Huku kwetu Kwamtogole ukiwa na sherehe, "self service" ya chakula inaumiza wengi

Huku kwetu Kwamtogole ukiwa na sherehe, "self service" ya chakula inaumiza wengi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1580182822733.jpeg
Ni rahisi huku kwetu kuweka chakula kwenye sinia watu wale kwenye majamvi. Kama ni single plates basi zipakuliwe jikoni watu watolewe.

Huu utaratibu wa watu kujichikuliia nyama wenyewe, ni watu 10-15 wamwanzo ndiyo watabeba nyama zote. Unakuta mtu amepanga nyama kama mlima Kilimanjaro.

Usiombe useme ladies first, wanaume hawatakuta kitu hao ladies ndiyo wataalamu wa kupanga milima ya nyama.

Hapa hata uwe umechinja kuku 50 na ng’ombe mmoja bado kuna watakao kosa nyama. Mchele si big deal ingawa unashushia nyama.

Kuna wanaokuja na mabakuli kwenye pochi, akichukua nyama anapunguzia kwenye bakuli ili na watoto nyumbani wapate.
Ukiweka caterers wagawa chakula kuna watakao rudia foleni mara tatu kwanza kabla hawajala.

Ustaarabu huku kwetu ni sinia watu wagawane nyama wenyewe. Kwenye sinia hakuna atakaebeba nyama atie kwenyebakuli.
 
Waliwahi Tenga Sinia la wali namna hiyo huko kwetu, Cha ajabu Ile linashuka tu dah! Naweka mkono kwenye bakuli la nyama ghafula nashika mchuzi tu.

Kumbe Kila mtu keshachukua hata sekunde mbili hazijaisha nilitumia Sana😀
 
Back
Top Bottom