Hukumu ya lema ilipikwa.

Kwani anayeathirika na ubunge wa Arusha ni Batilda peke yake? Waathirika wa kwanza ni wananchi, so kama wananchi wameweza kuprove kuathirika kwao basi hiyo tort unayozungumzia imeheshimiwa.
 
Reactions: EMT
hakika naamini Lema atarudi mjengoni hilo la kuchakachua lilikuwa wazi tangia awali.hukumu ilijulikana mapemaaaaaaaaaaa.
 
hebu tupeni cv ya huyo jaji kwanza

ndugu yangu kwani hujui cv za bongo zinapatikana vp na wapi? Cv inaweza kuwa nzuri kuliko hata ya jaji mkuu na hayo ni makaratasi tu tatizo ni content ya kichwa chake kimeoza. Labda sema akapimwe akili.
 

Jaji aliyejitoa katika kesi hii anaitwa Aloycius Mujulizi, ni mmiliki mwenza wa IMMMA advocates.

Kama ni huyu ... then hatuna sababu ya kushangaa.
Huyu ni kati ya wale waliopewa "ujaji wa kulipa fadhila" na jk mara tu alipopata "urahisi".
 
By Avanti





Wakuu hapa nadhani kuna hoja ya ku Reveal tuone huo ushahidi ulivyo kuwa maana report ya jinsi kesi ilivyo kuwa ikiendesha na watu wanavyo toa ushahidi kabisa ilikuwa inaonyesha hakuna kesi ya kujibu.

My Take;

Waandishi wa habari za mahakamni mturudishie tena mwanzo wa kesi na mahojiano ya mashahidi jinsi ulivyo enda mpaka ulipo fikia hukumu.

Tujiridhishe twataka kupima uwezo wa majaji wetu

NB;
Mfumo wa kenya kuwa pata Jaji ndio mzuri unakuwa interviewed live na Nation TV sio hapa unakuwa appointed na Presdaaaaa


 
Halafu wewe mjinga na kingereza chako cha makengeza! Mimi siyo mwanasheria ila huu ni upuuzi kwani huwezi ukamhukumu mtu bila hata audio au video inayoonsesha alitukana. Na ninakuahidi ujinga wako utakoma siku Lema akichukua jimbo tena. Na huyo jaji wako na waliomshitaki na kumbambikiza Lema inabidi watafute pahali pakuishi nadhani arusha hapawatosha.
 
Hata sasa ivi hapawatoshi subiri......
 


Mkuu mbona unaji-contradict wewe mwenyewe..?
 
wenzetu wakenya huwa wana ka utaratibu kazuri sana wa kuwapata viongozi wa kuongoza taasisi nyeti zote.huku kwetu hawa mabwana ni ma president appointees,hv rais akisema make sure that kesi funali ushindi unapatikana atagoma jaji?

hamia huko
 
Ila jamaa anaonekana siyo mtanzania au kama ni hivyo basi ni ule wa kugawiwa.
 
Wanajamii, nauliza hivi, Lema anruhusiwa kugombea tena?
 

Jaji aliyejitoa katika kesi hii anaitwa Aloycius Mujulizi, ni mmiliki mwenza wa IMMMA advocates.
Mmmh, now I got it. Kumbe tayari kuna judge aliyeiona hii kesi kwamba ina mizengwe akaamua kunjitoa? Huu nao ni ushahidi tosha kwamba hii hukumu ni ya kihuni.
 
[h=2]Bold Jina la Jaji aliyetoa hukumu ya lema. Rushwa hapa haipingiki, ni CCM damu damu, na utanzania wake ni wakutilia shaka.
Wednesday, March 5, 2008[/h][h=3]Mtoto wa Kikwete ahusishwa na ufisadi[/h]

Na Saed Kubenea

MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete anafanya kazi katika kampuni iliyoshiriki kusajili kampuni ya Deep Green Finance Ltd., ambayo ilikwapua mabilioni ya shilingi kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

MwanaHALISI linazo taarifa kwamba kampuni ya mawakili ya IMMA Advocates and Co. ya Dar es Salaam ndiyo ilisadia usajili wa Deep Green Finance Ltd iliyochota Sh. 8 bilioni kutoka BoT.

Hakuna maelezo yoyote yaliyowahi kutolewa kueleza kwa nini Deep Green Finance Limited ililipwa mabilioni hayo na BoT wakati wa uongozi wa gavana Daudi Billali ambaye Rais Jakaya Kikwete alifukuza kazi miezi miwili iliyopita.

Mtoto wa rais, ambaye anafanya kazi katika kampuni iliyosaidia kusajili Deep Green Finance Ltd., ni Ridhwani Kikwete.

