Huko kwenu wapo watu wa namna hii?

Huko kwenu wapo watu wa namna hii?

o_2

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2017
Posts
428
Reaction score
385
Habari za mausiku,

Mmelala sio, mkiamka mtaikuta.

Jana nilianza safari kutokea Tukuyu kwenda Tanga. Tukuyu, Busokelo ndani ndani huko. Ipo changamoto ya usafiri ya hatari. Na kama unavyojua shule zinafunguliwa kwa hiyo usafiri ni 'mtihani' kwelikweli. Bahati mbaya zaidi hakuna basi la moja kwa moja kutokea Tukuyu-Tanga halipo.

Basi bwana nikaanza safari yangu mdogo mdogo kwa kupanda 'Noah' kutokea Busokelo mpaka Tukuyu, baada ya hapo nikapanda 'coaster' mpaka Mbeya city, stendi kuu.

Nikawaza leo nataka nile winga mpaka 'morning' . Silali lodge. Muda unavyokwenda baridi inaongezeka, basi nikafikiria kununua chai ya moto, kahawa basi ilimradi tu ujoto ujoto uje mwilini.

Basi wapo wamama wamejipanga, unachagua tu, mmama wa kwanza nikamsalim, nikapita kwa mmama mwingine kupata nilichokuwa nakihitaji. Nikakikapata. Lakini mmama wa kwanza alikua na jiko la mkaa linawaka kama mwenge. Nikaona isiwe tabu zaidi, nikamuomba, "Samahani, naweza kukakaa kwenye benchi lako niotee moto kidogo?" Mmama kaniangalia tu kauzu kweli kweli. Nikamuomba tena akakubali.

Nikakaa, nikainjoy joto la 'abuja' raha sana kutokana na baridi iliyokuwepo. Nikamaliza pale, nikaendelea kuzunguka zunguka kidogo kushangaa mazingira. Baadae nikaona mwili umepata ubaridi. Nikarudi tena kwa mmama yule, nikamuomba tena...

Mmama amenikatalia katu katu, usikae hapa kaa kule, wewe si ulikuwa umekaa kule.

Ye!!!??

Nikaona isiwe bugudha, yule mmama mwingine kusikia yule mmama ananiambia vile akaniambia njoo ukae hapa. Basi bwana nikaenda kukaa na nikanywa chai na alikuwa na moto.

Saa hizi ni saa 2:07 usiku, bado na vutavuta muda ifike saa 05:30 asubuhi safari ikaanze.

Roho nyeusi zipo na Roho nyeupe zipo.

Tuishi.
 
Habari za mausiku,

Mmelala sio, mkiamka mtaikuta.

Jana nilianza safari kutokea Tukuyu kwenda Tanga. Tukuyu, Busokelo ndani ndani huko. Ipo changamoto ya usafiri ya hatari. Na kama unavyojua shule zinafunguliwa kwa hiyo usafiri ni 'mtihani' kwelikweli. Bahati mbaya zaidi hakuna basi la moja kwa moja kutokea Tukuyu-Tanga halipo.

Basi bwana nikaanza safari yangu mdogo mdogo kwa kupanda 'Noah' kutokea Busokelo mpaka Tukuyu, baada ya hapo nikapanda 'coaster' mpaka Mbeya city, stendi kuu.

Nikawaza leo nataka nile winga mpaka 'morning' . Silali lodge. Muda unavyokwenda baridi inaongezeka, basi nikafikiria kununua chai ya moto, kahawa basi ilimradi tu ujoto ujoto uje mwilini.

Basi wapo wamama wamejipanga, unachagua tu, mmama wa kwanza nikamsalim, nikapita kwa mmama mwingine kupata nilichokuwa nakihitaji. Nikakikapata. Lakini mmama wa kwanza alikua na jiko la mkaa linawaka kama mwenge. Nikaona isiwe tabu zaidi, nikamuomba, "Samahani, naweza kukakaa kwenye benchi lako niotee moto kidogo?" Mmama kaniangalia tu kauzu kweli kweli. Nikamuomba tena akakubali.

Nikakaa, nikainjoy joto la 'abuja' raha sana kutokana na baridi iliyokuwepo. Nikamaliza pale, nikaendelea kuzunguka zunguka kidogo kushangaa mazingira. Baadae nikaona mwili umepata ubaridi. Nikarudi tena kwa mmama yule, nikamuomba tena...

Mmama amenikatalia katu katu, usikae hapa kaa kule, wewe si ulikuwa umekaa kule.

Ye!!!??

Nikaona isiwe bugudha, yule mmama mwingine kusikia yule mmama ananiambia vile akaniambia njoo ukae hapa. Basi bwana nikaenda kukaa na nikanywa chai na alikuwa na moto.

