Tetesi: Huenda chama kipya cha Lissu kikasheheni watu waadilifu kama Dkt. Slaa, Prof. Safari, Mnyika, Heche, Wenje na wale wote waliotoka CHADEMA kwa figisu

Tetesi: Huenda chama kipya cha Lissu kikasheheni watu waadilifu kama Dkt. Slaa, Prof. Safari, Mnyika, Heche, Wenje na wale wote waliotoka CHADEMA kwa figisu

Mimi namwomba Mungu CHADEMA isipasuke,tofauti zao ziishe! Waungane then waendelee na mapambano!
 
Mbowe ndo chadema imara na upizani imara kwa nyakati hizi, bila mbowe kuwa mwenyekiti chadema, hakuna chadema, ya upizani kwa ccm, na hakuna chama kitakachotetelesha ccm.
 
Aulizwe Tundu LIsu, kwanini asianzishe chama chake kipya? mbona atachukua wafuasi wote.
 
Sikio la kufa halisikii dawa.
Kweli tume ya uchaguzi inakasoro hiyo haipingwi.
Ila kumbuka tume hii hii ndio iliyoleta upinzani 2010 Kikwete chupu chupu na 2015 kujaza kwa wingi wapinzani bungeni.
Unategemea Ccm watakuletea katiba na tume bora ili watoke kirahisi madarakani?
Upinzani unatakiwa kuwa upande wa wananchi na sera za upinzani zieleweke kwa wananchi walio wengi.

Chadema ilikuwa chama kikuu cha upinzani ni kwa ajili ya juhudi za kina Dr Slaa, Mnyika, Zito n.k kupambana kupenyeza agenda zao kwa wananchi hadi vijijini huko. Leo imekuwa One man show.
Gia ya angani ndio anguko la chadema. Walionywa wakawa na matusi bila hoja.
Mbowe na Samia lao moja.
Tusidanganyane, ukweli usemwe chadema ya sasa haipo kwa wananchi, yaani haina tofauti na CCM.
Hiyo ni ramli ya kishirikina. Uchaguzi huru na wa haki HAUJAFANYIKA. Utajuaje kama CHADEMA ipo au haipo kwa wananchi?

Porojo nyingi za kukaririshwa huko CCM. “Gia angani” wakapata wabunge wengi kuliko nyakati zote na kuongoza halmashauri nyingi - pamoja na kuibiwa ushindi - ndio kuanguka huko? No logic. Maelezo yote hayaunganiki. Hayana mantiki.

2019 na 2020 uchaguzi umeporwa jumla na serikali ya CCM, CHADEMA ikakosa vyote bungeni na serikali za mitaa. Serikali ikalazimisha viti maalum 19 vya CHADEMA bungeni na bado inahangaika kutafuta maelewano na kukubalika na chama hicho kwa kutambua ndicho “chama kikuu cha upinzani” nchini. Rais kasambaza mabango yenye picha akiwa na viongozi wa CHADEMA kutafuta kukubalika na wananchi. Hilo ni anguko?

CHADEMA ikiitisha mikutano, maelfu ya wananchi wanakusanyika kwa hiyari kusikiliza. Unasema haiko kwa wananchi? Well, endeleeni na porojo mfu na ramli. Ndicho kilichobakia.
 
Mbinu za CCM zimekwama. Mbowe haondoki na Lissu haanzishi chama kingine.
 
Mimi sioni kama Chadema itameguka kuelekea uchaguzi mkuu 2025.
Kwani ikimeguka kwa namna yoyote utakuwa ushindi mkubwa kwa CCM.
Chadema wasiongezee matatizo they need to read between the lines,Ukiweka changamoto za Covid 19 + Msigwa na Kanda ya Nyasa +Katibu Mkuu Myika+ Mwenyekiti Mbowe + Makamu Lissu =???
Chadema imefika wakati mjitambuwe mapema vinginevyo........
 
Mimi sioni kama Chadema itameguka kuelekea uchaguzi mkuu 2025.
Kwani ikimeguka kwa namna yoyote utakuwa ushindi mkubwa kwa CCM.
Chadema wasiongezee matatizo they need to read between the lines,Ukiweka changamoto za Covid 19 + Msigwa na Kanda ya Nyasa +Katibu Mkuu Myika+ Mwenyekiti Mbowe + Makamu Lissu =???
Chadema imefika wakati mjitambuwe mapema vinginevyo........
mkuu tukiachana na hayo, hivi mtu anakuwa seniour member kwa siku mbili? Linawezekana vipi j hili jambo?
 
