Huduma ya Selcom ina utapeli

Andy2015

New Member
Joined
Mar 21, 2017
Posts
1
Reaction score
4
Kuna hii platform ya kimtandao inayojihusisha na kutoa huduma za kifedha inaitwa SELCOM HUDUMA.

Hawana huduma kwa wateja nzuri, kubwa lililonileta kwenu miamala imekwama kwa muda wa wiki moja Sasa hakuna msaada wowote ule tunaoupata imekuwa kero kwa watu wengi.

Nimejaribu kila njia kuwasiliananao lakini hakuna msaada nilioupata.

Naomba mamlaka husika za serikali zitusaidie.

Naomba kuwasilisha.
 
Me nilipigwa kama elfu 15 hivi mkuu
 
Hawa jamaa ni matapeli hata mimi nimepigwa na ni wengi sana wanalia TCRA tcra mko wapi?
 
Ni mara nne mfululizo pesa zangu zinaishia kupotea huko ,selcom ni wezi sana,pesa ya mwisho yalikua malipo ya kisimbuzi cha biashara dstv,baada tu ya muamala dstv kuurudisha kwa hoja ya kua pesa haitoshi /kifurushi kubadilirishwa mpka leo pesa imenasa selcom huku mtoa huduma halotel akisema hajarudishiwa pesa toka selcom
 

Mimi mwenyewe kuna muamala nilifanya wa tsh700,000/= pesa ikakwama wakasema watanirudishia kwenye account yangu ya mpesa ndani ya masaa 72 lakini muda ulipofika hawakurudisha walinizungusha na ile hela karibu wiki mbili nikatuma email BOT na TCRA za malalamiko kuona kama ntapata msaada wakaja baadae kurudisha muamala ila hawa jamaa sio wakuwaamini.
 
Hao jamaa, wananipiga chenga kila siku muamala wangu umekwama tangu mwaka jana na hawana time na mimi. Imagine mwaka jana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…