Saa hizi ni saa 2:07 usiku, bado na vutavuta muda ifike saa 05:30 asubuhi safari ikaanze.

Roho nyeusi zipo na Roho nyeupe zipo.

Tuishi.
Sasa ndio nn?
 
Nimekushangaaa !!!!! Una miaka mingapi??
 
Bwa mdogo huna haja ya kuanzisha thread hiyo hela bando ungelipa guest ulale.
Mi km babako nakupa kisa cha kupiga dochi.
Iringa mjini,nilifika na visenti toka huko mbeya,kata tiketi bus kingcross siku ya pili halitokei
Lala guest hela imekata bus haliji.
Nikahamia stendi,pale kutana na madingi yana hela kweli kweli ila tuko Safari moja.
Konda katukimbia na nauli ilikua buku jero tu iringa-dom.
Usiku wa kwanza ola tuko stendi.yale madingi yanapiga ulanzi tu masaa yanaenda.
Siku ya pili ndo mtaani huko nikamfuma konda aliyetutoroka na hela za tkt.
Nikamkaba mpk kwa wazee pale iringa stendi.
Karudisha nusu hasara.
Ikabidi plan b.
Tukapata bus shalawambe toka pale mpk mtera,ili mtera tuunge bus urafiki hadi dom.
Hiyo safari ni hadithi kitabu kabisa ntasimulia siku ingine.
Ila katika mda huo niligeuka kuwa kalevi ka ulanzi kadogodogo maana yale mafadha tuligeuka marafiki tu basi njia nzima ilikua ulanzi na safari.
Hatukuwai kulala bure ilikua 5 day trip with no usingizi.
 
Huwenda huo usumbufu wa wewe kukaa na kuondoka hakupenda. Pia sisi binadam sio wa kuaminiana, alipata mashaka. Ni vizuri kuwepo sehemu kwa wakati sahihi na shughuli sahihi sio kila mahala ni kuwepo tu ilimradi. Kimsingi wenzako wako kwenye biashara halafu wewe una mambo yako. Hii sio sawa kabisa.
 
Bwa mdogo huna haja ya kuanzisha thread hiyo hela bando ungelipa guest ulale.
Mi km babako nakupa kisa cha kupiga dochi.
Iringa mjini,nilifika na visenti toka huko mbeya,kata tiketi bus kingcross siku ya pili halitokei
Lala guest hela imekata bus haliji.
Nikahamia stendi,pale kutana na madingi yana hela kweli kweli ila tuko Safari moja.
Konda katukimbia na nauli ilikua buku jero tu iringa-dom.
Usiku wa kwanza ola tuko stendi.yale madingi yanapiga ulanzi tu masaa yanaenda.
Siku ya pili ndo mtaani huko nikamfuma konda aliyetutoroka na hela za tkt.
Nikamkaba mpk kwa wazee pale iringa stendi.
Karudisha nusu hasara.
Ikabidi plan b.
Tukapata bus shalawambe toka pale mpk mtera,ili mtera tuunge bus urafiki hadi dom.
Hiyo safari ni hadithi kitabu kabisa ntasimulia siku ingine.
Ila katika mda huo niligeuka kuwa kalevi ka ulanzi kadogodogo maana yale mafadha tuligeuka marafiki tu basi njia nzima ilikua ulanzi na safari.
Hatukuwai kulala bure ilikua 5 day trip with no usingizi.
Nauli ya buku jero - aisee hiyo itakuwa miaka ya 1996 flani wakati nauli ya Iringa - Dar ikiwa ni elfu 5, basi ni Scandnavia na Comfort Video Coach (CVC) na Computer (Toyota DCM) hii ilikuwa inakwenda Dar na kurudi siku hiyohiyo. King Cross ilikuwa king of the road, basi tu jamaa Shafii alishindwa kuendana na mabadiliko, angenunua michina au coaster kadhaa wakati huu wa lami Jina lingembeba
 
Nauli ya buku jero - aisee hiyo itakuwa miaka ya 1996 flani wakati nauli ya Iringa - Dar ikiwa ni elfu 5, basi ni Scandnavia na Comfort Video Coach (CVC) na Computer (Toyota DCM) hii ilikuwa inakwenda Dar na kurudi siku hiyohiyo. King Cross ilikuwa king of the road, basi tu jamaa Shafii alishindwa kuendana na mabadiliko, angenunua michina au coaster kadhaa wakati huu wa lami Jina lingembeba
Ilikua 92-93 huko, dom -ira ilikua ni king cross tu anapiga ndefu.
Shalawambe na mabus mengine route fupi tu mpk mtera.
Hata Urafiki mbabe enzi hizo pale Dom alikua bus lake mwisho dom- mtera.
Ila baadae aliweka route ya dom -moro-iringa. Ndo ikaanza kuua king cross mdogo mdogo.
 
Back
Top Bottom