Huduma hospitali za umma zinatisha..and...the way forward..

sekta ya afya inahitaji mabadiliko makubwa ya kiuongozi kwanza.
Nadhani viongozi waliopo hawajawahi kufanya kazi na kupata uzoefu katika mahospitali yetu ndio maana mipango na resources zinazotumika hazileti majibu.
Mleta thread nakushauri uwasilishe matokeo ya utafiti wako kwenye mkutano wa kila mwaka wa 'QUALITY IMPROVEMENT FORUM ,hii ni sehemu ambayo wadau mbalimbali wa maswala ya afya wanakutana na kujadili ni vipi tunaweza kuboresha utoaji wa huduma hasa katika hospitali za umma.
 
mkuu Ruta nitarudi!

Vipi meningitis? rudi bana umpe jamaa shule aelewe hali halisi, naona mkuu Jackbauer amefafanua ipasavyo. Wananchi hata wanapoambiwa huduma ya mama na mtoto ni bure wakati budget inayoletwa haitoshi ni issue kumweleza akanunue catheter ama IV fluids. Mkoa wa Kilimanjaro hospitali ya mkoa haina chumba chaupasuaji tangu 2010 december this is a holly joke!!
 
Last edited by a moderator:

mkuu nimeshawasilsha hoja zangu hapo juu! Jackbauer ameni pre-empty! measkron
 
Last edited by a moderator:
Ni lazima serikali na wananchi watambue kuwa afya ni bidhaa aghali!

Ni mihimu kudefine afya ya msingi ni ipi,hapa namaanisha emergence services ni zipi.baada ya kujua hili tutenge fedha kwa ajili ya huduma hizi.

Pili ni mhimu sana kwa serikali kutambua kuwa huduma za afya ni uwekezaji unaoweza kutuongezea mapato.

Tatu ni muhimu kwa serikali kubadilisha uongozi na watendaji wa wizara ya ya afya na kuweka watu wenye weledi wa hali ya juu.

Serikali ni lazima itambue kuwa afya ni mojawapo ya kipimo cha maendeleo hivyo ukiweka mgumo mzuri wa afya ni wazi kuwa tutaingia katika group la nchi zilizoendelea,afya sio huduma!

Serikali iwekeze katika maslahi ya watumishi wa afya na sio kujikita katika kusomesha watumishi ambao watakimbilia nje ya nchi baada ya kuhitimu.
 
MKUU RUTASHUBANYUMA NAKUPONGEZA SANA KWA THREAD HII!!

Jackbauer nakushukuru nawe pia.........na nilisahau ya kuwa huduma za maabara zapaswa kuwa masaa 24...............yawaje wagonjwa siku za wikiendi na sikukuu hususani wagonjwa wapya wasahaulike kupata vipimo kabla ya tiba na matokeo yake utakuta wanapewa matibabu ya kubahatisha kwa gharama kubwa kwa mgonjwa na kwa umma kugharimia magonjwa ambayo huenda siyo yaliyomsibu mgonjwa..................
 

measkron wahudumu siku hizi wanatarajia mgonjwa au jamaa zake waachie kitu kidogo na wasipofanya hivyo matusi au hata kupigwa hujitokeza..........
 
hospitali za umma ni maigizo matupu ya hii serikali nafikiri wanafanya makusudi kabisa kutoiboresha mana ni mtaji wao kwenda kutibiwa nje,matibabu private kwa zile kadi zenu zile na zaidi ya vyote wanajua kabisa kuchezea afya ya mtu/watu ni silaha tosha kutunyong'onyeza na kufa taratibu

kwakweli its a pathetic situation
 
Tatizo la huduma ya afya Tanzania linasabishwa na bad or non existent healthcare financing policy.
Hata Marekani na nchi nyingine zilizoendela kama zingekuwa na mfumo wa kutoa huduma za afya bure au kwa kuchangia basi huduma zingekuwa duni hivihivi.

Tunahitaji mfumo wa bima ya afya ambao utawezesha kusupport healthcare system na serikali kusubsidize kwenye mapungufu. Ni vema tungechukua utaratibu wa compulsory health insurance ambayo inakatwa kutokana na kipato cha mtu.

Nitafurahi siku nikiona mwanasiasa au chama cha siasa kinakuja na healthcare bill ambayo ina features zenye kuonyesha matumaini ya kuutoa mfumo wetu wa afya hapa ulipo.
 
Hapo sasa!
Tanzani bila UKIMWI... Hao juu ni wazazi uwezekano wa kuambukizana magonjwa ni MKUBWA sana hapo hasa ukimwi!
Kwani wengi wanakuwa na vidonda wazi na mitoko anuai baada ya kujifungua!
 

mkuu kwa swala maabara ni uzembe wa hospitali husika,wahudumu wa afya(madaktari au waganga) na wateja wenyewe.

Nianze na mteja,hivi unakubali vipi kupewa dawa kabla hujaambiwa tatizo lako?ukiambiwa una malaria unapaswa kuhoji uthibitisho wa matokeo ya vipimo au unapaswa kuelezwa na kuridhika kuwa kipimo hakijaonyesha lakini kwa dalili ulizonazo zinaelekea kuhusiana na ugonjwa flani hata kama vipimo havionyeshi hivyo.wazungu wana demand kujua tatizo lao kabla ya kutumia dawa,na sisi tuanze kujenga utaratibu huu.