Hiyo ni ramli ya kishirikina. Uchaguzi huru na wa haki HAUJAFANYIKA. Utajuaje kama CHADEMA ipo au haipo kwa wananchi?

Porojo nyingi za kukaririshwa huko CCM. “Gia angani” wakapata wabunge wengi kuliko nyakati zote na kuongoza halmashauri nyingi - pamoja na kuibiwa ushindi - ndio kuanguka huko? No logic. Maelezo yote hayaunganiki. Hayana mantiki.

2019 na 2020 uchaguzi umeporwa jumla na serikali ya CCM, CHADEMA ikakosa vyote bungeni na serikali za mitaa. Serikali ikalazimisha viti maalum 19 vya CHADEMA bungeni na bado inahangaika kutafuta maelewano na kukubalika na chama hicho kwa kutambua ndicho “chama kikuu cha upinzani” nchini. Rais kasambaza mabango yenye picha akiwa na viongozi wa CHADEMA kutafuta kukubalika na wananchi. Hilo ni anguko?

CHADEMA ikiitisha mikutano, maelfu ya wananchi wanakusanyika kwa hiyari kusikiliza. Unasema haiko kwa wananchi? Well, endeleeni na porojo mfu na ramli. Ndicho kilichobakia.
Ok ngoja tuone.
Ila mimi na wenzangu wengi tu ambao tupo pamoja hicho chama tulihama kuanzia 2015 tulimchagua Magufuli.
2020 hatukupiga kura.
NB: nilikuwa kiongozi wa CHADEMA ila gia ya angani ilituvuruga tukakaa kando.
Gia ya angani ilileta mamluki wengi kuja kuuwa chama na kuondoa wengi waliokipambania chama hadi kufikia mafanikio yale.
Mbaya zaidi kulikuwa hakuna majibu yenye mantiki ya kujibu kwanini kaletwa fisadi Lowasa kuwa mgombea tena kwa kuvunja katiba ya chama?
Hakukuwa na majibu zaidi ya mipasho na matusi.
Ccm 2015 ilikuwa taabani iliokolewa na Mbowe kwa gia ya angani.
Hayo unayosema ni mafanikio eti kuchukua baadhi ya halmashauri na kuongeza wabunge wengi ilikuwa ni matokeo ya kazi iliyofanyika nyuma na kina Dr Slaa na wengineo. Sio sababu ya Lowasa. Ndio maana baada ya hapo kila siku chama kinazidi kuzama.
Usijidanganye Chadema ya Mbowe haiaminiki.
 
Wasalaam, JF.

Wakati Tundu AM Lissu akiamua kuasisi chama kipya cha siasa na kuifanya Tanzania kuwa na jumla ya vyama 20 vya siasa akianzia kukisimika chama hicho kipya mkoani kwake Singida kabla ya kuanza harakati Tanzania nzima.

Tayari baadhi ya watu waadilifu kama Dkt. Slaa, Prof Safari, Boniface Mwambukusi, John Heche, John Pambalu, Godbless Lema, wanatajwa kuwa Viongozi wa awali wa Chama hicho ambacho bado jina lake halijajulikana.

Mkakati huu unakuja baada ya Katibu Mkuu wa CHADEMA John John Mnyika kukataa kuendelea kukaa ofisi kwa madai kwamba kazi zote za Katibu Mkuu anafanya Mpwa wa Mbowe ndugu John Mrema akisaidiwa na Bw Reginard Mtumishi ambae ni mjomba wa Freeman Mbowe.

Mkakati uliopo leo CHADEMA ni Freeman Mbowe kugombea tena nafasi ya Uenyekiti wa chama kwa mara ya nne mfululizo ukiacha mara mbili alizokuwa mwenyekiti kupitia BAVICHA na kufanya jumla ya mihula yote hiyo inamfanya Freeman Mbowe kuwa na miaka 30 kwenye uongozi wa CHADEMA bila kupisha yoyote kwenye uongozi Chama hicho.

Tundu AM Lissu ndio nembo pekee iliyosalia ndani ya CHADEMA ambayo imekuwa ikiibeba CHADEMA kama chama tangu kabla wakati na baada ya kupigwa kwake risasi 16 akiwa katika shughuli za kibunge Jijini Dodoma.

