Hili suala la lugha hebu tuliweke sawa kidogo. Kama angechaguliwa mtu ambaye kiingereza hakipandi, halafu baadaye wanaenda Sanya, China kwenye Miss World, hivi anafikiri ataulizwa maswali kwa Kifipa? As a matter of fact, lugha rasmi za Tanzania ni Kiingereza na Kiswahili na hili liwe changamoto kwa wale wote wanaotaka kugombea Umiss "wherever" bora wapandishe kiingereza chao na hata lugha nyingine za ziada. Hebu fikiria kama angekuwepo binti kati yao ambaye amepandisha Kiingereza na Kifaransa, halafu akijibu anajibu kwa kiingereza halafu anachombezea na kifaransa kidogo, huoni huyo angescore juu kuliko hata Richa!?
Kama tatizo ni kuwa wengine kiingereza kimekuwa "maimuna" sasa kwanini wamlalamike Richa? Sasa walitaka Richa naye azungumze kiingereza cha kuvunja vunja ili alingane nao?