila mchina ametoa hayo magari kadiri ya maisha yetu wa tz.hila sicania mkataba.
 
howo tipa la hp332 nadhani ni milioni 90 mpya..
fuso fighter hp210 milioni 80 mtumba
kipi bora
 
Umenena mkuu kweli kbsa
 
Hivi hizi HOWO zina nguvu ya kuvuta mzigo kweli au madereva wake huwa wanafanya mapozi wakati wanapanda milima ?maana huwa nazipita kama zimesimama barabarani...
Sio mapoz ndugu hizo gari huthubutu kuzilazimisha nazjua ukilazimisha safari inaishia hapo hapo tofauti na scania unaiimbisha inakubali kuimba hainaga mashida.
 
howo tipa la hp332 nadhani ni milioni 90 mpya..
fuso fighter hp210 milioni 80 mtumba
kipi bora
bora fuso yenye uhakika wa kukaa miaka 12 mbele pamoja na u-mtumba wake, kuliko box linalotembea barabarani ambalo halitafikisha hata kilometer million moja au 6 years ya kuwepo barabarani.

Fuso ni kama DCM, ikichoka unatengeneza mara moja(done), Howo ikichoka inaanza kutembea kwa nguvu za garage, bila kuingia garage, safari hakuna
 
Pole mkuu .Yaani nimecheka na kukuonea huruma .kaka kwani ubavu unaendesha gari kaka ,by the way asante sana mkuu nimeachana na hayo matoy ya hao watu wenye macho madogo mkuu .
Tatizo gear lever ngumu kwa sababu inatumia mfumo wa cable tofauti na scania inatumia upepo (valve) halafu accelerater pedal ni ngumu tofauti na scania unagusa tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…