Kama Tundu AM Lissu ataihama CHADEMA basi huenda CHADEMA ikasalia kuwa kama CUF, NCCR na hata TLP kwa tayari imeshapoteza agenda yake ya Msingi ambayo ni kupinga Uzembe, Wizi na Ufisadi.

Tetesi za Mbowe kulamba asali ili aendelee kuwako CHADEMA kama Mwenyekiti ili kumdhibiti Tundu AM Lissu zimemlemea Mbowe na kuamua kurejesha Majeshi yake matiifu kutoka katika orodha ya Wabunge 19 waliofukuzwa.

Mbunge mmoja toka miongoni mwao jina tunalihifadhi anasema namnukuu "Halima ametuambia tusiendee CCM ila tumpambanie Mbowe awe mwenyekiti na Heche makamu ili amtoe Mnyika na Lissu ili turudi CHADEMA" mwisho wa kunukuu.

Taarifa kutoka maeneo mbalimbali zinaunga mkono Lissu kuanzisha chama chake hicho kipya kwani CHADEMA tayari imechafuka na imekuwa ngumu kuitofautisha na Chama tawala cha CCM kimaadili na kimwenendo na hivyo kupoteza tafsiri ya neno "Upinzani"

Tundu AM Lissu anasifika kwa kukemea rushwa na ufisadi ndani na nje ya CHADEMA waziwazi na ndio turufu pekee inayomfanya azidi kuaminika na kipendwa zaidi na Watanzania hasa wa tabaka la chini.

Kitendo hicho kinampa wakati mgumu zaidi Mwenyekiti wa Sasa Freeman Mbowe ambae Uadilifu wake na nyendo zake hasa awamu hii ya sita zinamashaka mengi kutokana na tuhuma nyingi za ulambaji wa asali kwa maeneo na nyakati tofauti tofauti.

Mbowe anaamini mfumo sasa uko tayari kupeleka dola CHADEMA wakati Lissu anaamini mfumo ndio CCM na CCM ndio mfumo wenyewe.

Lissu anaamini katika kutwaa dola kupitia Wananchi wakati Mbowe anaamini katika kutwaa dola kupitia mfumo au dola yenyewe.

Kitendo cha Lemma kujitoa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa Kanda ya Kask ni ishara inayoakisi ninachokiandika hapa kwani ni dhahiri ananga'tuka CHADEMA na kuelekea kwenye hicho chama jipya,

Tanzania inahitaji upinzani safi sio bora upinzani, ndio maana waliwakataa CUF, wakawakataa NCCR na hivyo hivyo wakafanya kwa TLP na leo hii ni zamu ya CHADEMA kukataliwa wazi wazi

CHADEMA ndio chama Cha upinzani kinachomiliki mwenyekiti mmoja kwa miaka 30 huku wakiranda randa kuomba katiba mpya kwa wananchi wakati katiba yao inamatundu kama chekecheo.
Mbowe ni king'ang'a, ayatollah,kigando ,ruba,kupe hatoki wala atolewi 🤣🤣🤣🤣
 
Uadilifu wa Slaaa uko wapi? Mnakumbuka alihongwa nini na akakubali?
Heche nae si aliingia "mtego wa Polepole" nae akanunuliwa?
Tatizo lako unakurupuka kama uharo!
 
Ila kwanini Mbowe asipishe kama kweli anakipenda chama chake?
Yule mzee ni kilaza sana na true colors zake zimeshaonekana. Watanzania wanasali sana kuliombea taifa lao, kwenye wimbo wa taifa wanamtaja MUNGU na kuomba baraka zake. Ni ngumu sana sehemu penye ulinzi wa MUNGU mtu kama mbowe ambaye hana karama na Hekima ya uongozi kuweza kufanikiwa.

Jamaa ana tamaa sana. Hela anazo, kwanini analazimisha kuendelea kuwapo katika wadhifa ambao haumtaki for 30 years. Mzee takataka.
 
Wasalaam, JF.

Wakati Tundu AM Lissu akiamua kuasisi chama kipya cha siasa na kuifanya Tanzania kuwa na jumla ya vyama 20 vya siasa akianzia kukisimika chama hicho kipya mkoani kwake Singida kabla ya kuanza harakati Tanzania nzima.