Kwa upande wa madaktari/waganga ni muhimu na wajibu kwao kuhakikisha wanatoa matibabu kulingana na ushahidi wa vipimo isipokuwa pale mazingira ya ya kupata majibu au vipimo yanapokuwa magumu na mgonjwa yupo kwenye hatari ya kufa.mfano ni upuuzi kumpa mtu dawa ya malaria wakati vipimo vya malaria vinapatikana kwa urahisi ndani ya muda mfupi.

Kwa upande wa uongozi wa hospitali,hawa wanawajibika kuhakikisha vipimo muhimu na vya kawaida vinapatikana muda wote.

Ni kichekesho kukuta maabara ya hospitali ya mkoa au wilaya inashindwa kutoa huduma kwa masaa 24 !
 
Well said mkuu Rutashubanyuma!

Kwa maoni yangu hii nchi imeshindikana au niseme watawala wameshindwa kuitawala nchi hii kwa mafanikio na kama alivyosema Okonkwo, ".....they have put a knife into the things that held us together, now things are falling apart"

Kuna pahala Tanzania hii huku western regions(tabora na kigoma) nimewahi kufika, huko hakuna kitu kinaitwa Tanesco, watu wananunua majenereta makubwa yenye kutumia diesel na kisha wanatawanya nyaya za umeme na kuwauzia watu umeme mithili ya Tanesco.

Mfano wa hilo nililiona Dsm, watu wanachimba visima virefu vya maji safi na kisha wanatawanya mabomba na mita za maji na kuwaunganishia watu maji mfano wa DAWASA na kuwauzia.

Unapoona mambo yaliyotakiwa yafanywe na mamlaka za nchi yamehamia kwa wananchi tena kienyeji pasi na kuwepo kwa regulation zozote ya kulinda consumers, unapashwa kujiuliza hivi hiyo nchi inaekekea wapi?

Mbaya zaidi ni pale inapofika watu kuanza kuzoea na kuona kuwa hiyo ni hali ya kawaida...ni hatari sana jamii kukubali na kufanya upuuzi kuwa ni sehemu ya maisha yao!!!:A S angry:
 
Mkuu Rutashubanyuma fikiria hospital ya rufaa machine ya CT Scan imeharibika kwa kipindi cha mwaka mzima unategema nini.......ni sio kwamba nini serikali inaweza kununua machine zaidi ya moja kama wataacha ubinafsi......Hospital kama Mount Meru ilipashwa kuwa na hiyo machine......wao wanajali nini wakati wahatatibiwa kwenye hizo hosp wametuachia sie wakata mkonge
 
Last edited by a moderator:
Tanzania kwa sasa hatuna huduma za afya bali tuna usanii wa kiafya.
Kumpeleka hospitali za umma mgonjwa wako ni sawa na kumsindikiza kaburini.

mh hata hizo za binafsi ni pesa tu mbele halafu huduma baadae, tena hosp km aghakhan ni ghali mno mno mtu wa kawaidi hatamuddu kwa urahisi itabidi kulundikana tu hosp za serikali. lakini muhimbili kuna madaktari sana kama wangefanya vitu kwa haki na mpangili ni hosp nzuri sana. kwa ujumla wafanyakazi wa sekta ya afya wana kazi kubwa, ngumu na ya kujitolea zaidi kuliko ajira ya kuingiza kipato magonjwa ni mengi nowdays, hosp ni chache na hivyo kuzidisha ugumu wa kazi bila huduma kuboreshwa itakuwa kasheshe zaidi ya hapa tulipofikia.
 

kwa mara ya kwanza tunajenga nchi moja bila kugombea fito!
 

Blaki Womani hii rasimu ya katiba itakapotoka tushinikize ya kuwa hakuna sumni ya serikali kugharimia yeyote matibabu nje ya nchi.........hapo hospitali za umma zitaanza kuboreshwa..........
 
kwa mara ya kwanza tunajenga nchi moja bila kugombea fito!

Tatizo lako wewe huwa unag'ang'ania fito zote ukae nazo hata kama wenzako hawana fito mkononi - just a joke.

Seriously, sera zetu za sasa zinazungumzia outcomes - huduma bure kwa watu wote, lakini hazingumzii jinzi ya kuicover hiyo huduma financially. Sasa tunahitaji sera na sheria zitakazozungumzia financing aspects of healthcare. Tupige hesabu kiasi gani kinahitajika na wajibu wa kila mhusika kuhakikisha kinapatikana. Bila hivyo itakuwa mbio za sakafuni tu kama za kutaka kuuza cement sh. elfu 5.
 
ndio maana Tanzania Tunaongoza kwa usugu wa magonjwa, dawa zinapatikana mpaka sokoni. kila unapoenda kuna dawa za marelia, za kutuliza maumivu n.k. mtu akisikia kichwa kinauma anasema nina maleria, tumbo linauma nina amiba, mara taifodi n.k. anajitibu mwenye huyo. Mwisho wa siku magonjwa hayo yakikupata hizo dawa hazikuponyi tena ndio mwanzo wa kupanda kwa gharama za matibabu na wenye uwezo kwenda india.
 
duu naona umefanya research ya kutosha..hayo yote ndio yanayotokea na wahusika wako kimya!
 
juzi mtoto wa jirani yangu alipelekwa zahanati moja ya serikali hapa Dar
Dr akamuwekea thermometer amcheki homa ikapasuka,
akaitwa nesi alete nyingine alizunguka hosp nzima hakupata eti hakuna.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…