Hu ndo upimaji wa uelewa kwa wanafunzi wa chuo kikuu

son of king john2

Senior Member
Joined
Jan 11, 2014
Posts
131
Reaction score
33
Inashangaza kwa Mhadhiri wa chuo kikuu ambaye kila siku anakuja darasan na kuanza kufundisha haraka haraka tena kwa kasi za ajabu......yaaani anasoma kwenye kitabu(densa) kisha baada ya hapo ni mwenye spidi ndo ataelewa kwa kuwa atakuwa amenakili kilichosemwa.ila utashangaa siku ya mtihani. Yan hiyo siku utakuta anakuja on time.Ingia kwenye mtihani yami utakuta misamiati iliyotumika ni ya ajabu hata yeye hakuwai kuitumia...swali hapa ni je mtu anapimwa kwa kuulizwa alichosoma au anapimwa kwa kufumbua misamiati anayoijua mwalimu......??
 
..anapimwa kwa kila kitu, kuanzia mambo mwalimu aliyofundisha na mambo ambayo ajafundisha lakini mwanafunzi alitakiwa ajue kulingana na malengo ya somo..
au ulitakaje?
 
Hapo kaka wahadhiri wengi hasa wa vyuo vya sirikali wanaficha madhaifu yao(incomptence) kwa kigezo cha lecture method. Baadhi ya wahadhiri wanasoma hand out au kitabu kama anasoma gazeti! Hana cha kuongeza wala kupunguza! Hahitaji kuulizwa swali yeye anachotaka ni kumaliza moduli na kutokomea. Hii huwa inakera sana na ni njia rahisi kwa mhadhiri alieajiriwa kwa njia za panya kuficha madhaifu yake japo huwa wanaumbuka kadiri muda unavyoenda. Njia ambayo inashauriwa na wataalamu wengi wa elimu ni modified lecture na sio pure lecture method.
 
Hmm! Mkuu unachokiongea ni kweli kabisa! Utamkuta mwengine anafundisha kimkato kwa kuwatajia vipengele tu (kama Open University vile!), subilia mtihani wake ukione chamoto!
 
..anapimwa kwa kila kitu, kuanzia mambo mwalimu aliyofundisha na mambo ambayo ajafundisha lakini mwanafunzi alitakiwa ajue kulingana na malengo ya somo..
au ulitakaje?

. sidhani kama huu ni mfumo wa kumpima mwanafunzi ambaye anaandaliwa kwenda kuwa mfanyakazi......mtu huyu anatakiwa kuandaliwa namna gani ya kupambana na changamoto kazini lkn utashangaa leckecher mwenye spid ya kusoma densa. anakwambia kwenye mtihan wangu hakuna atayepata zaid ya alama fulan inamana hizo alama zinazobaki kaziandaa kwa ajili ya nan na ni kwa nn
 
mi nazan ni vema upimaji na ufundishaji uendane siyo kwa kutumia hii mifumo ya leo....just imagine kazini siendi kupambana na misamiati lkn leo nabebeshwa koz et kwa sababu tu-----sijui msamiati fulan ambao swali lake lna maks 20 wakat kama angetumia msamiati wa kawaida kuuliza swali lilelile ningejb saf kabsa na kufaulu vzr........inaboa sana
 
Hmm! Mkuu unachokiongea ni kweli kabisa! Utamkuta mwengine anafundisha kimkato kwa kuwatajia vipengele tu (kama Open University vile!), subilia mtihani wake ukione chamoto!

katika level ya university usitegemee kufundishwa sana kama mtoto wa primary.ingia library soma vitabu
 
ndio maana hua tunapewa course outline, unadhani za kufungia maandazi zile!!!?
 
Acha ubwete wewe, elimu ya chuo kikuu sio kusubiri ufundishwe kila neno, ukipewa course outline unatakiwa ukachimbe kwelkwel
 

Kwani nawe upo chuo?ama ulipita?"Leckecher!" ndio nini mkuu?

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
mwanachuo hatafuniwi kila kitu...lecturer anakupa mwongozo tu...yaliyobaki utayajua wew mwenyew....wanaotafuniwa topic nzima ni primary na secondary...na mitihan inapima upeo wako wa kufikiria sio jinsi gan unaweza kukariri uliyofundishwa klas
 
mwanachuo hatafuniwi kila kitu...lecturer anakupa mwongozo tu...yaliyobaki utayajua wew mwenyew....wanaotafuniwa topic nzima ni primary na secondary...na mitihan inapima upeo wako wa kufikiria sio jinsi gan unaweza kukariri uliyofundishwa klas
Sijui kama unayajua madhara ya hicho ukizungumzacho au la!
 
Inasikitisha sana kwa namna tabia ya lecturers ku-download materials toka kwenye internet na kuja kusoma kama zilivyo pasipo hata chembe ya inputs zao ilivyokuwa kubwa hivi sasa. Umeme ukikatika, lecturer hana uwezo wa kuendelea na somo; maana materials hayapo kichwani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…