Tayari baadhi ya watu waadilifu kama Dkt. Slaa, Prof Safari, Boniface Mwambukusi, John Heche, John Pambalu, Godbless Lema, wanatajwa kuwa Viongozi wa awali wa Chama hicho ambacho bado jina lake halijajulikana.

Mkakati huu unakuja baada ya Katibu Mkuu wa CHADEMA John John Mnyika kukataa kuendelea kukaa ofisi kwa madai kwamba kazi zote za Katibu Mkuu anafanya Mpwa wa Mbowe ndugu John Mrema akisaidiwa na Bw Reginard Mtumishi ambae ni mjomba wa Freeman Mbowe.

Mkakati uliopo leo CHADEMA ni Freeman Mbowe kugombea tena nafasi ya Uenyekiti wa chama kwa mara ya nne mfululizo ukiacha mara mbili alizokuwa mwenyekiti kupitia BAVICHA na kufanya jumla ya mihula yote hiyo inamfanya Freeman Mbowe kuwa na miaka 30 kwenye uongozi wa CHADEMA bila kupisha yoyote kwenye uongozi Chama hicho.

Tundu AM Lissu ndio nembo pekee iliyosalia ndani ya CHADEMA ambayo imekuwa ikiibeba CHADEMA kama chama tangu kabla wakati na baada ya kupigwa kwake risasi 16 akiwa katika shughuli za kibunge Jijini Dodoma.

Kama Tundu AM Lissu ataihama CHADEMA basi huenda CHADEMA ikasalia kuwa kama CUF, NCCR na hata TLP kwa tayari imeshapoteza agenda yake ya Msingi ambayo ni kupinga Uzembe, Wizi na Ufisadi.

Tetesi za Mbowe kulamba asali ili aendelee kuwako CHADEMA kama Mwenyekiti ili kumdhibiti Tundu AM Lissu zimemlemea Mbowe na kuamua kurejesha Majeshi yake matiifu kutoka katika orodha ya Wabunge 19 waliofukuzwa.

Mbunge mmoja toka miongoni mwao jina tunalihifadhi anasema namnukuu "Halima ametuambia tusiendee CCM ila tumpambanie Mbowe awe mwenyekiti na Heche makamu ili amtoe Mnyika na Lissu ili turudi CHADEMA" mwisho wa kunukuu.

Taarifa kutoka maeneo mbalimbali zinaunga mkono Lissu kuanzisha chama chake hicho kipya kwani CHADEMA tayari imechafuka na imekuwa ngumu kuitofautisha na Chama tawala cha CCM kimaadili na kimwenendo na hivyo kupoteza tafsiri ya neno "Upinzani"

Tundu AM Lissu anasifika kwa kukemea rushwa na ufisadi ndani na nje ya CHADEMA waziwazi na ndio turufu pekee inayomfanya azidi kuaminika na kipendwa zaidi na Watanzania hasa wa tabaka la chini.

Kitendo hicho kinampa wakati mgumu zaidi Mwenyekiti wa Sasa Freeman Mbowe ambae Uadilifu wake na nyendo zake hasa awamu hii ya sita zinamashaka mengi kutokana na tuhuma nyingi za ulambaji wa asali kwa maeneo na nyakati tofauti tofauti.

Mbowe anaamini mfumo sasa uko tayari kupeleka dola CHADEMA wakati Lissu anaamini mfumo ndio CCM na CCM ndio mfumo wenyewe.

Lissu anaamini katika kutwaa dola kupitia Wananchi wakati Mbowe anaamini katika kutwaa dola kupitia mfumo au dola yenyewe.

Kitendo cha Lemma kujitoa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa Kanda ya Kask ni ishara inayoakisi ninachokiandika hapa kwani ni dhahiri ananga'tuka CHADEMA na kuelekea kwenye hicho chama jipya,

Tanzania inahitaji upinzani safi sio bora upinzani, ndio maana waliwakataa CUF, wakawakataa NCCR na hivyo hivyo wakafanya kwa TLP na leo hii ni zamu ya CHADEMA kukataliwa wazi wazi

CHADEMA ndio chama Cha upinzani kinachomiliki mwenyekiti mmoja kwa miaka 30 huku wakiranda randa kuomba katiba mpya kwa wananchi wakati katiba yao inamatundu kama chekecheo.
Wapinzani wakuu wa CHADEMA wanapenda sana vyama vyenye viongozi maskini wa fedha na mawazo ili wapate mtelemko ndiyo maana ya kelele za kuhusu uwenyekiti wa Mbowe.
 
