Hukumu ya mtoto Gujonja Said Gilabi (13)

Hukumu ya mtoto Gujonja Said Gilabi (13)

Duuu hii inatakiwa ikemewe na kumsaidia huyu mtoto kwa kweli.....JF pse naomba tuungane kwa uwezo wetu tumsaidie huyu mtoto kwa kwelii maana sidhani kama hakukuwa na option zaidi kifungoo......hapana sio kiihivyoo...atakosa haki zake kimsingi......kama shule hata future yake itaharibika pia umri wake haikupaswa kutiwa hatiani hapa kuna mazingira ya rushwa lazima......wanaharakatii...psee
 
Duuu hii inatakiwa ikemewe na kumsaidia huyu mtoto kwa kweli.....JF pse naomba tuungane kwa uwezo wetu tumsaidie huyu mtoto kwa kwelii maana sidhani kama hakukuwa na option zaidi kifungoo......hapana sio kiihivyoo...atakosa haki zake kimsingi......kama shule hata future yake itaharibika pia umri wake haikupaswa kutiwa hatiani hapa kuna mazingira ya rushwa lazima......wanaharakatii...psee

Kwa kukumbushia mtoto huyu alitakiwa awe amefanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka jana lakini hakuweza kutokana na mwendelezo wa kesi nzima
 
Na huko jela anapopelekwa ndio chuo kikuu cha majambazi, na hata netwirk zao hutengenezwa huko sasa unapompeleka mtoto kama huyo ni kuandaa future jambazi.
 
hii ni hukumu iliyotolewa na mahakama uko wilaya ya bunda na kumtia hatiani mtoto huyu wa miaka 13 na kuhukumiwa kwenda jela miaka mitano (5). Kwa kosa la kunywesha mifugo maji kwenye mto rubana. Jamani ebu tujadili uhalali wa hukumu hii hata kama vifungu vya sheria vinasema hivyo lakini na busara pia inakiwa itumiwe na mahakimu wetu kwa kuangalia mazingira ya kosa na umri wa mkosaji pia. Mimi nafikiri taasisi za kutetea haki pamoja na wanajamii wote tunatakiwa kulizungumzia hili kwa kina ili kuweza kuwaweka sawa mahakimu wetu.




tanzania ilikufa na nyerere wake.
Nchi hii si mali ya wazalendo tena, ni ya wageni.
Je wewe hujasikia maamuzi dhidi ya wale waarabu watatu wa rujewa mbalali mbeya, laiompiga mtoto wa shule na kumuua kwa kosa la kuiba mapera????
Leo tunaambiwa eti amekufa baada ya kujirusha kwenye gari,
lakini taarifa za awali zilisema kuwa mtoto alipigwa hadi kufa...
Mi yangu mamcho.
 
tanzania ilikufa na nyerere wake.
Nchi hii si mali ya wazalendo tena, ni ya wageni.
Je wewe hujasikia maamuzi dhidi ya wale waarabu watatu wa rujewa mbalali mbeya, laiompiga mtoto wa shule na kumuua kwa kosa la kuiba mapera????
Leo tunaambiwa eti amekufa baada ya kujirusha kwenye gari,
lakini taarifa za awali zilisema kuwa mtoto alipigwa hadi kufa...
Mi yangu mamcho.

Bujibuji please yako yasiwe macho tu. Tukemee kwa nguvu zote hata kwa kutoa tamko la kutoridhishwa na hukumu hii ili jumuiya ya kitaifa na kimataifa isikie kilio hiki cha wanyonge wa Tanzania. Bujibuji kumbuka sisi ni watanzania wachache ambao tumepata nafasi na uwezo wa kuongea na kusikika.
 