Deep Green Finance Limited ilichota fedha hizo kati ya Septemba na Desemba 2005 wakati wa mchakato kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

IMMA inasimamia majina ya wamiliki wa kampuni hiyo ya mawakili ambao ni Protase Ishengoma, Lawrence Masha, Aloysius Mujulizi na Sadock Magai.

Mmoja wa wamiliki wa kampuni hiyo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha aliithibitishia MwanaHALISI kwamba ni mwanzilishi na mmiliki wa IMMA.

Hata hivyo aliharakisha kusema kwamba kwa sasa amekabidhi majukumu yake kwa wakurugenzi wake wengine baada ya kuchukua wadhifa serikalini.

"Ni kweli kwamba mimi ni mmoja wa wakurugenzi waanzilishi wa IMMA, lakini kwa sasa siko huko. Nimeacha kujishughulisha na shughuli za kampuni hiyo tangu mwaka 2005 nilipoingia serikalini," alisema Masha.

Aidha, Masha alithibitisha pia kwamba kampuni ya IMMA ndiyo iliyosajili kampuni ya Deep Green Finance Limited na kwamba ni kweli kuwa inamwajiri Ridhwan.

Hata hivyo, Masha amesema mwenye nafasi nzuri zaidi ya kuzungumzia masuala ya IMMA hivi sasa ni mkurugenzi mwendeshaji, Protase Ishengoma.

Ridhwani alifanya kazi katika kampuni hiyo ya uwakili akiwa bado kwenye mafunzo mara baada ya kupata shahada yake ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye amezungumza kwa sharti la kutotajwa jina ameliambia MwanaHALISI, "Tuombe kusipatikane ushahidi wa moja kwa moja kati ya IMMA na mafisadi; vinginevyo hadhi ya rais wetu itaathirika vibaya sana."

Wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, kipindi mabilioni ya shilingi yalipokwapuliwa na Deep Green Finance Limited iliyoanzishwa kwa msaada wa IMMA, Ridhwani alikuwa tayari anafanya kazi katika kampuni ya mawakili.

Masha amethibitisha kuwa Ridhwani bado anafanya kazi kwenye kampuni hiyo hadi sasa.

Ridhwani hakupatikana hadi tunakwenda mitamboni kujibu swali iwapo hana wasiwasi wa kufanya kazi katika kampuni inayotuhumiwa kuibia taifa.

Kuhusu vigezo vya kuajiriwa, Masha amesema Ridhiwani alitimiza vigezo vyote na kwamba ana sifa zinazohitajika.

Imefahamika pia kuwa Fatuma Karume, mtoto wa Rais wa Zanzibar, Abeid Amani Karume, anafanya kazi IMMA.

Ni katika kampuni ya IMMA pia rais aliteua wakili Aloysius Mujulizi, ambaye ni mmoja wa wanahisa, kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Hivi karibuni kumekuwa na minong'ono na tuhuma za chichini kuhusu kampuni iliyosaidia kusajili Deep Green Finance Limited ambako mtoto wa rais anafanya kazi na ambako rais ameteua wakili kuwa jaji na wakili mwingine kuwa waziri.

Taarifa kutoka kwa Msajili wa Makampuni zinawataja watu wawili, Protase Ishengoma na Stella Ndikimi kuwa wakurugenzi waanzilishi wa Deep Green Finance Limited.

Ishengoma alithibitisha katika mahojiano yake na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu juzi Jumatatu, kwamba alishiriki kusajili Deep Green Finance Limited.

Kampuni ya Deep Green ilifilisiwa mwaka 2006, kabla ya kufikisha hata mwaka moja wa uhai wake, katika kile wachunguzi wa mambo wanasema, "baada ya kukidhi matakwa na matarajio yake."

Hadi sasa haijafahamika Sh. 8 bilioni zilizochotwa zilichukuliwa ili zifanye kazi gani na wapi.

Wakili Ishengoma alikiri pia kuwa ni yeye aliyeteuliwa kuifilisi kampuni aliyoanzisha.

MwanaHALISI ina ushahidi wa malipo kutoka Deep Green Finance Limited kwenda IMMA ingawa haikufahamika ilikuwa kwa kazi gani; kama vile ambavyo malipo kutoka BoT kwenda Deep Green hayajapatiwa maelezo hadi sasa.

Taarifa za ukwapuaji mabilioni ya shilingi kutoka BoT ziliwahi kuanikwa na kundi la wanasiasa likiongozwa na Mbunge wa Karatu, Dk. Willibrod Slaa siku lilipotangaza "orodha ya mafisadi" kwenye viwanja vya Mwembeyanga jijini Dar es Salaamn mwaka jana.

Kutopatikana maelezo halisi juu ya kazi ya Deep Green Finance Limited; maelezo kuhusu matumizi ya mabilioni yaliyochukuliwa benki na sababu za kufilisiwa haraka kwa kampuni hiyo, vinamweka mtoto wa rais karibu na lawama na tuhuma lukuki.