Wasalaam, JF.

Wakati Tundu AM Lissu akiamua kuasisi chama kipya cha siasa na kuifanya Tanzania kuwa na jumla ya vyama 20 vya siasa akianzia kukisimika chama hicho kipya mkoani kwake Singida kabla ya kuanza harakati Tanzania nzima.

Tayari baadhi ya watu waadilifu kama Dkt. Slaa, Prof Safari, Boniface Mwambukusi, John Heche, John Pambalu, Godbless Lema, wanatajwa kuwa Viongozi wa awali wa Chama hicho ambacho bado jina lake halijajulikana.

Mkakati huu unakuja baada ya Katibu Mkuu wa CHADEMA John John Mnyika kukataa kuendelea kukaa ofisi kwa madai kwamba kazi zote za Katibu Mkuu anafanya Mpwa wa Mbowe ndugu John Mrema akisaidiwa na Bw Reginard Mtumishi ambae ni mjomba wa Freeman Mbowe.

Mkakati uliopo leo CHADEMA ni Freeman Mbowe kugombea tena nafasi ya Uenyekiti wa chama kwa mara ya nne mfululizo ukiacha mara mbili alizokuwa mwenyekiti kupitia BAVICHA na kufanya jumla ya mihula yote hiyo inamfanya Freeman Mbowe kuwa na miaka 30 kwenye uongozi wa CHADEMA bila kupisha yoyote kwenye uongozi Chama hicho.

Tundu AM Lissu ndio nembo pekee iliyosalia ndani ya CHADEMA ambayo imekuwa ikiibeba CHADEMA kama chama tangu kabla wakati na baada ya kupigwa kwake risasi 16 akiwa katika shughuli za kibunge Jijini Dodoma.

Kama Tundu AM Lissu ataihama CHADEMA basi huenda CHADEMA ikasalia kuwa kama CUF, NCCR na hata TLP kwa tayari imeshapoteza agenda yake ya Msingi ambayo ni kupinga Uzembe, Wizi na Ufisadi.

Tetesi za Mbowe kulamba asali ili aendelee kuwako CHADEMA kama Mwenyekiti ili kumdhibiti Tundu AM Lissu zimemlemea Mbowe na kuamua kurejesha Majeshi yake matiifu kutoka katika orodha ya Wabunge 19 waliofukuzwa.

Mbunge mmoja toka miongoni mwao jina tunalihifadhi anasema namnukuu "Halima ametuambia tusiendee CCM ila tumpambanie Mbowe awe mwenyekiti na Heche makamu ili amtoe Mnyika na Lissu ili turudi CHADEMA" mwisho wa kunukuu.

Taarifa kutoka maeneo mbalimbali zinaunga mkono Lissu kuanzisha chama chake hicho kipya kwani CHADEMA tayari imechafuka na imekuwa ngumu kuitofautisha na Chama tawala cha CCM kimaadili na kimwenendo na hivyo kupoteza tafsiri ya neno "Upinzani"

Tundu AM Lissu anasifika kwa kukemea rushwa na ufisadi ndani na nje ya CHADEMA waziwazi na ndio turufu pekee inayomfanya azidi kuaminika na kipendwa zaidi na Watanzania hasa wa tabaka la chini.

Kitendo hicho kinampa wakati mgumu zaidi Mwenyekiti wa Sasa Freeman Mbowe ambae Uadilifu wake na nyendo zake hasa awamu hii ya sita zinamashaka mengi kutokana na tuhuma nyingi za ulambaji wa asali kwa maeneo na nyakati tofauti tofauti.

Mbowe anaamini mfumo sasa uko tayari kupeleka dola CHADEMA wakati Lissu anaamini mfumo ndio CCM na CCM ndio mfumo wenyewe.

Lissu anaamini katika kutwaa dola kupitia Wananchi wakati Mbowe anaamini katika kutwaa dola kupitia mfumo au dola yenyewe.

Kitendo cha Lemma kujitoa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa Kanda ya Kask ni ishara inayoakisi ninachokiandika hapa kwani ni dhahiri ananga'tuka CHADEMA na kuelekea kwenye hicho chama jipya,

Tanzania inahitaji upinzani safi sio bora upinzani, ndio maana waliwakataa CUF, wakawakataa NCCR na hivyo hivyo wakafanya kwa TLP na leo hii ni zamu ya CHADEMA kukataliwa wazi wazi

CHADEMA ndio chama Cha upinzani kinachomiliki mwenyekiti mmoja kwa miaka 30 huku wakiranda randa kuomba katiba mpya kwa wananchi wakati katiba yao inamatundu kama chekecheo.
Uadilifu wa Dr Slaa uko wapi?
Dr Slaa hana jipya zaidi ya FRUSTRATION. na siyo mtu wa kuaminika.