Huu ni uonevu wa hali ya juu. Kwanza kimaisha mtoto huyu ameshayaumba tayari kwa kuwa elimu tena hakuna, kama hakumaliza darasa la saba then atasomaje secondary?? Au akitoka jela atakuja kusoma MEMKWA??? Na hata kama atapata nafasi ya kusoma hiyo elimu ya ngumbaro unataka kuniambia atasoma kweli wakati akiwa jela for sure anapata elimu dunia ya kumpatia short cut za maisha?? Ni wakati sasa umekuja tuwe na dedicated community Lawyers.

Nafikiri nahitaji kwenda kusoma sheria sasa, nibadili proffession totally na nijikite fully katika advocate wa community causes. Nina amini nikiandika proposal kwa ajili hii na nikiji commit kabisa bila tamaa nitapata wafadhili na nitafungua law firm kubwa sana na ya maana kuliko za sasa za biashara tu bila kujali haki. Inaniuma sana kama mzazi.
 
Huu ni uonevu wa hali ya juu. Kwanza kimaisha mtoto huyu ameshayaumba tayari kwa kuwa elimu tena hakuna, kama hakumaliza darasa la saba then atasomaje secondary?? Au akitoka jela atakuja kusoma MEMKWA??? Na hata kama atapata nafasi ya kusoma hiyo elimu ya ngumbaro unataka kuniambia atasoma kweli wakati akiwa jela for sure anapata elimu dunia ya kumpatia short cut za maisha?? Ni wakati sasa umekuja tuwe na dedicated community Lawyers.

Nafikiri nahitaji kwenda kusoma sheria sasa, nibadili proffession totally na nijikite fully katika advocate wa community causes. Nina amini nikiandika proposal kwa ajili hii na nikiji commit kabisa bila tamaa nitapata wafadhili na nitafungua law firm kubwa sana na ya maana kuliko za sasa za biashara tu bila kujali haki. Inaniuma sana kama mzazi.

Mawakili wetu tunaowategemea na maprofesa waliobobea ndio hao wanaokwend kuwatetea akina Lyumba, Wahalifu waliokamatwa wakiibia nchi rasilimali zetu i.e samaki wa Magufuli, EPA n.k Wananishangaza sana hawa wansheria wetu hata kama wanataka pesa lakini this is too much tuwasaidie basi na Watanzania wanaoonewa pasipo sababu na kwa kukosa usaidizi wa kisheria.
 
Hii inaonyesha ni jinsi gani watu wanavyotumia elimu yao ndivyo sivyo.Elimu lazima iangalie mazingira. mimi ninavyojua ni kwamba, huyu ni mtoto anatakiwa apewe hukumu kulingana na umri. nina hofu kwamba huyo mtoto kapelekwa mahabusu ya watu wazima!!!!
 
Nakumbuka maneno ya Dr Sengondo,M aliyasema akihojiwa na mwandishi kuwa Mawakili na wasomi wako busy kuwatetea matajiri na watu wakubwa na kuwasahau walalahoi na masikini wa_Tz. Jamani hivi hakuna mawakili wa kumtetea huyu mtoto,mko wapi NGO's, Mko wapi TAWLA,NEMC, Mama Ananilea Nkya na team yake ?

Nashindwa kuelewa upeo wa hakimu na baraza lake waliotoa hukumu hiyo, ni wazazi kweli,je ni kiasi gani maji hayo yameharibiwa na hao mifugo ukilinganisha na yale ya mto(nimesahau jinale) yaliyoharibiwa na Mgodi wa North Mara na kusababisha mifugo kufa na majani kukauka? Je kama ni hukumu Mgodi huo utafungiwa miaka mingapi?.

Jamani sijui Sheria wala sijasomea, lakini kwa upeo nilionao hukumu mara nyingi inalenga mafundisho, sasa haya ni mafundisho au kumkomoa mzazi? Nini matarajio ya kijana akitoka jela? je kijana akitoka jela na kusikia au kuona kuwa North Mara-mgodi bado wanaathiri mazingira na maji ya mto bila kuchukuliwa hatua atakuwa amejifunza nini.