Shutuma na tuhuma, za chinichini na za wazi zinatokana na matukio makuu yafuatayo:

Kwanza, IMMA ndio walirahisisha usajili wa kampuni ya Deep Green Finance Limited iliyokwapua mabilioni ya shilingi kutoka benki kuu.

Pili, baadhi ya wakurugenzi wa IMMA ndio walikuwa waanzilishi wa Deep Green Finance Limited inayotuhumiwa kufanya ufisadi.

Tatu, kampuni ya mawakili waliohusika katika shughuli zinazotiliwa mashaka, ndiyo imepata "ngekewa" ya mawakili wake kuteuliwa, mmoja kuwa jaji na mwingine kuwa waziri.

Nne, ni kampuni hiyohiyo ambayo inamwajiri mtoto wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na mtoto wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Hata kama malalamiko hayana msingi, mlolongo huo unastua watazamaji.

Deep Green inadaiwa kuwa na uhusiano wa karibu na makampuni ya Meremeta Gold Limited na Tangold Limited. Meremeta ambayo nayo imefilisiwa. Ndiyo ilikuwa ikiendesha mgodi wa dhahabu wa Buhemba ulioko mkoani Mara. Tangold ndiyo ilirithi mali za Meremeta.

Makampuni yote yalichota mabilioni ya shilingi nchini na kutokomea.

Deep Green Finance Limited ambayo wakurugenzi wake wote watatu wanatajwa kuwa raia wa nje, Mark Ross Weston (New Zealand), Anton Taljaard na Rudolph van Schalkwyk wa Afrika Kusini), ilichotewa fedha hizo katika kipindi ambacho taifa hili lilikuwa katika hekaheka za uchaguzi mkuu mwaka 2005.

Baada ya kujineemesha kwa mabilioni ya shilingi kutoka BoT, Deep Green Finance Limited iliamua, Aprili mwaka jana, kujifilisi na kuteua kampuni ya Protase Rwezahura Gervas Ishengoma (IMMA) kuwa mfilisi kuanzia Julai 27 mwaka jana.

Waziri Masha, mmoja wa wamiliki wa IMMA, aligombea ubunge mwaka 2005 katika jimbo la Nyamagana, mkoani Mwanza na kushinda. Rais alimteua kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini kabla ya kumhamishia Wizara ya Mambo ya Ndani kwa nafasi ya unaibu wakati wa mlipuko wa kwanza wa sakata la Richmond.

Katika mabadiliko makubwa ya baraza la mawaziri ya hivi karibuni, ambapo Wizara ya Usalama wa Raia na ile ya Mambo ya Ndani ziliunganishwa kama zamani, Masha aliteuliwa kuwa waziri kamili wa wizara hiyo.

Kama itathibitika kuwepo mahusiano ya kifisadi kati ya IMMA na Deep Green Finance Limited; wakati huohuo mtoto wa rais akiwa na ajira katika kampuni ambamo tayari rais ameteua mawakili kwa kazi za uwaziri na ujaji, hadhi ya rais inaweza kuwa mashakani.

Mwisho





Source: MKATAMBUGA: Mtoto wa Kikwete ahusishwa na ufisadi
Kweli hii kesi jamani ilipikwa. Hata hivyo huyu jamaa nadhani anamaslahi mengi kwenye serikali. Pia ni mkuu sijui wa chuo cha lushoto.
 
ilifunguliwa na third party, this is ridiculous judgement kwa karne hii.

Mkuu,

Kuna upotoshaji mkubwa unaofanywa na watu wanaojiita wanasheria kwenye huu mjadala kuwa third party haruhusiwi kufungua kesi. Sheria ya Uchaguzi ya Mwaka 1985 inasema wazi kuwa kesi ya uchaguzi inaweza kuletwa mahakamani na
1. Mtu ambaye kisheria alipiga kura au alikuwa na haki ya kupiga kura kwenye uchaguzi unaohusiana na hiyo kesi.
2. Mtu anayedai kuwa na haki ya kupitishwa au kuchaguliwa kwenye huo uchaguzi.
3. Mtu ambaye anadai kuwa alikuwa mgombea kwenye huo uchaguzi.
4. Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Kama unavyojua waliofungua kesi ni makada wawili wa CCM ambao wanadai pia walikuwa wapiga kura kwenye uchaguzi wa jimbo la Arusha. Kwa hiyo, mahakana haikufanya makosa kupokea na kusikiliza hiyo kesi kwa sababu Sheria ya Uchaguzi inaruhusu third party kufungua kesi ya namna hiyo.

Cha maana hapa ni kuipinga sheria husika kuruhusu third party lakini sio mahakama. Je, uko tayari kuwa na sheria ya uchaguzi ambayo hauruhusu third party kufungua kesi kama mhusika mkuu hataki kufungua kesi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…