Toka kuwa Padri wa RC hadi kuwa Mume wa Rose Kamili na Mushumbushi ni kukosa focus. Kisha Mgombea wa CCM Karatu mwaka 1995 na kuhmia CHADEMA. Mbunge na kuwa Katibu mkuu wa CDM na mgombea uRais mwaka 2010. Halafu akasaliti chama kwa kununuliwa na Magufuli kama andazi au bakuli. Kafanya ubalozi lakini kipindi kilipokwisha mke kakataa kurudi Tanzania

Baada ya Ubalozi ku expire maana aliyempa alikufa, ndipo anakuja na munkari wa kutaka kupindua Serikali.

Dr Slaa ni mnafiki, msaliti, mtu asiyekuwa na msimamo na yuko tayari kuuzwa kama bidhaa
 
Ok ngoja tuone.
Ila mimi na wenzangu wengi tu ambao tupo pamoja hicho chama tulihama kuanzia 2015 tulimchagua Magufuli.
2020 hatukupiga kura.

NB: nilikuwa kiongozi wa CHADEMA ila gia ya angani ilituvuruga tukakaa kando.
Gia ya angani ilileta mamluki wengi kuja kuuwa chama na kuondoa wengi waliokipambania chama hadi kufikia mafanikio yale.
Mbaya zaidi kulikuwa hakuna majibu yenye mantiki ya kujibu kwanini kaletwa fisadi Lowasa kuwa mgombea tena kwa kuvunja katiba ya chama?
Hakukuwa na majibu zaidi ya mipasho na matusi.
Ccm 2015 ilikuwa taabani iliokolewa na Mbowe kwa gia ya angani.
Hayo unayosema ni mafanikio eti kuchukua baadhi ya halmashauri na kuongeza wabunge wengi ilikuwa ni matokeo ya kazi iliyofanyika nyuma na kina Dr Slaa na wengineo. Sio sababu ya Lowasa. Ndio maana baada ya hapo kila siku chama kinazidi kuzama.
Usijidanganye Chadema ya Mbowe haiaminiki.
Mengi uliyoandika hapa yanaeleweka sana. Yapo mengi huko CHADEMA yanayotafakarisha sana. Yanatia shaka na kutibua. LAKINI niliyoyawekea rangi nyekundu yanaonyesha kasoro kubwa ya maamuzi na kukosa uhalisia.

Kuhama chama na kumchagua Magufuli 2015 haikuwa uamuzi wa busara. Nachukulia mlihamia CCM. Ulikuwa uamuzi mbaya kwa watu mliokuwa CHADEMA. Tuseme ilikuwa jazba tu. Najiuliza ilikuwaje 2020 msipige kura?

Wengi hatukufurahishwa na ujio wa Lowasa CHADEMA lakini CCM wala Magufuli hawakuwahi kuwa mbadala sahihi katika harakati za kuondoa matatizo ya nchi hii. Hata leo CCM bado ni tatizo kubwa la kitaifa. Labda mlifanya vile kwa vile mlikuwa makada viongozi kwamba kwenu nyinyi siasa ni kazi/ajira. Sisi tusiokuwa hata na kadi tuko huru zaidi kufikiri na kupima.

Mbowe hatutishi wala CHADEMA sio dini kwetu. Bado ina misingi mizuri na makada wa kuaminika sana. Naamini Mbowe wala mtu yeyote hana jeuri ya kubomoa misingi ya chama. Ataondoka yeye.

Halafu hakuna wakati wowote CCM imetishiwa au kuwa hatarini kuondolewa madarakani. 2015 CCM ingeshinda tu tena kwa kishindo hata kama Lowasa asingekuwa mgombea wa CHADEMA. Mbowe aiokoe CCM? Tena ya Magufuli? Dola itakuwa wapi kupanga matokeo ya uchaguzi mkuu?
 
Changamoto ni Kupata fedha za kuendesha Chama! Hao wote naoni wapo hoi kifedha!
 
Back
Top Bottom