Ingelikuwa Rwanda, watu wangeliuliza hakimu alikuwa kabila gani? je sisi hapa Tz tuseme nini kama sio UFISADI.
 
nakumbuka maneno ya dr sengondo,m aliyasema akihojiwa na mwandishi kuwa mawakili na wasomi wako busy kuwatetea matajiri na watu wakubwa na kuwasahau walalahoi na masikini wa_tz. Jamani hivi hakuna mawakili wa kumtetea huyu mtoto,mko wapi ngo's, mko wapi tawla,nemc, mama ananilea nkya na team yake ?

Nashindwa kuelewa upeo wa hakimu na baraza lake waliotoa hukumu hiyo, ni wazazi kweli,je ni kiasi gani maji hayo yameharibiwa na hao mifugo ukilinganisha na yale ya mto(nimesahau jinale) yaliyoharibiwa na mgodi wa north mara na kusababisha mifugo kufa na majani kukauka? Je kama ni hukumu mgodi huo utafungiwa miaka mingapi?.

Jamani sijui sheria wala sijasomea, lakini kwa upeo nilionao hukumu mara nyingi inalenga mafundisho, sasa haya ni mafundisho au kumkomoa mzazi? Nini matarajio ya kijana akitoka jela? Je kijana akitoka jela na kusikia au kuona kuwa north mara-mgodi bado wanaathiri mazingira na maji ya mto bila kuchukuliwa hatua atakuwa amejifunza nini.

Ingelikuwa rwanda, watu wangeliuliza hakimu alikuwa kabila gani? Je sisi hapa tz tuseme nini kama sio ufisadi.

huyo hakimu pasipo shaka ni labda fisadi au ni fisadi wa taaluma.

Niliwahi soma post hapa jf ya mtu mmoja ambaye alifuatilia suala la mama mmoja aliyekuwa na mtoto pale muhimbili ambaye alikuwa hapewi huduma na dr alitaka ampe rufaa ya kwenda kcmc kwa sababu ya ufisadi, mpiganaji wa jf alifuatilia mpaka ktk ngazi zote. Nashauri wapiganaji kama hao wampiganie huyu mtoto, waziri wa sheria ansemaje?

Mwanakijiji huwa unajitahidi sana kuwabana wanaotoa maamuzi ya utata, nilikusikia ulivyombana tarik azizi wa tz ilipofungiwa mwanahalisi, unaonaje ukiwahoji hao wala nchi?

Jamani mwenye email ya kina kijo gisimba awatumie haiyamkini hawana taarifa ya hili janga.

Inauma na kusikitisha sana.
 
Naitazama hukumu hii kama fundisho kwa wazazi wanaoweza kuwatumia watoto wao kuvunja sheria. Tukiacha watoto wafanye wanavyotaka, heunda hata 'mtoto' wa miaka 18 akatumwa kufanya 'maajabu' zaidi, Je, tutegemee wanaharakati wa haki za binadamu kutetea uvunjaji wa sheria?
 
Wana JF kwa kweli tujitahidi sana yule mtoto atolewe tena mapema sana kabla hajaathirika....Serikali ipo kweli??hata serikali ya mkoa ipo kweli??
 
Naitazama hukumu hii kama fundisho kwa wazazi wanaoweza kuwatumia watoto wao kuvunja sheria. Tukiacha watoto wafanye wanavyotaka, heunda hata 'mtoto' wa miaka 18 akatumwa kufanya 'maajabu' zaidi, Je, tutegemee wanaharakati wa haki za binadamu kutetea uvunjaji wa sheria?

Sasa hapa unataka kusema nini? Adhabu apewe mtoto au Mzazi?
Hapa watu wanasema kwanza mtoto atoke jela na mwisho mzazi aulizwe kulikoni kumtuma mtoto mdogo kuchunga ng'ombe peke yake? Je alimwambia au alimuelekeza mtoto aende wapi kunywesha maji hiyo mifugo?
Naona na wewe maneno yako yamekaa kama huyo hakimu.
 
Back
Top Bottom