𝗛𝗘𝗥𝗦𝗜 𝗔𝗜𝗞𝗔𝗡𝗔 𝗬𝗔𝗡𝗚𝗔
“Mimi sio mfanyakazi wa Yanga, Sipo kwenye orodha ya wanaolipwa na Yanga, sipati Tsh. 100 Yanga, mimi kwa maana ya Rais wa Klabu sio mfanyakazi wa klabu, wala haajiriwi na klabu, Makamu wa Rais pia, wajumbe wa kamati ya utendaji pia sio wafanyakazi wa Yanga.
“Wafanyakazi wa Yanga wanaanzia Level ya CEO hao ndio waajiriwa wa Yanga sisi ni viongozi ambao tumechaguliwa na Wanachama wa Yanga kuisimamia Yanga,” Rais wa Yanga Sc, Eng. Hersi Said.
Chanzo: Mitandaoni na Wasafi Media.
Kumbe ndiyo maana hata Jezi zao zinauzwa Tsh 40,000/= na Yanga SC inapata Tsh 1,800/= tu na zilizobaki ni za GSM.