Tetesi: Huenda chama kipya cha Lissu kikasheheni watu waadilifu kama Dkt. Slaa, Prof. Safari, Mnyika, Heche, Wenje na wale wote waliotoka CHADEMA kwa figisu

Mimi namwomba Mungu CHADEMA isipasuke,tofauti zao ziishe! Waungane then waendelee na mapambano!
 
Mbowe ndo chadema imara na upizani imara kwa nyakati hizi, bila mbowe kuwa mwenyekiti chadema, hakuna chadema, ya upizani kwa ccm, na hakuna chama kitakachotetelesha ccm.
 
Aulizwe Tundu LIsu, kwanini asianzishe chama chake kipya? mbona atachukua wafuasi wote.
 
Hiyo ni ramli ya kishirikina. Uchaguzi huru na wa haki HAUJAFANYIKA. Utajuaje kama CHADEMA ipo au haipo kwa wananchi?

Porojo nyingi za kukaririshwa huko CCM. “Gia angani” wakapata wabunge wengi kuliko nyakati zote na kuongoza halmashauri nyingi - pamoja na kuibiwa ushindi - ndio kuanguka huko? No logic. Maelezo yote hayaunganiki. Hayana mantiki.

2019 na 2020 uchaguzi umeporwa jumla na serikali ya CCM, CHADEMA ikakosa vyote bungeni na serikali za mitaa. Serikali ikalazimisha viti maalum 19 vya CHADEMA bungeni na bado inahangaika kutafuta maelewano na kukubalika na chama hicho kwa kutambua ndicho “chama kikuu cha upinzani” nchini. Rais kasambaza mabango yenye picha akiwa na viongozi wa CHADEMA kutafuta kukubalika na wananchi. Hilo ni anguko?

CHADEMA ikiitisha mikutano, maelfu ya wananchi wanakusanyika kwa hiyari kusikiliza. Unasema haiko kwa wananchi? Well, endeleeni na porojo mfu na ramli. Ndicho kilichobakia.
 
Mbinu za CCM zimekwama. Mbowe haondoki na Lissu haanzishi chama kingine.
 
Mimi sioni kama Chadema itameguka kuelekea uchaguzi mkuu 2025.
Kwani ikimeguka kwa namna yoyote utakuwa ushindi mkubwa kwa CCM.
Chadema wasiongezee matatizo they need to read between the lines,Ukiweka changamoto za Covid 19 + Msigwa na Kanda ya Nyasa +Katibu Mkuu Myika+ Mwenyekiti Mbowe + Makamu Lissu =???
Chadema imefika wakati mjitambuwe mapema vinginevyo........
 
mkuu tukiachana na hayo, hivi mtu anakuwa seniour member kwa siku mbili? Linawezekana vipi j hili jambo?
 
Ok ngoja tuone.
Ila mimi na wenzangu wengi tu ambao tupo pamoja hicho chama tulihama kuanzia 2015 tulimchagua Magufuli.
2020 hatukupiga kura.
NB: nilikuwa kiongozi wa CHADEMA ila gia ya angani ilituvuruga tukakaa kando.
Gia ya angani ilileta mamluki wengi kuja kuuwa chama na kuondoa wengi waliokipambania chama hadi kufikia mafanikio yale.
Mbaya zaidi kulikuwa hakuna majibu yenye mantiki ya kujibu kwanini kaletwa fisadi Lowasa kuwa mgombea tena kwa kuvunja katiba ya chama?
Hakukuwa na majibu zaidi ya mipasho na matusi.
Ccm 2015 ilikuwa taabani iliokolewa na Mbowe kwa gia ya angani.
Hayo unayosema ni mafanikio eti kuchukua baadhi ya halmashauri na kuongeza wabunge wengi ilikuwa ni matokeo ya kazi iliyofanyika nyuma na kina Dr Slaa na wengineo. Sio sababu ya Lowasa. Ndio maana baada ya hapo kila siku chama kinazidi kuzama.
Usijidanganye Chadema ya Mbowe haiaminiki.
 
