Huduma mbovu yamponza Mganga Mfawidhi hospitali ya Wilaya Siha, Waziri amshusha cheo

Huduma mbovu yamponza Mganga Mfawidhi hospitali ya Wilaya Siha, Waziri amshusha cheo

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel ameonyesha kukasirishwa na huduma mbovu inayotolewa katika Hospitali ya Wilaya ya Siha baada ya wananchi kulalamikia huduma mbovu huku akikiri kujionea kwa macho yake baada ya kushuhudia mgonjwa akiachwa zaidi ya saa moja bila kuhudumiwa.

"Ninaagiza Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Siha aondolewe katika nafasi hiyo abaki kama Daktari wengine, nilifika hapa zaidi ya mara sita na jana nimekuja tena nikakuta Askari aliyepata ajali akiwa ametelekezwa bila msaada wowote," - Dkt Molle Naibu Waziri wa Afya.

FLJes-fX0AIr5kS.jpg

FLJeuY2WYAISv5z.jpg
 
Kama dr aligundua mgonjwa ni King Guy unategemea angeendelea kutoa huduma kweli au kutokomea kusikojulikana?
 
Watumishi wapo wa kutosha?
Hilo nalo
Alafu Mganga mfawidhi hawezi kuzunguka kila section muda wote wakati Kuna majukumu mengine yanaendelea kumkaba na ni majukumu ya wizara huku akitakiwa taarifa zake zifike immediately.
That's not fair. Then amejaribu hata kuangalia walioko zamu kuwa nao walikuwa na Majukumu gani? Maana wakati mwingine Kuna emergency kubwa zaidi au wapo kwenye chumba Cha upasuaji na waliobaki hawana uwezo wa kuhudumia kutokana na elimu yao na Majukumu yao.
Ukiwa na cheo usitumie mamlaka Yako kuumiza wengine ili kuonekana upo vizuri na kutetea cheo chako.
Ila all in all MUNGU anatuona, na MUNGU atusaidie tu tushushe viburi vya Maisha tukifanikiwa na tukiwa na nafasi Fulani katika jamii.
 
Back
Top Bottom