Mbowe ni king'ang'a, ayatollah,kigando ,ruba,kupe hatoki wala atolewi 🤣🤣🤣🤣
 
Uadilifu wa Slaaa uko wapi? Mnakumbuka alihongwa nini na akakubali?
Heche nae si aliingia "mtego wa Polepole" nae akanunuliwa?
Tatizo lako unakurupuka kama uharo!
 
Ila kwanini Mbowe asipishe kama kweli anakipenda chama chake?
Yule mzee ni kilaza sana na true colors zake zimeshaonekana. Watanzania wanasali sana kuliombea taifa lao, kwenye wimbo wa taifa wanamtaja MUNGU na kuomba baraka zake. Ni ngumu sana sehemu penye ulinzi wa MUNGU mtu kama mbowe ambaye hana karama na Hekima ya uongozi kuweza kufanikiwa.

Jamaa ana tamaa sana. Hela anazo, kwanini analazimisha kuendelea kuwapo katika wadhifa ambao haumtaki for 30 years. Mzee takataka.
 
Wapinzani wakuu wa CHADEMA wanapenda sana vyama vyenye viongozi maskini wa fedha na mawazo ili wapate mtelemko ndiyo maana ya kelele za kuhusu uwenyekiti wa Mbowe.
 
Uadilifu wa Dr Slaa uko wapi?
Dr Slaa hana jipya zaidi ya FRUSTRATION. na siyo mtu wa kuaminika.

Toka kuwa Padri wa RC hadi kuwa Mume wa Rose Kamili na Mushumbushi ni kukosa focus. Kisha Mgombea wa CCM Karatu mwaka 1995 na kuhmia CHADEMA. Mbunge na kuwa Katibu mkuu wa CDM na mgombea uRais mwaka 2010. Halafu akasaliti chama kwa kununuliwa na Magufuli kama andazi au bakuli. Kafanya ubalozi lakini kipindi kilipokwisha mke kakataa kurudi Tanzania

Baada ya Ubalozi ku expire maana aliyempa alikufa, ndipo anakuja na munkari wa kutaka kupindua Serikali.

Dr Slaa ni mnafiki, msaliti, mtu asiyekuwa na msimamo na yuko tayari kuuzwa kama bidhaa
 
Mengi uliyoandika hapa yanaeleweka sana. Yapo mengi huko CHADEMA yanayotafakarisha sana. Yanatia shaka na kutibua. LAKINI niliyoyawekea rangi nyekundu yanaonyesha kasoro kubwa ya maamuzi na kukosa uhalisia.

Kuhama chama na kumchagua Magufuli 2015 haikuwa uamuzi wa busara. Nachukulia mlihamia CCM. Ulikuwa uamuzi mbaya kwa watu mliokuwa CHADEMA. Tuseme ilikuwa jazba tu. Najiuliza ilikuwaje 2020 msipige kura?

Wengi hatukufurahishwa na ujio wa Lowasa CHADEMA lakini CCM wala Magufuli hawakuwahi kuwa mbadala sahihi katika harakati za kuondoa matatizo ya nchi hii. Hata leo CCM bado ni tatizo kubwa la kitaifa. Labda mlifanya vile kwa vile mlikuwa makada viongozi kwamba kwenu nyinyi siasa ni kazi/ajira. Sisi tusiokuwa hata na kadi tuko huru zaidi kufikiri na kupima.

Mbowe hatutishi wala CHADEMA sio dini kwetu. Bado ina misingi mizuri na makada wa kuaminika sana. Naamini Mbowe wala mtu yeyote hana jeuri ya kubomoa misingi ya chama. Ataondoka yeye.

Halafu hakuna wakati wowote CCM imetishiwa au kuwa hatarini kuondolewa madarakani. 2015 CCM ingeshinda tu tena kwa kishindo hata kama Lowasa asingekuwa mgombea wa CHADEMA. Mbowe aiokoe CCM? Tena ya Magufuli? Dola itakuwa wapi kupanga matokeo ya uchaguzi mkuu?
 
Changamoto ni Kupata fedha za kuendesha Chama! Hao wote naoni wapo hoi kifedha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…